Wednesday 25 February 2009

Wikipedia ya Kiswahili

Watanzania wote wanakaribishwa kuchangia habari za mahali wanapoishi au wanapotoka katika wikipedia ya Kiswahili! (sw.wikipedia.com) Ijulikane ya kwamba wikipedia ni mradi mkubwa wa elimu unaojengwa na wachangiaji wanaojitolea bila malipo yoyote. Kila mtu anakaribishwa kuchangia!

Kwa sasa tumeanzisha makala fupi za kila kata kwenye mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Iringa, Kilimanjaro, Kigoma, Lindi, Mara, Mwanza, Mbeya, Manyara, Morogoro, Mtwara, Pwani na Tanga.

Angalia mfano huu: sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa_wa_Mjini_Magharibi_Unguja

Chini kuna sanduku inayoonyesha mikoa yote. Ukiingia katika mkoa fulani unapata majina ya wilaya. Kila safari ukibonyeza kwenye neno lenye rangi ya buluu unapelekwa kwenye makala mpya. Ukifika kwenye wilaya utaona sanduku lenye majina ya kata za eneo hili. Makala mengi yana habari fupi tu kama "ABC ni kata ya wilaya DEF katika Mkoa wa XYZ. Idadi ya wakazi wake ilihesabiwa kuwa xxxxx katika sensa ya 2002". Kila mtu yuko huru kubonyeza kwenye sehemu ya "hariri" juu ya makala na kuongeza habari.

Baada ya kuongeza habari unabonyeza sehemu ya "Hifadhi ukurasa" iliyoko chini.


Taarifa hii imeletwa kwenu kwa hisani kubwa ya Bw. Kipala anayesimamia kamusi hiyo

Tuesday 24 February 2009

Zanzibar Hakuna Sheria za Ujenzi?

Zanzibar kama nchi, mji mkuu wake ni Zanzibar ambao unaundwa na Mji Mkongwe na Ng'ambo, kiutawala upo katika mkoa wa Mjini Magharibi. Mji wa Zanzibar unapata huduma zake kupitia Halmashauri ya Manispaa ya Zanzibar na Mamlaka ya Hifadhi na Uendelezaji wa Mji Mkongwe.

Halmashauri ya Manispaa kama halmashauri zingine duniani imepitia katika mabadiliko mengi ya kiutawala na sheria za kuongoza mji huo na hasa katika suala zima la ardhi na maendeleo yake kwa kushirikiana na idara zingine kama ofisi ya Mkuu wa wilaya, ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Kamisheni ya Ardhi na baadae Idara ya Mipango Miji na Idara ya Ardhi.

Masterplan ya kwanza kabisa ya mji wa Zanzibar ilitolewa mwaka 1923 chini ya sheria ya mji(Town Decree Cap 79). Master plan ilitolewa kutatua matatizo ya ukuaji wa mji kiholela, kupanua wigo wa miundo mbinu na kurahisisha mizunguko katika mji huo ambao ulikuwa na watu 35000 huku asilimia 30 ya watu hao wakiishi Mji Mkongwe na asilimia 70 wakiishi Ng'ambo sehemu iliyokithiri kwa ujenzi holela.

Mwaka 1958 kulifanyika mabadiliko katika Master plan kwa kuingizwa kwa "Town Scheme" chini ya sheria ya mwaka 1955- "Town and Country Planning Decree" ambapo lengo lilikuwa kuandaa rasimu ya usafirishaji/usafiri katika mji mkongwe na kuendeleza maeneo ya wakaazi yaliyopimwa chini ya viwango huko Ng'ambo (semmi planned settlements)

Master plan ya pili "The Town Master Plan -1968" ilifanywa na Wajerumani, ikiwa na lengo la kuboresha zaidi maeneo ya Ng'ambo ambayo yalikuwa yakipanuka kwa kasi, huku umuhimu mkubwa ukiwekwa kwenye upatikanaji wa huduma muhimu kama vile mifereji, taa za kwenye mitaa na misingi ya maji taka.
Mafanikio yake ni pamoja na Majumba ya Mjeru pale Kikwajunina Majumba ya Kilimani.

Master plan kubwa na ya mwisho ilitolewa mwaka 1982 na wataalmu kutoka China. Pamoja na mabo mengine, master plan hiyo iliangalia zaidi kupanuliwa kwa mji wa Zanzibar kwa kupima maeneo mengine mapya ili kuruhusu nafasi kubwa zaidi kwa ya asilimia 68 ya wazenj waliokuwa wamebanana kupatiwa maeneo ya ujenzi huku wengi wakiishi katika maeneo yasiopimwa kisheria, aidha kutoa nafasi kubwa zaidi ya ujenzi kuanzia nyumba za kuishi shule na maeneo ya biashara, ilitizama vilevile kupunguza umwagaji wa maji taka baharini na kuzuia tabia iliyoanza ya kujenga nyumba katika maeneo yenye mafuriko.

Tokea master plan hiyo ya wachina kumekuwepo na nyongeza mbili moja ikiwa ni ya mwaka 1996 The Tourism Zoning Plan ambayo iliingizwa kwenye Master plan kukidhi mahitaji ya mahoteli na maeneo ya kitalii. Ya pili ni pendekezo la kuimarisha na kuanzisha miundo mbinu hasa katika maeneo ya Ng'ambo iliyopendekezwa na Zanzibar Sustainable Programm (ZSP) mwaka 1998.

Kwa nyakati tofauti maendeleo ya ujenzi na udhibiti wake yalikuwa yakisimamiwa na Joint Building Authority (JBA)ambayo ilianzishwa chini ya sheria ya Town and Country Planning Decree (cap 85) ya mwaka 1955, ikiwa na wajumbe watatu toka ambao ni Mkuu wa Afya, Mkuu wa Wilaya na Building Inspector. Kazi zao kubwa ilikuwa ni kutoa vibali vya ujenzi wa aina zote ndani ya mji wa Zanzibar na kudhiti ujenzi ndani ya mji huo kwa mujibu wa sheria ya mji. "Town Decree Cap 79 Subsidiary"

Mwaka 1969 SMZ ilizivunja Halmshauri za Miji na hivyo ukawa mwisho wa awamu ya kwanza ya JBA. Awamu ya pili ya JBA ilianza tena mwaka 1986 baada ya kurejeshwa kwa serikali za mitaa katika ikiwa na wajumbe wengi zaidi huku mkuu wa mkoa akiwa ndie mwenyekiti wake. Wajumbe wengi walitoka baraza la Manispaa, wakifuatiwa na wajumbe toka idara ya Ardhi, idara ya Upimaji na Mhandisi wa ujenzi. Kazi za JBA ziliendelea kufanyika chini ya sheria na taratibu za ujenzi kama zinavyooneshwa katika Cap 79 Subsidiary. Kati ya Mwaka 1969 na 1986 shughuli za ujenzi zilikuwa zikisimamiwa na serikali za majimbo, pasipo kufuata sheria yoyote za ujenzi zaidi ya uzoefu uliopatikana katika Cap 79 ya Town Decree.

Mwaka 1994 Sheria ya uendelezaji na uhifadhi wa Mji Mkongwe ilianza kufanya kazi, hivyo kuitoa JBA kama mdhibiti wa ujenzi katika eneo la Mji Mkongwe. JBA iliendelea kufanya kazi kufuata mipaka ya Master plan ya mwaka 1982 nje ya Mji mkongwe hadi mwaka 1995 ambapo kulitokea tena mgongano wa sheria. Mwaka 1995 ilianzishwa sheria mpya ya halmashauri za Miji Zanzibar, ikichukua sehemu kubwa za sheria za Town decree na kupunguza ukubwa wa Manispaa ya Zanzibar hali kadhalika kuibana zaidi JBA katika utendaji wake.

Kufikia hapa kazi za JBA ziliendelea kufanyika ila ni kwa ubabe tu, kwani chini ya sheria ya mwaka 1995 ya Manispaa ilionekana wazi kuwa JBA haikuwa na nafasi ya utendaji katika manispaa yenyewe na wilaya ya Magharibi. Ikiwa chini ya Mkuu wa Mkoa kama mwenyekiti na Baraza la Manispaa kama katibu, JBA iliendelea kufanya kazi huku ikijua inafanya hivyo kinyume na sheria na taratibu. Udhaifu wa Halmashauri ya wilaya ya Magharibi, nguvu ya kisheria ya Idara ya Ardhi na Idara ya Upimaji iliipa uhai kidogo JBA kutokana na kuwa na wajumbe toka katika Idara hizo.

Mwaka 2000 JBA ilivunjwa rasmi na moja ya sababu kubwa ya uvunjwaji wake ilikuwa ni zoezi la uvunjaji wa nyumba katika mitaa kadhaa ya Mkoa wa Mjini Magharibi iliyofanyika katika mwaka 1996, katika vyanzo vya maji, karibu na njia ya grid ya umeme wa Kidatu na maeneo mengine yaliyovamiwa, ambapo ilionekana zoezi zima limefanyika kisiasa zaidi kuliko kufuata taratibu. Manispaa kwa upande mwingine chini ya sheria ya mwaka 1995 waliona kuwa JBA ni mzigo kwao na walitaka ichukuliwe na asasi nyingine yoyote ya serikali. Kuvunjwa kwa JBA kulitoa nafasi ya kuanzishwa kwa UDCA (Urban Development Control Authority)ambayo ilianzishwa chini ya sheria ya 1955 ya Town and Country Planning decree ambayo ipo chini ya Wizara ya Ardhi na Upimaji. Safari hii Mwenyekiti wake akiwa ni Mkurugenzi wa Manispaa na katibu akiwa ni Town Planner wa Manispaa na wajumbe wengine 10 toka katika asasi zingine zinazohusika na ujenzi. Kwa ufupi UDCA ipo lakini haina nguvu kisheria kutokana na kuwepo kwa sheria ya Halmashauri ya Manispaa ya Mwaka 1995. Aidha sheria iliyotumika na Waziri huyo haina nafasi katika Halmashauri ya Manispaa, kwani Mkurugenzi wa Halmshauri anawajibika kwa Waziri wa Tawala za Mikoa na si venginevyo. UDCA inaendelea kufanya kazi kutokana na mazoea ya kuwepo na kitengo kama hicho katika miaka iliyopita.

Tukio lililotokea hivi karibuni la uvunjaji wa nyumba na misingi ya nyumba katika shehia ya Tomondo lililo fanyika chini ya amri ya Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Mhe. Abdallah Mwinyi, licha ya kuwa ni la kinyama halikufuata utaratibu wowote wa kisheria, zaidi limenikumbusha mojawapo ya sababu ya kumwondoa Mkuu wa Mkoa katika kudhibiti ujenzi visiwani humo. Aidha limenikumbusha kuwa Zanzibar Mjini hakuna sheria ya Ujenzi na kuna asasi nne zote hizo zikidai kuhusika na maendeleo ya ardhi katika mji huo na kufanya kuwepo na vurugu tupu katika kusimamia masuala ya ujenzi katika Mkoa huo wa Mjini Magharibi.

Aidha kuna umuhimu mkubwa kuona kuwa migongano ndani ya Mipaka ya Master plan ya mwaka 1982 inakwisha na kuna umuhimu mkubwa kuona kuwa Idara ya Upimaji, Idara ya Ardhi, Mamlaka ya Hifadhi na Uendelezaji Mji Mkongwe, Halmshauri ya Manispaa ya Zanzibar, Halmashauri ya Magharibi, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya magharibi pamoja na ofisi ya Mwanasheria mkuu wa serikali wanakaa pamoja na kuamua ni sheria gani ya ujenzi itumike katika eneo la master plan ya mwaka 1982. Kwani kwa sasa hakuna sheria inayotumika zaidi ya wizi mtupu. Yaani inatia aibu kwa wizi huu wa mchana kweupe, huku wanaoumia ni wananchi wasio jua wafuate sheria gani kupata kibali halali cha ujenzi wa nyumba zao.

Wednesday 18 February 2009

E-governance for African Municipalities...Ni Wizi Mtupu....!


Zenj mara nyingi imekuwa ikiingia kwenye rekodi mbalimbali barani Afrika na Duniani kutokana na matukio ya maisha maendeleo na teknologia. Rekodi kadhaa zimeandikwa ndani ya visiwa hivyo, hivyo kuongeza umaarufu wake na wakati huo huo kuboresha huduma mbalimbali kwa wananchi wake.

Zanzibar inaendelea kujivunia rekodi zake mbalimbali hadi wakati huu ingawa zingine zilishindwa kuendelezwa na hivyo kubakia kwenye kumbukumbu tu na kuwa hadithi kwa vijana kutambiana na hasa wanapokuwa katika ubishi na wenzao wa bara. Mapema mwaka huu Zenj iliibuka tena na kujiwekea rekodi nyingine mpya katika Afrika ya Mashariki, na iwapo rekodi hii itakuwa na mafanikio hapana shaka itaanza kusambaa taratibu kwa nchi zote za jirani. Safari hii rekodi hiyo haikupokelewa vizuri na nchi jirani, hata hivyo nina hakika baada ya muda wataifuata tu. Hii ni rekodi ya kuwa nchi ya kwanza katika Afrika ya Mashariki kutoa leseni ya udereva yenye kumbukumbu zote muhimu za mwenye leseni pamoja na namba yake ya ulipaji kodi. Hii ni hatua nzuri na kubwa kwa nchi zenye matatizo ya ukusanyaji wa kodi.

Mafanikio haya yote siku zote yanakuwa na lengo moja kubwa la urahisishaji wa utendaji na uongezaji wa ufanisi katika utoajo wa huduma, ambapo ni hatua muhimu ya kuondokana na ukiritimba ambao umekuwa ukichangia kwa asilimia kubwa kuwepo na rushwa na hatimae ufisadi.

Hata hivyo sio mambo yote ambayo yamekusudiwa kufanikisha na kurahisisha utoaji huduma katika Zanzibar yamefanikiwa. Ni watu wachache ambao watakumbuka kuwepo na mradi wa E-governance for African Municipalities kwa Manispaa tano tu barani Afrika ikiwemo Zanzibar, Manispaa zingine zilikuwa ni Bamako (Mali), Maputo (Mozambique), Niamey (Niger) na Lusaka (Zambia). Lengo la mradi huu ambao ulianza mwaka 2001 ilikuwa ni kuziunganisha Manispaa hizo tano katika mtandao mmoja aidha kuwezesha Manispaa hizo kuwa karibu na wananchi wake kwa utoaji wa huduma ya habari kwa njia ya mtandao. Kwa Manispaa ya Zanzibar kupitia mtandao uliofungwa katika Idara zake zote ilikusudiwa kurahisisha ubadirishanaji wa habari za kiutendaji katika idara hizo kwa njia ya umeme(electronically). Zaidi ilikusudiwa kutoa habari juu upatakanaji wa leseni mbalimbali kwa wananchi wake kupitia kwenye tovuti yake, pamoja na wananchi hao kupata nafasi ya kutumia mtandao huo bure katika sehemu maalumu kwa ajili ya kupata habari juu ya sheria ndogo ndogo mpya, muhtasari wa vikao vya kamati za Manispaa na Baraza Kuu, ukusanyaji wa mapato na matumizi yake na kuweza kujionea bajeti ya Manispaa hiyo ndani ya mtandao.

Mradi huu ambao ulikuwa unadhaminiwa na DANIDA/UNESCO, ulikamilika mwaka 2003, ambapo pamoja na Manispaa kupatiwa vitendea kazi vyote na taaluma kwa watendaji wake, wadhamini hao waligharamia na uanzishaji wa tovuti ya manispaa hiyo, ambayo tokea mwaka 2003 hadi leo hii imedumaa. Huu ni wizi mtupu.

Mradi huu ulikuwa wa thamani ya dola za kimarekani elfu arobaini haukuweza kuendelea kama ilivyokusudiwa kwa sababu zisizo na msingi zaidi ya kuendeleza tabia za ukiritimba ndani ya vyombo vya utoaji wa huduma ambapo ni wizi mtupu.

Madiwani ambao kwa namna moja ama nyingine ndio wanao wawakilisha wananchi wao katika Manispaa, ilitegemewa wawe mstali wa mbele kuona huduma hii muhimu iliyokuwa inaweza kuwapunguzia bughuza za waombaji wa fomu kugonga milango ya nyumba zao alfajili, kuwabana wahusika kuikamilisha tovuti hiyo ili kuwezesha wananchi kujaza fomu online walikaa kimya na kufumbia macho kudumaa kwa mradi huu ili waweze kuendelea kuwazungusha wananchi wao juu ya upatikanaji wa fomu mablimbali... Huu ni wizi mtupu!

Mkurugenzi wa Manispaa ama kwa kutojua ama kushindwa kwenda na mabadiliko katika utoaji wa huduma nae alishindwa kuendeleza mradi huu. Kwa nafasi yake angeweza kuhakikisha kuwa kila Idara inapeleka taarifa zake za mapato katika tovuti hiyo na kila idara inaweka fomu za maombi katika tovuti hiyo na hivyo kupunguza ama kuondoa foleni zisizo na ulazima wowote katika Ofisi ya manipaa hiyo. Hata hivyo kwa miaka saba sasa amekaa kimya tokea alipoweka ada za kupaki magari mwaka 2003... Wizi mtupu!

Mstaki Meya ambae huwa anaalikwa kwenye matukio muhimu yote yanayofanyika katika Manispaa yake nae ameshindwa kumbana afisa uhusiano kuona kuwa Matukio muhimu yote yanawekwa katika tovuti hiyo, hii ingekuwa ni njia mojawapo ya kuelekea kuweka hata matangazo ya matukio kwa njia ya kulipia hivyo kuifanya tovuti hiyo kuingiza mapato. Nae kama wengine ameamua kukaa kimya... Ni wizi mtupu!

Tovuti ya Baraza la Manispaa ilifanyiwa marekebisho kwa mara ya mwisho mwaka 2003, na hata yale ambayo yamo katika tovuti hiyo yanatia kichefuchefu. Yaliyoandikwa humo yana uhusiano mdogo kabisa na shughuli za Manispaa hiyo huu ni wizi mtupu. Hata design na layout ya tovuti hiyo ni vichekesho vitupu... Yaaaani ni Wizi mtupu!

Thursday 12 February 2009

Ni wiki ya Sauti za Busara (Sounds of Wisdom) huko Zanzibar



Tamasha la sita la Sauti za Busara limeshaanza rasmi siku ya Jana kwa maanandamo ya ufunguzi wa tamasha hilo ambalo sasa ni mojawapo ya tamasha kubwa kabisa barani Afrika. Tamasha hili litadumu kwa muda wa siku sita(12-18/02/2009)na tokea kuanza kwake limekuwa likifanyika katika wiki ya pili ya mwezi wa pili.

Tamasha la mwaka huu litatumbuizwa na wasanii maarufu toka karibu pande zote nne za Afrika, kwa mjibu wa tovuti ya sauti za busara wasanii ambao wana washabiki wengi kwa mwaka huu ni Bi Kidude, Culture Musical Club, DJ Yusuf, Samba Mapangala & Orchestre Virunga, Jagwa Music, Best of WaPi, Iddi Achien'g, Natacha Atlas, Segere Original na Joh Makini

Kwa habari zaidi tembelea hapa chini

Tuesday 10 February 2009

Kichekesho kingine toka kwa Shamsi Vuai Nahodha



Mwishoni mwa mwezi Januari mwaka huu, Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi alinifanya nicheke kwa kauli yake ya kuamua kushika fagio na kuanza kufagia barabara za Zenj kutokana na barabara hizo kujaa michanga na vumbi kiasi cha kutojulikana kama ni za kiwango cha lami au la. Hii si mara ya kwanza kwa Mh. Nahodha kujitolea kusafisha Halmashauri ya Manispaa ya Zanzibar. Hata hivyo pamoja na juhudi zake hizo kwa Halmashauri hiyo ambayo kipindi fulani kupitia kwa Mkurugenzi wake Mr Mabrouk Makame Jabu ilikuwa ikidai kupewa hadhi ya Jiji(Sina hakika kama tayali ombi hili limeshakubaliwa)bado mji huo umeendelea kuwa mchafu.

Juhudi zote za Waziri Kiongozi zimekuwa na mafanikio ya muda mfupi, kwani huwa zinafanyika katika mtindo wa Operation ambao siku zote huwa hauna uendelevu wa aina yoyote, kwani operation inapokwisha shughuli nzima uwekwa kando na watu wakaendelea na shughuli zao zingine, huku wakisubiri kutokea kwa operation mpya. Watendaji wengi na hasa wa kimacha chini upenda aina hii ya utendaji kwani ndio wakati wao wa kuwa na kipato zaidi kutokana na overtime. Kwa Waziri Kiongozi ambae mara kwa mara amekuwa akisisitiza kuwepo na utendaji wa uendelevu katika shughuli za serikali, kilimo na biashara huku akiongoza kufanya operation za usafi ni kichekesho kitupu. Inakuaje unahutubia kila siku mambo ya uendelevu huku kazi unafanya za kizima moto kama sio vituko vitupu!

Moja ya barabara ambao siku zote huwa inajaa michanga na kusababisha vumbi la kuweza kusababisha chafya kila baada ya sekunde kadhaa, na hatari ya kupata kikohozi kikali ni barabara ya Benjamin Mkapa(zamani creek road). Barabara hii ndio inatenganisha Mji Mkongwe na Ng'ambo, ni moja ya barabara yenye pilika kubwa kabisa katika Zenj ikipitiwa na magari mengi zaidi, itumiwayo na wapanda baiskeli wengi zaidi na wapanda vespa,huku wakipigana vikumbo na mamia ya watembeao kwa miguu. Ndio barabara pekee visiwani humo yenye taa za kuongozea magari, kwa ufupi ndio barabara maarufu kabisa visiwani humo.

Kwa miaka nenda rudi barabara hiyo imekuwa ikifagiliwa pasipo kutakata na sasa naona imeshakuwa sugu, na kama hakuna mipango ya kuweza kujua ni kwa nini barabara hiyo haikosi vumbi licha ya kuwa ndio picha ya mji wa Zenj, kamwe haitokuja kuwa safi na ni wazi kuwa vumbi litaendelea kuwepo tu, licha ya ombi la watendaji wa Halmshauri hiyo kununuliwa gari la kufagia barabara hivi karibuni.


Barabara hiyo pamoja na kupita katika bustani za Mnazi Mmoja, Jamhuri, Donge na viwanja vya Malindi, haikupaswa kabisa kuwa na vumbi. Lakini kutokana na sababu za kutokuwa na mipangilio mizuri vumbi limeendelea kuwepo licha ya ufagiaji wa kila siku. Kitu cha kwanza ambacho kina kasoro kubwa katika barabara hiyo ni kukosekana kwa njia ya watembeao kwa miguu. Kama kungekuwa na njia hiyo ingetumika vile vile kama buffer ya kutenganisha barabara na sehemu zinazoingiza michanga barabarani na kusababisha vumbi. Aidha aina za kuegesha magari na hasa teski katika barabara hiyo unachangia kuingia kwa michanga barabarani, kuna maegesho ya magari ya mizigo na haya uegeshwa karibu kabisa na barabara hiyo, hivyo uchangia kuingia kwa michanga barabarani.Kwa upande mwingine Feeder road zinazo ingia katika barabara hiyo vile vile uchangia kuingiza michanga.

Ili kumfanya Waziri Kiongozi aendelee kufanya kazi zake za kawaida, badala ya kutafuta fagio, upo umuhimu wa lazima kuona kuwa barabara ya Benjamin Mkapa inafanyiwa mabadiliko makubwa ili kukidhi mahitaji ya watumiao barabara hiyo ambao ni maelfu. Kuna umuhimu wa kuweka njia kwa watembeao kwa miguu ambayo iwe inafanya kazi ya kuzuia kuingia kwa michanga katika barabara hiyo. Kuboresha maegesho ya teski na magari ya mizigo kama kituo cha daladala kilivyoboreshwa, kufanyia matengenezo feeder roads ambazo huingiza michanga kwa wingi na hasa wakati wa masika. Kuangalia tena eneo la Darajani kwani nalo linachangia sana katika uchafuzi wa barabara hiyo. Maeneo mengine kama Mkunazi,Donge, Ben Bella na Ofisi za Zec zinatakiwa kuangaliwa kwa vizuri zaidi.

Kwa utengenezaji wa njia ya wapita kwa miguu, Halmashauri ya Manispaa ya Zenj, inaweza kufanya kazi hiyo kwa kutumia mitambo yake mikubwa ya kutengeneza vigae, kwa kuweka vigae pembeni ya barabara hiyo. Hizo milioni 135,000,000 ambazo Manispaa wanahitaji kwa ununuzi wa mashine ya kusafisha barabara mnaweza kuwapa japo nusu yake ili waweze kutumia kwa utengenezaji wa vigae.

Friday 6 February 2009

Athari za Utalii kwa Mazingira ya Zanzibar




Moja ya masharti wanayopewa watalii mara waingiapo Zenj, ni juu ya uvaaji wa nguo ambazo hazistiri mwili mzima, yaani uvaaji wa suruali kipande, vichupi, ama kutembea vifua wazi ni sawa na kwenda uchi ndani ya Zenj. Hivyo watalii uambiwa wavae nguo zinazofunika mwili wote wakati wao wote watakapo kuwepo visiwani humo. Kwa watalii sharti hili ulipokea kwa shingo upande kwani wanapotoka ni sehemu za baridi na kwa muda mrefu wanakuwa wakivaa nuo nyingi kujikinga na baridi, na hivyo wanapotalii katika nchi za joto hupenda kuipa nafasi miili yao kufaidi joto hilo ambalo kwao ni adimu.

Hata hivyo linapokuja suala la ujenzi wa hoteli za kitalii Masharti na Taratibu zake hazijulikana kabisa, kwani vyombo vinavyosimamia ujenzi huo havina ushirikiano wa moja kwa moja na Idara ya Mazingira ambayo ipo kisheria kusimamia mazingira ya Visiwa hivyo chini ya sheria ya mwaka 1996.

Utalii katika visiwa vya Zanzibar sasa umeshapanuka sana na visiwa hivyo vimeshashuhudia mambo mengi yaliyokuja na utalii, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa hoteli nyingi za kitalii karibu kwa fukwe zote visiwani humo pamoja na visiwa vidogo dogo, ongezeko la wageni wahamiaji kwa ajili ya kazi za kitalii, ongezeko la uvuvi kwa ajili ya vyakula vya watalii, ongezeko la safari za anga na ardhini, ongezeko la maduka rasmi kwa ajili ya watalii na mambo mengine mengi yanayoendana na utalii kwa ujumla.

Mengi katika haya yalikuja pasipo kwa wenyeji wengi kujiandaa na sasa inakaribia miaka ishirini tokea mfumuko wa utalii visiwani kuanza, na kumekuwepo na malalamiko mengi toka ndani ya visiwa hivyo na nje ya visiwa hivyo kwa jinsi suala zima la utalii lilivyobadili mambo mengi visiwani humo. Wenyeji wengi wanalalamikia sehemu kubwa ya ajila kushikwa na wageni, ongezeko la bei kwa vyakula vya baharini, kupigwa marufuku kutembea ama kuvua katika baadhi ya hoteli hizo. Huku asasi za kimataifa zikipigia kelele uharibifu wa mazingira kutokana na aina za ujenzi wa baadhi za hoteli visiwani humo, uharibifu wa coral reef kutokana na uvuvi uliokithiri, kutokuwepo na miundo mbinu ya kutosha kwa ajili ya kuhifadhi maji taka na utupaji holela wa taka toka mahotelini humo.

Hadi kufikia mwaka 2003 takwimu za ZIPA zinaonyesha kuwa, jumla ya miradi 242 ilidhinishwa yenye thamani ya jumla ya dola za kimarekani milioni 403. Mwaka 2001 Zanzibar iliingiza dola za kimarekani milioni 46 kutokana na utalii pekee ikiwa ni asilimia 15 ya GDP. Makisio yanaonyesha kuwa kutakuwa na ongezeko la asilimia 21 la GDP kufikia mwaka 2012 na kufanya mgawanyo wa mapato kufikia million 116(makadirio haya yalifanyika kabla ya Global recessionya mwaka huu).

Ripoti ya maendeleo ya utalii ya Zanzibar iliyoandaliwa na na UNDP inaonyesha kuwa katika mwaka 1983 kulikuwa na sehemu kumi tu za malazi visiwani humo zenye vyumba 215 na jumla ya vitanda 467 ambazo hazikuwa kwenye daraja la aina yoyote(utalii au malazi ya wageni wa kawaida). Leo hii sekta ya utalii visiwani humo ina sehemu zaidi ya 180 za malazi, zenye zaidi ya vyumba 3160 na zaidi ya vitanda 6490.

Kufikia mwishoni mwa mwaka 2006, ripoti ya Umoja wa Mataifa(UN) ilionya kuwa Zanzibar imekuwa mojawapo ya nchi duniani inayoongoza kwa uchafuzi wa mazingira ya baharini kutokana na umwagaji wa maji taka katika bahari ya Hindi pamoja na uharibifu wa vyanzo vya maji. Mtafiti Stefan Gossling toka Sweden, yeye alionya kuwepo na uharibifu mkubwa wa coral reef kwa lengo la uuzaji wa viumbe vyake kwa watalii. Maeneo yenye uharibifu mkubwa wa mazingira kutokana na utalii visiwani humo ni ya Kaskazini na yale ya Mashariki.

Ukuaji wa utalii, licha ya kuendelea kuharibu mazingira umesababisha kuwepo na ushirikiano mdogo kati ya serikali na wananchi wake. Kwa upande wa mazingira wananchi wengi wanalalamikia hatua kadhaa za wenye hotel kuwanyima sehemu zao za uvuvi, ulimaji(seaweeds), minazi na hata kutembea karibu na hotel hizo. Mwaka 2002 wananchi wenye hasira katika kijiji cha Kendwa walichoma moto hoteli ya kitalii kwa madai ya hoteli hiyo kuharibu coral reef, tabia hii ilisambaa kwa baaadhi ya vijiji vya Nungwi.

Baadhi ya hotel( Fundu lagoon, Matemwe Bungalow, Blue Bay, Mnemba Island na Chumbe) zimeonyesha kujali athari ambazo zinatokana na ujenzi wa hoteli zao kwa mazingira. Wamejitahidi kufuata aina za ujenzi usio tumia resources kwa wingi, aidha wamejitahidi kufuata aina ya ujenzi wa nyumba za vijiji zinavyowazunguka. Hivyo kupunguza uharibifu wa maji safi na bahari.

Serikali kwa upande wake imeendelea kutoa vibali vya ujenzi pasi kuzingatia uharibifu wa mazingira au namna ya kujenga pasipo kuwepo na uharibifu wa mazingira. Hoteli zinaendelea kujengwa pasipo kuwepo na mfumo unaotambulika wa ukusanyaji na usafishaji wa maji taka, ukusanyaji na utupaji wa taka ngumu na utunzaji wa vyanzo vya maji. Aidha hakuna taratibu zozote ambazo zinatolewa kwa kutumia materials ambazo zinaendana na mazingira ya fukwe zinazojengwa.

Na kama kawaida yao, mambo yanapokwenda kombo, viongozi huja na amri kede kede. Nakumbuka miaka miwili iliyopita Mh. Mansour Yussuf Himid alinukuliwa akisema;
“Serikali imegundua ukiukwaji wa taratibu za utunzaji wa mazingira katika ukanda wa fukwe”
Aidha alikubali kuwa sekta ya utalii ndio inaongoza katika uchafuzi wa mazingira visiwani humo na kuzitaka Idara zinazohusika kujipanga kukabiliana na tatizo hilo hilo, huku Ofisi ya Mwanasheria Mkuu ikisema kuwa yeyote ambae atakiuka taratibu za Mazingira ataburuzwa mahakamani na kupigwa faini ya Sh million 2 ama kwenda Chuo cha Mafunzo kwa kipindi cha miezi sita.

Wednesday 4 February 2009

Child Custody after Divorce



In Tanzania, custody is governed by civil law, regardless of the type of marriage. The 1963 Law of Persons Act declared that children born inside marriage belonged to the father. However, the 1971 Marriage Act requires custody to be decided in the best interest of the child, but routinely defers to custom in individual cases. Prior to 1971, custody of Muslim children was administered under Islamic Law; however, the uniform codification of the Marriage Act included child custody regulations. Practically, if a woman files for custody, the father will not contest the motions. Here means that when woman open a case for custody father will not be able block the case. However, in absence of contestation, the father generally gets custody. Further, the Marriage Act provides that a father is responsible for maintenance of children until 18 years of age, regardless of custody
Custody patterns also vary depending on local lineage patterns. Among the matrilineal Muslims, the child belongs to his or her mother and her lineage, and remains with the mother in case of divorce, until age of 7; courts also directed to consider: customs of community to which parents belong; economic circumstances of both parents; housing that both parents can provide; and behaviour of mother and whether she contributed to marital breakdown If the mother dies, the child still remains with the members of the matriline and is usually maintained by a maternal uncle.

Looking to law governing marriage and divorce in Tanzania Act of 1971 (LMA) Section 125 of LMA provide for custody of children after divorce that may be granted either to the father or mother or any third party who is in position to provide for welfare of the children.
Section 126 provides for condition to custody order and section 127 provides for principle of welfare of child and in determining custody of children the welfare of the child is paramount and the court will grant custody to the one who is in better position to grant custody, however court always prefer before deciding on granting custody divorce parties to agree themselves to whom the child will leave with.

Welfare of the child including food, clothes, shelter, education, culture as well as good moral or attitude of the parent. So this is not only a matter of financial position of the parent.
Looking to the cases concerned the child custody after divorce in Tanzania based on the group focus, “why always mother have more right to be granted custody of child”. Here are examples which shows that even father can be granted custody of child

In case of Vestina Kibutu vs. Mbaya (1985) Tanzania Law Report (TLR) 42 custody was granted to the father because he was in the position to provide education and psychological development.
Another case of Re Steven Christopher Newborn (1975) TLR 24, courts in discussing welfare of the child takes into consideration social aspect and culture of divorcee. In this case spouses were English and divorced in Mwanza Tanzania. Mother decided to stay in Tanzania with her son Steven, Husband wanted to go England with his son. Court in its decision said it is better for father to go with his son England to be raised with English culture.

Monday 2 February 2009

Mapenzi ya Tanzania Bara na Zanzibar mashakani...


Wengi wetu siku hizi tunapenda kufananisha muungano wa Tanganyika na Zanzibar na ndoa ya watu wawili wapendano. Ndoa huja baada ya wawili walioshibana kuamua kuishi pamoja kwa muda wote wa maisha yao. Zipo aina kadha wa kadha za ndoa zote hizo huwa na lengo moja la kuunganisha wale wapendanao.

Mapenzi siku zote uzaliwa na kukua na hatimae kupevuka, siku zote mapenzi hukuzwa na wapendanao kwa kujaribu kuheshimu yale apendayo mwenza wake. Hii ni kwa kila upande na sio jukumu la mmoja tu ndani ya hayo mapenzi. Yapo mambo mengi ambayo ufanyika kwa lengo la kudumisha na kuendeleza mapenzi. Na haya yote hufanyika kwa moyo wa dhati ili mradi tu kuona penzi linakuwa kila siku.

Tofauti ndogo ndogo siku zote uwepo katika mapenzi, na wale ambao hupenda kuona mafanikio na kudumisha mapenzi yao hupenda kuzijadili tofauti hizo kungali mapema ili kuzuia tofauti hizo kuwa tatizo baina yao. Hii ni mojawapo ya vitu vya msingi sana katika ndoa zinazojali mapenzi.

Ndoa ya Tanzania Bara na Zanzibar sasa ipo kwa muda mrefu kiasi cha kusema kuwa imekomaa ila mapenzi katika ndoa hii muhimu yamekuwa yakipungua kila siku na katika spidi kubwa kiasi cha kuhatarisha ndoa yenyewe.Vitu vyote muhimu katika kukuza penzi zimewekwa kando badala yake chuki na kusingamana vimechukua nafasi.

Katika nyakati tofauti tumeshuhudia mambo kadha wa kadha yakifanyiwa marekebisho ili mradi kulienzi penzi na kudumisha ndoa, tokea wakati ule wa kusafiri kwa passport hadi kuongezwa kwa mambo kadhaa ndani ya ndoa hiyo. Hata hivyo kwa upande mmoja wa wanandoa hawa amekuwa akiburuzwa mno, mambo mengi amekuwa akinyang'anya tokea kuwa na sauti ya pili kwa ukuu ndani ya ndoa hiyo hadi sasa ambapo hana sauti yoyote, hata uhalali wake umeanza kuhojiwa, mbaya zaidi pamoja na kukubali kufutwa kwa kutumia karatasi baina ya nchi mbili hizi, inashangaza sana kuona kuwa makaratasi yameondolewa kwa binadamu tu.Iwapo una gari ukitokea upande wa Visiwani, gari hilo linabidi kuwa na karatasi ili liweze kutembea upande wa pili wa ndoa.

Kuna kero zingine zinachosha sana, na wala hazisaidii kurutubisha ndoa zaidi ya kuitia ubovu ambao mwisho wake ni kuvunjika tu.