Wednesday 23 February 2011

Mamma Mia...



Mustafa Hassanali kuhamasisha uzazi salama nchini Tanzania

Maonyesho ya bure ya kwanza ya mavazi kufanyika tarehe 5 Machi

Fedha zaidi zahitajika toka serikalini kupunguza vifo vinavyotokana na uzazi


Yale maonyesho ya mavazi yajulikanayo kama ‘mamma mia’ yenye nia ya kuhamasisha uzazi salama, sambamba na sherehe za miaka 50 ya uhuru Tanzania, na miaka mia moja ya siku ya mwanamke duniani , kwa kushirikiana na shiriki lisilo la kiserikali la utepe mweupe ‘White Ribbon Alliance’ na ‘Vodacom Foundation’, yazinduliwa rasmi.

Akizungumza katika uzinduzi huo, mbunifu wa mavazi, aliyejipatia umaarufu kitaifa na kimataifa, Mustafa Hassanali amesema “ntazindua toleo langu jipya la ki-afrika katika maonyesho haya ya ‘Mamma Mia’ siku ya tarehe 4 na tano mwezi Machi hapahapa jijini Dar es salaam, na nategemea kupata ushirikiano wa watu wote, katika kuhamasisha uzazi salama kwa msaada wa shirika la utepe mweupe”

‘Mamma Mia’ ni jukwaa la maonyesho ya mavazi ambalo limelengwa mahsusi katika kusambaza ujumbe kuhusu uzazi salama, litafanyika tarehe nne mwezi machi, katika hoteli ya ‘Moevenpick Royal Palm’ kuanzia saa mbili na nusu usiku, na onyesho jingine kwa siku ya Jumamosi ya tarehe tano kuanzia saa tisa na nusu jioni, katika viwanja vya Mnazi Mmoja.

“nimefurahi sana kuwa wa kwanza kuandaa onyesho la mavazi la bure nchini kwa siku ya tarehe tano, ambalo madhumuni yake sio tu kuhamasisha uzazi salama, bali pia kuifanya tasnia ya ubunifu wa mavazi na mitindo iweze kufikiwa na wengi pale katika viwanja vya Mnazi Mmoja.” Alieleza Hassanali

Akizungumza kuhusu ‘Mamma Mia’ ni jina lililotokana na wimbo uliovuma sana katika miaka ya 80 na kundi la ‘ABBA’, ambapo mia inasimama kuiwakilisha sarafu ya shilingi mia , na miaka mia moja ya ya siku ya mwanamke duniani, Mustafa anaongeza kuwa, “kwa kila atakae kuja kuangalia shoo, atatoa shilingi mia moja, si kwa maana nyingine bali ni kama mchango wake katika kuhamasisha uzazi salama nchini”

Akiongezea katika suala zima la uzazi salama, mratibu wa Taifa wa Muungano wa jumuiya ya utepe mweupe na uzazi salama nchini, Bi Rose Mlay amesema kuwa, toka mwaka 2004, wamekuwa mstari wa mbali katika kuhamasisha and kuiomba serikali kuongeza fungu katika bajeti ya sekta ya afya na uuguzi, ili kupunguza vifo vitokanavyo na matatizo ya uzazi.

“mpaka sasa, ni asilimia 51 tu ya wanawake wote Tanzania , ndio wanaojifungua chini ya usimamizi na kusaidiwa na wataalamu wa afya, na sababu kuu ya hili ni upungufu wa vifaa na wafanyakazi wa afya katika sekta ya uzazi kwa mikoa mingi ya pembezoni mwa Tanzania, hii sio nzuri na Haikubaliki, kwani kila mwanamke ana haki ya kujifungua salama chini ya wataalamu wa afya. Na ndio maana tunahamasisha uzazi salama.”aliongezea kusema Mama Mlay.

Msukumo wa hili hautawezekana bila ushirikiano kutoka watu na mashirika mbalimbali, ambapo Mamma mia kwa ushirikiano na shirika la utepe mweupe ( White Ribbon Alliance) pamoja na ‘Vodacom Foundation’ ikiwa na baadhi ya waliojitolea kusaidia hili ni pamoja na ‘Johns Hopkins Centre for Communication Programs in Tanzania’, The Citizen, ‘Uhuru one’, ‘Moevenpick Royal Palm Hotel’, Novamedia, Ultimate Security, Darling Hair na Image Masters.

Wabunifu wengine watakaoshiriki katika kampeni hizi ni pamoja na mshindi wa tuzo za ubunifu kutoka Zanzibar Farouque Abdella, Henrietta Ludgate na Minna Hepbum wote toka ‘London Fashion Week’, Uingereza.


Nukuu kwa Mhariri:

KUHUSU MUSTAFA HASSANALI

Mustafa Hassanali ni mbunifu mjasiriamali anaeamini katika ‘daima sitashindwa’ huku akitumia kipaji chake na ubunifu wake wa mavazi katika kuleta maisha bora ya sasa na ya baadae.

Kazi za mbunifu Mustafa zimekuwa zikithaminika na kuonyeshwa kimataifa, ambapo Mustafa alifanikiwa kuonyesha ubunifu wake katika nchi kama Angola ‘Angola Fashion Business’, FAFA (Festival of African Fashion and Arts in Kenya), Kameruni, Wiki ya Mitindo India 2009, Naomi Campbell’s fashion for relief 2009, Arise Africa Fashion Week 2009, Wiki ya mavazi Durban & Cape town, Vukani Fashion Awards Pretoria, Miss Ethiopia Beauty Pageant, Mediterranean Fashion Festival, Sicily, Italia, M’net Face of Africa, Msumbiji, Uganda, na Wiki ya Mitindo Kenya, ambayo kwa pamoja yamemletea heshima kubwa, ndani na nje ya nchi.



KUHUSU SHIRIKA LA UTEPE MWEUPE
Ni shirika la kimataifa lisilo la kiserikali, lenye nia ya kuleta mabadiliko katika suala zima la uzazi salama, kati ya mama na mtoto duniani kote.

Katika jamii nyingine, rangi nyeupe ina maana ya majonzi, na jamii nyingine, nyeupe in maana ya matumaini na uhai, hivyo basi utepe mweupe umetwaliwa kama kumbukumbu kwa wanawake wote waliofariki kwa mimba , na katika harakati za kujifungua.
Toka ilipoanzishwa mwaka 1999, shirika la utepe mweupe limekuwa likikuwa kwa kasi duniani kote, hadi kufikia kuwa na nchi wanachama 148 ambao wanapaza sauti zao kwa ajili ya wanawake na jamii zao kwa ujumla. Ambapo kwa sasa linaongoza katika kuyakabili majanga yanayotokana na vifo vya uzazi.

KUHUSU MUSTAFA HASSANALI NA SHIRIKA LA UTEPE MWEUPE.

Mustafa Hassanali, ni mbunifu wa mavazi anayeshirikiana kwa karibu sana na shirika hili, ambapo kwa pamoja waliwahi kufanya onyesho na Naomi Campbell lililofahamika kama ‘Naomi Cambpell’s fashion for Relief’ mwaka 2009, ambapo zilokusanywa kiasi cha dola 65,000.

Mustafa Hassanali, mwenye shahada ya udaktari, anaamini kwa moyo mkunjufu kabisa katika kutumia mitindo kama njia yakusaidia kuchangisha fedha, na kusambaza ujumbe wa masuala ya afya kwa jamii yote.

Kwa maelezo zaidi tembelea www.mustafahassanali.net

Tuesday 22 February 2011

Prince William ashauriwa kwenda honeymoon yake Zanzibar...

Zanzibar's New Star of the East Hotel Is Fit for a Royal Honeymoon

While Prince Wills and Princess-to-be Kate Middleton are rumored to be spending their honeymoon in Isles of Scilly, we can't help thinking the royal couple should maybe pull a switcheroo and shack up at the newly opened Star of the East on Zanzibar.

The Tanzania hotel would provide a paparazzi-free zone. It only offers 11 villas, and each has its own private plunge pool, Jacuzzi, personal butler, ginormous furnished terrace and lush garden full vegetation, from which the newlyweds will be able to watch the sunset and get all romantic.

Plus, the all-inclusive hotel offers a private beach where the couple can frolic without getting bothered by stalker fans. Though we think we could spend the entire time chillaxing in the terrace (see picture). And though it's a small, exclusive resort, there's a spa, the Mvua African Rain Spa, where the lovebirds can get some post-nuptial pampering.

The villas, two of which are two-bedroom spaces, have a traditional hut shape with retaining walls made of local stone and coral rock. They also are eco-friendly, sporting solar panels and using an irrigation system where outgoing water is used to irrigate the gardens instead of wasted.

Rooms start at around 635 Euros, or $868 a night. A two-week stay there would definitely require a royal-sized budget.


Hotelchatter

Sunday 20 February 2011

Mchungaji wa Kimarekani wa Kanisa la Anglikan kwenda Zanzibar


The Rev. Jerry Kramer, the Episcopal priest who threw his church into the recovery of Broadmoor after Hurricane Katrina, has left the church for a more conservative Anglican community.

Kramer, the former rector of the Free Church of the Annunciation, said by e-mail he now is affiliated with the Anglican Church in North America.

That community is composed of former Episcopalians who split with the U.S. church in 2008 over deep theological differences.

Kramer is now a member of an Anglican community in New Braunfels, Texas, with his wife and three children.

He said he is awaiting training before moving to Zanzibar, off the coast of Tanzania in east Africa, to do missionary work in a predominantly Muslim region.

Kramer left New Orleans in 2009 on a medical disability. He said he was physically and psychologically exhausted, suffering from difficult-to-manage diabetes, heart and liver problems.

After Katrina ruined his church, Kramer and his congregation put off rebuilding.

Instead, they opened the campus to the needs of Broadmoor residents, who received food, washed their clothes, got health care and used trailers on the site to house the offices of the Broadmoor Improvement Association, which planned the recovery of the devastated neighborhood.

Kramer's gifts fit the moment. Hyperactive and inventive, he spun off ministries and blew up established conventions in pursuing the work, almost erasing the distinctions between the church and the surrounding community.

In other ways, however, he was deeply orthodox.

He was increasingly ill at ease with changes in the Episcopal church's theology, particularly what critics saw as its diminution of the authority of Scripture and its increasing openness to faithful, same-sex relationships.

Those were the changes that caused the rift between the Episcopal church and those who left to form the Anglican Church in North America. That body, which says it has 100,000 members in nearly 1,000 congregations, now seeks to become a recognized member of the worldwide Anglican Communion.

From Texas, Kramer said the Epsicopal church "simply no longer believes what Christian have always believed."

He said the Anglican community he is now affiliated with "is in the process of replacing (the Episcopal Church) as the authentic expression of Anglicanism in the Americas."

Kramer said his Type 2 diabetes is now "completely cured," and he is medically cleared to resume work.


nola.com

Saturday 19 February 2011

Washington state sells 2 ferries to Tanzania

The state finally has sold two of its discarded passenger-only ferries, the Kalama and the Skagit, to the African nation Tanzania.




The ferries have been docked and inactive since September 2009. The Legislature ordered the state to get out of the passenger-only ferry business in '06.

The two ferries had been sold to a boat broker in Port Coquitlam, B.C., which sold them to Tanzania. They will be put in service between the mainland of Tanzania and the Zanzibar archipelago. They were sold for $400,000 combined, far below the $900,000 value the state said they were worth in December 2009.

Marta Coursey, spokeswoman for Washington State Ferries, said the two boats will be taken to Africa by cargo ship.

The state had hoped to sell the two 112-foot boats locally, but when that failed, it placed them for auction on eBay, asking $300,000 each, with no success. The ferries were built in New Orleans and purchased in 1989 for $5 million.

Ferry historian Steve Pickens said the Kalama and the Skagit were the first two passenger-only boats the state built. They were supposed to go into service in 1989 but were tied up because there was no money to run them. Following the Loma Prieta earthquake of 1989, the two vessels were sent to San Francisco and served commuters crossing the bay while the city's bridges were repaired.


TST