Monday 5 November 2007

Safarini South Africa

Wapenzi wa kona hii, napenda kuwapa taarifa kuwa nitakuwa safarini South Africa kwa masuala ya kifamilia. Kwa wapenzi wa blog mliopo South napenda kupiga hodi rasni. Kwa muda wote ambao nitakuwepo South nitaendelea na blog hi kwa kuwapa Uhondo,visa na ujumbe wowote ule kuhusu zenj africa ya kusin,

Monday 15 October 2007

Leo ni Sikukuu Zenj (15/10/07)

Wananchi wa Zanzibar leo watendelea kuwepo mapumzikoni, katika kusherekea sikukuu ya Idd El Fitri. Hayo yalitangazwa na Mkurugenzi wa Idara ya Utumishi visiwani humo. Kwa kawaida sikukuu hii huwa na mapumziko ya siku mbili rasmi, hata hivyo mwaka huu iliangukia siku ya mapumziko, hivyo pengine SMZ wakaona ni vema na siku ya Jumatatu wananchi wake waendelee kufaidi kusherekea sikukuu.

Visiwani sikukuu za Idd husherekewa kwa muda wa siku nne mfululizo,ambapo siku mbili kati ya hizo huwa ni mapumziko rasmi, na zingine mbili husherekewa baada ya saa za kazi kwisha. Viwanja rasmi hutengwa na Halmashauri za miji kwa ajili ya watu kwenda huko kushereheka, karibu kila aina ya burudani huwepo katika viwanja hivyo. katika viwanja hivyo huwepo na maduka ya kuuza toys,vibanda vya vyakula, vibanda vya kupiga picha, vibanda vya tombola, vibanda vya taarabu, disco na uchekeshaji na vibanda vingine. Kwa Halmashauri hizo ni wakati mzuri wa kukusanya kodi kubwa katika kipindi kifupi zaidi cha ukusanyaji wa kodi. Aidha kwa wananchi ni wakati wa kutumia kwa nguvu katika kipindi kifupi.

Kwa wafanyakazi wa SMZ sherehe hizi hufana zaidi iwapo zitaangukia mwisho wa mwezi, kwani wengi wao hua na uhakika wa kupeleka familia zao katika viwanja hivyo kwa muda wote. Iwapo una familia, mke/wake na watoto, basi hupenda kuwa na nguo mpya kwa siku zote za sikukuu, pesa ya kwenda na kurudi na za kujichana wawepo viwanjani humo.. huku watoto ukiwa ndio wakati wao wa pekee kununua toys wazipendazo. Hivyo kwa mfanyakazi wa SMZ inabidi awe amejinyima sana ili kuweza kufurahisha familia yake.

Kujinyima kwa wafanyakazi hao si kitu rahisi sana kutokana na viwango vya mishahara na hali halisi ya maisha visiwani humo, hii husababisha wasiwe na mipango ya muda mrefu ya kujiandaa na sherehe hizo, zaidi ya kuomba Mungu sherehe hizo ziangukie karibu na mwisho wa mwezi.

Katika ile awamu ambayo wafanyakazi walikuwa wakilipwa mishahara yao katika siku ya arobaini, kulikuwepo na tabia ya wafanyakazi kulipwa nusu msharaha iwapo sikukuu itaangukia katikati ya mwezi. Hii iliwapunguzia machungu ya kusubiri mshahara wa siku ya arobaini na kuweza angalu kuvinjali na familia zao katika viwanja vya sikukuu. Hata hivyo wakati huu nusu mshahara haikutoka na zaidi leo wameambiwa kuwa wapumzike. Kwa upande wa wengi hii ni kero kwao. Iweje upumzike wakati huna hata senti mfukoni. Wengi wanaona bora wangeenda huko kwenye maofisi yao kufanya kazi kuliko kukaa nyumbani pasipo kuwa na kitu. Mbaya zaidi iwapo mfanyakazi ana akaunti ya katika Benki ya Watu wa Zanzibar(PBZ), ina maana kuwa leo hatoweza kutoa fedha zozote, kwani benki itakuwa imefungwa na PBZ hawana ATM...

Hivyo nina imani kuwa pamoja na nia nzuri ya SMZ, kuwapa wafanyakazi siku ya leo kuwa ya mapumziko, sio wengi ambao wamefurahia tangazo hilo. Zaidi limewaweka katika wakati mgumu wa kujibu maswali mengi toka kwenye familia zao.

Tuesday 9 October 2007

TANZANIA Food and Culture

Na Mwandishi Wetu

TANZANIA imepata fursa pekee miongoni mwa nchi za bara la Afrika, kushiriki Tamasha la Chakula litakalofanyika mwisho wa mwezi huu mjini Conwy, Wales.

Katika taarifa ya mratibu wa tamasha hilo la chakula, Gloria Mutahanamilwa, hiyo itakuwa fursa kwa Tanzania kujitangaza katika nyanja mbalimbali za utali, utamaduni, biashara, uchumi, kilimo, uvuvi na nyinginezo.

"Hili ni tamasha la chakula ambacho ni kitu kinachopewa umuhimu zaidi, lakini tutajumuisha mambo mengine mbalimbali kupitia tamasha hilo, kuna uwezekano wa kufungua njia kwa Tanzania katika kushirikiana na nchi nyingine kupitia nyanja tofauti" alisema mratibu huyo.

Katika tamasha hilo, ujumbe wa Tanzania wa watu takriban 25 pia utahusisha wacheza ngoma, wapiga muziki na wapishi.

Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mwanaidi Maajar anaunga mkono jitihada hizi na amethibitisha kuhudhuria tamasha litakaloonyesha vyakula, mapishi, utamaduni na vivutio pamoja na kutoa malelezo kuhusu Tanzania.

Tamasha hilo litafanyika katika mji wa kihistoria wa Conwy uliopo Wales kwa siku mbili yaani Oktoba 27 na 28, mwaka huu na inakadiriwa watu 20,000 toka kona mbalimbali za dunia watahudhuria kwani Conwy ni miongoni mwa miji mikuu ya kihistoria na kitalii.

"Ushiriki wa Tanzania ni wa kujitolea, wajumbe wote wanajitolea lakini bado kuna gharama nyingi ili Tanzania tuwakilishwe ipasavyo," alisema mratibu na kuhimiza watu binafsi na taasisi mbalimbali kuchangia na pia kushiriki.

Taarifa zaidi kuhusu TANZANIA Food and Culture zinapatikana kwenye tovuti yao kwa kubonyeza hapa au kwa kuwasiliana na wandaaji,
Tanzania Centre UK kwa barua pepe tanzaniacentre@hotmail.co.uk au
simu +447745891595.

Tuesday 2 October 2007

Lugha rasmi za SMZ



Hizo hapo juu ndio lugha rasmi zinazotambuliwa na SMZ hapa kisiwani Zanzibar.. Mpangilio unaoonekana hapo juu, ni kutokana na uhumimu wa lugha hizo katika SMZ na wananchi wake kwa ujumla..