Monday 10 May 2010

Pemba imeanza kujaribu umeme toka Tanga


Huduma ya umeme mpya wa grid ya taifa kutoka Tanga hadi Pemba umewashwa leo kwa majaribio kiswani humo na kwa mafanio mafaniko.

Akizungumza katika zoezi hilo Naibu waziri wa maji ujenzi nishati na ardhi Tafana Kassim Mzee amesema umeme huo kisiwani Pemba umeanza kuwashwa majira ya saa tano Asubuhi.(Jana Jumapili)

Bw.Mzee amesema majaribio hayo yatachukua muda wa wiki mbili na umeme huo unatarajiwa kuwashwa rasmi Tarehe 2 June ambapo rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa bara za la mapainduzi Dr.Amani Abeid Karume anatarajiwa kuuzindua rasmi huduma hiyo…
Akizungumza na zenji Fm Radio Miongoni mwa mafundi waliokuwa wakifanikisha kazi hiyo kutoka shirika la umeme Tanzania Tanesco amesema umeme huo ulitarajiwa kuwashwa saa 12 Asubuhi na umechelewa kutokana na kutokea hitilafu katika baadhi ya viungo vya waya wa umeme huo……

Kisiwa cha Pemba kwa muda mrefu hakina huduma ya umeme wa uhakika kutokana na vinu vya kuzalisha umeme kuwa vibovu.

Kuwepo kwa huduma hiyo ya grid ya taifa kutoka Tanga kutachochea maendeleo ya kisiwa hicho hasa katika uwekezaji wa sekta ya utalii na kukuza maendeleo ya kiuchumi kwa wanachi wake.

Source: ZenjFM

No comments: