Tuesday 11 August 2009

Friday 7 August 2009

Wapemba waendeleza ual-qaeda...!


Baada ya Uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1995,Visiwa vya Zenj vilishuhudia vituko kibao, ikiwa ni pamoja na mabomu ya baruti na ya petroli yakilipuriwa katika maeneo mbali mbali ya visiwa hivyo. Toka katika maakazi ya watu, ofisi za serikali na hata sehemu nyeti kama za usambazaji wa umeme visiwani humo zilipata makasheshe ya milipuko ya mabomu. Mabomu mengine yaliweza kulipuka huku mengine yakishindwa kulipuka.

Kipindi hicho kilikuwa ni kabla ya ulipuaji wa mpigo(sambamba)wa mabomu kuanza. Ni katika mwaka 1998 ambao ulipuaji wa sambamba uliponza na kukikuhisha kikundi maarufu cha Al-Qaeda, pale walipoweza kulipua kwa wakati mmoja ofisi ya balozi wa Marekani katika majiji ya Dar es Salaam na Nairobi.

Hapo Majuzi nyumba za Masheha huko Pemba ziliweza kulipuliwa kwa staili hiyo na kufanya wengi kufananisha milipuko hiyo kama ile ya kundi la Al-Qaeda. Huu ni muendeelezo wa ulipuaji wa mabomu huko Pemba kwa madai ya kuwa Masheha wanawanyima wakaazi wa huko kuandikishwa kwenye daftali la kudumu la kupiga kura.

Wapemba katika hili wapo mbele, kwa kumbukumbu za haraka haraka, tokea uchaguzi wa mwaka 1995, kumekuwepo na vituko vingi sana huko Pemba, kama vile vya kugeuza visima vya maji kuwa vyoo, kupaka vinyesi katika skuli,ili kuzuia wanafunzi kusoma, kunyang'nya polisi silaha na kuteka kituo cha polisi, kususia shughuli za maziko na arusi, kubagua watu wa kufanya biashara nao, talaka kwa wanandoa kutokana na tofauti za kisaisa na vituko vingine kaza wa kaza.

Pamoja na yote, ili la mabomu ambalo linaendela sasa, linatakiwa kuchukuliwa hatua za haraka la kulidhibiti, kwani litaweza kuleta madhara makubwa sana hapo mbele, na hasa siku ambayo Wapemba hao watakaweza kuwa na mabomu yenye nguvu(haya ya sasa hayana nguvu kubwa)au mabomu ya sumu! Hivyo basi ni vema kwa vyombo vinavyohusika kuwatafuta watu hawa wanaolipua mabomu na kuwafikisha kwenye vyombo husika. Na ni wakati wa kuanza kuitumia sheria ya magaidi iliyotungwa mara baada ya milipuko ya Dar na Nairobi.

7th August 2009

Nyumba za Masheha wawili zalipuliwakwa mpigo

Milipuko miwili tofauti imetokea sambamba nyumbani kwa masheha wawili kisiwani Pemba na kusababisha zaidi ya watu 30 kunusurika kifo.
Akizungumza na Nipashe juu ya matukio hayo yanayofanana na ile milipuko ya kupanga ya kikundi cha kigaidi cha Al- Qaeda kwa kulipuka kwa wakati mmoja, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, Yahya Bugi, alisema matukio hayo ni ya kupanga.
Alisema katika tukio la kwanza, watu wasiojulikana walitega bomu la kutengenezwa kienyeji kwa kutumia baruti (TNT) na kulilipua nyumbani kwa Sheha wa Mihogoni, Salim Said Salim (59).
Kamanda huyo aliliambia Nipashe kwamba nyumbani kwa Sheha Salim kulikuwa na mkusanyiko wa watu waliokuwa wakihudhuria harusi nyumbani kwake saa sita usiku wa kuamkia jana.
Alisema bomu hilo lililipuka wakati Sheha na wageni wake wakiwa wamelala na kusababisha athari kubwa kwenye ukuta wa nyumba yake na mabati sita yaliyoezekwa nyumba hiyo kung’oka.
Kamanda Bugi alisema kwa mujibu wa Sheha Salim, walisikia kishindo kikubwa kikitokea nyuma ya nyumba yao na baada ya kukimbilia katika eneo hilo waliwaona vijana wawili wakikimbilia eneo lenye migomba.



Zaidi: tembelea Nipashe

Thursday 6 August 2009

Pinda amefulia...


Kwa kauli yake juu ya Muungano Waziri Mkuu Mizengo Pinda amefulia na ameonyesha ufahamu mdogo juu ya Muungano huu. Kauli yake ya kuondoa kero za muungano ni kuifuta SMZ haiwezi ikaachwa hivi hivi. Kauli ambayo aliitoa huku akijua kuwa hakuna dalili zozote za sasa za SMT kujaribu kuondoa kero za Muungano achilia mbali jitihada za kuona kuwa Muungano unakwenda vizuri zaidi ya kuburaza upande mmoja wa Muungano. Kauli yake inaweza kuwa sahihi iwapo Muungano huu utakuwa hauna kero yoyote na nchi zote mbili kuridhia kuwa hakuna kero.

Zaidi Pinda anahitaji kupatiwa tuition ya haraka kuhusu Muungano na mambo yote ambayo yahusianayo na Muungano huo. Hii itamuwezesha kujua na kupata ufahamu mkubwa wa Muungano huu kabla ya kujikuta akishitumiwa na kuandamwa na Katiba na kukimbilia kulia.

Wednesday 5 August 2009