Thursday 20 August 2009

Wapemba watangaza hujuma dhidi ya Masheha na Vingunge wengine...


Huko PBA mambo si shwari kabisa

Kuna madai ya kuibuka kikundi kinachoitwa Hujuma kwa Masheha, ambacho lengo lake ni kudhuru viongozi.

Kundi hilo linalofananishwa na Mungiki la Kenya, limeanza kutoa vitisho kwa kusambaza vipeperushi kwa baadhi ya masheha, kwamba wajiandae kupokea kipigo, huku sheha mwingine akionja adha ya kundi hilo kwa kupambana nalo.

Akizungumza jana, Ofisa Tawala wa Wilaya ya Wete, Khamis Juma Silima, alisema ofisi yake imepokea taarifa za kundi hilo, ambalo lina mrengo wa kisiasa kwa nia ya kuwadhuru masheha hao, kwa madai kuwa ndio kikwazo cha upatikanaji wa fomu za vitambulisho vya Mzanzibari Mkazi, ambazo ni kigezo cha kuandikishwa kwenye Daftari la Kusumu la Wapiga Kura.

Silima alisema masheha kadhaa wamepeleka malalamiko ofisini kwake katika siku za karibuni ya kupokea vipeperushi vya vitisho kuhusu utoaji fomu kwa wananchi wao.

Source: Habari Leo

2 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Kazi kwelikweli.

Kibunango said...

Nashindwa kuelewa tatizo lipo wapi huko kisiwa cha pili...!