Tuesday 9 April 2013

Wanafunzi ni Kosa Kufanya Kazi Ugenini- SMZ



Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imesema itawachukulia hatua wanafunzi wanaokwenda kusoma nje ya nchi kwa kulipiwa na serikali na kisha kufanya kazi katika nchi hizo kwa kwenda kinyume na sheria.

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Ali Juma Shamhuna bodi ya mikopo ya elimu ya juu ya Zanzibar ina wadhamini wanafunzi 161, wanaosoma katika vyuo mbali mbali vya nje ya nchi vikiwemo Uganda, China, Ukraine, Malaysia na nchi yengine.

Alisema wanafunzi hayo wanalipwa ada ya masomo, gharama za mitihani, chakula, usafiri na bima ya matibabu ambapo kwa mujibu wa viza zao za wanafunzi hawatastahiki kufanya kazi na kama kuna wanaofanya kazi basi watachukuliwa hatua za kushitakiwa na kuadhibiwa.

Majibu hayo ameyatoa Shamhuna katika kikao cha baraza la wawakilishi kinachoendelea Mjini Unguja alipokuwa akijibu suali la msingi la Mwakilishi wa Jimbo la Muyuni (CCM) Jaku Hashim Ayoub, aliyetaka kujua ni hatua gani serikali inachukua kwa wanafunzi ambao wapo nje ya nchi na wana kilio cha muda mrefu cha kucheleweshewe fedha za masomo hali inayowalazimisha kufanya kazi za vibarua badala ya masomo.

Habari zaidi: Zanzibari Yetu

No comments: