Sunday 19 November 2006

SMZ iamke sasa...

Kisiwa cha Zanzibar ni kidogo sana,hata hivyo kimejaliwa kuwa na mambo mengi sana kiasi cha kuwa kivutio cha aina yake!Anyway sina haya ya kueleza mengi kuhusu kisiwa hicho...

Kitu ambacho nataka kuzungumzia ni juu ya utunzaji wa mazingira na hasa sehemu ambazo wanaishi wazenj wenyewe. Makaazi ya wanavisiwa hao na hasa wale waishio maeneo ya Ng'ambo sio ya kuridhisha kabisa. Na hapana shaka yoyote kuwa Halmashauri ya mji wa Zanzibar inashindwa kuuweka eneo hilo katika hali ya usafi inayostahili.

Cha kusikitisha zaidi, wananchi wa maeneo hayo wanapotaka kujiondolea kero zao kwa upande mmoja wanakutana na pingamizi na Halmashauri hiyo, na kufanya juhudi zao kutozaa matunda yoyote.

Hapa nina mfano wa mradi ambao ulifunguliwa ili kusafisha na kutunza mazingira ya wadi ya Mkele. Mradi huo kwa sasa umekufa na tatizo la uchafu wa mazingira ukiendelea. Kinachosikitisha zaidi ni sababu za msingi ambazo zimepelekea kufa kwa mradi huo ambao ulitazamiwa kuwa ni mradi dila katika kuondoa kero za mazingira machafu ambao unasimamiwa na wananchi wenyewe.

Moja ya sababu kubwa ya kufa kwa mradi huo ni kwa manispaa ya zanzibar kutoachia maeneo ambayo yangeweza kuingiza kipato ili mradi huo uweze kujiendesha. Labda hapa nieleze kwa ufupi aina ya mradi huo. Huu ulikuwa ni mradi wa ukusanyaji na utupaji wa taka, ambapo wananchi waliokuwa akipata huduma hii ilipaswa kuchangia gharama za ukusanyaji na utupaji wa taka hizo. Maeneo yote ya wadi yaliorodheshwa katika mradi huu.. nikiwa na maana ya sehemu za kuishi na zile za biashara.

Hata hivyo Manispaa ilikata kutua maeneo ya biashara yaliyopo kwenye eneo la mradi huu ingawa mradi ulikuwa ukisafisha maeneo hayo vile vile. Kukosekana kwa mapato toka katika maeneo ya wanafanya biashara, ambao kwa kiasi kikubwa ndio wazalishaji wakubwa wa taka, kulizoretesha kabisa mapato ya mradi huo. Ikumbukwe kuwa wafanyabiashara hao nao walitiwa hesabuni kama ndio sehemu kubwa ya kupatikana kwa mapato ya mradi huo kabla ya kuanza. Hata hivyo Manispaa ilikataa kabisa kuachia maeneo ya wafanyabiashara kuhudumiwa na mradi huo.

Sababu nyingine ni migongano ya viongozi juu ya kuendesha mradi huo. Viongozi wa kisiasa katika eneo hilo walitumia mradi kujionyesha kwa viongozi wenzao na wananchi kwa ujumla, hii ilijenga vita vya ndani kwa ambavyo lengo lilikuwa ni kuzolotesha mradi mzima...na lengo hilo limefanikiwa.

Wakati wote huu wa mvutano juu ya uendeshaji wa mradi huu serikali kuu SMZ ilika kimya tu, pamoja na kuwa wao pia walichangia kiasi fulani kuanzishwa kwa mradi huo. Ukaaji kimya wa SMZ pengine ulitokana na kutotambua kero za wananchi juu ya taka, au tu ilitaka kuridhisha upande mmoja(manispaa) na kuacha mradi ukifa kwa matatizo ambayo yalikuwa yanawezekana kutatuliwa pasipo bughuza zozote.

Ili hali ya mazingira iwe nzuri kisiwani huko ni vema SMZ sasa wakaamka na kuheshimu maamuzi ya wananchi. Sio vema SMZ kuchangia kuanzishwa kwa miradi na kushindwa kuona miradi hiyo ikisimama yenyewe na kuendelea. Ubinafsi miongoni mwa watendaji wa SMZ, vita kati ya viongozi wa kisiasa ni mambo ambayo yanatakiwa kupigwa msasa na hasa kwenye suala zima Utunzaji wa Mazingira.

Ni jambo la aibu sana kwa kisiwa hicho kuwa kichafu kiasi cha kusababisha ugonjwa wa kipindupindu, ambao haukuwepo miaka ya huko nyuma!

SMZ siku zote inanichekesha

Hivi karibuni SMZ imefuta kiwanja cha ubalozi wa Oman kwa madai ya kuwa kipo sehemu mbaya kiusalama! eti kipo karibu sana na beach!

Mwee! hivi nani hasa huwa anaomba kiwanja?
Nijuavyo mimi ni kuwa Taasisi au mtu binafsi huomba Kiwanja kwa kutaja sehemu ambayo huona ni muafaka kwake kuwa na kiwanja. Hivyo nina amini kuwa ubalozi wa Oman uliomba kiwanjwa hicho kwa kuwa wao waliona kuwa eneo hilo ndio linafaa kwako kujenga ofisi ya ubalozi na sio sehemu nyingine yoyote ile. Na SMZ wakati ule iliridhia kutoa kiwanja hicho kwa ubalozi wa Oman, licha ya kwenda kinyume na maelekezo ya masterplan ya hifadhi na uendelezaji wa Mji Mkongwe.

Hata hivyo Ubalozi haukujengwa zaidi ya eneo hilo kuzungushiwa ukuta tu ambao kwa kiasi fulani ulikuwa ni kero tupu kwa watu ambao walikuwa wanaegesha magari katika eneo hilo... Zaidi kuzuia sehemu ya kuanzia kwa mashindano ya ngalawa.

Leo hii SMZ kama kawa imeibuka na kusema kuwa eneo hilo halifai kwa ujenzi wa ofisi ya ubalozi, kwa sababu za kiusalama?

Usalama wa aina gani ambao SMZ wanaosema?... Ikulu ipo beach, Hospitali kuu ipo beach, Mahakama Kuu ipo beach, ubalozi wa Misri upo beach.. yaani kila ofisi muhimu hapo zenj zipo beach! sasa ni kwanini tu Ubalozi huo usiwe beach?
Kama mmefuta umiliki wa uwanja huo kwa ajili ya kubadilisha matumizi ya ardhi kwa kiwanja hicho, itakuwa ni jambo la busara iwapo kiwanja hicho kitarudishiwa matumizi yake ya awali kama eneo wazi.

Kuwepo kwa ukuta katika eneo hilo kwa kiasi fulani kulizorotesha sana maendeleo ya kibiashara kwa maeneo ya karibu kama vile Starehe Club, Wings, Garage Club, n.k

Maji ya Dezo yafikia kikomo Zenj...

Baraza la Wawakilishi hatimae kwa shingo upande limepitisha mswaada wa kulipia huduma ya maji katika visiwa vya zenj. Hii ina maana kuwa ile kauli ya "maji ya Karume(maji ya bure)" inafikia kikomo. Wananchi wa visiwa hivyo wamekuwa wakitumia maji bure tokea mwaka 1964. Gharama zote za matumizi ya maji zilikuwa chini ya serikali hivyo kufanya sekta hiyo kwa kiasi fulani kudumaa na hasa baada ya Azimio la Zanzibar, ambapo Visiwa hivyo vilishuhudia ongezeko kubwa la mahitaji ya maji.

Wafadhili kadhaa kwa wakati tofauti waliishauri SMZ kubadili mfumo wake ili kuweza kupatikana kwa huduma bora ya maji bila mafanikio.

Hata hivyo kutokana na shida kubwa ya maji, na kuanzishwa kwa sustainable programme kupitia NGO na CBO Baadhi ya wananchi walianza miradi ya kujitafutia maji ya bomba kwa gharama zao wenyewe. Miradi hii imekuwa ya mafanikio sana kwao.

Nina matumaini makubwa kuwa wafadhili ambao walisusa kuanzisha mfumo mpya wa ugawaji maji katika visiwa vyenye maji safi na matamu duniani nzima(nunua Drop kama huamini), watarudi na kuendeleza shughuli zao pale walipoachia.

Kwa upande mwingine wananchi wa Zenj wawe tayali kukubali kulipia maji na kutumia maji kwa uangalifu na zaidi kutunza huduma hiyo.
Hii ni kwa faida yetu wenyewe, vilevile kutawezesha huduma hiyo kuwa endelevu. Tukumbuke kuwa Hudumu ya maji ni Kwa faida yetu sisi wananchi na ni wakati wetu kusimamia hudumu hiyo ili iweze kuwa endelevu.