Wednesday 15 August 2007

Mbinu za Kizenj za Kusafirisha Mizigo...



Moja ya mambo niliyo yaona huko UK ni jinsi wazenj wanavyojitahidi kusafirisha malundo ya vitu vilivyotumika toka UK kwenda Zenj... Mazagazaga hayo ni kuanzia mafriji, mavideo(VHS), maprinter, mamonitor, makomputer, majiko ya umeme /gasi mabafu, vyoo, n.k.




Makontena ya size ya futi 40 ndio maalufu katika kusafirishia mazagazaga hayo.. ambayo mengine yapo katika hali mbaya sana kutumika zaidi ya kufaa kwa kutupwa tu.



Leo hii tuangalie jinsi ya kusafirisha magari matano katika kontena la futi 40......






















Wednesday 8 August 2007

Safarini Suomi...

Baada ya kuona Vituko kibao vya wazenj hapa Uk... takribani kwa miezi minne sasa, Nageuza safari na kurudi kijiweni huku nikiwa na rundo la vituko vya wazenj hapa uk... tokea wazungu wa unga, hadi vitangi, wasomi na wafanyabiashara, wazazi hadi wajane... ili mradi ni vituko kede kede.. nikipata nafasi nitakuwa nawapasha baadhi ya vituko vyao...

Thursday 14 June 2007

Mahakama Kuu ni Kimeo....

Nimewahi kuandika kuhusu mashaka makubwa ya mahakama za zenj katika mabandiko yaliyopita, leo hii kumeibuka kadhia nyingine ambayo hapana shaka ipo kwa muda mrefu tu huko zenj..

Imeripotiwa kuwa mahakama za zenj, hasa Mahakama Kuu haina majaji wa kutosha hivyo kukosa hadhi ya kuitwa Mahakama Kuu kwa mujibu wa katiba ya visiwa hivyo. Tatizo la Majaji huko visiwani lipo kwa muda mrefu sana, ingawa kuna wakati smz ilijitia kifua mbele kwa kukodisha majaji toka nje ya visiwa hivyo(Mapopo).

Kwa mwananchi wa kawaida hawezi kuamini kuwa Visiwa hivyo havina majaji, kwani wao mtu yoyote afanyae kazi mahakamani basi ni jaji, kama ilivyokuwa katika hospitali zao kwa wafanyakazi wote huitwa ni madokta.

Pengine ujuha huu wa kushindwa kutofautisha mgawanyiko wa ngazi za wafanyakazi, upo ndani ya vibosile wa SMZ kiasi cha kujisahau kuwa hawana Majaji wa kutosha kuendesha kesi lukuki katika Mahakama Kuu. Udhaifu wa mahakama za zenj na hasa katika watendaji wake umekuwa ni gumzo kubwa katika kipindi hiki, wakati kuna fufunu ya uteuzi wa Jaji Mkuu mpya wa Tanzania,

Ukiachana na hayo ambayo yanatia kichefuchefu, Mahakama ya Mkoa wa Mjini Magharibi ina Mahakimu watatu tu, ambao kwa maneno mengine ndio Mahakimu wa Mikoa yote ya Zanzibar! kwani sio siri kuwa sijawahi kusikia Hakimu wa Mikoa mengine minne wakitajwa, licha ya kesi walizohukumu kuripotiwa...! Hao Mahakimu wa wilaya wapo kwa hesabu ya vidole, na wengi wao wapo katika Mahakama za wilaya ya Mjini na ile ya Magharibi... Nasikia huko Pemba kuna mahakama ya Mkoa vilevile, hata hivyo Hakimu wake kutwa yupo Vuga!

SmZ kupitia kwa ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali wanapaswa kuja na suluhisho la kudumu kuhusu kadhia hii, na sio kila siku kuwa ni watetezi wa uchovu wa SMZ. Iwapo wao ndio wanasimamia Mahakama na sheria zake, basi hawana budi kuwa na mipango madhubuti ili kuona kuwa vyombo vya haki visiwani humu vimekamilika kwa mujibu wa sheria na katiba ya visiwa hivyo. Kitendo cha kuwaondoa Wapopo katika Mahakama zetu kilikuwa kizuri kwa manufaa ya watu na uchumi wetu unaodorola, aidha ipo haja basi ya ofisi hiyo kupanda Jahazi hadi bara ili kupata Majaji wenye kujua sheria zetu na maadali ya Mtanzania.

Friday 8 June 2007

'Ongezeko la Uzaaji UK' Wazenj Hawako Nyuma....

Imeripotiwa kuwa kumekuwepo na ongezeko kubwa la uzaaji hapa UK, ikiwa ni ongezeko kubwa kwa miaka 26. Ongezeko hilo la uzaaji, limechangiwa na wahamiaji miongoni mwao wakiwa ni wazenj.

Moja kati ya watoto watano wanaozaliwa hapa, amezaliwa na mhamiaji, hivyo kufanya ongezeko la asilimia kumi kwa mwaka kwa watoto wanaozaliwa na wahamiaji. Mwaka 2006 walizaliwa watoto 669,531 kwa wastani wa kila mzazi wa 1.87 huku wahamiaji wakizaa asilimia 21.9 ya watoto wote waliozaliwa mwaka 2006. Wahamiaji wengi ni kutoka nchi za ulaya ya mashariki, wengi wao wakiwa ni Wapoland. Zaidi kumekuwepo na ongezeko kubwa watoto toka kwa wanawake wa Pakistan, India, Afrika na Mashariki ya Kati. Wachunguzi wa mambo wanasema tokea mwaka 1997 (labour ilipoingia madarakani) kiasi cha wahamiaji milioni 1.5 wamehamia UK.[1]

Wanawake wengi toka Zenj hawapo nyuma katika suala la uzaaji, wengi wa wanawake hao ni kinamama wa nyumbani. Nilipojaribu kuulizia zaidi kuhusu uzaaji huo wa kasi, wengi wao walisema ni kutokana na mafao mazuri ambayo hutolewa na serikali ya hapa, hivyo kutokuwa na wasiwasi juu ya malezi na usomeshaji wa watoto hao tofauti na kama ingekuwa huko Zanzibar, ambapo jukumu lote lipo kwa mzazi pekee..!



1.Source: Daily Mail, June 8 2007.