Tuesday 12 January 2010

Rais Karume aupongeza Muafaka wake na Maalim Seif




Ni katika hotuba yake ya kuadhimisha miaka 46 ya Mapinduzi huko Pemba. Dondoo muhimu ya hotuba hiyo ni kama zifuatavyo:-

1. Amesema hatogombea tena kwa mujibu wa katiba.

2. Ameupongeza muafaka wake na Maalim Seif na kusifu matokea mema yake ya awali.

3. Ametumia lugha ya kistaaranu iliyojaa hekima na busara, huko nyuma zilikuwa ni mafumbo na vijembe.

4. Amezungumzia issue zote muhimu kwa mustakabali wa Zanzibar

5. Amezungumzia Muungano ni Dhima.

6. Ametoa hakikisho la Uchaguri huru na wa haki.

7. Wenye sifa wote, wataandikishwa. ZEK itapitisha tena uandikishaji upya.

8. Wote wenye sifa za kupata ZID, watapatiwa na wote wenye ZID walionywima kwenda kuzichukua, wakazichukue.

9. Kwa ujasiri mkubwa na lugha ya kistaarabu sana, ameyaomba gesi na mafuta yao, yawe yao, kama ilivyo bara na dhahabu yetu.

10. Amemsifu sana Rais Kikwete, na kumalizia kwa ile ile kauli Adhimu "Mapinduzi Daima".

Chanzo: Jamii Forums

Miaka 46 Gizani




Leo ni sikukuu ya Mapinduzi ambapo yanatimiza miaka 46, tofauti na miaka iliyopita sherehe za mwaka huu zinafanyika gizani. Katika kusherekea sherehe hizo kitaifa zitafanyika kule kwenye matatizo ya muda mrefu ya giza na action za kelele za jenereta.
Kila la heri katika kusherekea mapinduzi

Mapinduzi Daima

Saturday 2 January 2010

Mapacha Walioungana Wazaliwa Zenji...

Mwanamke mmoja mkazi wa Zanzibar, Farihati Maulid (18) amejifungua watoto pacha wa kiume walioungana.

Mwanamke huyo alijifungua kwa njia ya upasuaji katika Hospitali ya Mnazi Mmoja jana saa tatu asubuhi na mapacha hao wako katika chumba cha uangalizi maalumu.

Mkunga wa hospitali hiyo, Halima Habiba Abdallah, na Dk. Mwana Omar ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Uzazi, wakizungumza kwa nyakati tofauti, walisema tukio hilo ni la kwanza kwa muda mrefu katika hospitali hiyo wanaendelea kupata ushauri kutoka kwa wataalamu wengine wa afya.

Pacha hao wana moyo mmoja, na wameunganika kuanzia kwenye kitovu hadi kwenye mfupa wa kidari.

“Tunasubiri wataalamu kufanya uchunguzi zaidi, lakini kwa sababu wana moyo mmoja na wana uzito wa kilo 2.8 itakuwa ngumu kuwatenganisha na kupona, haijulikani ni viungo gani vingine kila mmoja anavyo vya peke yake,” alisema Dk. Omari.

Habari zaidi zinasema mama wa watoto hao ni mkazi wa Mwanyanya, Bububu katika Manispaa ya Zanzibar na mimba hiyo ilikuwa ya kwanza.

Friday 1 January 2010

Zenjiflava: Mtandao Mpya.....




Mtandao mpya umefunguliwa kwa ajili ya kuleta habari tofauti (muziki, matukio, mitindo, utamaduni, burudani na kadhalika) kutoka Zanzibar na Pemba. www.zenjiflava.com

Kwa wale ambao wanataka kutuma habari zao zinazohusu Zanzibar na Pemba ili ziwekwe kwenye mtandao, naomba mtumie barua pepe hizi: info@zenjiflava.com au zenjiflava@hotmail.com

Kwa wale ambao wanataka kupiga soga (online chat) huku mkicheki habari mbalimbali kwenye tovuti basi mnabidi mjiunge kwanza. Mkiangalia kwenye mtandao, hapo juu kulia mtaona majina ya watu mbalimbali waliojiunga ambao wako LIVE wanapiga soga, ukigonga katika jina basi utaweza kuongea nao.