Tuesday 23 July 2013

Unguja wakataa Serikali tatu...


Wajumbe wa Baraza la Katiba Wilaya Kaskazini (B) Unguja wameukataa Muundo wa Serikali tatu uliopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba Tanzania kwa madai kuwa utaliongezea taifa gharama zisizokuwa za lazima.

Wakizungumza wakati wa kutoa maoni yao kwenye rasimu ya Katiba, Wajumbe hao hamesema hawaoni haja wala ulazima wa kuwa kuliongezea taifa gharama hizo, wakati nchi bado ina mambo mengi yanayohitaji uwezeshwaji.

Abdallah Kombo Baraka kutoka shehia ya Zingwe zingwe akichangia alisema mfumo huo ambao ulipendekezwa na Tume haufai kwa sasa hivi Taifa lina mambo yakushuhulikia kuliko kuongeza jukumu lingine.

“Hivi sasa kupata huduma kume jaa urasimu halafu unaongeza Serikali ya tatu si hatari zaidi” alisema Baraka.

“Waheshimiwa hivi sasa uchumi wetu uko chini halafu tunataka kuongeza Serikali ya tatu njaa si itatisha jamani, mimi napendekeza muundo wa sasa uendelee” alisema Khamis Makame Mkombe akichangia katika Mkutano huo.

Alisema kuleta Muungano wa shirikisho ni njiia za kuua Mungano ambao umedumu kwa nusu karine.

Sambamba na hayo Salim Suleiman Ameir kutoka shehia ya Donge alisema Muundo wa serikali tatu si makubaliano ya Waasisi Abeid karume na Mwalimu Nyerere na kudai kuleta mfumo mpya ni kuvunja heshima yao.

“Tukiwa na Muungano wa shirikisho lazima kuwe na mkataba maalumu mmoja akiukiuka ndio Muungano ushavunjika uoo, kwa hiyo ni vyema tuendelee na mfumo wetu huu uliasisiwa na wazee wetu ili tupate radhi zao” alieleza Ameir.

Baadaye Mjumbe wa tume ya mabadiliko katiba Awadhi Ali Said alitoa ufafanuzi uliolenga kuelezea Serikali ziliopo Tanzania lakini wajumbe hao waliendelea na msimamo wao huo.



Mwananchi

No comments: