Tuesday 12 January 2010

Rais Karume aupongeza Muafaka wake na Maalim Seif




Ni katika hotuba yake ya kuadhimisha miaka 46 ya Mapinduzi huko Pemba. Dondoo muhimu ya hotuba hiyo ni kama zifuatavyo:-

1. Amesema hatogombea tena kwa mujibu wa katiba.

2. Ameupongeza muafaka wake na Maalim Seif na kusifu matokea mema yake ya awali.

3. Ametumia lugha ya kistaaranu iliyojaa hekima na busara, huko nyuma zilikuwa ni mafumbo na vijembe.

4. Amezungumzia issue zote muhimu kwa mustakabali wa Zanzibar

5. Amezungumzia Muungano ni Dhima.

6. Ametoa hakikisho la Uchaguri huru na wa haki.

7. Wenye sifa wote, wataandikishwa. ZEK itapitisha tena uandikishaji upya.

8. Wote wenye sifa za kupata ZID, watapatiwa na wote wenye ZID walionywima kwenda kuzichukua, wakazichukue.

9. Kwa ujasiri mkubwa na lugha ya kistaarabu sana, ameyaomba gesi na mafuta yao, yawe yao, kama ilivyo bara na dhahabu yetu.

10. Amemsifu sana Rais Kikwete, na kumalizia kwa ile ile kauli Adhimu "Mapinduzi Daima".

Chanzo: Jamii Forums

No comments: