Thursday 13 February 2014

Makaburi ya Wakristo Mwanakwerekwe Yapo Hatarini Kutoweka....



Kumekuwepo na hujuma za makusudi za kuharibu eneo rasmi la makaburi ya kuzikia Wakristo wa Zanzibar, liliopo Mwanakwerekwe katika Wilaya ya Magharibi, Mkoa wa Mjini/Magharibi.

Ni muda mrefu sasa kumekuwepo na vitendo vya ovyo kabisa vinavyofanyika katika eneo la makaburi hayo. Vitendo hivyo sio rahisi kuviona vikifanyika katika maeneo ya makaburi ya dini zingine ambazo makaburi yao yamepakana na haya ya Wakristo.

Kama inavyoonekana kwenye picha hapo juu, kuna hujuma za kulifanya eneo hilo kama Jaa la taka, kuna watu kwa makusudi kabisa wameligeuza eneo hilo kama sehemu ya kucimbia mchanga kwa ajili ya ujenzi wa nyumba zao.

Aidha vijana na watoto wanaoishi karibu na makaburi hayo, wao wameona eneo hilo linafaa zaidi kwa kuchezea mpira, huku waakazi wengine waishio karibu wameligeuza eneo hilo kuwa barabara ya kupitishia vipando vyao juu ya makaburi, huu ni utaarabu wa pekee ambao unaweza kuonekana Zanzibar pekee hapa duniani.

Kama vile haitoshi, wapo waliogeuza makaburi hayo kama sehemu ya kupata materials kwa shughuli zao za ujenzi, ambapo ubomoa zege katika misalaba na mifuniko ya makaburi ili kupata nondo, kumegua vigae (tiles) au kuchomoa misalaba ya mbao. Zaidi sio ajabu kukutana na mifugo ikuchungwa makaburini hapo.

Wakati huu udhalilishaji wa maeneo ya makaburi ya Wakristo ukizidi kuota mizizi na kuonekana kama ni jambo la kawaida serikali imeendelea kukaa kimya tofauti na hatua wanazochukua kwa makaburi ya Waislamu.

Mwishoni mwa mwezi wa kwanza, kupitia kwenye Baraza la Wawakilishi, serikali ilisema kuwa imepanga kulitumia eneo la Kama liliopo Wilaya ya Magharibi kwa ajili ya kuzikia watu.

Mpango huo unachukuliwa kutokana na eneo la makaburi ya Waislamu yaliyopo Mwanakwerekwe kuelekea kujaa. Hata hivyo Wawakilishi hawakuwa tayali kuzungumzia udhalilishwaji na hujuma zinazofanyika katika eneo la makaburi ya Wakristo ambalo lipo jirani tu na hayo yalioadiliwa.

Upofu na ukiziwi wa serikali juu ya yale yanayoendela katika makaburi hayo, ni moja ya sababu kubwa inayowatia kiburi baadhi ya watu ambao wameamua kuyahujumu makaburi hayo ya Wakristo.

Ni vema kwa serikali kutokimbilia kutafuta maeneo mapya kabla ya kudhibiti maeneo yanayo endelea kutumika. Kwani kwa kufanya hivyo bado hawatokuwa wametatua tatizo lilipo kwenye jamii.

Ikumbukwe kuwa hatua ya kutafuta eneo jipya la Kama, imetokana na kumwegwa na kubadilishwa kwa matumizi ya eneo la makaburi ya Waislamu, ambalo awali lilikuwa na ukubwa wa hekta 80 za mraba na sasa linakaribia kuwa na hekta 25 za mraba.

Kwa upande wa Wakristo wa Unguja mjini, ipo haja ya kuendelea na wazo lililotolewa na waumini wenzetu juu ya kulizungushia ukuta eneo hilo. Viongozi wa madhehebu yote yanayotumia eneo hilo itakuwa ni jambo la msingi iwapo mtakutana na kupanga namna ya kuweza kujenga uzio ili kuifadhi makaburi hayo na eneo lililobaki.

Ni jukumu letu kwa kiasi fulani kulilinda eneo hilo pasipo kutegemea sana serikali. Hii itasaidia kulitunza eneo hilo kwa muda mrefu. Tunaweza kuangalia na kuiga mfano wa Makaburi ya Wajerumani ya pale Mwembemadema, ambayo yamedumu kwa zaidi ya miaka 150, na tunaweza vilevile kuangalia jinsi makaburi yanavyoweza kuvamiwa kama ilivotokea kwa makaburi ya Wakatoliki hapo hapo Mwembemadema, ambapo baadhi ya watu walianza kuzika kabla ya kutiwa uzio.

Kisheria, maeneo ya makaburi yamekuwa na utata mwingi. Hakuna sheria rasmi juu ya udhibiti na utunzaji wa maeneo ya makaburi, zaidi ya ile iliyotungwa baada ya Mapinduzi ikitoa uhuru wa kubadili matumizi ya makaburi baada ya kupita miaka 40. Mfano wa karibu juu ya sheria hii ni pale ilipotumika katika makaburi ya kariakoo.

Sunday 9 February 2014

Matokeo ya Uchaguzi Kiembesamaki: CUF Watafute Sababu Nyingine Mpya.



Kama ilivyo ada kila baada ya uchaguzi, vyama vishiriki vimekuwa vikitoa maoni yao juu ya mwenendo mzima wa uchaguzi kuanzia wakati wa kampeni hadi upigaji kura. Maoni ya vyama vya siasa hivyo ni juu ya ushiriki wao na namna uchaguzi ulivyokwenda halikadhalika kujipima kufanikiwa kwao ama kutofanikiwa kwao katika chaguzi husika.

Mapema mwezi huu kulifanyika uchaguzi mdogo wa kuchagua mwakilishi mpya katika Jimbo la Kiembesamaki huko Unguja, ambapo chama cha CCM kilishinda uchaguzi huo kwa kupata asilimia 76 na mgombea wake Bw. Mahmuod Thabit Kombo kutangazwa mshindi.

Chama cha CUF ambacho ndio chama kikubwa cha upinzani visiwani humo kiliambulia asilimia 18, ikiwa ni asilimia ndogo sana kulinganisha na umaarufu wake na kukubaliwa kwake visiwani humo. Hii inatoa picha mbaya kwa wafuasi wa chama hicho na inatia kichefuchefu kwa uongozi wa chama hicho. Ikumbukwe kuwa chama hicho baada ya kutoridhisha na matokea mengi ya uchaguzi visiwani humo ilifikia hatua ya kutoitambua serikali na kususia shughuli zote za kiserikali ikiwa ni pamoja na ushiriki katika Baraza la Wawakilishi.

Kwa kifupi kila mtu anajua miafaka iliyokuwa ikiundwa kila baada ya chaguzi kutokana na chama cha CUF, kupinga matokeo ya uchaguzi. Hatima ya miafaka hii ilipelekea kuanzishwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa baada ya maafikiano na chama cha CCM.

Moja ya sababu kubwa ambayo imekuwa ikisikika tokea kurudi kwa mfumo wa vyama vingi nchini, ni ile ya uchaguzi kutokuwa huru na wa haki pamoja na kuporwa kwa demokrasia visiwani humo na chama cha CCM, zaidi lawama kwa Tume ya Uchaguzi. Sababu hizi zimekuwa zikirudiwa rudiwa kila baada ya uchaguzi na hasa katika matokeo ambayo chama cha CUF ikishindwa. Pale wanaposhinda hamna sababu hizi.

Baada ya maridhiano na kuja kwa serikali ya umoja wa kitaifa, wengi wetu tulitegemea kutosikia tena sababu hizi kutoka katika chama hicho, kwani sasa nao ni waundaji wa serikali ambayo hapo awali walikuwa wakiilalamikia. Kitendo cha katibu mkuu wa CUF Bw. Maalim Seif Hamad na Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Mawasiliano ya Umma wa CUF, Bw. Salim Bimani kuibuka kupinga matokeo ya uchaguzi mdogo wa Kiembesamaki kwa kauli zilezile za miaka nenda rudi kinatia shaka na kinatoa maswali mengi miongoni mwetu.

Akiwa huko Pemba Bw. Seif Sharif Hamad, amerudia kauli zake za kudai kuwa uchaguzi haukuwa huru na serikali hiyo hiyo anayoifanyia kazi imehujumu uchaguzi huo kwa kupandikiza mamluki wakati wa upigaji wa kura.

Alisema "Kama kuna wananchi wa Kiembesamaki waliokwenda kupiga kura basi hawazidi elfu moja, wengi walichukuliwa katika maeneo tafauti, kama vile Makunduchi, Mtende, Kitope na Bumbwini na wakapelekwa kupiga kura huku wakilindwa na vikosi vya serikali".

Nae Bw. Bimani alisema "Chama cha CUF kilibaini tokea mapema maandalizi ya fujo na matumizi mabaya ya nguvu za dola pamoa na vikosi vya serikali, ambavyo viliandaliwa kwa dhamira ya makusudi ya kuwapa haki waisostahiki na pia kuwanyima watu wengi haki yao ya kufanya maamuzi ya demokrasia".

Kauli hizi toka kwa viongozi hawa zinatia shaka juu ya ukweli wa malalamiko ya chama hiki kabla na baada ya kuja kwa serikali ya umoja wa kitaifa. Ni kauli ambazo zimeshazoeleka sana katika masikio ya wananchi wengi visiwani humo na nchini Tanzania kwa ujumla. Sina budi kujiuliza ni nini mafanikio ya CUF kuwepo katika serikali ilhali bado wanaendelea kuilalamikia serikali hiyo hiyo. Ni nini faida iliyopatikana kwa kuwepo na maridhiano iwapo kero ya ulalamishi wa hujuma katika chaguzi ipo pale pale?

Kwa upande mwingine nashindwa kuelewa kama viongozi hao wameshindwa kuona impact iliyotokea baada ya kuja kwa serikali ya umoja wa kitaifa kwa wanachama na wapenzi na wapiga kura wao. Je bado wanachama wao wanaona kuna umuhimu wa kushiriki katika chaguzi ambapo matokeo yake hayatoweza kubadili nafasi ya chama hicho katika kuendesha serikali? Ni kwa kiwango gani chama hiki kina maamuzi katika kuendesha serikali ya maridhiano?

Ukiangalia vyama vingine ambavyo havipo kwenye serikali ya umoja wa kitaifa kama vile TADEA, ADS, SAU na kadhalika, wao wameyapokea matokeo haya kwa mikono miwili na zaidi wameendelea kuangalia kama kumekuwepo na mafanikio katika kushii na kukubaliwa na wananchi kupitia matokeo hayo. Zaidi wameonyesha kutokuwepo na hujuma yoyote wakati wote wa uchaguzi huo tofauti na madai yaliyozoeleka ya CUF.

Bw. Ali Mohamed Ali Mwenyekiti wa TADEA amekiri kutokuwepo kwa mamluki waliopata kupia kura katika vituo vyote vya uchaguzi huo, aidha waliopiga kura ni wananchi wa Kiembesamaki. Nini nafasi ya kauli ya Bw. Hamad hapa? TADEA ni mojawapo ya vyama vilivyoshiriki chaguzi zote visiwani humo tokea kuja kwa mfumo wa vyama vingi.

Ni vema kwa wakati huu chama cha CUF, kikajiangalia upya juu ya ushawishi wake kwa wanachama wake na nafasi yake kama chama kikubwa cha upinzani visiwani humo badala ya kuja na kauli rahisi rahisi kama hizi. Muda wa kufanya hivyo wanao na ni mwingi. Zaidi wapime nafasi yao serikalini na hatima ya chama chao.

Friday 7 February 2014

Is Tanzania the Next Target for Radical Islam?



Bishops of Kondou on Coexisting, Ministering in Peace

ROME, February 06, 2014 (Zenit.org) - Bishop Bernadin Francis Mfumbusa heads the almost three-year-old Diocese of Kondou, in the heart of Tanzania, one of 34 dioceses that serve a Catholic population of some 9 million, 20% of the population. Another 10% are Protestants of various denominations. Animists account for 35% of the population and Muslims another 35%, the majority of them Sunnis. The various faiths have lived peacefully side by side for many generations, but in recent years some worrisome signs are pointing at the emergence of extremist Islam.

Bishop Mfumbusa spoke to international Catholic charity Aid to the Church in Need on Monday about the future of Tanzania.

Q: You recently returned from celebrations of the 150th anniversary of the arrival of the faith on Zanzibar, where Muslims make up nearly the entire population. But the joy of the occasion was tempered by a growing radicalization of Islam on the island, and four attacks on the Church and its people in the last two years-most recently the brutal attack on a local priest with acid, which left the man severely burned. What can you tell us of the threat of extremist Islam in Zanzibar?

Bishop Mfumbusa: The threat of extremist Islam in Zanzibar should be understood in a specific context. One, the problem of Christian-Muslim tension in Zanzibar is not new. Some Muslims claim ownership of the archipelago saying Islam is the religion of Zanzibar. Two, radicalization of a certain segment of the population in Zanzibar is part of a worldwide trend. It should not be seen in isolation. Three, there is a political dimension to religious tensions, as some people and groups portraythemselves as defenders of Zanzibari values, namely, Islamic values and principles. Still, the vast majority of people in Zanzibar would prefer to live in peace as extremism poses a danger to the entire society-not only to Christians.

Q: Do you have concerns for such Jihadists elements causing trouble on the mainland?

Bishop Mfumbusa: The possibility of trouble in Mainland Tanzania is as real as it is in London or New York or elsewhere. Last year a Catholic church was bombed in Arusha, and the culprits are still at large. We read in the news recently that some Al Shabaab (Somalia-based militants) elements were spotted in Tanga, one of the major coastal towns. The greatest danger at the moment is the infiltration of foreign Jihadis and the return of Tanzanian radicals who have received training outside the country.

Q: Do you perceive a larger threat then to Tanzania, just as extremist Muslims have worked their way into Mali, Nigeria, the Central African Republic and elsewhere? What forces are behind this import of radical Islam?

Bishop Mfumbusa: Tanzania has a large Muslim population estimated at 35%. A group known as Uamsho in Kiswahili (or "awakening") is inciting violence, especially in Zanzibar. Pamphlets with specific messages against Christians and Christian institutions have been recovered. On the Mainland at least one radio station was banned because of inciting sectarian violence. Funding for these activities appears to come from abroad as the streets are awash with audio and videocassettes encouraging Muslims to harm kafirs (non-Muslims).

Q: What is happening to the peaceful Islam that has been characteristic of Africa for so long? Do you dialogue with moderate Muslim leaders? Are moderate Islamic leaders outspoken enough in denouncing anti-Christian violence?

Bishop Mfumbusa: A prominent Ugandan scholar, Mahmoud Mamdani, wrote a book titled, "Good Muslim, Bad Muslim," in which, among other things, he warned of the danger of oversimplifying issues. There is an extremist fringe, it is true, but the vast majority of Muslims are peaceful. In Kondoa where I live more than 90% of people are Muslims. About 80% of my own family are Muslims, and so far we are living together fine. The major problem is external influence, which brings with it new interpretations and even usages of Islam.

Tensions are evident, and signs of radicalization are increasing, but the Christian leadership stays in touch with Muslim leaders. Whether the so-called moderate Muslim leaders denounce anti-Christian violence is a moot question. Muslim leaders who appear to side with Christian themselves fall victims to extremist violence, as was the case last year in Zanzibar. Naturally, there is a fear to speak out among moderate Muslims. Unfortunately, this only emboldens the extremists.

Q:How do you explain the hatred of some Muslims for Christians and their faith?

Bishop Mfumbusa: Some Muslim scholars suggest that Islam is the original religion of Africa. This is far from true. Islam came to North Africa in the 7th century through conquest; and made its way to East Africa with Arab traders. Hatred of Christians by Muslims can be traced to a totalitarian tendency to expunge all non-Muslims. That is what happened in North Africa in the early days of Islam

Some Muslim leaders claim that Muslims are marginalized by Christians. That is how the justify interventions, like the recent one in the Central African Republic by Seleka Muslim rebels who made their forays under the pretext of protecting Muslims. Christians are scapegoats for all that is wrong among the Muslim populace-and the demagogues use such arguments to work up people into hatred.

Q: What are your arguments in helping Christians themselves from turning to violence out of revenge?

Bishop Mfumbusa: Whenever I get an opportunity I remind people of Tolstoy, who held that there is an oft- forgotten verse in the Bible, namely, Matthew 5:39, where Jesus is telling his disciples: "don't resist evil." Our best hope is forgiveness. We cannot solve evil by doing evil. As best as we can, we must learn to "not resist evil." But as the situation in the Central African Republic has made clear, it can be hard to control people after a certain point.

Q: How can the Church help build bridges between Christians and Muslims?

Bishop Mfumbusa: Inter-religious dialogue in Tanzania is going on at different levels. At the national level there is a multi-faith committee, which brings together leaders from all religions. Even here in my diocese Kondoa there is a committee trying to address inter-religious problems. Also the church welcomes all people to make use of its institutions such as schools, universities, hospitals, etc.

Q: Have you personally been confronted with evil?

Bishop Mfumbusa: Evil is part of human life, and no one can escape it. It is easier to hear of horrors of war, hatred, hunger and so forth when such things are happening in far off countries. Personally I have experienced tragedy when Father Ambroce Mkenda was shot and gravely wounded on Christmas Eve 2012. His crime, apparently, was to be a Catholic priest on Zanzibar. I know him well, as we were in the seminary together in the late 1980s. Indeed, as some say, man is wolf to man.

Q: How do you cope with the loneliness of the life of a pastor-particularly that of a bishop?

Bishop Mfumbusa: I remember when I was elected bishop of Kondoa a fellow bishop told me that loneliness would be now part of my life. To some extent this is true. I have to make difficult decisions alone. Often I live alone as we have only a handful of priests. Luckily, in Africa, most people are part of a large extended family, so people do drop in to greet me all the time. Generally, there are no official appointments and there is a steady flow of visitors- so there is no time to be lonely, really! There is also the consolation of prayer, knowing that the Lord is always near, even when we feel lonely for some reason.

Q: Does the Church in Tanzania see a growth in vocations?

Bishop Mfumbusa: At the moment, we have more than 500 seminarians doing philosophy and theology in five seminaries run by the Tanzanian bishops' conference. There has been an uptick in the number of seminarians. Generally, the number of seminarians tends to ebb and flow over the years. We need to commission a study to find out why more young men have been drawn to the priesthood lately.

Q: What do you think are the particular gifts of African Catholicism-and can they benefit the Church in the West?

Bishop Mfumbusa: I think one of the greatest gifts of Tanzanian Catholicism is unity. Despite ethnic, regional and other differences, the faithful, for example, accept pastors and bishop from other parts of the country or from other ethnic groups without a problem. Another gift which can be emulated elsewhere are our "Small Christian Communities," which have become a strong embodiment and expression of the local Church in our country.

Q: What is the biggest challenge for you personally in 2014?

Bishop Mfumbusa: The biggest challenge is the limited number of priests. Here in my diocese, there are only 13 priests working in 11 parishes. And there is a potential-a need-to open six new parishes immediately. We simply don't have the personnel. For example, my secretary doubles as the parish priest of the cathedral parish. It can be overwhelming.

Q: And what are the main challenges for the new year for the Church in Tanzania-family life, catechism, formation of priests and religious?

Bishop Mfumbusa: The greatest challenges lie in the area of priestly formation and religious education. Developments in the secular education sector are outpacing our capacity to provide religious formation for students. For example, there are now secondary schools in many villages, yet we don't have enough catechists to teach at this level. We need to improve the capacity of our catechists and lay ministers. In the area of priestly formtion the main problem is lack of books, as well as a limited information and communication infrastructure in our seminaries.

Q: Pope Francis stresses the need for the Church-indeed, the world at large-to care for the poor. In what ways is the Diocese of Kondoa serving the poor, the sick and the marginalized?
Bishop Mfumbusa: We have an orphanage with more 70 children, most of whom were abandoned. We care for them irrespective of their religion or ethnicity. The local Church also operates a health center and a few dispensaries in some of the remotest areas in the district. We would wish to do more but limited human resources hamper our efforts.

---

Source:EWTN.com

Monday 3 February 2014

Matokeo ya Uchaguzi Mdogo Kiembesamaki



Jumla ya kura zilizopigwa 2458.
CCM imepata kura 1856 sawa na 76.5%
CUF kura 445 sawa na 18.3%
CHADEMA kimeambulia kura 84 ikiwa ni sawa na 3.5%.

Hivyo basi mwakilishi mpya wa Kiembesamaki ni Mh.Mahmuod Thabit Kombo pichani hapo juu.