Wednesday 1 August 2012

Hassan Nassor Moyo- "Nipo tayali kurudisha kadi ya CCM"

Awataka Vijana kuendelea na harakati za ukombozi wa nchi ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar

Mzee Hassan Nassor Moyo leo amefanya mkutano na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano wa Rumaisa Hotel Malindi Mjini Zanzibar, kujibu hoja mbalimbali zilizo zagaa nchini.

Katika mkutano huo ambao pia ulihudhuriwa na Vijana wa Umoja wa Kitaifa na wanafunzi wa Vyuo Vikuu Mzee Moyo alielezea kuwa msimamo wake anaouonesha sasa si kwa sababu kama Serikali imemtenga kama inavyovumishwa na baadhi ya watu.

Aliwataka vijana waendelee na harakati za ukombozi wa nchi kwani wao si wa mwanzo kuendesha harakati za ukombozi wa nchi.

''Fujo hamkuzianza nyinyi vijana vujo tulizianza sisi toka 1970'' alisema Mzee Moyo huku akishangiriwa na vijana.

Alisema vijana wana haki ya kuuhoji Muungano na wala yeye hawezi kuwazuwiya kwani wamewasomesha wao wenyewe ili kuleta maendeleo ya taifa hili.

Akijibu maswali yaliokuwa yakiulizwa na waandishi wa habari Mzee Moyo alisema yeye ni Mzaliwa wa Zanzibar na hajapata kuomba uraiya wa Zanzibar ila wapo wana CCM hawajazaliwa Zanzibar na wameomba uraiya wa Zanzibar mwaka 1963.

Katika maelezo yake ya awali Moyo alisema hawezi kuyumbishwa na CCM ati kwa kudai Mamlaka kamili ya Zanzibar na kudai Muungano wa Mkataba.

''Hawa Wana CCM wanaodai kuwa turudishe kadi za CCM ni wana CCM uchwara hakuna mwana CCM kindakindaki aliedai sisi turudishe kadi za CCM'' alisema Mzee Moyo huku akiendelea kusema kuwa Ali Ameir si muasisi wa Mapinduzi wala si Muasisi wa Muungano na hajawahi kuwa hata Memba wa Baraza la Mapinduzi''

Nao Vijana wa Umoja wa Kitaifa na Wanafunzi wa Vyuo Vikuu walimuhakikishia Mzee Hassan Nassor Moyo kuwa wapo wapamoja nae na kama atarudisha kadi ya CCM nao watarudisha kadi hizo na kumfata atakapo elekea.

Tayari Vijana wa Umoja wa Kitaifa wamekwisha towa tamko lao la indhari dhidi ya wana CCM wanaowakaripia na kuwatukana Wawakilishi pamoja na Wana CCM wanaotowa mawazo ya Muungano wa Mkataba na kuonya kuwa hali hiyo itahatarisha mchako wa Katiba Mpya.

Jamii Forums

No comments: