Friday 2 February 2018

Safari za Dr Shein nje ya nchi zinawakera nini jirani zetu?





Kila pale Dr Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar anapofanya safari nje ya nchi yake ya Zanzibar, lazima panuke kidudumtu. Hii ni mara ya pili mfululuzo Dr Shein amekuwa ziarani huku Zanzibar fitina nyengine imezuka. Hivi hizi fitna haziji wakati mwenye akiwa yupo hapa nchini!

Hivi karibuni Rais wa Jamhuri ya Muuungano, Dr John Pombe Magufuli kwa mamlaka aliyonayo amesimamisha usajili wa meli za nje, ambalo ni suala lililo chini ya mamlaka ya serikali ya mapinduzi (SMZ).

RaisMagufuli alimwita waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji wa Zanzibar na kumpa maagizo hayo ya kusitisha kama vile yeye Waziri Ali Karume anawajibika kwa Rais Magufuli. Ingawa Waziri Ali Karume ameteuliwa na Rais wa Zanzibar Dr Ali Mohamed Shein, lakini ndani ya katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kuna sura maalumu inayozungumzia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Hivyo kumfanya Rais Magufuli kutumia nguvu hii kunukisha kidudumtu.

Wakati Dr Shein yupo ziarani nchini Emirates, Rais Magufuli kachukuwa uamuzi wa kusitisha usajili wa meli za nje zinazofanywa na Zanzibar kupitia wakala wake. Huku Zanzibar ikiamini kuwa ni kuingiliwa kwenye anga za mamlaka yake, kwani usajili wa meli sio suala la Muungano. Kitendo hichi kimemchukiza sana Dr Shein na kutowa maelezo mara tu alipowasili uwanja wa ndege.

Dr Shein alisema “Sisi tulianzisha wenyewe Kampuni yetu ya Usajili wa Meli, Hili la kusajili Meli si jambo jipya, na nchi Duniani haya yanafanyika, Na mimi sidhani kama Zanzibar itazuiliwa kuregister, sidhani kama lipo hivyo, Mimi sijasikia hivyo, Mimi ninachojua kuna timu za Wizara za Serikali mbili zinazungumza na mazungumzo yatakavyo kwenda mimi nitayajua. Sidhani kama Zanzibar itaambiwa Isisajili”.

Katika mwezi wa March 2017 wakati Rais wa Zanzibar Dr Shein yupo ziarani nchini Indonesia, Rais Magufuli alitowa agizo kwa shirika la Tanesco kuikatia umeme Zanzibar kutokana na kutolipa madeni yake. Akijuwa fika kuwa suala la umeme linaendeshwa kisiasa pia ni suala la kibiashara baina ya kampuni mbili, Rais Magufuli hakuyazingatia hayo wakati wa kutoa kauli yake.

Rais Magufuli alisema “”ninaambiwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar haijalipa Sh121 billion. Ninyi (Tanesco) si wanasiasa…mnapaswa kuzingatia majukumu yenu ya kitaaluma…kata huduma ya umeme. Nimesema hata kama ni Ikulu, polisi, jeshi ama shule , hakuna mwenye deni anaepaswa kuachwa”

Amri hii iliwakera sio tu Dr Shein bali Wazanzibar wote kwa ujumla, kwani waliona ni udhalilishwaji uliopitiliza. Ikiwa nchi mbili zimeungana kwa umoja na upendo, wakati wa neema ziwe pamoja na wakati wa shida pia ziwe pamoja. Ilikuwa kinyume chake, wakati wa neema ni zetu sote lakini wakati wa shida ni zenu peke yenu.

Dr Shein alichukizwa na hatua ya kutishiwa kuzimiwa umeme na kusema hatishwi na vitisho vya TANESCO vya kuikatia umeme Zanzibar kwa sababu ya deni la Umeme kwani deni sio la leo, deni lina zaidi ya miaka 20. Alisema wote wanafahamu Zanzibar inadaiwa, na anaimani hamna anayeweza kuikatia umeme Zanzibar lakini kama wakitaka kukata wakate tu, tutawasha Vibatali.

Hapo ndio utaona picha kuwa Rais Magufuli kama anachukizwa na hizi ziara za Dr Shein anazofanya nje ya nchi. Inawezekana kuwa hapendelei Dr Shein asafiri kwa vile yeye mwenyewe amefuta safari za nje. Pia amepiga marufuku kwenda nje kiholela. Na yule atakayekwenda nje lazima apate kibali kutoka kwake. Inaweza, pia, hafurahii ziara za nje anazokwenda Dr Shein kwa vile ni zenyesura na maslahi kwa Zanzibar. Dr Shein anapokwenda nje ya nchi anakwenda kwa cheo cha Rais wa Zanzibar, hivyo haiwakilishi Tanzania hata aisemee.

Miongoni mwa sababu ambayo sitaki niipigie chapuo ni kukuwa na kuwepo tofauti baina ya viongozi wawili hawa tokea kabla na baada ya kumalizika uchaguzi wa viongozi wa ccm. Ikumbukwe marekebisho ya katiba ya chama yalipofanyika yalipitishwa na wote wakiyaridhia. Wakijuwa fika yanampa madaraka zaidi


Source: Jamii Forums

No comments: