Sunday 27 July 2008

Zenj imejaa tele Bara


Hivi karibuni nilitembelea katika Jiji la Mwanza na kubahatika kukutana na bango hili, nilijaribu bila mafanikio kuitafita ofisi hiyo ya Bima ambayo ni mojawapo wa Ofisi zinazojiendesha zenyewe visiwani Zenj. Hapana shaka pamoja na kero zinazozungumziwa Shirika hili linafaidi Muungano kwa kuweza kujitanua hadi Jijini Mwanza.

Pengine Mashirika makubwa huko Zenj, ukiondoa Shirika la magari ambalo limepigwa stop kwa namba zake za magari kutumika huko Bara zikafuata mfano wa Shirika la Bima. Asasi zingine ambazo zinaweza kujitatumua huko Bara ni kama asasi ya jeshi la kujenga uchumi, wao wanaweza kuingia katika masuala ya ulinzi, kwani ni soko ambalo linakuwa kwa kasi... Jamaa wa Zenj state engineering ambao pamoja na uwezo wa kujenga nyumba ndani ya siku saba wameendelea kudorora kama sio kufa kibudu kwa kukosa kazi huko zenji, wanayo nafasi nzuri ya kufufuka iwapo wataweza kufuata nyayo za Zantel na Shirika la Bima Zenj

No comments: