Thursday 18 September 2008

Ndoto inapoyeyuka....


Kwa muda mrefu kumekuwepo na uvumi wa kuwepo kwa mafuta katika visiwa vya Zanzibar, hii ni kutokana na chunguzi mbalimbali zilizowahi kufanyika katika visiwa hivyo katika nyakati tofauti. Uvumi huo kwa kiasi uliweza kuwafanya Wazenj waanza kutembea vifua mbele wakiwa na imani siku moja itafika na mafuta yatachimbwa katika visiwa hivyo katika kiwango cha biashara. Hii ilipelekea hata serikali ya muungano kuingiza kinyamela suala la gesi asilia na mafuta katika mambo ya muungano, na kufanya neema hiyo kama itakuwepo basi itakuwa ni ya muungano.

Taarifa za hivi karibuni kuwa kuna uwezekano mdogo wa kuwepo kwa mafuta hayo kumesababisha Wawakilishi kutoamini masikio yao toka kwa mtaalamu wa uchunguzi wa mafuta.... Kwa maelezo zaidi soma hapa

1 comment:

Yasinta Ngonyani said...

kama kweli ndoto hiyo ni uvumi wa kweli basi TZ itakuwa tajiri.