Tuesday, 24 March 2009

Agha Khan na Mji Mkongwe....

Agha Khan Development Network kwa zaidi ya miaka kumi sasa imekuwa ikifanya ukarabati mkubwa katika baadhi ya Majengo ya Mji Mkongwe wa Zanzibar. Na hivi karibuni walikuwa katika hatua za mwisho mwisho za kukamilisha ukarabati wa Forodhani Park.
Leo nitaangalia majengo mawili, nikianzia na Stone Town Culture Centre maarufu kama Old Dispensary ambalo ni mojawapo ya majengo yaliyofanyiwa ukarabati na AKDN baada ya kutupwa na SMZ. Aidha jengo lingine lililolembewa na SMZ ni Extelcom, ambalo leo hii kuingia ndani ya jengo hilo inabidi uwe nazo mfukoni.

Old Dispensary.

Jengo hili ujenzi wake ulikamilika mwaka 1894 chini ya ushauri wa kihandisi toka Uingereza. Michoro na mafundi wa jengo hili ni kutoka India ambako ndipo alipotoka mwenye jengo Bw. Tharia Topan ingawa hakuweza kuona kukamilika kwa ujenzi wa jengo hilo.

Mjane wa Topan aliweza kuendeleza ujenzi na baadae kuliuza. Lengo la Topan lilikuwa kujenga shule na zahanati, ambapo mmiliki wa mwisho wa jengo hilo aliweza kufanya sehemu ya chini ya jengo hilo kuwa zahanati na sehemu ya juu kuwa sehemu ya makaazi yake. Huu ndio ukawa mwanzo wa jina maarufu la Old Dispensary.

Miaka 70 baadae jengo hilo likawa tupu, na kuendelea kuwa tupu huku likiendelea kuchakaa na kuharibika ni hadi pale Agha Khan walipopewa ruhusa ya kulifanyia ukarabati ili kunusuru ufundi mkubwa uliotumika katika ujenzi huo kupotea na hasa nakshi zake za kihindi.


Miaka 100 baadae Agha Khan waliweza kupata kibali cha ukarabati wa jengo hilo, zaidi walipewa mkataba mpya wa kukodishwa jengo hilo na SMZ chini ya muda maalumu. Pichani hapo juu ni old dispensary baada ya kufanyiwa ukarabati mkubwa .


Extelcom
Jengo lingine ambalo lilikuwa chini ya SMZ na kuachwa bila aina yoyote ile ya usimamizi hadi pale walipotokea tena agha khan na kuamua kuligeuza toka ofisi hadi kuwa hoteli ya kitalii. Sasa jengo hili linajulikana kama Serena Inn

Thursday, 19 March 2009

Movie...Hobbie iliyokwisha huko Zenj


Jengo hili sasa halitumiki tena kama jumba la Sinema..!

Wednesday, 18 March 2009

Amin Salmin Amour, aonja tamu ya siasa

Ni baada ya kushindwa kutamba kwenye kura za awali za kumtafuta mgombea kwa tiketi ya CCM katika jimbo la Magogoni huko Zenj. Amin ambaye ni mtoto wa rais mstaafu wa Zenj Salmin Amour maarufu kama Komandoo, alikuwa ni miongoni wa wagombea 10 wa CCM waliojitokeza kuwania nafasi hiyo.

Umaarufu wa Amin unakwenda nyuma zaidi kipindi cha kwanza cha Komandoo Salmin alipokuwa madarakani,umaarufu wake ulijengeka kwa kuwa mjasirimali zaidi ya siasa na kwa kujaribu kila aina ya biashara za muda mfupi! Hatua yake ya kuingia kwenye siasa kwa wengi ilikuwa ni karata yake muhimu ya kujinyanyua tena baada ya kushindwa kudumu katika sekta ya biashara.

Kwa habari zaidi tembelea hapa

Sunday, 8 March 2009

Nani Mjinga Hapa?


Pichani ni mwanamke wa kizenj akiwa katika pilika pilika zake ufukweni, na pembeni kushoto ni mtalii akicheza na maji.

Jaribu kuangalia tofauti ya mavazi kati ya wanawake hawa wawili, halafu jaribu kufikilia hali ya hewa ya Zanzibar, bila kusahau udhaifu wa ngozi za watalii dhidi ya jua kali la ikweta.

Je unafikili kati ya hawa wanawake ni nani mjinga kutokana na aina ya mavazi yake?