Monday 30 July 2012

"Kuna Harufu Chafu CCM Zanzibar" - Ameir

Mwanasiasa Mkongwe Zanzibar Ali Ameir Mohamed, amesema wakati umefika kwa viongozi wa juu wa Chama Cha Mapinduzi kuwachukulia mapema hatua za kimaadili na kinidhamu wanachama,Wawakilishi na Wabunge wa chama hicho wenye mwelekeo hasi.

Ameir ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa zamani wa CCM Zanzibar na Mbunge wa zamani wa Donge, alisema hayo kupitia mahojiano maalum yaliyofanyika Kijijini kwake huko Donge Mbiji Zanzibar juzi.

Alisema kuwa kuendelea kuwavumilia wanachama wa aina hiyo ni hatari kwa mustakabali wa uhai wa chama hicho akiifananisha hali hiyo ni sawa na mfiwa kufuga maiti ya ndugu yake ndani ya nyumba anayoishi.

“Chama cha siasa ni mkusanyiko wa kundi la watu wanaokubaliana kisera, kiitikadi na kimfumo hivyo anayejitokeza akipingana na masuala hayo hapaswi kubembelezwa au kuonewa muhali”,alisema Ameir ambaye pia amewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Tanzania.

Alisema kiongozi, mwanachama, mbunge au Mwakilishi anayepingana na sera ya msingi ya chama chake analazimika kujitoa ili kuonyesha msimamo wa hisia zake.

Ameir anasema anaamini kuwa taratibu za kikanuni na kikatiba ndani ya chama chake zitafutwa ili kusafisha hewa chafu inayoonekana kutanda.

“Kila mwanachama au kiongozi ana wajibu na haki ya kutambua chimbuko la historia ya vyama vya TANU na ASP, muundo wa Muungano na harakati zilizoleta Mapinduzi mwaka 1964, asiyekubaliana na ukweli huo nadhani hatoshi kubaki na kuwa mtetezi wa sera za CCM kwa uhai wake”.Alisikika akisema

Aidha mwanasiasa huyo ambaye ni mmoja kati ya wajumbe walioshiriki kuandaa mchakato wa uundwaji wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar, alieleza kuwa yeye anaamini kuwa taratibu husika kupitia vikao vya katiba vya CCM zitafuatwa.

Ameir alieleza kuwa kumejitokeza baadhi ya wanasiasa Zanzibar wanaojigamba kuwa wao ni waasisi wa TANU na ASP wakati ni wazee wa CCM na kwamba si haki yao kujiita ni wana Mapinduzi kinyume na ukweli ulivyo. Alisema waasisi wa Mapinduzi ya Zanzibar, wanafahamika kwa majina yao na kwamba anayejitokeza sasa na kudai yeye ni miongoni mwao, ni sawa na mtu anayejipaka damu ya ng’ombe aliyechinjwa na wengine.

“Wana Mapinduzi wa Zanzibar wamebaki wawili hadi sasa,wote sasa ni wazee, Ramadhani Haji Faki na Hamid Ameir Ali, anayethubutu kunyoosha kidole chake na kujiita muasisi wa Mapinduzi, anajivika kilemba cha ukoka”Alisema Ameir.

Alipinga jina la Hassan Nassor Moyo kuwa miongoni mwa waasisi wa ASP na kuwa mmoja kati ya wanamapinduzi kwamba hakuwemo katika harakati za kukiasisi chama hicho wala hakujua siku ya kufanyika Mapinduzi ya 1964 kwa mujibu wa maelezo ya wazee wenzake.

“Moyo ninamheshimu sana, ni mkubwa kiodogo kwangu kiumri ,alikuwa katika Trade Union, hakuwa mwanasiasa aliyeshiriki kukiasisi chama cha ASP,wenzake wanatueleza hata siku yaliofanyika Mapinduzi ya umma hakuijua”Alisisitiza

Akizungumzia kujitokeza kwa Mzee Moyo anayeonekana kutaka Muungano wa mkataba kinyume na sera ya CCM kinachofuata Serikali mbili chini ya Katiba.

Ameir alisema wajumbe hao kufika kwao ndani ya BLW kunatoka na chama cha siasa hivyo matamshi yao hayapingani na sera hiyo ila wanavutana na mfumo wa chama chao.

‘Mzee Moyo nijuavyo ni mwana Muungano wa kikwelikweli, asili yake upande mmoja ni Ruvuma Tanganyika na upande wa pili hapa Zanzibar, anapobeza Muungano huu unaotokana na matokeo ya Mapinduzi na Uhuru wa nchi zetu, sidhani kama anaamua kuafikiana na misimamo tuliokuwa tukipingana nayo kabla ya 1961 na 1964 ”Alisema Ameir.

Kauli hii inakuja wakati kukiwa na katika kampeni kubwa ya kutaka Zanzibar kujitenga katika Muungano wakishirikiana na Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara, (JUMIKI) hali iliyosababisha vurugu za makanisa na baa kuchomwa moto Zanzibar.

Mwinyi Sadallah

Friday 27 July 2012

"Kuitetea Zanzibar Katika Muungano." Balozi Ali Karume


Mtu yoyote ambae anadai kuitetea Zanzibar katika Muungano, hawezi wakati huo huo kudai Muungano uvunjike. Iwapo Muungano utavunjika, hiyo Zanzibar utaiteteaje katika Muungano ambao umeshavunjika? Lazima kuitetea Zanzibar katika mfumo wa Muungano ambao unatoa haki sawa kwa nchi mbili ambazo zimeungana. Mwanzo wa haki hizo ni katika kuongoza Muungano kwenye safu zote za Serikali ya Muungano, kuanzia ngazi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Nchi mbili zikiungana huwa zinasaka "Equity" kwenye huo Muungano. Uwiano wa haki huleta usawa kwa pande zote mbili na kuchelea upande mmoja kujihisi wametawaliwa au wamemezwa. Kujihisi au kuwa na hesia ya kutawaliwa huleta unyonge wa kuhisi kuna ukosefu wa utetezi; maana kwenye utetezi kamili, hakuna kupunjwa, kunyanyaswa, au kuonewa. "In politics, perception is everything". Kwenye siasa, kilakitu hutokana na hesia. Ukihisi unadhulumiwa, huwachi kulalamika.

Kwenye nchi zinoungana kisiasa, tatizo la kwanza ni kupanga safu ya uongozi utoridhisha sehemu zote za Muungano. Mara nyingi, katika kuepuka vurugu za kuchagua Rais mpya wa Muungano, mapendekezo ni kwamba Rais wa nchi moja ndie awe Rais mpya wa huo Muungano. Hii humaanisha kwamba Rais wa ile nchi nyengine awe Makamo wa Rais, ili wale Marais wawili kabla ya Muungano, waongoze serikali ya Muungano kwenye safu ya Rais na Makamo wake. Pia, humaanisha kwamba baada ya kipindi au vipindi muafaka, na yule Makamo au kiongozi mwengine kutoka nchi yake, aweze kuongoza kwenye safu ya Urais wa Muungano. Na upande wa pili wa Muungano utowe Makamo wa Rais.

Katiba ambayo tumepania kuibadili, imetamka wazi kwenye hilo, na watetezi wa Zanzibar hilo wamelifurahia. Katika Katiba mpya, bora hilo libaki, na katika kutilia mkazo "Equity" na uwiano utaochelea migogoro na malalamiko ya kuelemewa, ni bora Katiba itamke wazi juu ya suala la kupishana na kuwepo zamu kwenye Urais na vyeo vyengine vya juu.

Kila Katiba huwa na Yaloagizwa, Yaloelezwa, na Yanotegemewa kutokana na itikadi. "Traditions" ni kitu muhimu katika uteuzi wa viongozi, na katika Muungano ni lazima kujenga itikadi ya kuteua viongozi kutoka pande zote mbili. Watetezi wa nchi zao ni lazima kusimamia hilo. Lazima kuwe na "Deliberate attempt" Jaribio la makusudi na la dharura kutoa zamu kwenye uongozi, ilimradi watoteuliwa wakidhi sifa zinotegemewa. Hayo yamefanyika katika historia ya Muungano wetu, na sioni kwanini iwe mwiko kuirejea historia hiyo. Katika demokrasia, wengi wape kutokana na wingi wa kura, na tusipofanya jaribio la makusudi na la dharura kuwapata viongozi wa safu za juu kutoka sehemu zote za Muungano wetu, basi wengi watatoka sehemu moja na kuendelea kujenga hisia kwamba sehemu moja ya Muungano imeelemewa. Ndio maana kuna wengine wanajihisi wamesakamwa na wanaomba waachiwe wapumuwe.

Tunapopata fursa ya kuchagua viongozi wa juu, kama vile Rais wa Jamhuri ya Muungano, ni vyema wale wanaodai kuitetea Zanzibar wawe mstari wa mbele katika kumpata mgombea bora kutoka Zanzibar na kumsaidia ili ateuliwe. Hili ni muhimu kufanyika, hasa baada ya uongozi wa ngazi ya juu kabisa kukamatwa na viongozi kutoka sehemu moja ya Muungano kwa muda mrefu. Mwenyekuitetea Zanzibar kikweli kwenye hilo, hawezi kudai kwamba hakuna Mzanzibari anofaa kwenye wadhifa huo. Anayechukua msimamo huo, anachangia Zanzibar kusakamwa na kukosa pumzi. "Tuacheni tupumuwe" aambiwe na yeye pia. Mzanzibari anayewakataa wagombea wote kutoka Zanzibar na kumuunga mkono mgombea kutoka bara kwa hali na maji aendelee kutawala, asidai kwamba anaitetea Zanzibar na kudai "Tuacheni tupumuwe". Kwani kwenye kusakamwa na Bara, na yeye si alichangia? Ya yeye alichangia katika kutukosesha pumzi, ilimradi yeye apumuwe vizuri zaidi baada ya kutuuza. "We were sold down the river to the highest bidder by our own kith and kin". Kikulacho kinguoni mwako.

Umefika wakati Watanzania tuwe makini sana. Tutetee haki zetu kwenye Muungano wetu, na tujizatiti katika kuepusha "Dhana" ya aina yoyote ya kwamba upande mmoja wa Muungano wetu, umeelemewa. Tuunde Katiba mpya itoondowa dhana ya kutawaliwa na tutoe fursa kwa pande zote ziachwe zipumuwe. Tukishindwa kwenye hilo, tutajitakia maradhi. Na wahenga walisema "Maradhi ya kujitakia; Mtu hapewi pole".

Balozi Ali Abeid Amani Karume.

Thursday 26 July 2012

Pope Benedict Asikitishwa na Vifo Vilivyotokea Zanzibar

Sunday after praying the midday Angelus with crowds gathered at the papal summer residence, the Pope said he was "deeply shocked by the senseless violence which took place in Aurora, Denver."

A heavily armed man in full body armor opened fire on movie-goers at the midnight release of "The Dark Knight Rises." A dozen people were killed and several dozen more were wounded.

The suspect appeared in court for the first time today.

Strength in the risen Lord

The Pope also expressed his sadness at the loss of life in a ferry disaster near Zanzibar.

The MV Skagit hit choppy waters last Wednesday as it crossed from Tanzania to Zanzibar and sank. At least 145 of the 290 passengers were rescued, but by today nearly 80 bodies had been recovered, with more than 65 still missing.

Police have said there is no hope the missing will be found alive, meaning the death toll might be as high as half the number of passengers aboard.

"I share the distress of the families and friends of the victims and the injured, especially the children," the Pontiff said. "Assuring all of you of my closeness in prayer, I impart my blessing as a pledge of consolation and strength in the risen Lord."


GZN

Wednesday 25 July 2012

Mv Serengeti mashakani (injini yake imezima)

Kuna taarifa kuwa meli ya Mv Serengeti imeshindwa kuendelea na safari yake baada ya injini yake kuzima ikiwa njiani kuelekea Unguja ikitokea Pemba.

Tuesday 24 July 2012

Tetesi: Karume atakiwa kurudisha kadi ya CCM

Makamo Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar Abeid Karume, Mshika Fedha wa CCM, na baadhi ya wajumbe wa baraza la wawakilishi watakiwa kurejesha kadi za CCM haraka baada ya kukiuka maadili ya chama chao.

Monday 23 July 2012

Hamad Masoud Amejiuzulu...


Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Hamad Masoud amejiuzulu rasmi leo jioni.

Sunday 22 July 2012

Nahodha Katapika


"Watu wameiba mamilioni ya fedha, wamepora maekari ya ardhi ya waznz lakini Leo hii akisimama na kusema hautaki muungano anaoenekana ndio mtetezi wa waznz" mh. Shamsi Nahodha

Wednesday 18 July 2012

Meli Kwa Jina la Skagit Imezama Karibu na Chumbe

Ilikuwa ikitokea Dar es Salaam kwenda Unguja, ikiwa na abiria 200. Kazi za uokoji zimeshaanza.

Boat za Sea Star na Kilimanjaro zimekwenda kwenye eneo la tukio kwa ajili ya uokoaji.. Habari zinasema kuwa miili ya abiria imeanza kuonekana ikielea. Hali ya bahari ina upepo mwingi kwa sasa.

Aidha kutokana na hali mbaya ya hewa meli moja imeshindwa kufika katika eneo la tukio na imerudi bandarini.

Mamia ya watu wapo bandarini Malindi wakiendelea kusubiri watakao okolewa.


Baadhi ya abiria waliookolewa

Uamusho Wawachimbia Mkwara Polisi...


Lidia Kucharcyk Anatafutwa na Familia yake.


Saturday 14 July 2012

Friday 13 July 2012

Makontena yameondolewa Darajani

Jana usiku kulikuwa na vunja vunja kwenye Makontena ya darajani ili kupisha ujenzi wa bustani na parking za magari

Monday 9 July 2012

Mji Mkongwe(Stone Town) Wasafishwa


Siku ya Jumapili iliyopita, Mji Mkongwe ulisafishwa kwa kufagia barabara na chochoro zake pamoja na kuzoa taka mbalimbali katika Mji huo. Usafishaji uliwashirikisha Sustainable East Africa, FAZACH, Conservation & Education-Chumbe Island Coral Park na skuli kadhaa za Mji Mkongwe.

Sunday 8 July 2012

Friday 6 July 2012

BARUA YA WAZI KWA MH.RAIS Dr.SHEIN – UTEUZI WA MAJAJI





Our Ref:ZLS/IKULU/001

Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti
wa Baraza la Mapinduzi
Ikulu, Zanzibar

Mheshimiwa Rais,

KUH: “PETITION” YA CHAMA CHA MAWAKILI WA ZANZIBAR JUU YA KUTORIDHIKA KWAO NA UTEUZI WA MAJAJI WA MAHKAMA KUU ULIOTANGAZWA TAREHE 29 NOVEMBA 2010

Kwanza kabisa sisi Chama cha Mawakili wa Zanzibar tunapenda kukupa pongezi zetu za dhati kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi katika utaratibu mpya wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Tunakuombea kheri na mafanikio katika kuwatumikia Wazanzibari ambao wamekupa ridhaa zao na kuonesha imani kubwa juu yako

Chama cha Mawakili wa Zanzibar (ZLS) ni Chama kinachowaunganisha Mawakili wote wa Zanzibar ambao wanafanya kazi ya uwakili katika Mahkama Kuu ya Zanzibar pamoja na mahkama zinazofanya kazi chini ya Mahkama Kuu isipokuwa Mahkama za Mwanzo na Mahkama za Makadhi. Mawakili hawa pia huendesha kesi katika Mahkama ya Rufaa ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania. Katika nafasi yao hiyo, Mawakili wanakuwa ni maofisa wa mahkama. Chama hiki kimeanzishwa mwaka 1998 chini ya Sheria ya Jumuiya ya mwaka 1995. Chama kinaongozwa na Baraza lake lenye Rais, Katibu Mkuu, Mshika Fedha na wajumbe wengine wawili.

Mhe Rais, tarehe 29 Novemba 2010 ulitangaza uteuzi wa majaji wanne wa Mahkama Kuu pamoja na Mwenyekiti wa Mahkama ya Ardhi. Uliowateua kuwa Majaji ni:
1. Mhe: Abdul-hakim Ameir Issa
2. Mhe. Fatma Hamid Mahmoud
3. Mhe. Mkusa Isaac Sepetu, na
4. Mhe. Rabia Hussein Mohamed

Mhe. Rais, katika uteuzi wako huo, ulikuwa unatumia mamlaka uliyopewa na Katiba ya Zanzibar, 1984 kifungu cha 94(2) na (3). Aidha Chama cha Mawakili hakina mashaka na uteuzi wa Mhe. Abdul-hakim Ameir Issa, wala uteuzi wa Mwenyekiti wa Mahkama ya Ardhi, Mhe. Haroub Shehe Pandu. Mashaka yetu yapo katika uteuzi wa waheshimiwa kuanzia nambari 2 mpaka 4 hapo juu.

Mhe. Rais, sisi tunaelewa kwa dhati kabisa kwamba wewe binafsi humjuwi wala huna sababu ya kumjuwa yeyote katika Majaji wanne uliowateua. Uteuzi wako, tunaamini kabisa, unatokana na ushauri uliopewa na Tume ya Utumishi ya Mahkama iliyoanzishwa chini ya Sheria Namba 13 ya mwaka 2003 ambayo Mwenyekiti wake ni Jaji Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Hamid Mahmoud Hamid pamoja na wasaidizi wako wengine katika sekta ya sheria.

Mhe. Rais, sisi mawakili ambao tumetia saini barua hii tukiwa ni wadau wakubwa katika sekta hii, tuna imani kubwa nawe Mheshimiwa Rais, lakini tunaamini washauri wako hawakukutendea haki walipokushauri uwateue Mhe. Fatma, Mhe. Mkusa na Mhe. Rabia kuwa ni Majaji wa Mahkama Kuu. Mhe. Rais, haitoshi tu kusema kwamba Jaji Mteule ametimiza masharti ya Katiba na hivyo anafaa kuwa Jaji wa Mahkama Kuu. Mhe. vipo vigezo vyengine ambavyo ni lazima viangaliwe kabla ya uteuzi wa Jaji wa Mahkama Kuu kufanyika. Nafasi ya Ujaji ni nafasi ya juu kabisa katika ngazi ya Mahkama zetu na pia ni nyeti. Utaalam uliobobea, rekodi iliyothibitika, umakini wa hali ya juu, kujiamini, uadilifu na umahiri wa hali ya juu – vyote kwa pamoja vinahitajika.
Mhe. Rais, kifungu cha 94(2) cha Katiba kinasomeka ifuatavyo:
Majaji wa Mahkama Kuu watateuliwa na Rais kutokana na mapendekezo ya Tume ya Utumishi ya Mahkama.

Mhe. Rais, Chama cha Mawakili kina mjumbe katika Tume ya Utumishi ya Mahkama. Pia wajumbe wengine wa Tume ni watu walio karibu na Chama cha Mawakili. Tunapenda kukuthibitishia kwamba hakuna kikao chochote cha Tume hiyo ambacho kimejadili jina la Mhe. Rabia Hussein. Hivyo uteuzi wa Mhe. Rabia umefanywa kinyume kabisa na Katiba ya Zanzibar na hauwezi kusimama katika macho ya sheria.

Mhe. Rais, sisi kama Chama cha Mawakili, tunaamini hata uwepo wa Mhe. Hamid Mahmoud kama Jaji Mkuu wa Zanzibar una mashaka tele ya kikatiba. Inaeleweka kwamba Mhe. Hamid Mahmoud alistaafu kwa hiari alipotimiza miaka 60. Baada ya hapo, Kikatiba, alisita kuwa Jaji Mkuu na Jaji wa Mahkama Kuu. Iwapo alitakiwa kuendelea kushika wadhifa, alipaswa kwanza kupewa mkataba wa kuwa Jaji wa Mahkama Kuu.

Mkataba wa aina hiyo ulilazimu kujadiliwa na Tume ya Utumishi ya Mahkama kwa mujibu wa kifungu cha 95 cha Katiba ambacho tunaomba kukinukuu:
95(1) Bila ya kuathiri masharti ya kifungu hiki, Jaji wa Mahkama Kuu ataendelea kushika wadhifa wake hadi kufikia umri wa miaka sitini ambapo anaweza kustaafu kwa hiari ama kuendelea hadi kufikia umri wa miaka sitini na tano ambapo atastaafu kwa lazima.

(2) Bila ya kuathiri masharti ya kijifungu cha (1) cha kifungu hiki, Rais kwa kushauriana na Tume ya Utumishi ya Mahkama anaweza kumteua tena Jaji aliekwisha staafu kushika madaraka ya Jaji wa Mahkama Kuu kwa muda au kwa ajili ya kesi maalum. (Msisitizo ni wetu).

Mhe. Rais, ni wazi kwamba pale Mhe. Jaji Mkuu alipoamua kustaafu kwa hiari alipotimiza umri wa miaka 60, hakukuwa na sababu yoyote kuendelea kufanya kazi katika mkataba kwa kuwa Katiba ilikuwa inamruhusu kuendelea na ajira hadi kufikia miaka 65. Vyovyote iwavyo, endapo Mhe. Jaji Mkuu alitakiwa aendelee na nafasi yake baada ya kumaliza utumishi wake, ililazimu mambo yafuatayo yafuatwe kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar (kifungu cha 94(1), 94(2), 94(6)(a) na (b). Mambo yenyewe ni:
a) Ateuliwe kuwa Jaji wa Mahkama Kuu;
b) Mapendekezo ya (a) yatokane na Tume ya Utumishi ya Mahkama;
c) Endapo ni Jaji wa Mkataba, “masharti ya kazi, marupurupu na kiinua mgongo cha Jaji wa mkataba wa kipindi maalum yataamuliwa na Tume ya Utumishi ya Mahkama.” (Kif.94(6)(b).
d) Iwapo atateuliwa kuwa Jaji basi atakula kiapo cha Jaji wa Mahkama Kuu.

Mhe Rais, Jaji Mkuu wa sasa ambae ndio Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi ya Mahkama, alipostaafu kwa hiari, utaratibu ulioainishwa hapo juu haukufuatwa na magazeti yaliripoti na jamii ya wanasheria pia ilifadhaishwa mno. Aidha, iwapo Mhe. Hamid Mahmoud alitakiwa awe Jaji Mkuu, pia ilipaswa masharti ya Katiba yafuatwe. Vyenginevyo kuendelea kwake kuwa Jaji Mkuu kunakuwa na mashaka ya Kikatiba na sisi tusingependa nchi yetu iwe na Jaji Mkuu ambae uteuzi wake umegubikwa na kasoro kadhaa za Kikatiba.

Hata suala la kuwa Jaji au Jaji Mkuu wa Mkataba ni suala linalopigwa vita sana katika Mahkama za Jumuiya ya Madola kwa sababu mikataba inaondowa kinga ya Kikatiba aliyonayo Jaji wa Mahkama Kuu na hivyo kudumaza uhuru wa Mahkama (independence of the Judiciary). Aidha Jaji wa Mkataba hawezi kufanya kazi yake bila ya hofu wala woga kwa mamlaka ya uteuzi.

Mhe. Rais, siri ya maiti aijuwae muosha; na sisi mawakili ndio waosha wa waheshimiwa majaji na mahakimu wetu. Mhe. Rais, bila ya kuzunguka, sisi tunataka tukuthibitishie kwamba Mhe. Fatma na Mhe. Mkusa hawana sifa kiutendaji na kiuwezo za kuwa majaji wa Mahkama Kuu ya Zanzibar. Mhe Rais, uwezo wa Jaji unapimwa kwa namna anavyoendesha kesi na kuandika hukumu zake. Chombo cha Mahkama ni chombo cha kutoa haki. Na haki inatakiwa isifanywe tu lakini ionekane waziwazi kuwa inafanywa. Mhe Rais, haki haiwezi kupatikana ikiwa wanaosimamia haki hiyo ni watu wasiokuwa na sifa zinazotakiwa.

Mhe. Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, tunakuhakikishia kwamba sisi Mawakili wa Zanzibar ambao saini zetu zimetiwa hapa chini tuna imani kabisa na wewe binafsi na wala hatuandiki barua hii kuhoji mamlaka yako ya Kikatiba ila tunatoa tahadhari hii kama mchango wetu katika kujenga mahkama iliyotukuka, hasa kwa vile wananchi wamepoteza imani kwa mahkama zetu ziliopo sasa.

Ni vyema kuepuka mambo yanayoonekana dhahiri kulenga katika kudumaza zaidi ufanisi wa mahkama katika suala zima la utoaji haki. Tujinasuwe sasa kuliko kuendelea kujizamisha kwa kuweka watendaji wasiofaa.

Sisi, kama wadau wa jamii, tunahisi tuna wajibu wa kukutanabahisha kuhusu uteuzi huu. Aidha tusingependa Mahkama Kuu ambayo tayari kuna malalamiko mengi ya utendaji usiokidhi haja iendelee kuchukuwa Majaji bila ya ushauri wa Tume ya Utumishi ya Mahkama na bila ya umakini katika tathmini ya wateule hao.

Mhe. Rais, wateule wa Ujaji tuliowataja hapo juu, hawatokuwa Majaji rasmi Kikatiba na kuanza kazi ya Ujaji wa Mahkama Kuu mpaka baada ya kula kiapo. Hilo likishafanyika, itakuwa dhiki sana kuondosha uteuzi huo. Hivyo, tunakuomba Mhe. Rais, utafakari upya juu ya uteuzi huo na uridhike kuusitisha. Tunaamini wanasheria wenye sifa na maadili yanayotakikana wapo na wanaweza kufanya kazi ya ujaji, Zanzibar.

Wako katika kusimamia haki,
Yahya Khamis Hamad Salim Rais
H. B. Mnkonje Katibu Mkuu
Abdulla Juma Mohammed Mshika Fedha
Salma Ali Hassan Mjumbe, ZLS
Mussa Kombo Mjumbe, ZLS
1. Ajar Amar Patel …………………………..
2. Ussi Khamis Haji …………………………….
3. Hamid A. S. Mbwezeleni …………………………….
4. Salum Toufiq Ali ………………………………
5. Awadh A. Said ……………………………….
6. Nassor Khamis Mohammed ……………………………….
7. Adam S. Abdulla ………………………………
8. Is-Haq Ismail Shariff ………………………………..
9. Uhuru Hemed Khalfan ………………………………..
10. Mahadhi J. Maalim (ameridhia)
11. Masoud H. Rukazibwa ………………………………..
12. Ramadhan Makame ……………………………….
13. Mbwana J. Mbwana ………………………………
14. Fatma A. Karume …………………………….
15. Rajab Abdalla Rajab ……………………………….

Thursday 5 July 2012

Vunja Jungu - Golf Club



Memba wa gofu wakiwa katika vunja jungu jana jioni katika ukumbi wa gofu...

Wednesday 4 July 2012

Maharamia Yawavamia Watalii Zanzibar...

Machete-wielding pirates attack Yoav and Esther Peled; Yoav fights back, loses some fingers – but surgeons managed to reattach them.

A honeymoon turned sour this week for an Israeli couple who were attacked by pirates in Zanzibar.

Yoav and Esther Peled of Givatayim married on May 30 and travelled to the Tanzanian islands after the wedding. On Sunday, a group of pirates armed with machetes attacked the couple. Yoav, who confronted them, lost some of his fingers to the pirates' blades.

Peled managed to reach medical help, and was flown from Zanzibar to Dar es-Salaam, the largest city in Tanzania, where he had emergency surgery. The cut he sustained from the pirates' machete was extremely deep, reaching the nerves of his hand, but the doctors nevertheless reattached his severed fingers.

The Foreign Ministry said that it was familiar with the incident. "It happened Sunday during a robbery. The man is currently hospitalized in Zanzibar. His family knows, and so does (the couple's) insurance company, Harel."

Hilik Magnus, who conducts search and rescue operations for the Phoenix insurance company, said that tourists must act with the understanding that if they encounter pirates, they must cooperate quietly.

"Tourists are the preferred targets for criminal incidents, because they're defenseless. In addition, from the perspective of politics, everyone involved wants to gloss over the incident so the place doesn't gain a reputation as dangerous for tourists," Magnus added.

Source: Ynetnews

Tuesday 3 July 2012