Thursday 30 August 2007

Wednesday 29 August 2007

Kauli ya Nahodha ina Walakini

Waziri Kiongozi wa Zenj, ambae yupo mkoani Ruvuma ametoa kauli ya kusisitiza kuwa, Elimu ndio njia pekee ya kuwaletea maendeleo wakazi wa Mkoa huo,kutokana na mkoa huo kukosa Umeme wa kuhaminika na kuwa na barabara mbovu. Msisitizo wa kauli hiyo aliutoa kwa kufananisha ukuaji wa kasi wa uchumi wa Singapore na udodoraji wa maendeleo ya mkoa huo na Tanzania kwa ujumla.

Kauli hii ina utata mkubwa kwani elimu pekee haiwezi kuleta maendeleo yoyote iwapo njia zingine za kuleta maendeleo zitakuwa zimebanwa kwa wananchi. Mkoa wa Ruvuma unasifika kwa kuzalisha Mahindi, Kahawa, Tumbaku,Alizeti na mazao mengine. Kabla ya mwaka 1984, usafiri wa kwenda huko ulitegemea zaidi njia ya anga (ATC).Usafiri wa barabara ulikuwa ni wa usumbufu mkubwa na uliweza kuchukua muda mrefu kufika mkoani. Kufunguliwa kwa barabara ya Makambako - Songea katika kiwango cha lami, kulitoa fursa kubwa kwa mkoa huo kuvuma katika uzalishaji wa Mahindi. Barabara hii haikuja kutokana na elimu ya waakazi wa huko bali ni kutokana na umuhimu mkubwa wa taifa kupata Mahindi na Kahawa toka mkoani huko.

Mkoa wa Ruvuma kwa miaka mingi umekuwa ukitegemea umeme wa nguvu ya jenereta, ambao licha ya kuwa ni ghali kuuendesha, upatakanaji wake umekuwa ni wa kimgao kwa zaidi ya miaka ishirini sasa. Sasa hapa sijui elimu ya aina gani inatakiwa ili mkoa huo uunganishwe kwenye gridi ya taifa, ambayo inapita katika mikoa ya jirani zake.

Nimeshindwa kuelewa kauli ya Nahodha, kati ya kuwa na elimu na uwewezeshaji wa miundo mbinu na uchumi wa mkoa husika. Kwa mfano majumba ya michenzani huko Zenj hayakujengwa kwa kuwa waakazi wa zenj wote walikuwa ni wajuzi wa ujenzi. Yalijengwa kwa sababu uchumi wa Zenj kipindi hicho ulikuwa unaruhusu, na viongozi kwa kushirikiana na wananchi waliona upo umuhimu wa kufanya hivyo.

Kwa mkoa wa Ruvuma kuwaambia kuwa tatizo lao la umeme litatatuka kwa kuwa na elimu na sawa na kuwaondoa njiani tu...

Tuesday 21 August 2007

Wadau



Altune na Kibunango

Umbeya Wenye Manufaa...

Hatua ya mradi wa Usimamizi wa Uhifadhi na Mazingira ya Ukanda wa Pwani "MACEMP" kanda ya Zenj kuanzisha mpango wa kuwafanya wavuvi kuwaripoti kwa siri wavuvi haramu ni mzuri kwa lengo la kuwajua wavuvi haramu. Hatua hii imechukuliwa ili kudhibiti uvuvi haramu ambao kwa kiasi kikubwa wamekuwa wakiharibu mazingira ya baharini, pamoja na kuhatarisha maisha ya viumbe wa baharani.

Lengo kubwa la mradi huo ni kuhifadhi na kutunza mazingira ya pwani kwa kuondoa umaskini wa wavuvi. Malengo yao kwa kiasi fulani yamefanikiwa kupitia kwa kamati mbalimbali za wavuvi katika kisiwa hicho. Mradi huo umeshatoa boti,ndege,mikopo na nyavu kwa kamati mbalimbali ili kuondoa tatizo la uvuvi haramu huku ikikuza kipato cha wavuvi hao.

Hata hivyo pamoja na utoaji wa vifaa hivyo, tatizo la uvuvi haramu limekuwa likiendelea. Kuendelea kwa tatizo hilo kwa upande mwingine ni kuonyesha kuwa mradi huo bado kuwafikia wadau wote katika sekta ya uvuvi. Zaidi kuna tatizo ndani ya kamati za uvuvi ambao wamelalamikiwa na mradi kwa kuvujisha siri za mikakati ya kudhibiti uvuvi haramu.

Mradi huu ili kuwa endelevu unapaswa kuangalia tena malengo yake, na njia ambazo wanatumia kuwafikia wadau wake. ushirikishwaji wa kamati hizo za uvuvi na wavuvi wenyewe. Iwapo mojawapo wa malengo ni kuondoa umaskini wa wavuvi, hapana shaka basi wawatafutie au kuwaelekeza jinsi ya kupata soko la uvuvi wao(soko la ndani na nje), uhifadhi endelevu wa maeneo yanayotumika kwa uvuvi, maana na athari za uvuvi haramu.
Kutoa vifaa pekee sio njia ya kuweza kufanikisha kuondoa uvuvi haramu na hata umaskini wa wavuvi hao.

Ipo mifano mingi ya miradi ambayo ilipewa vifaa vingi kwa miradi hiyo lakini ikashindwa kuendelea na kuishia kufa baada ya muda mfupi. Hii ilitokana na wadau kutojiona kuwa wapo ndani ya miradi hiyo, na kujenga tabia kuwa maendeleo ya miradi hiyo sio yao bali ni ya serikali au watoa miradi hiyo.

Iwapo mradi wa MACEMP watataka mradi huu uwe endelevu, inawabidi kuangalia ni njia gani ambayo wataweza kuitumia kuhakikisha kuwa wadau wao wanajua umuhimu wa mazingira ya bahari ambalo ndio shamba lao la kuwaingizia kipato. Inawabidi wawafikie hadi wale wavuvi wa chini kabisa,zaidi ya kuishia kwenye kamati na wale wavuvi wanaojulikana huko vijijini. Zaidi ya kuwafikia itawabidi kuwapa elimu tosha ambayo itawafanya wathamini na kutambua umuhimu wa mradi huo kuwa upo kwa ajili ya kuwaondolea umaskini huku mazingira ya bahari na viumbe vyake yakiwa salama.

Sunday 19 August 2007

TV Zanzibar(TVZ): Jionee mwenyewe walivyochoka

Pamoja na kushikilia rekodi ya kuwa kituo cha kwanza cha television ya rangi katika Afrika ya Mashariki kama sio Afrika, Television hiyo imekuwa ikirudi nyuma kimaendeleo kila kukicha. Sababu za kuanguka kimaendeleo zinajulikana sana, kwani zimekuwa zikisikika kila siku masikioni mwetu, toka kwa Viongozi wa Kisiasa hadi kwa Watendaji wa kituo hicho.

Lengo la bandiko hili si kuzungumzia uchakavu wa Majengo au vyombo vya kurushia matangazo ya tv hiyo, bali ni kuzungumzia muundo wa web site yao, ambayo umeniacha hoi bin taabani.

Tovuti ya kituo hicho kikongwe unakatisha tamaa, na haina uhusiano wowote wa moja kwa moja na shughuli za kila siku za kituo hicho. Zaidi Tovuti hiyo ni kama imewekwa kuhifadhi baadhi ya hotuba za Rais na Waziri kiongozi wa Zenj. Pengine ingependeza zaidi iwapo tovuti hiyo ingekuwa ni ya Ikulu au ya Ofisi ya WK!

Sijui ni kazi ya Mkurugenzi au Afisa Uhusiano au Mwangalizi wa ofisi kusimamia update za tovuti hiyo. Kwa yoyote ambae anahusika basi ameshindwa kabisa kuelewa ni kwa nini TV huwa na tovuti, au ndio hadithi ile ile ya vyombo vya SMZ kujipendekeza zaidi kwenye Ofisi za Wakubwa wao, na kusahu kushughulikia maendeleo ya Ofisi zao!

Kwa ufupi ni aibu kubwa na ni kituko kikubwa kama si kioja kwa TVZ kuiweka hewani tovuti yao. Kama walikuwa hawajawa tayali kuweka tovuti, wangeweza tu kushikiria domain yao bila ya kuirusha hewani kitu ambacho hakina uhusiano wowote na shughuli zao za kiutendaji, hata historia yao. Zaidi hiyo Elimu kwa Televisheni naona bado kufikiwa au kufanyiwa kazi

Wednesday 15 August 2007

Mbinu za Kizenj za Kusafirisha Mizigo...



Moja ya mambo niliyo yaona huko UK ni jinsi wazenj wanavyojitahidi kusafirisha malundo ya vitu vilivyotumika toka UK kwenda Zenj... Mazagazaga hayo ni kuanzia mafriji, mavideo(VHS), maprinter, mamonitor, makomputer, majiko ya umeme /gasi mabafu, vyoo, n.k.




Makontena ya size ya futi 40 ndio maalufu katika kusafirishia mazagazaga hayo.. ambayo mengine yapo katika hali mbaya sana kutumika zaidi ya kufaa kwa kutupwa tu.



Leo hii tuangalie jinsi ya kusafirisha magari matano katika kontena la futi 40......






















Wednesday 8 August 2007

Safarini Suomi...

Baada ya kuona Vituko kibao vya wazenj hapa Uk... takribani kwa miezi minne sasa, Nageuza safari na kurudi kijiweni huku nikiwa na rundo la vituko vya wazenj hapa uk... tokea wazungu wa unga, hadi vitangi, wasomi na wafanyabiashara, wazazi hadi wajane... ili mradi ni vituko kede kede.. nikipata nafasi nitakuwa nawapasha baadhi ya vituko vyao...