Friday 26 April 2013

Muungano Oyeee!


Somewhere near Shangani...

Union Day... Tanganyika and Zanzibar

Ulipoanzia





Ulipofikia

Thursday 25 April 2013

Sokoni...

Sunday 21 April 2013

Unakumbuka Hii? JEANS AND ORNAMENTS BANNED IN ZANZIBAR SCHOOLS

The Zanzibar President, Dr Salim Amour, has banned jeans and ornaments worn by secondary and primary school teachers, saying these were indecent and gave a bad example to children.

Dr Salim made the call recently when he was officiatingat the free education festival in Pemba. He said that the teachers' dressing in the Isles typified a great deal of moral erosion.

The president also expressed disappointment over the recent examination results which contained a majority of second and third class passes and ordered teachers and students to double their efforts to improve this. He urged them to seriously compete and use extra time to promote educational standards in the Isles. The Zanzibar government would extend an invitation to the State House for a tea party for all students who scored first class results in the future.

He also said that the government plans to build a university in the Isles to promote education as the world enters the 21 century.

9 October 1997

Friday 19 April 2013

Mwaka Mmoja wa Kumbukumbu ya Brigadier General Adam Clement Mwakanjuki


Umetimia mwaka mmoja sasa tokea Brigedia Jenerali Mwakanjuki kufariki dunia. Familia, ndugu, jamaa na marafiki wanaendelea kumkumbuka marehemu. Marehemu alizaliwa Oktoba 17, 1939 katika mtaa wa Kikwajuni, Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar. Hadi kifo chake marehemu alikuwa ana umri wa miaka 73.

Brigedia Jenerali alipata elimu yake ya msingi katika skuli iliyokuwa ikijulikana kwa jina la St Paul - Kiungani katika mwaka 1947-1954.

Mwaka 1954-1959, Marehemu alipata fursa ya kujiunga na masomo ya sekondari katika skuli ya St Andrew ya Minaki jijini Dar es Salaam.

Mwaka 1960-1962, alijiunga na chuo kikuu cha Frizt Heckert Ujerumani ya Mashariki, na kupata fursa ya kusomea masomo ya juu ya siasa.

Baada ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar mwaka 1964, Marehemu Mwakanjuki alikuwa ni mmoja wa viongozi wa Umoja wa wafanyakazi wa Zanzibar.

Aidha, kuanzia mwaka 1964 hadi 1968 aliajiriwa na kufanya kazi katika idara ya Mambo ya Nje ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akishikilia wadhifa wa Afisa Mambo ya Nje.

JWTZ na JKT

Marehemu alijiunga na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania(JWTZ)tarehe 24 Juni, 1969 akiwa na wadhifa wa Mwalimu wa Siasa katika Jeshi la Kujenga Taifa(JKT).

Baadae Marehemu aliendelea na utumishi katika JWTZ katika nyadhifa mbalimbali kama ifuatavyo:-
-Mwaka 1972 - 1979: Alikuwa Mkuu wa Vikosi(CO)vya JWTZ, JKT na Mwenyekiti wa Tawi la CCM Jeshini.
-Mwaka 1980-1981: Kamisaa wa Divisheni ya 20 ya Jeshi(JWTZ)
-Mwaka 1982 aliteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Elimu ya Siasa Makao Makuu ya Jeshi- Dar es Salaam.

Mafunzo Kazini
Marehemu Mwakanjuki alipata fursa mafunzo mbalimbali:
-Mwaka 1975: Mafunzo ya Afisa Mwanafunzi(Officer Cadets Course)katika chuo cha Mafunzo ya Maofisa - Mgulani Dar Es Salaam.
-Mwaka 1976: Mafunzo ya Ukamanda wa Kombania(Company Commanders Course) katika chuo cha Taifa cha Uongozi-Monduli, Tanzania.
-Mwaka 1977: Mafunzo ya Ukamanda wa Vikosi(Battalion Commanders Course) katika chuo cha Taifa cha Uongozi- Monduli, Tanzania.

Marehemu Mwakanjuki alifanikiwa kupandishwa vyeo Jeshini katika ngazi tofauti kama ifuatavyo:-
-01.07.1975: Cheo cha Meja.
-05.05.1977: Cheo cha Luteni Kanali(lieutenant Colonel)
-25.02.1980: Cheo cha Kanali(Full Colonel)
-10.04.1988: Cheo cha Brigadia Jenerali(Brigadier General), cheo alichoendelea kuwa nacho hadi alipostaafu jeshi mwezi Juni, tarehe 30 mwaka 1994.

Medali
Medali alizowahi kutunukiwa katika uhai wake ni pamoja na ujasiri wake akiwa kazini, Marehemu alipata heshima zingine zikiwemo:-
-Medali ya Uhuru.
-Medali ya Muungano
-Medali ya Vita.
-Medali ya Kagera.
-Medali ya Miaka 20 ya JWTZ.
-Medali ya Utumishi Mrefu Tanzania.
-Medali ya Utumishi Uliotukuka Tanzania.

Siasa
Katika siasa Brig Jenerali Mstaafu Mwakanjuki, alijiunga na Chama cha Afro-Shiraz(ASP)mwaka 1958, akiwa mwananfunzi wa skuli ya sekondariya Minaki. Aidha, katika mwaka 1958-1959, alikuwa kiongozi wa Chama cha Wanafunzi wa Kiafrika wa Zanzibar.

Kutokana na hekima, busara na uwezo mkubwa aliouonesha katika masuala ya siasa, ASP ilimuamini na kumkabidhi nyadhifa mbalimbali za uongozi ndani ya chama hicho.

Aidha, Uongozi wa Chama ulimteua ili akiwakilishe Chama katika shughuli muhimu mbalimbali zilizofanyika ndani na nje ya nchi yetu, miongoni mwake, mwaka 1962 alishiriki katika Mkutano Mkuu wa Kwanza wa kupitisha Muundo wa Katiba ya ASP.

Mwaka 1963, alishiriki katika mkutano wa Afro-Asian(The Afro- Asian Solidarity Conference)uliofanyika Moshi, Tanzania.

Mwaka 1961-1964 alikuwa akitumikia katika shughuli za Chama cha Wafanyakazi katika kazi mbalimbali za chama kama vile matayalisho ya Uchaguzi, Uenezi wa Siasa, Kuhudhuria mikutano ya kisiasa inayofanyika ndani na nje ya Taifa letu, pamoja na kushiriki kikamilifu katika harakati za Mapinduzi ya Zanzibar ya 12.01.1964.

Baada ya kuungana kwa Vyama vya TANU na ASP mwaka 1977, Marehemu alijiunga na Chama cha Mapinduzi kupitia tawi la Makao Makuu ya Jeshi la Kujenga Taifa(MMJKT)liliopo mkoani Dar es Salaam, mnamo tarehe 01.04.1977.

Mwaka 1982 alichaguliwa kuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kwa tiketi ya Jeshi baadae mwaka 1983 aliteuliwa kuwa Katibu wa Mkoa wa Ruvuma kabla ya kuhamishiwa Mkoa wa Singida Mwaka 1987- 1990. Marehemu aliendelea kuwa mjumbe wa Halmshauri Kuu ya Taifa hadi alipofariki dunia mwaka 2012.

Uongozi Serikalini
Brigedia Jenerali Mstaafu Mwakanjuki alishika nyadhifa mbali mbali za Uongozi katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

-1990-1992: Waziri asiye na Wizara Maalumu.

-1992-1995: Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais Tawala za Mikoa na Vikosi vya SMZ.

-1995-2000: Waziri wa Kilimo na Mifugo.

-2001-2004: Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Katiba na Utawala Bora.

-2004-2010: Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi.






Imeandaliwa na Mwantanga Ame - Zanzibar Leo. 2012

Imeeditiwa na Che Guevara Mwakanjuki.








Wednesday 17 April 2013

RIP Fatma Bint Baraka (Bi Kidude)



Mwanamuziki mkongwe katika Taarab Fatma Bint Baraka maarufu kwa jina la Bi Kidude amefariki dunia muda mchache uliopita huko Bububu Zanzibar, sehemu alikokuwa anaugulia kwa kipindi sasa. Mwili wake utahamishiwa kwake Rahaleo na mazishi yatakuwa kesho. Bi Kidude alizaliwa katika kijiji cha Mfagimaringo, alikuwa binti wa mchuuzi wa nazi, hakuna anayejua haswa Bibi huyu alizaliwa tarehe ngapi, kuna hata mawazo kuwa alikwishafikisha miaka 102.

Katika mwaka 1920 tayari alikuwa amekwisha anza kuimba katika vikundi vya sanaa kule kwao, mwaka 1930 alijiunga na Egyptian Musical Club ya Dar es Salaam na kuzunguka miji mingi ya Tanganyika wakati ule , mwaka 1940 alirudi Zanzibar ambako awali alikuwa amekimbia kwa kuwa aliozwa kwa nguvu na mtu aliyemzidi sana umri.


Bi Kidude pia liwahi kuimba na Sitti Binti Sadi wakati wa ujana wake, na katika maisha yake Bi Kidude amekwisha zunguka mabara yote akiimba katika majukwaa na wanamuziki maarufu ulimwenguni.


Wednesday 10 April 2013

Wachina wajitetea juu ya ujenzi wa chini ya viwango wa Zanzibar Airport(T2)....


Chinese contractor on the defensive over Z’bar airport


A Chinese company has fended off criticism about the construction of terminal two (T2) at the Zanzibar airport.

Some construction experts allege that Beijing Construction Engineering Group (BCEG) Ltd did a shoddy work.
But top BCEG officials maintain that the construction met all required standards and specifications.

“Of course, like in any project, not everything can be perfect but in as far as the use and safety of T2 of Zanzibar Airport is concerned, we have no regrets,” BCEG general manager Geng Bingjian told The Citizen in Dar es Salaam on Thursday last week. “There is no problem with the use and functions of the terminal.”

Mr Geng was accompanied by finance manager Cheng Longhai when responding to allegations by some experts who claim that more funds are needed to provide a safe and efficient landing of aircraft at T2 of the Zanzibar Airport .
The experts argued that the facility had been constructed at the wrong level.

“In short, Terminal 2, meant for passengers at the airport has been constructed on an area that was meant to be an aircraft packing bay,” an expert, who preferred not be named told The Citizen in Dar es Salaam recently.
According to the source, a comprehensive study done by an independent firm has also established that Zanzibar Airport’s T2 has been constructed at the wrong level and more funds are required to rectify the error. The source said it was due to the technical mistakes that the terminal gets filled with water when it rains.

But Mr Bingjian said: “We met all the criteria and the general alignment of the structures to allow for safe landing...Ours is a company that is owned by the government of China and therefore, there was no way we could undertake the project poorly.”

He said even the space on which the terminal is located was provided by the Zanzibar Airports Authority and that the designing of the project was done by Chinese North Civil Airport Design Company, a qualified firm in airport structures.

“Our record, and that of the designer speaks for itself....we have built terminals 1, 2 and 3 of Beijing Airport....we are among 200 top construction firms in the world and among top ten such firms in China...we are very credible,” said Mr Bingjian.


TC

Tuesday 9 April 2013

Wanafunzi ni Kosa Kufanya Kazi Ugenini- SMZ



Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imesema itawachukulia hatua wanafunzi wanaokwenda kusoma nje ya nchi kwa kulipiwa na serikali na kisha kufanya kazi katika nchi hizo kwa kwenda kinyume na sheria.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Ali Juma Shamhuna bodi ya mikopo ya elimu ya juu ya Zanzibar ina wadhamini wanafunzi 161, wanaosoma katika vyuo mbali mbali vya nje ya nchi vikiwemo Uganda, China, Ukraine, Malaysia na nchi yengine.

Alisema wanafunzi hayo wanalipwa ada ya masomo, gharama za mitihani, chakula, usafiri na bima ya matibabu ambapo kwa mujibu wa viza zao za wanafunzi hawatastahiki kufanya kazi na kama kuna wanaofanya kazi basi watachukuliwa hatua za kushitakiwa na kuadhibiwa.

Majibu hayo ameyatoa Shamhuna katika kikao cha baraza la wawakilishi kinachoendelea Mjini Unguja alipokuwa akijibu suali la msingi la Mwakilishi wa Jimbo la Muyuni (CCM) Jaku Hashim Ayoub, aliyetaka kujua ni hatua gani serikali inachukua kwa wanafunzi ambao wapo nje ya nchi na wana kilio cha muda mrefu cha kucheleweshewe fedha za masomo hali inayowalazimisha kufanya kazi za vibarua badala ya masomo.

Habari zaidi: Zanzibari Yetu