Saturday 30 May 2009

Ajali ya Mv Fatih



Tunasikitika kuwatangazia ajali mbaya ya meli ya mizigo (Mv. Fathi ya kampuni ya Seagul mali ya Bwana Said Mbuzi) ambayo ilikuwa ikitokea Zanzibar kuja Dar. Inasemekana kuna idadi kubwa ya watu waliopoteza maisha

Source: Jamii Forums



All pictures by Kibunango

Tuesday 26 May 2009

Bia, Konyagi na Sigara


Zenj unaweza kwenda baa na Konyagi yako ulionunua katika duka la ulevi na kuinywa hapo baa pasipo kupata usumbufu toka kwa mwenye baa. Unachotakiwa kufanya ni kuagiza maji au bia na glasi tu!

Friday 22 May 2009

Maili Nne- Zenj


Maili Nne ni kitongoji ambacho kimejengwa bila ya viwanja vyake kupimwa na Idara ya Upimaji. Ni kitongoji ambacho ni mfano katika kupanga nyumba pasipo kuwashirikisha wataalumu ambao wamekuwa na visingizio chungu nzima katika suala la kupima ardhi.

Monday 4 May 2009

Avumae Baharini ni Papa.....


Kwa mara ya kwanza vidagaa baharini vimeanza kujiuliza ni nani mkubwa kati ya Papa na Nyangumi, huku wakiwa wamesahau kuwa avumae bahari ni Papa lakini kubwa lao ni Nyangumi..!

Papa ndie anaye aminika kutamba baharini, kwa mwendo wake wa kasi na mashambulizi ya ghafla tena ya kutisha, kiasi ya kumfanya awe ni maarufu sana baharini.

Hivi karibuni katika vita vya mafahali wawili wa baharini, imeonekana kuwa pamoja na ukubwa wa Nyangumi, Papa bado ni maarufu sana kwa ukubwa katika bahari ya maharamia wa meli hadi kule kwa prez asie tumia ndomu. Hata hivyo wataalumu wa mambo wanasema ni nadra sana kwa vidagaa, vibua, ngisi, pweza, changu,tasi na aina nyingine ya visamaki katika eneo hilo kumwona Nyangumi, hivyo kwao Papa bado ndio samaki/mnyama mkubwa kabisa licha ya kuwepo kwa Nyangumi.

Kama vile haitoshi vidagaa hivyo, ambavyo mara nyingi hukaa mbali na Papa, wameendelea kuhoji ni kwa nini Papa ametumia televisheni ya taifa la wanyama wa baharini,kujinadi kama yeye sio mkubwa kama Nyangumi, wakisahau kuwa Papa hana ubavu kama wa Nyangumi ambae ametumia televisheni yake yenye uwezo wa kuonekana live katika eneo lote avumalo Papa!

Kuna taarifa ambazo sio rasmi kuwa Nyangumi atajaa tena kwenye televisheni yake akipinga madai kuwa yenye ndie mtafunaji wa kwanza wa vidagaa na aina nyingine ya visamaki katika eneo hilo la bahari, huku vidagaa vingine vikifanya mpango wa kwenda kwenye maeneo ambayo Nyangumi amekuwa akivuliwa kwa wingi ili kuweza kujionea samaki hilo lipo la aina gani, na kama inawezekana kuliondoa katika eneo lao la bahari, licha ya madai yake kuwa yupo katika kuwatetea vidagaa na umaarufu wa Papa.


__________________