Sunday 31 December 2006

Mahakama za Zenj na Matatizo ya Ubabe

Mahakama za zenj katika ngazi zote kuanzia mahakama ya wilaya hadi mahakama kuu ya rufaa zimekuwa zikukutana na wababe ambao hupinga maamuzi ya mahakama hizo kwa muda mrefu sasa.

Tukio la hivi karibuni huko Kibeni katika mkoa wa Kaskazini linathibitisha kuwa maamuzi mengi ya mahakama yamekuwa hayakubaliwi na wanajamii na hasa yale ambayo yamekuwa yakihusisha ujenzi wa nyumba.

Zipo kesi nyingi kuhusu migogoro ya ardhi katika Zanzibar, kesi hizi nyingi zimetokana na kutokuwepo na uwazi katika sheria ya ardhi ya mwaka 1985. Kwa ufupi ardhi yote ya Zanzibar ni mali ya serikali na sio vipando katika ardhi hiyo. SMZ ndio yenye jukumu la kupanga na kugawa ardhi visiwani humo, na kutoa umiliki wa ardhi kwa mtu binafsi, taasisi, mashirika n.k

Kwa upande mwingine serikali hiyo hiyo imekuwa ikitambua baadhi ya hati miliki za ardhi ambazo zilitolewa kabla ya mapinduzi ya Zanzibar(1964) mwa madai kuwa ardhi hizo hazikuwahi kutaifishwa na kuwa mali ya serikali au zimetiwa wafku hivyo serikali haiwezi kuzitaifisha...! Sasa unaposema kuwa ardhi yote ya Zanzibar ni mali ya serikali huku ukijua kuwa sio kweli maana yake ni nini? ka si kupotosha ukweli na kujenga mazingira ya dhuluma!

Matatizo mengine ambayo yanachangia kuwafanya wananchi kuwa wababe dhidi ya maamuzi ya serikali na vyombo vyake, ni kutojulikana kwa wigo za kiutawala visiwani humo. Haijulikani ni wapi ardhi ya serikali inaanzia na wapi inaishia, hata hizo wizara zimekuwa kimya kuelimisha wananchi juu ya suala zima la ardhi.. Wananchi wameachwa kwenye giza huku watawala wakijua hilo pasipo kufanya lolote za ya kukurupuka pale yanapotokea matatizo ya ardhi kwa kutoa amri kubwa kubwa.

Ubabe wa wananchi katika kupinga Hukumu za Mahakama umetokea huko Shakani katika wilaya ya Magharibi mkoa wa Mjini/Magharibi na sasa zimehamia katika mkoa wa Kaskazini. Hii yote ni kwa sababu SMZ imeshindwa kusimamia sheria zake. Iwapo serikali hiyo ingekuwa wazi na hasa kwenye eneo la ardhi lenye migogoro mingi, hapana shaka kusingekuwepo na matatizo haya ya baadhi ya watu kukejeri na kupuuza amri za mahakama.

Kingine watendaji wa SMZ, kwa kujua mapungufu ya serikali wamekuwa ndio mashawishi wakubwa wa kuwepo kwa migongano ya ardhi. Aina hii ya undumilakuwili inatisha na inapaswa kufanyiwa kazi

4 comments:

Egidio Ndabagoye said...

Habari za hapo bwana Kibunango.

Ninaweza kupata mawasilino na bwana Kitia Senagwena.Mimi yangu ni: gaphiz@yahoo.com


Ahsante sana.

Kibunango said...

Mmhm... hilo jina ni geni kwangu!

Simon Kitururu said...

Che Upo !tunasubiri atiko nyingine

Kaziyabure said...

Good article but mbona hamna news mpya Muzee, kulikoni au.....