Friday 30 January 2009

Wazenj na Mashairi




PONGEZI kwake Shamhuna, pamoja na Ali Mzee
SMZedi kujikuna, na kuridhisha wazee
Shabashi na kujivuna, Zanzibar isiteketee!

Zanzibar isiteketee, vigogo kuyabaini
Mwakanjuki atutetee, nahodha wa mapinduzi
Na Salmini tuletee, salamu za uzinduzi!

Salamu za uzinduzi, kutia ghera na moyo
Kumbukeni mapinduzi, ni kombozi si uchoyo
Zanzibar si Bata Shuzi, si Lindi si Bagamoyo!

Si Lindi si Bagamoyo, Dola ya Mwinyi Mkuu
Isikatwe yake roho, Dunga ... Unguja Ukuu
Nayo Pemba si Mohoro, imefungasha na Bweju!

Kufungasha na Bweju, Mafia na huko Kilwa
Lakini hayo ni makuu, Mrima kukaripiwa
Na tudai Siku Kuu, Zanzibar kuheshimiwa!.

No comments: