Friday 5 February 2010

Ofisi mpya ya Nahodha


Ofisi mpya ya Waziri kiongozi inayokamlishwa ujenzi wake huko Pemba. Kwa muda mrefu viongozi wengi wa SMZ wamekuwa hawapendi kwenda kufanya kazi zao katika kisiwa hiko. Kwa kukamilika kwa ujenzi huu kutatoa nafasi kubwa kwa Waziri Kiongozi kufanya kazi zake huko Pemba sawa na huko Unguja.

Aidha baada ya BLW kuridhia maridhiano ya Rais Amani na Maalim Seif, ni nafasi nzuri kwa Nahodha kuwepo muda mrefu kisiwani huko ili aweze kuzoeleka kwa wananchi wa huko, iwapo bado na ndoto za kuja kuwa Prez wa Zenj.

Awali Ofisi hiyo ambayo ilikuwa ikimfanya Nahodha kufikili mara mbili kabla ya kwenda huko ilikuwa kama inavyo onekana kwenye picha hii hapa chini...

Haikuweza kufahamika mara moja jengo hilo litatumika kwa shughuli gani mara baada ya Waziri Kiongozi kuhamia kwenye jengo jipya katika siku chache zijazo.

No comments: