Monday 3 September 2007

Zenj Watatoa Lini Miss Tz......?



Mshindi wa Miss Tz mwaka huu amewasha moto mkubwa kwa wadau wa urembo wa huko bara, ikiwa ni pamoja na mamiss kadhaa waliopita. Moto huo ambao kuzimika kwake ni songombindo unatokana na madai kuwa miss huyo hana asili ya Utz bara, ukinondoni n.k Usishangae sana kusema Utz bara, kwani huko visiwani hakuna mambo ya Umiss, na nina shangaa huyo mdosi...sori huyo miss kuitwa Miss Tz wakati Warembo wa Zenj hawakushiriki mashindano hayo...

Mara ya mwisho kwa kumbukumbu zangu, warembo wa marashi ya karafuu walishiriki mashindano hayo wakati yakidhaminiwa na fegi za aspen.. sijui bado zipo au la! manake fegi hizo zimeadimika sana mitaani.

Awali ya yote inaonekana kuwa Watz wameshindwa kabisa kuficha makucha yao ya kibaguzi kwa kupiga kelele kwa mdosi huyo mzalendo kutwaa taji hilo. Mimi binafsi sishangai sana, kwani ile dhambi ambayo ipo visiwani huku, imeweza kuvuka bahari na kutua huko Bongo...Tz bara.

Iwapo kungekuwpo na Miss Zenj basi yoyote yule ambae angebahatika kutwaa taji hilo, angechunguzwa kuwa ana asili ya wapi...! Kama ni kutoka kisiwa cha pili basi angeitwa ni mpemba, na iwapo angekuwa anakaa Ng'ambo iliyo karibu na Mji mkongwe basi wangesema ni Mngazija, zaidi iwapo angekuwa na chongo basi moja kwa moja angeitwa ni mnyamwezi( mtu yoyote toka bara).

Utamaduni wa kuangalia mtu ana asili ya wapi upo muda mrefu katika visiwa hivi, kiasi kwamba umeleta kujitenga kimakaazi kwa watu... Tabia hii huko bara haikuwepo huko zamani, lakini sasa naona inaingia kwa kasi kubwa. Sijui inaashiria kitu gani, kwani, huko bara waasia wamekuwa wakishika dhamana kubwa kubwa katika kuongoza nchi pasipo mashaka wala malalamiko yoyote. Leo hii kupatikana kwa miss mdosi wa kitz imekuwa nongwa!

Iwapo tulikuwa tukitembea vifua mbele kupinga ubaguzi wa rangi miaka ile, iweje leo tutoe machozi kwa mtz wa kiasia kutwaa taji la Utz? Au ile dhambi toka Zenj tayali imeshaanza kuingia huko bara? Tuliwahi kuonywa kuwa dhambi ya ubaguzi ni mbaya sana, eti ni sawa na kula nyama ya binadamu, kwani hutoishia kuionja tu, bali utaendelea kuila tu!... Mwakani Watz watahoji ni kwanini Mass wanatoka Kinondoni, au kwa nini wamiss wanatoka katika kabila fulani kila mara... Dhambi hiyo itaendelea tu!

Wazenj mara nyingi wamekuwa wakisoma mifano imara ya Tz bara katika suala zima la kuishi bila kujali huyu anatoka wapi au ana asili ya wapi... Iwapo leo hii mmefikia hatua hii, basi mnapoelekea sio kuzuri kabisa. Mfano wa karibu upo huku visiwani!

Thursday 30 August 2007

Wednesday 29 August 2007

Kauli ya Nahodha ina Walakini

Waziri Kiongozi wa Zenj, ambae yupo mkoani Ruvuma ametoa kauli ya kusisitiza kuwa, Elimu ndio njia pekee ya kuwaletea maendeleo wakazi wa Mkoa huo,kutokana na mkoa huo kukosa Umeme wa kuhaminika na kuwa na barabara mbovu. Msisitizo wa kauli hiyo aliutoa kwa kufananisha ukuaji wa kasi wa uchumi wa Singapore na udodoraji wa maendeleo ya mkoa huo na Tanzania kwa ujumla.

Kauli hii ina utata mkubwa kwani elimu pekee haiwezi kuleta maendeleo yoyote iwapo njia zingine za kuleta maendeleo zitakuwa zimebanwa kwa wananchi. Mkoa wa Ruvuma unasifika kwa kuzalisha Mahindi, Kahawa, Tumbaku,Alizeti na mazao mengine. Kabla ya mwaka 1984, usafiri wa kwenda huko ulitegemea zaidi njia ya anga (ATC).Usafiri wa barabara ulikuwa ni wa usumbufu mkubwa na uliweza kuchukua muda mrefu kufika mkoani. Kufunguliwa kwa barabara ya Makambako - Songea katika kiwango cha lami, kulitoa fursa kubwa kwa mkoa huo kuvuma katika uzalishaji wa Mahindi. Barabara hii haikuja kutokana na elimu ya waakazi wa huko bali ni kutokana na umuhimu mkubwa wa taifa kupata Mahindi na Kahawa toka mkoani huko.

Mkoa wa Ruvuma kwa miaka mingi umekuwa ukitegemea umeme wa nguvu ya jenereta, ambao licha ya kuwa ni ghali kuuendesha, upatakanaji wake umekuwa ni wa kimgao kwa zaidi ya miaka ishirini sasa. Sasa hapa sijui elimu ya aina gani inatakiwa ili mkoa huo uunganishwe kwenye gridi ya taifa, ambayo inapita katika mikoa ya jirani zake.

Nimeshindwa kuelewa kauli ya Nahodha, kati ya kuwa na elimu na uwewezeshaji wa miundo mbinu na uchumi wa mkoa husika. Kwa mfano majumba ya michenzani huko Zenj hayakujengwa kwa kuwa waakazi wa zenj wote walikuwa ni wajuzi wa ujenzi. Yalijengwa kwa sababu uchumi wa Zenj kipindi hicho ulikuwa unaruhusu, na viongozi kwa kushirikiana na wananchi waliona upo umuhimu wa kufanya hivyo.

Kwa mkoa wa Ruvuma kuwaambia kuwa tatizo lao la umeme litatatuka kwa kuwa na elimu na sawa na kuwaondoa njiani tu...

Tuesday 21 August 2007

Wadau



Altune na Kibunango