Thursday 6 August 2009

Pinda amefulia...


Kwa kauli yake juu ya Muungano Waziri Mkuu Mizengo Pinda amefulia na ameonyesha ufahamu mdogo juu ya Muungano huu. Kauli yake ya kuondoa kero za muungano ni kuifuta SMZ haiwezi ikaachwa hivi hivi. Kauli ambayo aliitoa huku akijua kuwa hakuna dalili zozote za sasa za SMT kujaribu kuondoa kero za Muungano achilia mbali jitihada za kuona kuwa Muungano unakwenda vizuri zaidi ya kuburaza upande mmoja wa Muungano. Kauli yake inaweza kuwa sahihi iwapo Muungano huu utakuwa hauna kero yoyote na nchi zote mbili kuridhia kuwa hakuna kero.

Zaidi Pinda anahitaji kupatiwa tuition ya haraka kuhusu Muungano na mambo yote ambayo yahusianayo na Muungano huo. Hii itamuwezesha kujua na kupata ufahamu mkubwa wa Muungano huu kabla ya kujikuta akishitumiwa na kuandamwa na Katiba na kukimbilia kulia.

2 comments:

saluya said...

kaka nime kusoma nitajilekebisha kwani huu ni mwanzo kaka

Kibunango said...

Bila shaka Saluya..! Karibu sana