Showing posts with label Zenj. Show all posts
Showing posts with label Zenj. Show all posts

Friday 19 March 2010

Pilika pilika za Ijumaa....


Kitoweo


Markiti


Dafu


Bar'za


Kujinafasi

Thursday 4 September 2008

Huu ni mwezi mgumu kwenda Zanzibar


Seagull ikishusha abiria hapo Zenj wakitokea Dar mwishoni mwa wiki iliyopita.


Sea Express ikushusha abiria tokea kisiwa cha pili


Msongamano wa abiria wa kwenda Zenj kabla ya mfungo wa Ramadhani katika bandari ya Dar.


Kwa wale ambao husafiri mara kwa mara kati ya Zenj na Dar au Zenj na Kisiwa Cha Pili watakubaliana nami kuwa sasa kwenye boti kuna viti vya kulala na ni tofauti kabisa na siku kadhaa zilizopita au kwa maneno mafupi kabla ya kuanza kwa mwezi wa Ramadhani. Kwa kawaida mwezi wa Ramadhani abiria wa boti na hata ndege hupungua sana kati ya Zenj-Dar na Pemba.

Sababu kubwa ya kupungua kwa wasafiri ipo wazi, kwani huu ni mwezi ambao wengi hufunga na hasa wakaazi wa visiwa hivi viwili, Hivyo wengi wao hawapendi kusafiri ili kuepuka adha ya kupata futari na misukosuko mingine ambayo inaweza kuwasababisha kufuturu kabla ya wakati. Zaidi waumini wengi utumia muda huu kuhudhuria sala zote za siku ili kukamilisha funga yenye uhakika na iliyokamilika.

Wageni ambao hupenda kufakamia kila wakati, nao ujiepusha kwenda Zenj ama Kisiwa cha Pili, kwani kuanzia mama lishe, migahawa na hoteli hufungwa hivyo kuwafanya kuwa katika hali ngumu sana ya kushawishi matumbo yao kuwa hakuna chakula asubuhi wala mchana... Hii uwakuta hata watalii ambao zaidi ya kukimbia kutofunga hata mavazi yao huwa hayana nafasi visiwani humo.

Hata hivyo, baada ya futari hakuna sehemu nyingine hapo Bongo ambayo unaweza kufaidi misosi ya nguvu kama Zenj... Kwani sehemu nyingi hufunguliwa na kuuza misosi ya nguvu hadi saa sita ya usiku. Maduka huwa wazi usiku na hata zile baa zinazojificha mchana na kuuza ulabu kwa mlango wa nyuma huwa wazi. Kwa ufupi Usiku huwa kunachangamka sana kuliko usiku wa miezi ya kawaida. Wengi ambao hawapendi kuamka alfajili kwa kuwahi daku hupenda kushindilia misosi hiyo hadi mishale ya saa sita na akilala inakuwa imetoka.