Tuesday 7 May 2013

Jaa la Jang'ombe na Usalama wa Watoto...


Watoto hawa pichani walionekana katika jaa la Jang'ombe wakitupa taka. Jaa hilo lina kontena la kuhifadhia taka hata hivyo wakati watoto hawa wakitupa taka zao lilikuwa limefurika na kusababisha taka kutupwa nje ya kontena.

Mbaya zaidi watoto hawa hawakuwa na hata na viatu wakati wakitupa taka zao. Hii ni hatari kwa maisha yao na kiafya kwa ujumla. Itakuwa ni jambo la busara kwa wazazi kuhakikisha kuwa watoto wao wanapowatuma kwenda kutupa taka wawe wamevaa viatu.

Aidha kwa upande wa mamlaka husika ya ukusanyaji wa taka, hawana budi kuhakikisha sehemu za kutupia taka zinakuwa katika hali nzuri kila wakati ili kuweza kuzuia tatizo lolote ambalo litaweza kuokea kutokana na mirundiko ya takataka.


Picha kwa hisani ya Sabri Juma