Wednesday, 18 May 2016
Monday, 16 May 2016
Maalim Seif Awasha Moto Upya Zanzibar

Maalim Seif Awasha Moto Upya Zanzibar.....Awataka Wananchi Wasilipe Kodi na Waandae Siku ya Mgomo.
Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, amewasha moto upya visiwani Zanzibar kwa kuwahimiza wananchi kufanya vitendo vinavyoonyesha kuikataa serikali inyoongozwa na Rais wa Zanzibar Dr. Ali Mohamed Shein
Maalim aliyasema hayo jana alipokuwa akizungumza na watendaji na viongozi wa CUF kutoka Wilaya ya Micheweni katika Mkoa wa Kaskazini Pemba ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku tano hapa.
‘Tukikazana, serikali hii itaondoka, ikiwa mnangoja Maalim Seif au Marekani kuiondoa, kwa sheria ya kimataifa haitawezekana kwani Marekani haiwezi kuingilia mambo ya ndani ya Zanzibar,” aliongeza Maalim Seif, ambaye alijitoa kwenye uchaguzi wa marudio wa Zanzibar uliofanyika Machi 20, mwaka huu na Dk Ali Mohamed Shein kuibuka mshindi.
Uchaguzi wa marudio wa Zanzibar ulifanyika baada ya Tume ya Uchaguzi ya huko kufuta matokeo ya uchaguzi uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana.
Hata hivyo, Maalim Seif alisema Serikali ya CCM imeanza kutikisika kutokana na vikwazo vinavyoendelea kuwekwa na wahisani pamoja na hatua ya chama chake CUF kutowatambua viongozi wake pamoja na serikali.
“CCM wajue wamekalia kuti kavu, siku yoyote wataanguka...tufanye kazi mpaka haki yetu tuhakikishe imerudi na wenzetu hawana safari ya kudumu,” alisema Maalim Seif.
Aidha, alisema Mataifa ya Ulaya zikiwamo Marekani, Uingereza, Norway pamoja na Umoja wa Ulaya, yameanza kuchukua hatua za kuinyima misaada ya maendeleo Tanzania ikiwamo Zanzibar kutokana na mgogoro wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka jana.
Alisema wahisani hao pamoja na Shirika la Changamoto la Milenia (MCC) wamesema hawatotoa msaada mpaka suala la uchaguzi la Zanzibar likae sawa na kupatiwa muafaka wake.
Maalim Seif aliwataka wanachama wake kuonyesha kwa vitendo vya kweli vya kutoitambua serikali ikiwamo kukataa kulipishwa kodi za ovyo vyo pamoja na kujitenga na viongozi wa serikali katika utekelezaji wa majukumu yao.
"Mfano tunaweza kuamua siku flani kuanzia saa sita, tunasimamisha vyombo vyote vya usafiri na siku nyingine tunaamua kupiga honi Zanzibar nzima kuonyesha hatuitaki serikali ya CCM" Alisema Maalim Seif huku akishangiliwa na umati uliofurika katika ofisi za chama hicho.
"Wanasema ukitaka kumshinda adui unampiga akiwa dhaifu na udhaifu wao hawana fedha, na ili kuwadhibiti ni kuwanyima fedha na kuwachokoza kwa kuwaita majina mabaya kama dikteta, Nduli," alisema.
Kuhusu suala la wakulima kuuzia serikali karafuu au kutoiuzia, alisema wananchi wenyewe ndiyo watakaoamua, lakini lengo la CUF ni kuona Serikali ya CCM inashindwa kuongoza Zanzibar kabla ya kumalizika miaka mitano.
Kwa mujibu wa Maalim Seif, tayari hali mbaya ya kiuchumi imeanza kujitokeza Zanzibar kutokana na bajeti ya mwaka huu kupoteza miradi mingi ya maendeleo kwa ufinyu wa fedha.
Kuhusu vitendo vya uvunjaji wa haki za binadamu, Maalim Seif alisema tayari yupo mwanasheria mzalendo ambaye ameanza kukusanya vielelezo mbalimbali kabla ya kufungua kesi katika Mahakama ya Kimataifa dhidi ya viongozi wenye dhamana ya kusimamia vyombo vya ulinzi na usalama wa raia.
Alisema tayari Waziri wa Mambo ya Ndani, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Muungano, wamepewa notisi ya kuarifiwa kufunguliwa mashtaka katika Mahakama ya Kimataifa kutokana na vitendo vya uvunjwaji wa haki za binadamu uliofanyika Zanzibar.
Alisema kwa sasa wanasheria wanapitia sheria kwa umakini za kuanzishwa kwa mahakama hiyo ya kimataifa ili kuangalia uwezekano wa serikali ya Zanzibar kufunguliwa mashtaka katika mahakama hiyo.
Wakati wa ziara hiyo, Maalim Seif alipata wakati mgumu kutokana na barabara kufungwa na wafuasi wake wakimtaka atoe kauli juu ya hali ya kisiasa ya Zanzibar.
Posted by
Kibunango
at
16:48
0
comments
Thursday, 31 March 2016
Nyumba inauzwa Maungani - Zanzibar
Nyumba inauzwa ipo Maungani, ina vyumba 4 na vyoo 3. ni ya kisasa na ipo katika hali nzuri. Pia ipo ndani ya uzio.
Kuna banda la mtumishi au housegirl ambalo lina chumba na choo jiko na stoo.
Bei ni shs 95,000,000
Kwa maelezo zaidi au kuiona piga simu namba 0777275551. ulizia nd. Khalid
Posted by
Kibunango
at
15:19
0
comments
Monday, 21 March 2016
Dkt Shein Ashinda Uchaguzi Zanzibar

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar nd.Jecha Salum Jecha amemtangaza Dkt Ali Mohamed Shein kuwa Rais Mteule wa Zanzibar kwa kura 299,982 sawa na 91.04% ya kura zote zilizopigwa.
Kwa ushindi huo anayefuata kwa matokeo hayo ni Hamad Rashid ambaye amepata kura 9734 sawa na 3%.
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar, ametangaza matokeo hayo kama ifuatavyo.
1 Khamis Iddi Lila ACT-Wazalendo kura 1225 sawa na 0.4%
2 Juma Ali Khatib ADA-TADEA kura1525 sawa na 0.5%
3 Hamad Rashid Mohamed ADC kura 9734 sawa na 3%
4 Said Soud Said AFP kura 1303 sawa na 0.4%
5 Ali Khatib Ali CCK kura 1980 sawa na 0.6/
6 Ali Mohamed Shein CCM kura 299,982 sawa na 91.04%
7 Mohammed Massoud Rashid CHAUMMA kura 495 sawa na 0.2%
8 Seif Sharif Hamad CUF kura 676 sawa na 1.9%
9 Taibu Mussa Juma DM kura 210 sawa na 0.1%
10 Abdalla Kombo Khamis DP kura 512 sawa na 0.2%
11 Kassim Bakar Aly JAHAZI kura 1470 sawa na 0.4%
12 Seif Ali Iddi NRA kura 266 sawa na 0.1%
13.Issa Mohammed Zonga SAU kura 2018 sawa na 0.6%
14 Hafidh Hassan Suleiman TLP kura 1499 0.5%
Aidha Mwenyekiti wa Tume hiyo amesisitiza kwamba wagombea wote 14 walishiriki uchaguzi huo na hakuna aliyejitoa kama vyama vilivyotangaza kwa sababu hawakufuata sheria ya uchaguzi iliyowataka kujitoa siku ya kutangazwa kushiriki uchaguzi ambayo ilikuwa ni tarehe 06.09 2015.
Posted by
Kibunango
at
18:17
0
comments
Saturday, 5 March 2016
Zanzibar Poll Will Be Successful - Samia

The government remains committed in ensuring that the elections in Zanzibar are conducted and concluded well later this month.
Vice-President, Ms Samia Suluhu Hassan made the remarks yesterday in Dar es Salaam when officiating at the 9th Inter-Parliamentary Relations Seminar known as Nanyuki IX Series.
"During the forthcoming Zanzibar elections citizens should comply with all set election laws, guidelines and principles," said the VP. She praised the selection of the theme "Compliance with African Union and Sub-Regional Blocs' Election Benchmarks: the case of the EAC" as being timely.
Through the seminar, the East African Legislative Assembly (EALA) has taken a strong resolve to appropriately remind governments, electoral management bodies and all stakeholders engaged in electoral process to conduct polls in transparent manner while upholding the declaration of results.
"The issue of credible election in Africa and the attendant sub-regional bodies and the smooth transfer of power is one that cannot and must never be wished away.
Source:Daily News
Posted by
Kibunango
at
13:36
0
comments
Sunday, 7 February 2016
Mazombi Zanzibar....
Kumekuwepo na watu wanaojifunika soksi kichwani ambao kwa muda sasa wamekuwa wakipiga watu kwa kutumia silaha za aina mbalimbali katika mji wa Unguja. Watu hao wanajulikana kama Mazombi.
Kupitia kwa Kamishna wa Polisi Zanzibar, Jeshi la Polisini Visiwani humo linasema, halina taarifa za kuwepo kwa Mazombi...
Habari zaidi ingia hapa
Posted by
Kibunango
at
14:22
0
comments
Friday, 25 September 2015
Mch. Mtikila na Maoni Yake Juu ya Tafiti zilizofanywa na Twaweza na Synovate...
MIJADALA - SEPT.25.2015 | STAR TVMwenyekiti wa DP azungumzia tafiti zilizofanywa na SYNOVATE pamoja na TWAWEZA juu ya nani ana nafasi ya kushinda uraisi katika uchaguzi mkuu.
Posted by Simu.TV on Friday, 25 September 2015
Posted by
Kibunango
at
17:14
0
comments
Saturday, 19 September 2015
ILANI YA CCM KWA AJILI YA UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2015 - UTANGULIZI
Utangulizi
1. Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 wa kuwachagua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais wa Zanzibar, Wabunge, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Madiwani imeandaliwa ikiwa ni mkataba kati ya CCM na wananchi. Ilani hii imeandikwa kwa kuzingatia Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2025 na Mwelekeo wa Sera za CCM zenye lengo na nia ya kuendelea kuwatumikia wananchi kwa kipindi cha miaka mitano ijayo (2015-2020).
2. Ilani hii ni tamko maalumu kwa wapiga kura kuhusu nia ya CCM ya kuendelea kushika dola na kuwaongoza Watanzania kwa njia ya kidemokrasia, na hasa kuendelea kudumisha amani, umoja wa Kitaifa, usawa, ustawi wa wananchi, Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kwa kipindi kingine cha miaka mitano.
3. Nia na uwezo wa CCM wa kuendelea kuongoza Taifa hili unajidhihirisha katika uzoefu ambao tumeupata kwa miaka 38 tangu kuanzishwa kwake na kuwa madarakani, ambapo katika kipindi chote hiki kimeiwezesha nchi yetu kupata mafanikio makubwa katika nyanja za kiuchumi, kisiasa na kijamii.
4. Katika miaka mitano ijayo (2015-2020), CCM ikiwa madarakani, itazielekeza Serikali zake kutumia nguvu zake zote kuendelea kupambana na changamoto kubwa nne:-
Kwanza kuondoa umaskini; pili kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira hasa kwa vijana; tatu kuendeleza vita dhidi ya adui rushwa na ubadhirifu wa mali ya umma; na nne kuendelea kudumisha amani, ulinzi na usalama wa maisha ya wananchi na
mali zao.
Kupambana na Umasikini
5. Pamoja na mafanikio ya kukua kwa uchumi na ongezeko la huduma za kijamii yaliyopatikana katika kipindi hiki, bado ipo changamoto kubwa ya umasikini wa kipato na usio wa kipato. Takwimu zinaonesha kwamba asilimia 28.2 ya Watanzania ni masikini. Wengi wa wananchi hao wanaishi vijijini (asilimia 75) na wanategemea kilimo katika maisha yao. Wapo pia wananchi masikini wanaoishi mijini ambao wanaendesha maisha yao kupitia shughuli za biashara ndogo ndogo zisizo rasmi.
6. Katika kupambana na changamoto hii, CCM itazielekeza Serikali zake kuboresha
maisha ya wananchi wote na hususan wa vijijini, kwa kuchukua hatua zifuatazo:-
(a) Kuhamasisha kilimo kupitia kauli mbiu ya Kilimo Kwanza kwa kuwawezesha wakulima kupata mafunzo ya kilimo cha kisasa, pembejeo, zana za kisasa na wataalamu wa ugani pamoja na mbinu za kuyafikia masoko ya uhakika ya mazao yao;
(b) Kuongeza kasi ya kupima ardhi yao na kuwapatia hati miliki za kimila ambazo watazitumia kama dhamana ya kuwawezesha kupata mikopo ya kuendeleza shughuli zao za kilimo, ufugaji na uvuvi;
(c) Kuendeleza juhudi za kuimarisha huduma za kijamii ikiwemo elimu, afya, maji, umeme na ujenzi wa nyumba bora; na
(d) Kuongeza kasi ya kurasimisha biashara na kuwapatia wafanyabiashara wadogo maeneo ya kufanyia biashara, leseni na fursa za kupata mikopo yenye masharti
nafuu.
7. Mafanikio ya utekelezaji wa masuala haya yote kwa pamoja yanatarajiwa kuleta mabadiliko makubwa ya kimaendeleo mijini na vijinini, na hivyo kupunguza kwa kiwango kikubwa hali ya umasikini nchini.
Ajira kwa Vijana
8. Suala la ukosefu wa ajira kwa vijana ni moja ya changamoto zinazolikabili Taifa letu na dunia yote kwa ujumla. Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita yapo mafanikio yaliyopatikana katika kuongeza ajira. Hata hivyo, mafanikio katika upanuzi wa elimu ya Sekondari na Vyuo yameongeza mahitaji ya ajira ya vijana wasomi kila mwaka ikilinganishwa na nafasi zinazokuwepo.
9. Katika kipindi cha miaka mitano ijayo jitihada za kulipatia ufumbuzi tatizo la ajira nchini zitaendelezwa. Kipaumbele kitakuwa katika kukuza na kuanzisha viwanda vidogo, vya kati na vikubwa vilivyo na uwezo wa kuajiri watu wengi na vyenye kuzalisha bidhaa zinazotumiwa na watu wengi wa ndani ya nchi na zile za kuuza nchi za nje. Aidha, kwa upande wa Tanzania Zanzibar, mikakati ya kuongeza ajira kwa vijana itazingatia mazingira maalamu ya fursa za uchumi wa visiwa.
10. Katika kipindi cha 2015-2020, sekta za uzalishaji mali kama kilimo, ufugaji, uvuvi, viwanda vikubwa na vidogo na huduma za kiuchumi kama vile miundombinu ya nishati, uchukuzi na ujenzi zitaelekeza mipango yao katika kupunguza umasikini na kuanzisha ajira hususan kwa vijana. Aidha, huduma za jamii za elimu, afya na maji
zitajielekeza kusaidia kuondoa umasikini na kuongeza ajira.
Vita dhidi ya Rushwa
11. Jitihada za kuinua uchumi na kuongeza huduma za jamii hazitaleta manufaa kwa wananchi na kuondoa umasikini iwapo adui rushwa ataendelea kulitafuna Taifa letu.
Rushwa ni adui wa haki pia ni adui wa maendeleo na ustawi wa wananchi, hivyo ni moja ya changamoto kubwa inayoikabili nchi yetu na dunia kwa ujumla.
12. Katika kipindi cha miaka mitano ijayo, CCM itazielekeza Serikali zake kuendeleza mapambano dhidi ya adui rushwa kwa nguvu zake zote na kuendelea kuziba mianya ya rushwa katika taasisi za umma; kuchukua hatua kali na za haraka kwa wale wote watakaobainika kuendeleza rushwa Serikalini na katika sekta binafsi; na kuimarisha
vyombo na taasisi zinazohusika na kuzuia na kupambana na rushwa; ikiwa ni pamoja na kuanzisha Mahakama Maalumu kwa ajili ya makosa ya rushwa na uhujumu uchumi.
13. Sambamba na kupambana na tatizo la rushwa, Serikali pia zitatakiwa kushughulikia kwa ukali zaidi tatizo la ubadhirifu na wizi wa mali ya umma, matumizi mabaya ya madaraka, ukiukwaji wa maadili ya uongozi na utumishi wa umma, kuchelewesha kutoa maamuzi yenye maslahi kwa umma na kusimamia uwajibikaji katika kutekeleza masuala yenye maslahi kwa umma.
Ulinzi na Usalama
14. Nchi yetu imepata mafanikio makubwa ya kuwa na amani na utulivu tangu tupate uhuru mwaka 1961 na Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964. Imekuwa kimbilio la watu wa Mataifa ya jirani kila wapatapo matatizo ya uvunjifu wa amani katika nchi zao. Hata hivyo, siku za karibuni vimeanza kuonekana viashiria vinavyoleta hofu ya usalama wa wananchi, hasa vitendo vya mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino), kuuawa kwa vikongwe, ukatili dhidi ya wanawake na watoto na tishio la vitendo vyenye mwelekeo wa kigaidi.
15. Katika kipindi cha miaka mitano ijayo, CCM itazielekeza Serikali zake kuendelea kuimarisha vyombo vyote vya ulinzi na usalama kwa kuviongezea raslimali fedha, raslimali watu, maslahi, zana za kisasa na mafunzo. Aidha, elimu kwa umma itatolewa ili kukomesha imani potofu za kishirikina zinazosababisha mauaji ya albino na vikongwe na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wale wote watakaobainika kujihusisha na vitendo vya mauaji ya makundi hayo.
Utekelezaji wa Ilani
16. Kazi kubwa ya Serikali za CCM katika kipindi cha miaka mitano ijayo itakuwa ni kuendeleza mapambano dhidi ya umasikini, ukosefu wa ajira, rushwa; na kudumisha umoja, amani, ulinzi na usalama. Ili kutimiza azma hiyo, CCM itazielekeza Serikali zake zisiwe kubwa, zenye watumishi weledi, waadilifu na wawajibikaji. Serikali zisizo na urasimu unaokwamisha na kuchelewesha maamuzi na utekelezaji. Serikali zitakazongeza maradufu au hata zaidi ukusanyaji wa mapato yake ili zijitegemee kadri inavyowezekana kwenye bajeti zake.
17. Vile vile katika kipindi cha Ilani hii, Chama Cha Mapinduzi kitaziagiza Serikali zake kuendeleza na kuimarisha mfumo wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN na BRP) katika kutekeleza Ilani na kusimamia utekelezaji wa miradi ya kimkakati na kipaumbele unaozingatia nidhamu ya utekelezaji katika muda uliopangwa, ufuatiliaji makini na wa kina, pamoja na kupata ufumbuzi wa vikwazo na changamoto za utekelezaji.
#HapaKaziTu
Posted by
Kibunango
at
11:22
0
comments
Tuesday, 17 February 2015
Kendwa Rock Beach Hotel Yaungua Moto
Chanzo cha moto:Hitilafu ya umeme.
Jengo lilioungua ni la Jiko, Duka na Sehemu ya burudani.
Hasara iliyosababishwa na moto huo, inakisiwa kuwa ni Shilingi bilioni moja.
Picha na OMPR
Posted by
Kibunango
at
02:42
1 comments
Zanzibar Is Safe, German Leader Prove It.
Germans have had very interesting relations with Zanzibar. They were here on commercial terms and with counsellor representation before Berlin Conference and occupation of Tanganyika. Almost all their explorers took off for the interior Africa using Zanzibar as their launch pad and least one forget the issue of Heligoland Island that put the two sides on international level when the Sultanate was in control of the whole East African Coastal strip.
Also German soldiers are buried here after their war vessel Konisberg sunk in our territorial water. In all humility they are our family after a German business man eloped with Seyyida Salme, a princess and hence out there is our royal blood.
Zanzibaris would never forget the interest that East Germany took over Zanzibar soon after the 1964 Revolution in recognizing the nascent state and helping out as close friend. Hence it was befitting gesture and high note endorsement of Zanzibar made by the German President when he walked along the Forodhani Road on his arrival, something never done by any visiting leader. The visiting German President was at home.
I am sure President Gauck was thrilled as he was boisterously cheered by the friendliest people on earth chanted for him and Germany which they admire their football and hard work.
The Forodhani Road passes through many land mark buildings such as the Old Dispensary, the Big Tree, the Custom House, the Sultan Palace, The Forodhani Gardens, The Old Fort and the Tembo House. It always feels pleasure to walk the road. To me it was more than a walk surely to see the sea front which needs repair badly and which the German government would intervene to re-enact and strengthen, the same as it has done to pave the narrow streets in one of the biggest project it had undertaken in Zanzibar. Whoever planned for that walk must have thought very well for Zanzibar which for a long time now has been suffering heaps and heaps of blame on insecurity so much at times the exaggeration is beyond belief. The visit killed it all.
A Western Europe leader walking in the streets of Zanzibar, what a script to run for security endorsement in a place where the Western media bombard with stories on religious violence, extremism and connections made with Al Qaeda, Al Shabab and such groups mainly because certain individuals have collaborated with them.
The walk is big public relations to Zanzibar that tourists here are safe despite hiccups on mugging, acid attacks something that can happen anywhere and in fact such attacks are prone at any big city anywhere in the world.
The walk has sent good messages to potential German visitors to Zanzibar being the second biggest group after the Italians. But to the rest like the Britons, the Scandinavians, the Spanish, the Belgians and the Swiss who come to Zanzibar in their droves. Of course the endorsement by German President Gauck comes with very high price which the Zanzibar Government has to pay, as they say there is no free lunch.
It means it has to clear its house and put it into order to match the gesture. Granted there are religious frictions that can lead to extremism. Not refuted that tourists have been attacked and foreign residents have been targeted as criminality is a real threat. Drugs are galore.
Zanzibar cannot relax at all when tourism sector is being threatened because it now its heartbeat with 200,000 visitors per year channelling over 60 per cent in the Zanzibar Government financial machinery.
To me, the doors have been just opened for Zanzibar and it is for us to decide how to walk the distance.
By Ally Saleh
Posted by
Kibunango
at
00:09
0
comments









