Thursday 13 September 2007

Wajane waweka rekodi mpya huko zenj....!

Wajane wa kisiwa cha Zanzibar wameweka rekodi mpya katika fani ya mavazi. Ni baaada ya kuwa wabunifu wa kwanza kupaka/kuchora hinna kwenye vitambaa ambavyo hutumika kutengenezea nguo mbalimbali. Ubunifu huu waliupata kutokana na kuhudhulia kozi ya muda mfupi juu ya kuchora hinna kwenye vitambaa.

Ili lengo la mafunzo hayo liweze kufanikiwa ambalo ni kuongeza kipato kwa Wajane hao, ni muhimu kuona kuwa wanakuwa na sehemu rasmi ya kufanyia biashara zao. Kwa upande huu wa fani zisizo rasmi kuwekuwepo na usumbufu mkubwa wa sehemu za kufanyia shughuli zao, pengine ni kutokana na serikali kutowajali, hivyo kuwasumbu sumbua kila kila.

Sehemu ambayo Wajane hawa na wafanyabiashara wengine katika fani hiyo wamekuwa wakiitumia ni Eneo la mji mkongwe na sehemu ya Uwanja wa Forodhani na baadhi ya mitaa ambayo hutokea katika uwanja wa forodhani kama vile mtaa wa gizenga. Halmashauri ya Mji kupitia maelekezo ya Mamlaka ya Mji Mkongwe, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mjini Maghalibi na ofisi ya Waziri Kiongozi wamekuwa mara kwa mara wakiwaondoa wafanyabiashara hao kwa madai mengi, ambayo mengine uhusisha mambo ya dini.

Kwa kuweza kuweka rekodi ya Dunia, ambapo sasa wataweza kujiongezea mapato yao maradufu, Ni vema kwa serikali kutowasumbua sumbua Wajane hao. Soko lao hilo linawalenga watalii ambao hupatikana katika maeneo ya forodhani ambako kuwa vivutio kadhaa vya Utalii. Na zaidi SMZ sasa iweke mikakati ya kuweza kutambua fani zisizo rasmi, kwani zaidi ya kutoa ajila kwa wahusika zitaweza vilevile kuingiza mapato ndani ya serikali na kusaidia juhudi za serikali kupunguza umaskini kwa wananchi wake.

No comments: