Friday 31 July 2009

SMZ:- Serikali Iliyokosa Dira




Ilikuwa ni katika awamu ya mwisho ya Komandoo, ambapo wazenj wengi walipata fursa ya kudhaminiwa na serikali yao ili kuongeza elimu yao na taaluma zao. Lengo lilikuwa ni kusomesha wazenji wengi kadiri uwezo wa serikali ya SMZ inavyoruhusu. Na ni kipindi hikohiko ambapo kulikuwa na wimbi la wakimbizi wa Kizenj kukimbilia hifadhi huko Uingereza. Ni kipindi hikohiko ambapo Komandoo alionekana kuwa ni msaliti baada ya jitihada zake za kubadili katiba kugonga ukuta. Zaidi ni kipindi hicho hicho ambacho wazenj waliona ongezeko kubwa la mapato yao na mabadiliko mengi katika miji yao. Kwa ufupi ni kipindi ambacho wizara ya fedha ilikuwa ni maarufu zaidi katika historia ya SMZ, ikifanya kazi nje ya uwezo wake huku ikivamia kazi za wizara zingine.

Ilikuwa ni mwaka 1996 ambapo SMZ kupitia Wizara ya fedha ilioanza kupeleka wafanyakazi wake na wasio wafanyakazi kwenda kusoma kwa wingi, hata hivyo kozi nyingi zilikuwa zile ambazo zinaweza kufanyika Tanzania Bara. Zenj ilishuhudia masekretari wakipelekwa kusoma UK na Malaysia, wakati kuna chuo cha Uhazili hapo Tabora, kozi za zilikuwa za chini ya mwaka mmoja na wengi hawakurudi tena kupiga chapa na kupokea wageni na sasa wanakula benefit zao huko UK wakijiita Wasomali ama Warundi. Na ni baada ya kuona wakimbizi wa kizenj wakifaidi benefit za UK. Kumbuka kuwa licha ya tofauti za kisiasa zinazo onekana nje ya wazenj, wengi wao wapo pamoja kimashauri na kimaisha kwani kwa namna moja ama nyingine wamehusiana.

Mwaka mmoja baade bila kupima mafanikio ya wanafunzi waliotangulia, SMZ ilikusanya masekreatari na wafanyakazi wengine na wake wasio na kazi na kuwapeleka Malaysia ili kuongeza ujuzi wao. Kwa wale ambao walikuwa hawana ajila katika SMZ walihaidiwa kupewa ajila mara watakapo maliza masomo yao.

Mtiririko mzima wa kwenda huko ulisimamiwa na wizara ya fedha, wala hapakuwa na haja ya kwenda Idara ya Utumishi ili kuweza kupata nafasi ya kwenda huko. Ilikuwa ni kwenda moja kwa moja wizara ya fedha na kueleza adhma yako ya kusoma, wao walitoa mkataba wao na biashara kuishia hapo hapo.

Kama katika mwaka uliotangulia wengi walikuwa ni masektretari, wakifuatiwa kwa karibu na wanafunzi waliopenda kusoma Computer Science, huku wengine wakitaka kusoma Business Management na baadhi kutoka katika idara za uhandisi. Tatizo kubwa lilikuwa hapa kwenye Uhandisi, kwani chuo ambacho SMZ iliingia nao mkataba hawakuwa na fani nyingi za uhandisi zaidi ya umeme! Hivyo kupelekea wafanyakazi toka idara ya Maji, TVZ, Manispaa kulazimika kusomea umeme! Kulikuwa na kundi lingine ambalo lilipenda kusomea Uhasibu na kundi la Sheria, hata hivyo wengi wao walipenda kozi hizo kutokana na ndota zao na walipoanza masomo walijikuta wakishindwa vibaja. Mbaya zaidi Idara ya Utumishi ilikataa kabisa kuwatambua kwa wale wachache waliorudi tena Zenj...

Muda wa kozi unatofutiana, hivyo masekretari walikuwa ndio wa mwanzo kurudi Zenj, katika kipindi chote ambacho walikuwepo hapa Kuala Lumpar na Petaling Jaya, Wanafunzi walishuhudia ziara zisizo na kikomo za viongozi wa ngazi za juu, malipo ya posho zao kwa wakati na kadhalika. Maisha yalikuwa ni mazuri sana na yenye neema nyingi.

Baada ya masekretari kuondoka, ndipo picha halisi ya SMZ kwa wanafunzi wake ilipoonekana. Huduma nyingi muhimu zilipunguwa ama kusimamishwa kabisa. Hii ilijenga chuki na hasira kwa wanafunzi juu ya serikali yao. Mbaya zaidi ni kujua kuwa hata wale ambao wamerudi Zenj wameshindwa kutambuliwa na Idara ya Kazi, hivyo ni sawa kama hawakusoma chochote kile.

Wanafunzi wengi walianza kufikilia kama kuna umuhimu wowote wa kurudi tena Zenj, hawa na pamoja na wale ambao tayali walikuwa wameajiliwa na SMZ. Huku ukumbizi ukizidi kuvuma visiwani humo, wengi waliona ni heri kutorudi tena visiwani huko. Tatizo lilikuwa ni fedha, kwani katika siku za mwisho mwisho SMZ ilikata kutuma fedha, na kutoa ahadi kuwa malipo yatafanyika mara wanafunzi watakaporudi visiwani. Kwao hili halikuwa tatizo kubwa. Na mara baada ya kurudi na kulipwa wengi walikimbilia UK na USA ambapo wapo hadi sasa.

Wanafunzi waliobaki Malaysia waliona joto ya jiwe,kwani walifikia kushindwa hata kulipia pango la nyumba zao na kujikuta wakifukuzwa. Hata hivyo wengi katika waliobaki walikuwa bado na mapenzi makubwa na SMZ hivyo baada ya miaka yao kadhaa walirudi nyumbani na kukutana na kadhia dhidi ya Idara ya Utumishi ambayo ilitaa kuwatambua, mbaya zaidi Komandoo alikuwa atayali amemaliza muda wake. hiki kilikuwa ni kipindi cha Karume ambaye aliamua kwa makusudi kutowatambua wanafunzi hao.

Cha msingi ni kujiuliza ni kwa nini SMZ chini ya Karume ilishindwa kuwatambua wanafunzi ambao waliona bora kurudi nyumbani ili kuendeleza maendeleo ya visiwa hivyo. Ukiangalia kwa kina utaona ni mabo mengi ambayo yalianzishwa na Komandoo yalibezwa na Karume, huku idara ya Utumishi ikilipa kisasi kwa kunyang'anywa kazi yake ya kusomesha wanafunzi wafanyakazi na wizara ya fedha. Mambo mengi yaliamuriwa kutokana na utashishi binafsi pasipo kufuata taratibu za kisheria, kiasi cha kuona kuwa SMZ haina dira yotote katika kumwendeleza mwanachi wake.

Leo hii ukiangalia ni wangapi katika mamia wale ambao walisomeshwa na SMZ, ambao bado wapo hapo visiwani ni kichekesho. Mpaka leo hii SMZ inadaiwa na wanafunzi hao, na Karume ambae mwakani anamaliza muda wake katia pamba masikioni mwake! Hataki kusikia chochote kuhusu madai wa wanafunzi hao! Na sio kama haoni mafanikio ya wale wachache waliobaki ili kuendeleza nchi hiyo bali ni kwa kuwa SMZ yote kwa ujumla haijui inafanya nini.... ipo ipo tu!

Wednesday 29 July 2009

Kadhia hii kwisha yakianza kuchimbwa...?


Vespa inapokuwa inainamishwa upande mmoja ni dalili ya upungufu wa wese, hata hivyo kwa muda sasa kumekuwepo na malumbano marefu juu ya uchimbaji wa mafuta huko Zenj na umiliki wa mafuta hayo... Je iwapo mafuta hayo yatachimbwa chini ya umiliki wa Zenj, kadhia hii kwa maelfu wa wenye vyombo vya moto visiwani humo itakuwa imefikia kikomo?

Tuesday 14 July 2009

Ngoma Africa Band Kupeleka Moto Mwingine Tampere! Finland




The Ngoma Africa Band aka FFU! wanatarajiwa kutumbuiza katika onyesho la
FEST AFRIKA, mjini Tampere, huko Finland siku ya Jumamosi 18-07-2009.

Katika maonyesho hayo pia kutakuwapo na bendi nyingine za mziki na vikundi vingine vingi vya sanaa za maonyesho kikiwemo kikundi maarufu cha The Mpondas Group chenye maskani yake mjini Tampere.bendi ya The Ngoma Africa ilikuwapo Ufini mwanzoni mwa mwezi wa February mwaka 2009 katika misimu wa barafu huko ufini,na kufanikiwa kuwasha moto wake wa mziki.

Wadau wa Scandinavia bendi yenu inakuja kufanya kazi mliyowatuma kufanya nanyo ni mziki moto moto!.

The Ngoma Africa bendi inayotingisha majukwaa kila kukicha bado inaendelea na kufuka majukwaa kama vile moto wa nyikani.

Wasilikize hapa www.myspace.com/thengomaafrica ukiwataka ngoma4u@googlemail.com

Sunday 5 July 2009

Kujinafsi....