Tuesday 10 February 2009

Kichekesho kingine toka kwa Shamsi Vuai Nahodha



Mwishoni mwa mwezi Januari mwaka huu, Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi alinifanya nicheke kwa kauli yake ya kuamua kushika fagio na kuanza kufagia barabara za Zenj kutokana na barabara hizo kujaa michanga na vumbi kiasi cha kutojulikana kama ni za kiwango cha lami au la. Hii si mara ya kwanza kwa Mh. Nahodha kujitolea kusafisha Halmashauri ya Manispaa ya Zanzibar. Hata hivyo pamoja na juhudi zake hizo kwa Halmashauri hiyo ambayo kipindi fulani kupitia kwa Mkurugenzi wake Mr Mabrouk Makame Jabu ilikuwa ikidai kupewa hadhi ya Jiji(Sina hakika kama tayali ombi hili limeshakubaliwa)bado mji huo umeendelea kuwa mchafu.

Juhudi zote za Waziri Kiongozi zimekuwa na mafanikio ya muda mfupi, kwani huwa zinafanyika katika mtindo wa Operation ambao siku zote huwa hauna uendelevu wa aina yoyote, kwani operation inapokwisha shughuli nzima uwekwa kando na watu wakaendelea na shughuli zao zingine, huku wakisubiri kutokea kwa operation mpya. Watendaji wengi na hasa wa kimacha chini upenda aina hii ya utendaji kwani ndio wakati wao wa kuwa na kipato zaidi kutokana na overtime. Kwa Waziri Kiongozi ambae mara kwa mara amekuwa akisisitiza kuwepo na utendaji wa uendelevu katika shughuli za serikali, kilimo na biashara huku akiongoza kufanya operation za usafi ni kichekesho kitupu. Inakuaje unahutubia kila siku mambo ya uendelevu huku kazi unafanya za kizima moto kama sio vituko vitupu!

Moja ya barabara ambao siku zote huwa inajaa michanga na kusababisha vumbi la kuweza kusababisha chafya kila baada ya sekunde kadhaa, na hatari ya kupata kikohozi kikali ni barabara ya Benjamin Mkapa(zamani creek road). Barabara hii ndio inatenganisha Mji Mkongwe na Ng'ambo, ni moja ya barabara yenye pilika kubwa kabisa katika Zenj ikipitiwa na magari mengi zaidi, itumiwayo na wapanda baiskeli wengi zaidi na wapanda vespa,huku wakipigana vikumbo na mamia ya watembeao kwa miguu. Ndio barabara pekee visiwani humo yenye taa za kuongozea magari, kwa ufupi ndio barabara maarufu kabisa visiwani humo.

Kwa miaka nenda rudi barabara hiyo imekuwa ikifagiliwa pasipo kutakata na sasa naona imeshakuwa sugu, na kama hakuna mipango ya kuweza kujua ni kwa nini barabara hiyo haikosi vumbi licha ya kuwa ndio picha ya mji wa Zenj, kamwe haitokuja kuwa safi na ni wazi kuwa vumbi litaendelea kuwepo tu, licha ya ombi la watendaji wa Halmshauri hiyo kununuliwa gari la kufagia barabara hivi karibuni.


Barabara hiyo pamoja na kupita katika bustani za Mnazi Mmoja, Jamhuri, Donge na viwanja vya Malindi, haikupaswa kabisa kuwa na vumbi. Lakini kutokana na sababu za kutokuwa na mipangilio mizuri vumbi limeendelea kuwepo licha ya ufagiaji wa kila siku. Kitu cha kwanza ambacho kina kasoro kubwa katika barabara hiyo ni kukosekana kwa njia ya watembeao kwa miguu. Kama kungekuwa na njia hiyo ingetumika vile vile kama buffer ya kutenganisha barabara na sehemu zinazoingiza michanga barabarani na kusababisha vumbi. Aidha aina za kuegesha magari na hasa teski katika barabara hiyo unachangia kuingia kwa michanga barabarani, kuna maegesho ya magari ya mizigo na haya uegeshwa karibu kabisa na barabara hiyo, hivyo uchangia kuingia kwa michanga barabarani.Kwa upande mwingine Feeder road zinazo ingia katika barabara hiyo vile vile uchangia kuingiza michanga.

Ili kumfanya Waziri Kiongozi aendelee kufanya kazi zake za kawaida, badala ya kutafuta fagio, upo umuhimu wa lazima kuona kuwa barabara ya Benjamin Mkapa inafanyiwa mabadiliko makubwa ili kukidhi mahitaji ya watumiao barabara hiyo ambao ni maelfu. Kuna umuhimu wa kuweka njia kwa watembeao kwa miguu ambayo iwe inafanya kazi ya kuzuia kuingia kwa michanga katika barabara hiyo. Kuboresha maegesho ya teski na magari ya mizigo kama kituo cha daladala kilivyoboreshwa, kufanyia matengenezo feeder roads ambazo huingiza michanga kwa wingi na hasa wakati wa masika. Kuangalia tena eneo la Darajani kwani nalo linachangia sana katika uchafuzi wa barabara hiyo. Maeneo mengine kama Mkunazi,Donge, Ben Bella na Ofisi za Zec zinatakiwa kuangaliwa kwa vizuri zaidi.

Kwa utengenezaji wa njia ya wapita kwa miguu, Halmashauri ya Manispaa ya Zenj, inaweza kufanya kazi hiyo kwa kutumia mitambo yake mikubwa ya kutengeneza vigae, kwa kuweka vigae pembeni ya barabara hiyo. Hizo milioni 135,000,000 ambazo Manispaa wanahitaji kwa ununuzi wa mashine ya kusafisha barabara mnaweza kuwapa japo nusu yake ili waweze kutumia kwa utengenezaji wa vigae.

Friday 6 February 2009

Athari za Utalii kwa Mazingira ya Zanzibar




Moja ya masharti wanayopewa watalii mara waingiapo Zenj, ni juu ya uvaaji wa nguo ambazo hazistiri mwili mzima, yaani uvaaji wa suruali kipande, vichupi, ama kutembea vifua wazi ni sawa na kwenda uchi ndani ya Zenj. Hivyo watalii uambiwa wavae nguo zinazofunika mwili wote wakati wao wote watakapo kuwepo visiwani humo. Kwa watalii sharti hili ulipokea kwa shingo upande kwani wanapotoka ni sehemu za baridi na kwa muda mrefu wanakuwa wakivaa nuo nyingi kujikinga na baridi, na hivyo wanapotalii katika nchi za joto hupenda kuipa nafasi miili yao kufaidi joto hilo ambalo kwao ni adimu.

Hata hivyo linapokuja suala la ujenzi wa hoteli za kitalii Masharti na Taratibu zake hazijulikana kabisa, kwani vyombo vinavyosimamia ujenzi huo havina ushirikiano wa moja kwa moja na Idara ya Mazingira ambayo ipo kisheria kusimamia mazingira ya Visiwa hivyo chini ya sheria ya mwaka 1996.

Utalii katika visiwa vya Zanzibar sasa umeshapanuka sana na visiwa hivyo vimeshashuhudia mambo mengi yaliyokuja na utalii, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa hoteli nyingi za kitalii karibu kwa fukwe zote visiwani humo pamoja na visiwa vidogo dogo, ongezeko la wageni wahamiaji kwa ajili ya kazi za kitalii, ongezeko la uvuvi kwa ajili ya vyakula vya watalii, ongezeko la safari za anga na ardhini, ongezeko la maduka rasmi kwa ajili ya watalii na mambo mengine mengi yanayoendana na utalii kwa ujumla.

Mengi katika haya yalikuja pasipo kwa wenyeji wengi kujiandaa na sasa inakaribia miaka ishirini tokea mfumuko wa utalii visiwani kuanza, na kumekuwepo na malalamiko mengi toka ndani ya visiwa hivyo na nje ya visiwa hivyo kwa jinsi suala zima la utalii lilivyobadili mambo mengi visiwani humo. Wenyeji wengi wanalalamikia sehemu kubwa ya ajila kushikwa na wageni, ongezeko la bei kwa vyakula vya baharini, kupigwa marufuku kutembea ama kuvua katika baadhi ya hoteli hizo. Huku asasi za kimataifa zikipigia kelele uharibifu wa mazingira kutokana na aina za ujenzi wa baadhi za hoteli visiwani humo, uharibifu wa coral reef kutokana na uvuvi uliokithiri, kutokuwepo na miundo mbinu ya kutosha kwa ajili ya kuhifadhi maji taka na utupaji holela wa taka toka mahotelini humo.

Hadi kufikia mwaka 2003 takwimu za ZIPA zinaonyesha kuwa, jumla ya miradi 242 ilidhinishwa yenye thamani ya jumla ya dola za kimarekani milioni 403. Mwaka 2001 Zanzibar iliingiza dola za kimarekani milioni 46 kutokana na utalii pekee ikiwa ni asilimia 15 ya GDP. Makisio yanaonyesha kuwa kutakuwa na ongezeko la asilimia 21 la GDP kufikia mwaka 2012 na kufanya mgawanyo wa mapato kufikia million 116(makadirio haya yalifanyika kabla ya Global recessionya mwaka huu).

Ripoti ya maendeleo ya utalii ya Zanzibar iliyoandaliwa na na UNDP inaonyesha kuwa katika mwaka 1983 kulikuwa na sehemu kumi tu za malazi visiwani humo zenye vyumba 215 na jumla ya vitanda 467 ambazo hazikuwa kwenye daraja la aina yoyote(utalii au malazi ya wageni wa kawaida). Leo hii sekta ya utalii visiwani humo ina sehemu zaidi ya 180 za malazi, zenye zaidi ya vyumba 3160 na zaidi ya vitanda 6490.

Kufikia mwishoni mwa mwaka 2006, ripoti ya Umoja wa Mataifa(UN) ilionya kuwa Zanzibar imekuwa mojawapo ya nchi duniani inayoongoza kwa uchafuzi wa mazingira ya baharini kutokana na umwagaji wa maji taka katika bahari ya Hindi pamoja na uharibifu wa vyanzo vya maji. Mtafiti Stefan Gossling toka Sweden, yeye alionya kuwepo na uharibifu mkubwa wa coral reef kwa lengo la uuzaji wa viumbe vyake kwa watalii. Maeneo yenye uharibifu mkubwa wa mazingira kutokana na utalii visiwani humo ni ya Kaskazini na yale ya Mashariki.

Ukuaji wa utalii, licha ya kuendelea kuharibu mazingira umesababisha kuwepo na ushirikiano mdogo kati ya serikali na wananchi wake. Kwa upande wa mazingira wananchi wengi wanalalamikia hatua kadhaa za wenye hotel kuwanyima sehemu zao za uvuvi, ulimaji(seaweeds), minazi na hata kutembea karibu na hotel hizo. Mwaka 2002 wananchi wenye hasira katika kijiji cha Kendwa walichoma moto hoteli ya kitalii kwa madai ya hoteli hiyo kuharibu coral reef, tabia hii ilisambaa kwa baaadhi ya vijiji vya Nungwi.

Baadhi ya hotel( Fundu lagoon, Matemwe Bungalow, Blue Bay, Mnemba Island na Chumbe) zimeonyesha kujali athari ambazo zinatokana na ujenzi wa hoteli zao kwa mazingira. Wamejitahidi kufuata aina za ujenzi usio tumia resources kwa wingi, aidha wamejitahidi kufuata aina ya ujenzi wa nyumba za vijiji zinavyowazunguka. Hivyo kupunguza uharibifu wa maji safi na bahari.

Serikali kwa upande wake imeendelea kutoa vibali vya ujenzi pasi kuzingatia uharibifu wa mazingira au namna ya kujenga pasipo kuwepo na uharibifu wa mazingira. Hoteli zinaendelea kujengwa pasipo kuwepo na mfumo unaotambulika wa ukusanyaji na usafishaji wa maji taka, ukusanyaji na utupaji wa taka ngumu na utunzaji wa vyanzo vya maji. Aidha hakuna taratibu zozote ambazo zinatolewa kwa kutumia materials ambazo zinaendana na mazingira ya fukwe zinazojengwa.

Na kama kawaida yao, mambo yanapokwenda kombo, viongozi huja na amri kede kede. Nakumbuka miaka miwili iliyopita Mh. Mansour Yussuf Himid alinukuliwa akisema;
“Serikali imegundua ukiukwaji wa taratibu za utunzaji wa mazingira katika ukanda wa fukwe”
Aidha alikubali kuwa sekta ya utalii ndio inaongoza katika uchafuzi wa mazingira visiwani humo na kuzitaka Idara zinazohusika kujipanga kukabiliana na tatizo hilo hilo, huku Ofisi ya Mwanasheria Mkuu ikisema kuwa yeyote ambae atakiuka taratibu za Mazingira ataburuzwa mahakamani na kupigwa faini ya Sh million 2 ama kwenda Chuo cha Mafunzo kwa kipindi cha miezi sita.

Wednesday 4 February 2009

Child Custody after Divorce



In Tanzania, custody is governed by civil law, regardless of the type of marriage. The 1963 Law of Persons Act declared that children born inside marriage belonged to the father. However, the 1971 Marriage Act requires custody to be decided in the best interest of the child, but routinely defers to custom in individual cases. Prior to 1971, custody of Muslim children was administered under Islamic Law; however, the uniform codification of the Marriage Act included child custody regulations. Practically, if a woman files for custody, the father will not contest the motions. Here means that when woman open a case for custody father will not be able block the case. However, in absence of contestation, the father generally gets custody. Further, the Marriage Act provides that a father is responsible for maintenance of children until 18 years of age, regardless of custody
Custody patterns also vary depending on local lineage patterns. Among the matrilineal Muslims, the child belongs to his or her mother and her lineage, and remains with the mother in case of divorce, until age of 7; courts also directed to consider: customs of community to which parents belong; economic circumstances of both parents; housing that both parents can provide; and behaviour of mother and whether she contributed to marital breakdown If the mother dies, the child still remains with the members of the matriline and is usually maintained by a maternal uncle.

Looking to law governing marriage and divorce in Tanzania Act of 1971 (LMA) Section 125 of LMA provide for custody of children after divorce that may be granted either to the father or mother or any third party who is in position to provide for welfare of the children.
Section 126 provides for condition to custody order and section 127 provides for principle of welfare of child and in determining custody of children the welfare of the child is paramount and the court will grant custody to the one who is in better position to grant custody, however court always prefer before deciding on granting custody divorce parties to agree themselves to whom the child will leave with.

Welfare of the child including food, clothes, shelter, education, culture as well as good moral or attitude of the parent. So this is not only a matter of financial position of the parent.
Looking to the cases concerned the child custody after divorce in Tanzania based on the group focus, “why always mother have more right to be granted custody of child”. Here are examples which shows that even father can be granted custody of child

In case of Vestina Kibutu vs. Mbaya (1985) Tanzania Law Report (TLR) 42 custody was granted to the father because he was in the position to provide education and psychological development.
Another case of Re Steven Christopher Newborn (1975) TLR 24, courts in discussing welfare of the child takes into consideration social aspect and culture of divorcee. In this case spouses were English and divorced in Mwanza Tanzania. Mother decided to stay in Tanzania with her son Steven, Husband wanted to go England with his son. Court in its decision said it is better for father to go with his son England to be raised with English culture.

Monday 2 February 2009

Mapenzi ya Tanzania Bara na Zanzibar mashakani...


Wengi wetu siku hizi tunapenda kufananisha muungano wa Tanganyika na Zanzibar na ndoa ya watu wawili wapendano. Ndoa huja baada ya wawili walioshibana kuamua kuishi pamoja kwa muda wote wa maisha yao. Zipo aina kadha wa kadha za ndoa zote hizo huwa na lengo moja la kuunganisha wale wapendanao.

Mapenzi siku zote uzaliwa na kukua na hatimae kupevuka, siku zote mapenzi hukuzwa na wapendanao kwa kujaribu kuheshimu yale apendayo mwenza wake. Hii ni kwa kila upande na sio jukumu la mmoja tu ndani ya hayo mapenzi. Yapo mambo mengi ambayo ufanyika kwa lengo la kudumisha na kuendeleza mapenzi. Na haya yote hufanyika kwa moyo wa dhati ili mradi tu kuona penzi linakuwa kila siku.

Tofauti ndogo ndogo siku zote uwepo katika mapenzi, na wale ambao hupenda kuona mafanikio na kudumisha mapenzi yao hupenda kuzijadili tofauti hizo kungali mapema ili kuzuia tofauti hizo kuwa tatizo baina yao. Hii ni mojawapo ya vitu vya msingi sana katika ndoa zinazojali mapenzi.

Ndoa ya Tanzania Bara na Zanzibar sasa ipo kwa muda mrefu kiasi cha kusema kuwa imekomaa ila mapenzi katika ndoa hii muhimu yamekuwa yakipungua kila siku na katika spidi kubwa kiasi cha kuhatarisha ndoa yenyewe.Vitu vyote muhimu katika kukuza penzi zimewekwa kando badala yake chuki na kusingamana vimechukua nafasi.

Katika nyakati tofauti tumeshuhudia mambo kadha wa kadha yakifanyiwa marekebisho ili mradi kulienzi penzi na kudumisha ndoa, tokea wakati ule wa kusafiri kwa passport hadi kuongezwa kwa mambo kadhaa ndani ya ndoa hiyo. Hata hivyo kwa upande mmoja wa wanandoa hawa amekuwa akiburuzwa mno, mambo mengi amekuwa akinyang'anya tokea kuwa na sauti ya pili kwa ukuu ndani ya ndoa hiyo hadi sasa ambapo hana sauti yoyote, hata uhalali wake umeanza kuhojiwa, mbaya zaidi pamoja na kukubali kufutwa kwa kutumia karatasi baina ya nchi mbili hizi, inashangaza sana kuona kuwa makaratasi yameondolewa kwa binadamu tu.Iwapo una gari ukitokea upande wa Visiwani, gari hilo linabidi kuwa na karatasi ili liweze kutembea upande wa pili wa ndoa.

Kuna kero zingine zinachosha sana, na wala hazisaidii kurutubisha ndoa zaidi ya kuitia ubovu ambao mwisho wake ni kuvunjika tu.