Tuesday 30 September 2008

Idd Mubaraka


Napenda kuwapa mkono wa idd wadau wote wa blog hii. Sikukuu njema

Monday 29 September 2008

Wanafunzi na Mazingira...Case: Mwanza





Mazingira ya shule ya Msingi Igoma. Shule hii ina klabu ya mazingira ya wanafunzi na moja ya kazi zake ni kutunza mazingira ya shule hiyo.




Wanafunzi wa shule ya Msingi Kirumba wakiandaa shimo kwa ajili ya utengenezaji wa mbolea kwa taka za jikoni. Klabu ya Mazingira katika shule hiyo hujishughulisha na usafishaji wa mazingira katika kata yao ya Kirumba.


Uandaji wa mashimo kwa ajili ya kutengeneza mboji kutokana na taka za jikoni, katika shule ya Msingi Isenga

Wednesday 24 September 2008

Chumbe...Na sifa zake





Chumbe ni kisiwa chenye ukubwa wa hekta 20 na kipo umbali wa kilomita 6 toka Mji Mkongwe - Zanzibar. Ni rahisi sana kukiona kisiwa hiki ukiwa unaingia ama kutoka Zanzibar kwa njia ya bahari... aidha iwapo unaingia kwa njia ya anga unaweza kukiona kisiwa hiki kilichojaliwa utajili wa mazingira ya baharini.

Umaarufu wa Chumbe kwa wakaazi wengi wa Zenj hautokani na umaarufu unaojulikana duniani kote katika mazingira ya kisiwa hicho, bali ni kutokana na kauli za viongozi wa kisiasa wa visiwa hivyo wakitumia kisiwa hicho kama mpaka wa mambo mengi ya kisiasa baina ya Zanzibar na Tanzania Bara. Viongozi wengi kuanzia Marehemu A.Karume, rais wa kwanza wa visiwa hivyo amehawi kunukuliwa akisema baadhi ya mambo ya Tanzania Bara mwisho wake ni Chumbe.... na wengi kwa wakati tofauti wamekuwa wakiendelea kutumia kisiwa hicho kutenganisha mambo ya SMZ na JMT.... Pengine hata sasa kwenye sakata la mgao wa mafuta wengi watadai kuwa JMT mwisho wao ni Chumbe...

Zaidi ya mambo ya kisiasa kisiwa hicho kinajulikana duniani kama ni kisiwa cha kwanza duniani kuwa na "Coral Park" inayomilikiwa kibinafsi, kisiwa cha kwanza katika Tanzania kuwa na "Marine Park" aidha ina hoteli ambayo ipo kwenye hoteli 20 bora duniani kimazingira "Eco Hotel". Zaidi, kisiwani humo unaweza kuwaona kobe kadhaa, na kuna kobe mwenye miaka zaidi ya 125 ndani ya kisiwa hicho.. Zaidi kisiwa hicho kimewahi kushinda tuzo ya British Airways- Tourism for Tomorrow, mwaka 2000

Saturday 20 September 2008

Jumba la Maajabu- Beit al Ajaib - House of Wonders....Ni kwanini likaitwa hivyo?



Ni rahisi kuliona unapoingia Zanzibar kwa njia ya bahari. Ni jumba lenye historia ndefu sana katika kisiwa cha Zenj. Leo hii Jumba hilo lenye zaidi ya nguzo 40 linatimiza miaka 125 tokea kujengwa kwake. Mengi yamelikuta jumba hilo kiasi cha kuwa mojawapo ya vivutio vya utalii katika Zanzibar.

Katika kusherehekea miaka 125 ya Jumba hilo ni vema kujikumbusha historia yake na umuhimu wake katika historia ya Zanzibar. Ubunifu wa jumba hili ulifanywa na askari wa meli toka Scottland na lilijengwa na surtan Barghash bin Said katika mwaka wa 1883, kwa ajili ya ofisi yake. Zaidi matumizi ya jumba hilo yamekuwa yakibadilika kadiri miaka ilivyokuwa ikienda na jinsi tawala zilivyokuwa zikibadilika visiwani humo.

Matumizi ya jumba hilo kati ya mwaka 1870-1888(miaka 120 nyuma)ilikuwa ni kwa ajili ya sherehe za kitaifa, kumbuka wakati huo Zenj ilikuwa chini ya utawala wa kisultan... Hadi kufikia mwaka 1913 Waingereza walilifanya jumba hilo kuwa ofisi ya serikali za mitaa. ofisi hizo zilidumu hadi wakati wa uhuru na baadae mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964. Kati ya mwaka 1964 na 1977 Jumba hilo maarufu lilitumika kama jumba la kumbukumbu za ASP na SMZ kwa ujumla... Kwa mfano ndio ilikuwa sehemu pekee ya kuweza kuona magari ya Rais wa kwanza wa Zanzibar Marehemu Abeid Karume.

Ilipoundwa CCM mwaka 1977, Jumba hili liliendelea kutumika kama makumbusho ya ASP na taifa na kama ofisi ya CCM, hali ya jumba haikuwa ya kuridhisha sana pamoja na kuwa na historia ndefu.


Kuja kwa mamlaka ya hifadhi na uendelezaji mji mkongwe kulifungua ukurasa mpya wa hifadhi ya mji mkongwe hii ilikuwa katika miaka ya mwisho ya 1988 hadi mwaka 1994 ambapo sheria ya mamlaka ya hifadhi na uendelezaji mji mkongwe ilipopata baraka za Baraza la wawakilishi na siginecha ya prezidenti.. Mwaka 1992 nilipata kufanya kazi na UNDP kaatika kukarabati Jumba hili na ni hapo nilipopata nafasi ya kuweza kuvinjari jumba hilo kwa mapana na marefu... ni wakati ambapo nilipenda kujua ni kwa nini jumba hilo likaitwa la maajabu, ni wakati ambapo nilipenda zaidi fani yangu ya ujenzi na nilikuwa na kila raha nafuraha ya kushiriki katika matengenezo/ukarabati wa jengo hilo...

Moja ya sifa kubwa ya ya jumba hili ni vita vilivyodumu kwa muda mfupi kabisa katika historia ya vita duniani! Vita hivi vilitokea mwaka 1896, na baada ya vita hivi ndio picha halisi ya jumba hilo kwa leo inavyoonekana. Hii ni baada ya kuunganisha mnara wa saa uliokuwa mbele ya jengo hilo na jengo lenyewe.

Lakini ni kwa nini likaitwa jumba la maajabu?... Wataalamu wa histori ya Zenj wanasema umarufu wa jengo hilo umejengwa kwa sifa zifuatazo;-
1. Ni jumba la kwanza Afrika ya Mashariki kuwa na Umeme.
2. Ni jumba la kwanza Afrika ya Mashariki kuwa na lifti( elevator)
3. Ni jumba la kwanza Afrika ya Mashariki kuwa na mfereji ndani ya nyumba( Bomba la maji)

Lakini kwa nini Jumba hilo sio maarufu sana miongoni mwa wakaazi wa visiwa hivyo? Hii inatokana na imani kuwa katika nguzo zaidi ya arobaini za jumba hilo ni makaburi ya watumwa waliozikwa wakiwa hai...

Thursday 18 September 2008

Ndoto inapoyeyuka....


Kwa muda mrefu kumekuwepo na uvumi wa kuwepo kwa mafuta katika visiwa vya Zanzibar, hii ni kutokana na chunguzi mbalimbali zilizowahi kufanyika katika visiwa hivyo katika nyakati tofauti. Uvumi huo kwa kiasi uliweza kuwafanya Wazenj waanza kutembea vifua mbele wakiwa na imani siku moja itafika na mafuta yatachimbwa katika visiwa hivyo katika kiwango cha biashara. Hii ilipelekea hata serikali ya muungano kuingiza kinyamela suala la gesi asilia na mafuta katika mambo ya muungano, na kufanya neema hiyo kama itakuwepo basi itakuwa ni ya muungano.

Taarifa za hivi karibuni kuwa kuna uwezekano mdogo wa kuwepo kwa mafuta hayo kumesababisha Wawakilishi kutoamini masikio yao toka kwa mtaalamu wa uchunguzi wa mafuta.... Kwa maelezo zaidi soma hapa

Monday 15 September 2008

Ngoma Afrika Band na Ziara yao Ulaya...









Bendi ya mziki wa dansi ya The Ngoma Africa inayoongozwa na mwanamziki nguli Ebrahim Makunja alimaarufu Ras Makunja hilifanikiwa kuufunga mtaa mrefu katikati ya jiji la mji mashuhuri wa Hamburg,katikati ya eneo maarufu hamburg-Haltona,
kulikuwa pata shika ya Nguo Kuchanika wakati bendi hiyo mashuhuri kwa kuwadatisha washabiki hakili na mziki wao wa dansi "Bongo dansi" kutoka Tanzania ukiwa unarindima
Live katikati ya mji katika tamasha kubwa la aina yake Afrika-Festival.

Hilikuwa majira ya saa 2.30 usiku wakali wa mziki wa dansi barani ulaya "The Ngoma Africa band walipanda jukwaani na kuanza kuporomosha nyimbo zao za kiswahili zilizo sindikizwa na mdundo mkali wa dansi ! mziki ambao uliweza kuwazoa mashabiki kwa kasi
ya aina yake na kuwatia kiwewe maelfu ya washabiki katika tamasha hilo.

*Ni Ras Makunja na Bendi ya The Ngoma Africa !
siku hiliyofuatia 30-08-2008 wakali wetu hawa walipanda jukwaa kubwa katikati ya
mji wa Krefeld,katika onyesho kubwa la wiki ya mwafrika (Africa Week) huko nako kuwa
patashika washabiki wamataifa mbali mbali wakiwa wamechanganyikiwa na mdundo wa
dansi wa Tanzania,jukwaa lilikuwa limezungukwa na walinzi wenye suti na miwani meusi,
Ras Makunja na kikosi chake wakiwa jukwaani na kuhakikisha mdundo huo unawamtingisha kila mtu.

Bendi hiyo ambayo imefanikiwa kuwanasa washabiki wa ulaya na mziki wao wa dansi
kutoka bongo Tanzania,inasemekana ndio bendi pekee ya mziki wa dansi iliyoweza kugusa hisia za kila mshabiki,si watoto wala wakubwa,vijana kwa wazee,wake kwa waume,wazungu na weusi hili mradi dansi lao linatingisha.

Taarifa hii imeletwa kwa hisani kubwa na Msema Kweli

Sunday 14 September 2008

Madawa ya kulevya na Zenj...Watoto matatani!




Matumizi ya madawa ya kulevya huko Zanzibar sasa yamechukua sura mpya ambayo ni mbaya sana na ya kutisha katika historia ya matumizi ya madawa hayo Visiwani humo. Athari za mwanzo kwa jamii ya visiwa hivyo ilikuwa ni pamoja na kuvunjika kwa ndoa, umalaya na wizi. Hatua ya sasa ni kuambukiza watoto wadogo virusi vya ukimwi kwa kuwachoma sindano zenye damu isiyo salama. Huu ni unyama wa aina yake kutokea huko visiwani.

Hadi kufikia mwaka 2001, Zanzibar ilikuwa tayali imepata umaarufu mkubwa wa kuwa bandari ya kupitishia madawa ya kulevya. Umaarufu huu ulisadikiwa kufunika hata umaarufu wa soko la watumwa uliotokea miaka mia mbili iliyopita. Ukuuaji wa biashara ya ya madawa ya kulevya katika Zanzibar ulikwenda sambamba na uporomokaji wa bei ya karufuu katika soko la dunia na kupanda chati kwa biashara ya utalii.

Awali, Zanzibar ilikuwa ni pepo ya wasafiri watumiao Bangi. Hii ilitokana na urahisi mkubwa wa kupatikana kwa bangi visiwani humo. Taratibu madawa mengine ya kulevya yalianza kuingia visiwani na kufikia kilele katika miaka ya tisini.

Zanzibar kuwa pitisho kubwa la madawa ya kulevya katika ukanda wa Afrika ya Mashariki, kunahusishwa sana na mabadiliko ya ya kiutawala huko Afrika ya Kusini, ambapo utawala wa kibaguzi ulifikia kikomo. Ulinzi mkali katika bandari ya Mombasa baada ya ulipuaji wa balozi za USA huko Nairobi na Dar es Salaam ni sababu nyingine inayotajwa ya Zanzibar kuwa kimbilio la kupitishwa kwa madawa hayo. Aidha ubinafishwaji wa Uwanja wa ndege wa Zanzibar katika miaka ya mwishoni ya tisini umetajwa kuchangia kwa kiasi kikubwa kukua kwa upitishaji wa madawa hayo katika Zanzibar.

Matumizi ya madawa ya kulevya yamekuwa yakienda pamoja na uongezekaji wa maambukizi ya virusi vya ukimwi. Hii hasa kwa wale wanaojidunga sindano. Uchunguzi unaonyesha kuwa asilimia 46 ya watumiaji wa madawa hayo hushare sindano, huku zaidi ya asilimia 50 wakifanya ngono (group sex na anal sex) ili kupata madawa hayo. Baadhi ya vijana huweza kutumia hadi US$ 240 kwa mwezi kupta madawa hayo.

Matumizi ya sindano yaliweza kuingia katika sura mpya katika miaka ya hivi karibuni, baada ya kuongezeka kwa watumiaji wasio kuwa na uweo wa kununua madawa hayo. Njia maarufu ya "flash blood" iligunduliwa ambapo mtumiaji wenye nazo mfukoni, hujidunga sindano yenye heroin, na akimaliza kijidunga ufyonza damu yake kutumia sindano hiyohiyo na kumpatia asie na uwezo damu yake ilichanganyika na heroin(diluted). Mchanganyiko huu uweza kumpatia nishai asiye kuwa na uwezo wa kununua herion.

Hali ya sasa ni mbaya mno kama si ya kutisha. Kwani watumiaji wa madawa hayo sasa hupita mitaani na kuwachoma sindano watoto wadogo, sindano hizo ni zile ambazo wanatoka kuzitumia kwa madawa yao ya kulevya, hivyo kuwepo na uwezekano mkubwa wa kuwapatia watoto hao maambukizi ya virusi vya ukimwi. Huu ni unyama mkubwa kabisa katika historia ya matumizi ya madawa hayo pamoja na ugonjwa wa ukimwi visiwani hapo. Kwa ufupi wazazi wengi wapo katika hali ya hofu na hasa wale wanoishi katika mitaa yanye vijana wengi wa kubembea, aidha kwa watoto ni adha kubwa mno kwao kwani inabidi kukaa ndani tu kwa usalama wao...

Saturday 13 September 2008

Weekend Njema...




Forodhani bado inaendelea kufanyiwa mabadiliko makubwa ambayo yatawezesha kupatikana kwa huduma bora kwa wadau wote watumiao eneo hilo maarufu sana hapo Zenj... Zaidi hata umiliki wa eneo hilo la historia utabadilika na kuwa chini ya Agha Khan Foundation. Kiutawala kuna mengi ndani ya eneo hilo, kuna migongano kati ya Mamlaka ya Mji Mkongwe, Baraza la Manispaa, Idara ya Mipango Miji, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi na Ofisi ya Waziri Kiongozi.. Hata NGO nazo kwa wakati mmoja au mwingine zimeweza kulitaka eneo hilo, mojawapo ni ZAYADESA...Upande mwingine wafanyabiashara hasa wale wauza vyakula usiku nao udai kuwa hilo ni eneo lao.

Lakini cha msingi eneo hilo linafanyiwa ukarabati katika muda muafaka, na ni ukarabati mkubwa kabisa kufanyika katika eneo hilo. Cha msingi ili eneo hilo liendelee kuwa katika mvuto na kupunguza uharibifu baada ya kufunguliwa tena, ni vema kwa sasa wadau wa eneo hilo wakapatiwa mafunzo juu ya kutunza mazingira ya eneo hilo. Hii isisubiri mpaka uchakavu mwingine utakapotokea. Wote tunajua kuwa "Samaki mkunje angali mbichi" Hivyo hatua za makusudi zinapaswa kuchukuliwa sasa kwa kutoa elimu ya utunzaji na matumizi ya eneo hilo kwa wadau wote watumiao eneo hilo kwa njia moja ama nyingine.

Wednesday 10 September 2008

SMZ Imejichokea....

Mwishoni mwa wiki iliyopita, Waziri wa kazi na maendeleo ya watoto katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar(SMZ) alinukuliwa akisema kuwa nusu ya wanzibari milioni wenye uwezo wa kufanya kazi hawana kazi. Hii ni kusema asilimia 50 ya watu wenye uwezo wa kufanya kazi hawana kazi. Ni idadi kubwa sana na yenye kutakiwa kufanyiwa kazi. Hesabu hii inajumuisha sekta rasmi na sekta zisizo rasmi visiwani humo.

Kama kawaida wimbo ukawa ni ule ule wa kushaauri kuwa wote wasio na kazi waande makondeni(mashambani) kwa ajili ya kulima, au kwa ufupi wawe wakulima, ila safari hii wimbo huo uliongezewa vionyo vingine kuwa wawe wakulima wa mazao ya biashara. Lakini kila nikijaribu kuangalia idadi ya watu hao na konde zilizopo sasa huko visiwani napata mashaka kama bado hili ni wazo madhubuti la kuondokana na ukosefu wa ajila visiwani humo.

Ikumbukwe kuwa wananchi wengi wa visiwa hivyo walishawahi kugaiwa ardhi kwa ajili ya kilimo, maarufu kama eka tatu. Wakati SMZ ikitoa eka hizo kwa wananchi wake ilikuwa na lengo la kuwafanya wengi wawe wakulima. Hata hivyo ugawaji wake haukuweza au kulenga wale wasio na ajila. Eka tatu hizo kwa sasa ni wachache mno ambao wamendelea kuzitumia kwa shughuli za kilimo, wengi wao walishaziuza kupisha ujenzi wa nyumba za kuishi na biashara.

Zanzibar ni nchi ambayo imekulia katika sekta kubwa ya kibiashara zaidi ya kilimo. Ingawa iliwahi kuvuma sana kwa kilimo cha karafuu, nchi hiyo haijawahi hata mara moja kujitoshereza kwa kilimo cha mazao mengine, pamoja na kuwa mbele sana kwa vifaa na taaluma katika sekta hiyo ya kilimo. Ukiondoa mazao ya Nazi na karafuu na matunda kuna mazao mengi yanalimwa huko kama mpunga ambapo bado kufikia nafasi ya kutosheleza mahitaji ya nchi nzima. Karafuu sasa imeanguka katika soko la dunia, Zao la nazi nalo lipo katika mashaka kutokana na kuongezeka kwa ujenzi wa nyumba. Viwanda ambavyo hapo awali vikitoa ajila kwa wakaazi wengi vingi vimekwisha vungwa na kufutika kabisa katika ramani ya utengenezaji wa ajila visiwani humo.

Kuanguka kwa zao la karufuu kulifungua milango kwa utalii, na serikali hiyo ikaona njia nyingine ya kuongeza pato lake ni kupitia utalii. Kuja kwa utalii kulileta sekta isiyo rasmi ya kutembeza watalii maarufu ka upapasi. Awali ilikuwa ni vita kati ya serikali na mapapasi, hii ilitokana na serikali kukataa kuwatambua hao au kukataa ukweli wa kuwepo na sekta isiyo rasmi visiwani humo. Ilichukuwa muda mrefu kwa mapapasi kuweza kutambuliwa na wizara ya utalii kama ni sehemu mojawapo ya utalii aidha inatoa ajila kwa vijana wa hapo zenj.

Kupanuka kwa utalii Zanzibar kulienda sambamba na ujenzi wa hoteli nyingi za kitalii, hii ilitoa picha kuwepo kwa ajila nyingi visiwani humo. Hata hivyo sio serikali au wananchi wa visiwa hivyo ambao walikuwa wamejiandaa na mabadiliko hayo. Kwani kuanzia kazi za ujenzi ziliwezwa kushika na wageni toka Kenya na baadhi ya watanzania Bara...hii iliianza kutoa malalamiko ya chini chini kuhusu ajila kuchukuliwa na wageni.
SMZ ina hotel zake za kitalii chini ya wizara ya utalii, na ina chuo chake cha utalii hapo Maruhubi,wafanyakazi wachache waliosoma hapo Maruhubi uajiliwa moja kwa moja katika hizo hoteli chache za SMZ Sijui ni kwanini SMZ kupitia wizara na chuo hicho walishindwa kuwavuta wananchi wengi kujiunga na chuo hicho ili kuweza kujipatia ajila katika hoteli lukuki zilizokuwa zikijengwa. mkakati wa kitaifa wa kuona kuwa wananchi wananufaika na hoteli hizo. Hata katikati ya miaka ya tisini wakati SMZ ilipokuwa ikipeleka wanafunzi kusoma nje ya nchi kwa mafungu, idadi ya waliokuwa wakienda huko kwa ajili ya masomo ya utalii ilikuwa ni ndogo mmno kulinganisha na wanafunzi wengine ambao kozi zao zinapatikana kwa wingi katika vyuo kibao Tanzania bara.

Mwishoni mwa miaka ya tisini Zenj iliweza kunufaika na mradi wa miji endelevu, ambao pamoja na mambo mengine ulikuwa na lengo la kutatua kero za wananchi, kwa kuwashirikisha wananchi hao katika kuzitatua. Moja ya mradi ambao uliweza kutengeneza ajila ni ule wa ukusanyaji na utupaji wa taka katika wadi ya Mkele. Ingawa idadi ya walioajiliwa mwanzo wa mradi huu walikuwa kidogo, mradi huu ulilenga kutengeneza ajila kwa wananchi, aidha ukiwa kama mradi kiongozi ulitakiwa kupata kila aina ya msaada ili kuendelea na kupanuka ili wadi na asasi zingine ziweze kuiga mfano na kuweza kutoa ajila kwa wengi. Pamajo na kushirikisha asasi zote tokea Wizara ya Kazi na Maendeleo ya watoto, Tawala za mikoa, Ofisi ya Waziri Kiongozi, ILO na Manispaa ya Mji, mradi huu ulikufa kutokana na baadhi ya Wadau katika asasi hizo kutuupa nafasi ya kuendelea.

Miaka ya elfu mbili, ILO walikuja na wazo jingine la kutoa ajila kwa vijana katika Mji Mkongwe na kama kawaida utashi binafsi wa watendaji wa SMZ mradi huo ulishindwa kufanyika.

SMZ imekuwa kama inawaweka wananchi wake kama rasilimali ya kushinda chaguzi tu, kwani kila ukaribiapo uchaguzi asasi za ulinzi visiwani humo hutangaza ajila lukuki kwa vijana. Ni vema sasa kuangalia sehemu nyingine ambazo zinaweza kutoa ajila kwa utaratibu mzuri na wa kuvutia kama vile uvuvi

Sekta ya uvuvi kwa miaka mingi sijapata kusikia kuwavuta wavuvi wapya kujiunga nao, kama ilivyo kwa sekta ya kilimo. Nina imani kama sekta hii nayo itaweza kupew msukumo kama kilimo ambacho vijana wengi hawapo tayali kujiunga nayo licha ya uchache wa konde zilizopo inaweza kutatua kwa kiasi kibubwa tatizo la ajila visiwani humo. Cha msingi ni namna gani ya kuwashirikisha vijana katika shughuli za uvuvi, kwani soko lake ni kubwa na bado uvuvi unahitaji watu wengi zaidi.

Kwa upande wa utalii ni vema kwa SMZ kutilia mkazo kwa wananchi wake na hasa vijana kusomea fani hiyo, ipo haya ya kupanua chuo kilichopo cha utalii sambamba na mahitaji ya hoteli zilizopo. Nina hakika wenye hoteli hizo watapenda kuajili wazaliwa wa hapo kwani wigo wao wa ufahamu wa visiwa hivyo ni mkubwa kuliko wageni na hili ni moja ya chachundu katika biashara ya utalii. Hili linawezekana kwani bado wazenj wengi hasa wazazi wanamtazamo tofauti sana na utalii.

Saturday 6 September 2008

Bandarini Zenj






Pilika pilika bandarini Zenj... Wikiendi njema na Ramadhani njema..

Friday 5 September 2008

Zenj Majaribuni tena....




Mwezi ujao tarehe 24, kisiwa cha Zanzibar kitawakaribisha visura wa Afrika kuweka kambi yao kabla ya kuanza safari ya kumtafuta kisura wa Afika(M-Net, Face Of Africa) visiwani humo. Jumla ya visura 24 watakuwepo kwenye kambi hiyo ambayo itaisha kwa kumchagua kisura wa Afrika katika kisiwa hicho. Aidha kwa Visura wa Tanzania watachujwa mapema wiki ijayo kabla ya kujiunga na wenzao 12 kutoka kona nchi kadhaa barani Afrika.

Zanzibar mara nyingi imekuwa ikipinga aina hii ya mashindano, ingawa kwa nyakati tofauti wazenj wamewahi kushiriki katika mashindano ya kutafuta mrembo wa zenj wa kushiriki Miss World. Nakumbuka niliwahi kuona Miss Aspen katika miaka ya tisini huko Zenj ambapo alikuwa akisakwa Miss Zenj, aidha ilikuwa ni vituko tupu, tofauti na jinsi warembo wanavyotafutwa huko Bara.

Wananchi wengi wa visiwani humo hupinga vikali aina yoyote ya ushindanishaji wa wasichana na hasa namna ya ushiriki katika mashindano kama hayo kwa kuwa yanaenda tofauti na maadili ya visiwa hivyo. Kuna wakati Miss Zenj aliwahi kutafutiwa katika mkoa wa Dar baada yakuwepo na upinzani wa hali ya juu kwa mashindano ya aina hii.

Wengi bado wanakumbuka jinsi washichana/wanawake toka Bara na Kenya walivyokuwa wakichezea fimbo huko Zenj na hasa katika mtaa wa Darajani na kundi moja la watoto wa simba. Pamoja na kundi hilo kujulikana hakuna hatua zozote zilizowahi kuchukuliwa dhidi yao na vyombo vinavyohusika kwa mashumbulio yao kwa wanawake ambao walivaa suruali ama sketi au kutovaa hijabu.

Nina mategemeo kuwa kambi hii ya kutafuta kisura wa Afrika haitopata kadhia za kupigwa bakora, kwani nina imani kuwa kambi yao itawekwa nje ya eneo la mji. Aidha ninategemea kuwa waandaji wa mashindano hayo watawapa kanuni za uvaaji kwa wasichana hao iwapo watatembelea huko mjini. Kwa upande mwingine hii ni mojawapo ya nafasi nzuri ya kisiwa hicho kuendelea kujitangaza ndani ya Afrika. Mshindi atakaepatikana hapo nategemea ataondoka na sifa nzuri za Tanzania na hasa Zanzibar kama hatochezea bakora....

Thursday 4 September 2008

Huu ni mwezi mgumu kwenda Zanzibar


Seagull ikishusha abiria hapo Zenj wakitokea Dar mwishoni mwa wiki iliyopita.


Sea Express ikushusha abiria tokea kisiwa cha pili


Msongamano wa abiria wa kwenda Zenj kabla ya mfungo wa Ramadhani katika bandari ya Dar.


Kwa wale ambao husafiri mara kwa mara kati ya Zenj na Dar au Zenj na Kisiwa Cha Pili watakubaliana nami kuwa sasa kwenye boti kuna viti vya kulala na ni tofauti kabisa na siku kadhaa zilizopita au kwa maneno mafupi kabla ya kuanza kwa mwezi wa Ramadhani. Kwa kawaida mwezi wa Ramadhani abiria wa boti na hata ndege hupungua sana kati ya Zenj-Dar na Pemba.

Sababu kubwa ya kupungua kwa wasafiri ipo wazi, kwani huu ni mwezi ambao wengi hufunga na hasa wakaazi wa visiwa hivi viwili, Hivyo wengi wao hawapendi kusafiri ili kuepuka adha ya kupata futari na misukosuko mingine ambayo inaweza kuwasababisha kufuturu kabla ya wakati. Zaidi waumini wengi utumia muda huu kuhudhuria sala zote za siku ili kukamilisha funga yenye uhakika na iliyokamilika.

Wageni ambao hupenda kufakamia kila wakati, nao ujiepusha kwenda Zenj ama Kisiwa cha Pili, kwani kuanzia mama lishe, migahawa na hoteli hufungwa hivyo kuwafanya kuwa katika hali ngumu sana ya kushawishi matumbo yao kuwa hakuna chakula asubuhi wala mchana... Hii uwakuta hata watalii ambao zaidi ya kukimbia kutofunga hata mavazi yao huwa hayana nafasi visiwani humo.

Hata hivyo, baada ya futari hakuna sehemu nyingine hapo Bongo ambayo unaweza kufaidi misosi ya nguvu kama Zenj... Kwani sehemu nyingi hufunguliwa na kuuza misosi ya nguvu hadi saa sita ya usiku. Maduka huwa wazi usiku na hata zile baa zinazojificha mchana na kuuza ulabu kwa mlango wa nyuma huwa wazi. Kwa ufupi Usiku huwa kunachangamka sana kuliko usiku wa miezi ya kawaida. Wengi ambao hawapendi kuamka alfajili kwa kuwahi daku hupenda kushindilia misosi hiyo hadi mishale ya saa sita na akilala inakuwa imetoka.

Wednesday 3 September 2008

Military Sonar and Life of Marine Mammals





In 2006 April, 28 Zanzibar villagers were in shock after their coastline was covered with 400 dead dolphins. Zanzibar government went on imposing warning to the villagers and fishermen not to consume the dead dolphins as the reason of their death is not know.

From that peace of story from my country which happened about two year ago, rises my eyebrow when I was thinking what should I write concerned the effects of military vessels on the whales. Soon after that incident in Zanzibar, different comments on what might be the cause of their death were discussed. For example, some scientists believe that, the death may be a result of loud burst of sonar, from miles away and can be heard in water therefore scare marine mammals causing them to surface too quickly. This type of movement is known as bends whereby is occur to the people who dive for feeling severe pains and difficulty in breathing as result come to the surface too quickly. Shortly is when sudden decompression forms nitrogen bubbles in tissue. Other speculates the death to be caused by U.S. Navy task force which patrols the coast of East Africa as part of counterterrorism operations. The villagers themselves were thinking that the cause of death was disoriented of those animals which lead them to shallow water and died. Later on the U.S Navy acknowledged that sonar is likely to contribute to the death of those dolphins.

According to Oxford Advanced Learner’s Dictionary, Sonar is described “as a device or system for finding objects under water by means of reflected sound waves.” The history of sonar goes back after the World War I where Britain and U.S develop the technology of navigating by sound in the sea. In the World War II sonar were used to counter attack the German ship. It was until the cold war era where the sonar technology was improved and was much used. In Word War II sonar was passive: essentially big microphones that listened for the distinctive sounds emitted by large submarines. Nowadays there are mid frequencies active sonar designed to find a new generation of smaller, stealthy submarine. Active sonar is working by sending out sound waves and listening for the reflections of the objects, as this provide the location of object detected.


This improvement and advanced system of sonar have been designed and used despite the knowledge of its effects to sea mammals. Even after the end of cold war, sonar has been used in military testing causing whales and dolphins to stranded and dead. The exercise of Navy using mid-frequency sonar which operates from 2,000 to 10,000 hertz has resulting in increasing to the numbers of mammal stranding. As this technology seem not enough to the military, they have now develop the new technology of sonar known as low – frequency sonar which is believed to cause wide range of sound travel. Environmentalists explain fear to this new technology as it will increase the number of whales and dolphins to stranding. Up to date there are numbers of cases which have been reported due to the effect of sonar, as will be mentioned in the following paragraphs.

In September 2002, fourteen beaked whales were stranded in the Canary Island close to the site of international naval exercise. This happened four hours after the mid frequency sonar was deployed. The effect of this tragedy is lost of ability to navigate for the whiles which force them to strand.

In 2003 US Navy Sonar in Pacific Northwest was direct linked to the number of death of whales. This blast draws attentions to many institutes. One of them was Natural Resources Defense Council (NRDC) which went on to stop US Navy of using the powerful active sonar system known as SURTASS LFA. NRDC was also involving other countries on restriction of using the sonar as to prevent the life of marine mammals.

The battle of protecting marine mammals with sonar have take a new look this January 2008, when President G.W Bush allow US Navy ships to use sonar during exercises off the California coast. The exercises is planned to take place in San Diego, where aircraft carries have been permitted to use sonar on detecting submarines. This decision of President Bush is opposing the court order of stopping the uses of sonar in the vicinity of whales.

Going back to my country four hundred dolphins were dead after beached, there is a need of positive thinking this effects which are caused by sonar. Further studies show that there even more effects to these sea mammals such as the reproduction of this endangered species; to disrupt the feeding of orcas; and to cause porpoises and other species to leap from the water, or panic and flee.

Nevertheless there is other dangerous noise which may also contribute on disturbing marine life. These dangerous sources of noise in the sea are manmade. There is ship traffic; the world is now witness increase of ships due to the increased of global business. These ships generate noise from their propeller, engine, generator and bearing. The propeller is one part of ship which provide a noise pollution to undersurface of sea. Propeller can provide noise from frequency range from 20Hz - 300Hz throughout the sea. Sea mammal such as whales whom they use frequency for navigating and communicating can be direct effected with this kind of noises which are traveling hundred of kilometer in the sea.

Bia zenye Vilemba.....


Huko Zenj bia ikifunguliwa shurti ivishwe kilemba...