Thursday 20 August 2009

Wapemba watangaza hujuma dhidi ya Masheha na Vingunge wengine...


Huko PBA mambo si shwari kabisa

Kuna madai ya kuibuka kikundi kinachoitwa Hujuma kwa Masheha, ambacho lengo lake ni kudhuru viongozi.

Kundi hilo linalofananishwa na Mungiki la Kenya, limeanza kutoa vitisho kwa kusambaza vipeperushi kwa baadhi ya masheha, kwamba wajiandae kupokea kipigo, huku sheha mwingine akionja adha ya kundi hilo kwa kupambana nalo.

Akizungumza jana, Ofisa Tawala wa Wilaya ya Wete, Khamis Juma Silima, alisema ofisi yake imepokea taarifa za kundi hilo, ambalo lina mrengo wa kisiasa kwa nia ya kuwadhuru masheha hao, kwa madai kuwa ndio kikwazo cha upatikanaji wa fomu za vitambulisho vya Mzanzibari Mkazi, ambazo ni kigezo cha kuandikishwa kwenye Daftari la Kusumu la Wapiga Kura.

Silima alisema masheha kadhaa wamepeleka malalamiko ofisini kwake katika siku za karibuni ya kupokea vipeperushi vya vitisho kuhusu utoaji fomu kwa wananchi wao.

Source: Habari Leo

Tuesday 18 August 2009

Hamad Masauni, na Siasa za kukariri...



Anavyosema kuhusu Pemba ni tofauti sana na hali halisi ya huko Pemba..

Mwenyekiti wa Vijana wa CCM, Hamad Masauni Yusuf alisema ingawa hajui vigezo vilivyotumika katika utafiti, anaamini kuwa wananchi wengi bado wana kasumba kwamba CUF bado ina ngome kubwa kisiwani Pemba wakati hali sasa ni kinyume.

Alisema sio kweli kwamba, CUF wana nafasi kubwa ya kushinda urais kwa Zanzibar na pia huko Pemba na kwamba hali imebadilika kwa sasa akidai kuwa, wananchi wengi wamekata tamaa na viongozi wao na hivyo, CCM ina nafasi kubwa ya kushinda.


Kauli hizi na hali halisi ya huko Pemba ni sawa na kujisuta

Kwa Anayetaka Uprez Zenj...

Saturday 15 August 2009

MMhm Huyu Nae...! CCM Maisara


Mdau wa CCM Maisara, sehemu maarufu hapo Zenj!