Wednesday 18 March 2009

Amin Salmin Amour, aonja tamu ya siasa

Ni baada ya kushindwa kutamba kwenye kura za awali za kumtafuta mgombea kwa tiketi ya CCM katika jimbo la Magogoni huko Zenj. Amin ambaye ni mtoto wa rais mstaafu wa Zenj Salmin Amour maarufu kama Komandoo, alikuwa ni miongoni wa wagombea 10 wa CCM waliojitokeza kuwania nafasi hiyo.

Umaarufu wa Amin unakwenda nyuma zaidi kipindi cha kwanza cha Komandoo Salmin alipokuwa madarakani,umaarufu wake ulijengeka kwa kuwa mjasirimali zaidi ya siasa na kwa kujaribu kila aina ya biashara za muda mfupi! Hatua yake ya kuingia kwenye siasa kwa wengi ilikuwa ni karata yake muhimu ya kujinyanyua tena baada ya kushindwa kudumu katika sekta ya biashara.

Kwa habari zaidi tembelea hapa

No comments: