Sunday 27 July 2008

Zenj imejaa tele Bara


Hivi karibuni nilitembelea katika Jiji la Mwanza na kubahatika kukutana na bango hili, nilijaribu bila mafanikio kuitafita ofisi hiyo ya Bima ambayo ni mojawapo wa Ofisi zinazojiendesha zenyewe visiwani Zenj. Hapana shaka pamoja na kero zinazozungumziwa Shirika hili linafaidi Muungano kwa kuweza kujitanua hadi Jijini Mwanza.

Pengine Mashirika makubwa huko Zenj, ukiondoa Shirika la magari ambalo limepigwa stop kwa namba zake za magari kutumika huko Bara zikafuata mfano wa Shirika la Bima. Asasi zingine ambazo zinaweza kujitatumua huko Bara ni kama asasi ya jeshi la kujenga uchumi, wao wanaweza kuingia katika masuala ya ulinzi, kwani ni soko ambalo linakuwa kwa kasi... Jamaa wa Zenj state engineering ambao pamoja na uwezo wa kujenga nyumba ndani ya siku saba wameendelea kudorora kama sio kufa kibudu kwa kukosa kazi huko zenji, wanayo nafasi nzuri ya kufufuka iwapo wataweza kufuata nyayo za Zantel na Shirika la Bima Zenj

Friday 8 February 2008

Lowassa Ajiwekea Rekodi Zake...



Siku ya jana imeingia katika kumbukumbu za serikali na maelfu ya wananchi wa Tz na wengine wenye uhusiano na Tz kwa namna moja ama nyingine.

Katika kuangalia angalia habari ya Lowassa nimekuja kufahamu kuwa ndie Waziri Mkuu wa kwanza kujiuzuru kutokana na tuhumu ambazo nimemgusa moja kwa moja tokea mwaka 1961. Hii ni rekodi kwake na rekodi ya kumbukumbu kwa viongozi wa ngazi za juu ambao kwa namna moja ama nyingine walijiuzuru, pasipo kuwa na tuhumu zinazowakuga wao Binafsi...

Kama vile haitoshi, Bw. Lowassa ameweka rekodi nyingine mpya ya kuwa kiongozi wa juu kabisa kujiuzuru huku akitizamwa na kusikilizwa na maelfu ya Watanzania kupitia Television ya Taifa (TVT). Rekodi nyingine ambayo ameiweka hapo jana ni kujiuzuru mbele ya Bi. Lowassa. Kwa ufupi Bw. Lowassa amejiwekea rekodi kama tatu hivi katika kipindi kifupi kabisa katika historia ya kujiuzuru kwa viongozi hapo Tz.

Mbaya zaidi, ni kuweka rekodi ya kiongozi wa kwanza kujiuzuru muda mfupi kabla ya ziara ya Prezedent Bush, ambaye anatoka huko kulikosababisha Bw. huyo kujiuzuru. Pichani hapo juu ni picha ambayo inaonyesha mapenzi yake na nchi ya Prez. Bush, ambapo sasa anaweza kumwona kwa kupanga foleni kama wananchi wa kawaida.

Sunday 20 January 2008

Friday 18 January 2008

Mambo ya Mapinduzi....


Tukiwa bado tunasheherekea Mapinduzi ya Zenj, nimeona bora leo tujikumbushe baadhi ya misukosuko ya wakati ule wa mapinduzi........