Thursday 20 September 2007

TV Zanzibar(TVZ): Kuondokana na Analogy kwenda Digital



Luninga ya SMZ imeingia mkataba na serikali ya Japan ambapo, Luninga hiyo itafanyiwa malekebisho ya hali juu toka mfumo wa sasa wa urushaji wa matangazo wa Analogy na kwenda kwenye mfumo wa Digital.

Kwa mjibu wa Mdau hapo juu kwenye picha, matengenezo hayo yanategemea kuanza mapema 2008. Mfumo huu wa digital katika Tanzania upo kwenye TVT, Star TV huku ITV na Channel 10 wakiwa semi digital. Zaidi Wachina nao wamekubaliana na serikali ya mapinduzi zanzibar kuvungua kituo kimpya na cha kisasa zaidi cha Tv. Kituo hicho kinatazamiwa kujengwa katika maeneo ya Masingini. Tv hiyo itakuwa ni full digital na yenye nguvu kubwa zaidi kuliko hiyo ya sasa (TVZ).

Wednesday 19 September 2007

Jumuwata inakuhitaji..


Jumuiya ya Wanablogu wa Tanzania inawakaribisha wanablogu wote katika kuchangia, kurekebisha, kukosoa, kutoa ushauri n.k katika katiba ya jumuiya.

Mchango wako wa kimawazo unahitajika sana ili kuweza kupatikana kwa katiba nzuri kwa manufaa ya wanablogu wote.

Usomapo Tangazo hili tafadhali mjulishe na mwanablogu mwenzako.

Thursday 13 September 2007

Wajane waweka rekodi mpya huko zenj....!

Wajane wa kisiwa cha Zanzibar wameweka rekodi mpya katika fani ya mavazi. Ni baaada ya kuwa wabunifu wa kwanza kupaka/kuchora hinna kwenye vitambaa ambavyo hutumika kutengenezea nguo mbalimbali. Ubunifu huu waliupata kutokana na kuhudhulia kozi ya muda mfupi juu ya kuchora hinna kwenye vitambaa.

Ili lengo la mafunzo hayo liweze kufanikiwa ambalo ni kuongeza kipato kwa Wajane hao, ni muhimu kuona kuwa wanakuwa na sehemu rasmi ya kufanyia biashara zao. Kwa upande huu wa fani zisizo rasmi kuwekuwepo na usumbufu mkubwa wa sehemu za kufanyia shughuli zao, pengine ni kutokana na serikali kutowajali, hivyo kuwasumbu sumbua kila kila.

Sehemu ambayo Wajane hawa na wafanyabiashara wengine katika fani hiyo wamekuwa wakiitumia ni Eneo la mji mkongwe na sehemu ya Uwanja wa Forodhani na baadhi ya mitaa ambayo hutokea katika uwanja wa forodhani kama vile mtaa wa gizenga. Halmashauri ya Mji kupitia maelekezo ya Mamlaka ya Mji Mkongwe, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mjini Maghalibi na ofisi ya Waziri Kiongozi wamekuwa mara kwa mara wakiwaondoa wafanyabiashara hao kwa madai mengi, ambayo mengine uhusisha mambo ya dini.

Kwa kuweza kuweka rekodi ya Dunia, ambapo sasa wataweza kujiongezea mapato yao maradufu, Ni vema kwa serikali kutowasumbua sumbua Wajane hao. Soko lao hilo linawalenga watalii ambao hupatikana katika maeneo ya forodhani ambako kuwa vivutio kadhaa vya Utalii. Na zaidi SMZ sasa iweke mikakati ya kuweza kutambua fani zisizo rasmi, kwani zaidi ya kutoa ajila kwa wahusika zitaweza vilevile kuingiza mapato ndani ya serikali na kusaidia juhudi za serikali kupunguza umaskini kwa wananchi wake.

Ni Msimu wa Beer za Mafichoni...Zanzibar


Mwezi wa Ramadhan huko Zanzibar, hubadilisha sura ya kawaida ya visiwa hivyo, aidha pilikapilika nyingi za kawaida huenda likizo ya muda, huku pilika nyingine huchukua nafasi katika kipindi hiki.

Kwa wanywaji wa bia ambao hawafungi, uungana na wananchi wengine ambao wana imani zingine kuendelea kunywa bia, kwa staili ya kujifungia ndani ya nyumba za ulevi....Kwa ufupi katika kipindi hiki cha mfungo, migahawa, hoteli, baa na majumba mengine yote ya starehe hufungwa. Hakuna sheria rasmi ya kufanya hivyo, ila kwa kuwa imekuwa ikifanyika kwa miaka nenda rudi sasa inaonekana ni kama sheria. Na iwapo ukishikwa unakula mchana katika mfungo huu, basi utasekwa rumande na kuachiwa baada ya siku moja au kushitakiwa kabisa!

Miaka kadhaa huko nyuma Beer ilikuwa ikiuzwa katika hotel za serikali tu wakati wa mfungo huu. Tena waliokuwa wanakusudiwa hapo ni watalii tu...! labda na wageni wa serikali ambao wana imani tofauti. Zaidi ya kuuza bia, hoteli hizo pia ndio zilikuwa zikiuza msosi. Hata hivyo mambo sasa yamechukua sura mpya. Baa nyingi huendelea kufanya kazi katika kipindi hiki, zikiuza bia na misosi. Tofauti ya mwezi huu na miezi mingine ni kuwa unywaji ufanyika kwa kujificha, na katika mazingira ya ukimya kabisa, huku wengi wakisubiri king'ora cha kufuturu...!

King'ora kikisharia, kumbi hizo ufunguliwa milango, redio hufunguliwa na kelele za kawaida za kwenye baa huanza kusikika! Hali hii uwepo kwa muda wa mwezi mzima.