Saturday 23 January 2010

Umeme wa uhakika kurudi 2012 huko Zenj...


New power supply cable for Isles to be built in 2012

The Zanzibar government yesterday disclosed that the project to lay-down a new sub-marine cable for power supply to the Isles from Tanzania Mainland will be completed in 2012, after the US government reduced the project implementation timeframe.

This was said by Isles Minister for Water, Construction, Energy and Lands Mansour Yussuf Himid, when responding to questions by Members of the House of Representatives here yesterday.

He said previously, the project was set for completion by 2013, but the Isles government requested the US Government to reduce the timeframe due to power problems facing Zanzibar.

The minister told the House that the tendering process had been floated and would be opened on February 19, this year.

Himid said already various companies had applied for the implementation of the long-awaited project adding that the financier of the project, Millennium Challenge Corporation (MCC), would go through all processes of picking the winner from the bidding firms.

The new power supply route would have the capacity of 100MW from the Tanzania Electric Supply Company Limited (Tanesco), he said, adding that the cable would pass under the Indian Ocean from Kiromono Cape on the Mainland to Fumba in Zanzibar.

Zanzibar spends 1.2bn/- every month in power expenses from the Mainland, however Isles customers have been living without hydro-electric power supply since December last year, after a key electric device exploded at Fumba main power station.

Prof. Issa Shivji ana haya ya kusema juu Maalim Seif na Rais Karume



Barua ya wazi kwa Mheshimiwa Rais Karume na Maalim Seif:

Ninawaaandikia barua hiyo ya wazi kwa sababu nimeguswa kwa karibu sana na jinsi mijadala kufuatia mkutano wenu inavyoendelea na inavyoendelezwa. Mijadala hii imepotoshwa, ama kwa kutokuelewa au kwa makusudi. Kwa maoni yangu, swali la msingi kabisa katika hali ya Zanzibar leo ni: Je, uchaguzi mwaka huu, bila kutanguliwa na mabadiliko katika hali ya kisiasa ya Zanzibar, utakuwa wa amani, haki na huru? Na nini ifanyike ili kujenga mazingira yatakayowezesha uchaguzi wa amani, haki na huru? Nitafupisha chimbuko la matatizo ya kisiasa ya Zanzibar katika vifungu vitatu:

Jamii ya Zanzibar kisiasa imegawanyika kati-kati, yaani ‘it is split in the middle’. Na jambo hilo limedhihirishwa katika takriban kila uchaguzi.

Kwa hivyo, hakuna mazingira ya ushindani katika Zanzibar; badala yake kuna mazingira ya uhasama. Katika mazingira ya uhasama, haiwezekani kabisa kuwa na siasa za kishindani, ambayo ni kiini cha mfumo wa vyama vingi.

Jitihada zote zilizochukuliwa, pamoja na miafaka miwili, hazikuzaa matunda kwa sababu mbalimbali, ambazo sinahaja kuzichambua katika barua hii. Isipokuwa sinabudi niweke wazi kwamba, kwa maoni yangu, sababu kuu ya jitihada hizi kutokuzaa matunda ni wanansiasa kuweka maslahi yao ya muda mfupi mbele ya maslahi ya taifa/jamii.
Kwa mara ya kwanza, katika kipindi cha karibu miongo miwili, maridhiano kati ya viongozi wakuu wa CCM na CUF wa Zanzibar, na sio wengine (na hili lazima lisisitizwe) imetoa kamatumaini kadogo ka uwezekano – sio uhakika – wa kutatua matatizo ya Zanzibar. Kinachotakiwa, tena bila kupoteza muda, ni kuiimarisha hatua hii iliyochukuliwa na kujenga juu yake. Na hili ifanyike kabla mijadala potofu inayoendelea haijawa sugu na kuwapotoshea malengo wananchi, hususun lengo la kuweka msingi wa amani.

Naposema mijadala potofu ninamaanisha hoja kama zifuatazo:

Karume asiongezewe muda wala kipindi kingine cha urais. Hii ni kinyume cha katiba ya nchi na katiba/sera ya CCM.

Katiba isichezewe kwa kubadilisha, badilisha.

Yaliyoanzishwa na Karume, yanaweza kuendelezwa na mrithi wake.

Huwezi kuwa na serikali ya umoja wa kimataifa bila ridhaa ya wananchi, kwa maana ya bila kuwa na kura za maoni.
Kwa hivyo, ifanyike nini:

Kama sote tunafahamu kwamba uchaguzi ujao hauwezi kufanyika katika hali ya uhasama tuliyanayo, na hali hiyo haiwezikubadilika au kubadilishwa katika muda uliobaki, basi ni wazi kwamba uchaguzi usogezwe.

Madhumuni ya kusogeza uchaguzi ni kutoa muda wa kutosha wa kuchukua hatua za awali lakini za lazima kujenga mazingira yatakayowezesha uchaguzi wa amani, haki na huru.

Kwa hivyo, kinachohitajika ni kipindi cha mpito (tuseme kama miaka miwili) kutekeleza hatua maalum, yaliyoainishwa na kukubaliwa kisheria. Kipindi hiki ni cha mpito (transitional period) kati ya mazingira ya uhasama tuliyonayo, na mazingira ya ushindani, tunayotaka.

Hatua gani ambazo ni muhimu na zinatakiwa kuzichukuliwa:

Kuunda serikali ya umoja wa kimataifa, (sio serikali ya mseto) mara baada ya sheria ya mpito (transitional law) kupitishwa na Baraza la Wawakilishi. Bila shaka washiriki wakuu wa serikali hii watakuwa CCM na CUF.

Kujadili na kukubaliana kuweka kikatiba vyombo huru vitakavyosimamia uchaguzi.

Kujadili na kukubali marekebisho mengine ya kikatiba na sheria yatakayowezesha mazingira ya ushindani.

Kujadili na kukubali, kati ya pande zote zinazohusika, marekebish ya Katiba ya Jamhuri katika vifungu vinavyohusika na muungano.

Kuweka taratibu na ratiba ya hatua zilizikubalika kuchukuliwa.

Kwa mantiki ya hoja yangu ya kuaahirisha uchaguzi, suala ambalo linajitokeza moja kwa moja ni kwamba hatutakuwa na rais, kiongozi wa nchi na serikali, kwa kuwa rais aliyoko madarakani atakuwa amemaliza muda wake. Sasa je, nani atachukuwa nafasi ya mkuu wa nchi na kiongozi wa serikali? Kuna njia tatu:

Moja, mtu ateuliwe na Baraza la Wawakilishi kushika hatamu wakati wa mpito. Hili kwa kweli ni kinyume na hulka ya kidemokrasia na huwa haifanyika wakati wa kawaida isipokuwa tu kama kuna hali ya dharura (emergency) na Katiba imewekwa kando. Kisiasa, mteule kama huyo hatakuwa na uhalali hata kama ikikubaliwa kwamba asiwe mwanachama wa chama chochote.

Pili, Jaji Mkuu achukuwe nafasi hiyo. Ninafikiri hii pia haina mantiki kwa sababu anyetakiwa kuongoza katika kipindi hichi ni yule ambaye, kwa kiasi fulani, ana uhalali wa kisiasa. Na vyovyote vile sio vizuri kwa demokrasia kumingiza mkuu wa muhimili wa mahakama katika mambo ya kisiasa.

Tatu, ni kumongezea muda (sio kipindi kingine) rais aliyopo madarakani kuedelea wakati wa kipindi cha mpito. Hii inawezekana kisheria, na njia pekee, itakayokuwa na uhalali wa kisiasa kwa sababu (a) alichaguliwa, (b) chama chake kina wawakilishi wa kutosha katika Baraza, (c) chama kikuu cha upinzani (CUF) kimemkubali, na (d) inaelekea wananchi kwa kiasi kikubwa kimeridhia kwamba amalize kazi aliyoanza. Ni kweli, wanasiasa wenzake katika chama chake wasipendezwe na hatua hii, lakini kwa wale ambao wanajiona marais-matarajiwa, bila shaka, hawawezi wakapendezwa. Wana haraka ya kuingia ikulu!

Mwishowe, je, kitaaluma, nini ifanyike na nini inawezekana?

Baada ya makubaliano kati ya CCM na CUF, waandishi wa sheria wataanda sheria maalum ambayo inakuwa na hadhi sawa na Katiba na huitwa ‘constituent act’. Kwa hivyo Baraza la Wawakilishi wataipitisha sheria (labda nitaje jina: The Constitution (National Unity Government) (Transitional and Temporary Provisions) Act, 2010) ambayo itaorodhesha hatua zote muhimu, pamoja na kuweka muundo wa serikali ya umoja wa kimataifa. Pia, itaweka kando (suspend) vifungu vinavyohusika na uchaguzi na kipindi cha urais kwa muda wa mpito, n.k. Sheria hiyo itatamka wazi kwamba uhai wake ni wa muda wa, tuseme, miaka miwili tu na kwamba baada ya miaka miwili, itapoteza nguvu yake ya kisheria. Sinahaja kuzungumzia mambo mengine ya kitaaluma isipokuwa kusisitiza kwamba muhimu ni utashi wa kisiasa na hakuna upingamizi wowote wa kitaaluma.

Waheshimiwa, nimesema mambo haya hadharani kwa sababu mbili. Moja ni jambo lenyewe ni muhimu mno kwa wanajamii wa Zanzibar na Watanzania kwa jumla. Kamwe, hatuwezi kustahimili machafuko mengine katika nchi yetu. Pili, ni maaridhiano yenu yanatuhusu sisi sote na yasiwe ya siri wala yasichezewe kwa maslahi ya wanasiasa.

Kila la heri.

Issa Shivji

Profesa wa Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Nyerere

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

15/01/2010.

Thursday 21 January 2010

Maalim Seif ajibiwa....

Maalim Seif asiachwe kuizunguka historia ya Zanzibar


LIMEFANYIKA jaribio dhaifu la hadaa ya kisiasa; jaribio ambalo maelfu ya Wazanzibari wameliamini na kulikubali na bila ya kujali itikadi zao na mirengo yao ya kisiasa, wamelikumbatia kama ukweli na kuandamana kuliunga mkono.

Jaribio hilo ni lile la kupotosha historia ya Zanzibar ili kujipa alama bora za kisiasa. Jaribio hilo limefanywa na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Seif Sharrif Hamad katika hotuba yake ya kuelezea juu ya “maridhiano na mustakabali wa Zanzibar”.

Kwa mtu yeyote aliyesoma hotuba hiyo ya Maalim Seif, ukweli mmoja unajionyesha wazi kama mwili wa mbuni aliyejificha kichwa chake mchangani, na kama mwangaza wa radi, hotuba hiyo imefunua ulaghai wa kisiasa ambao mtu makini anaweza kuuona toka mbali na kuukwepa.

Nasikitika wananchi wa Zanzibar katika kile kinachodhaniwa kuwa ni umoja wao, wamekumbatia historia hii mpya ya Zanzibar; historia ambayo kiukweli ni mpya!

Historia isiyo na doa ya Zanzibar

Kitu cha kwanza ambacho tunakiona katika historia hii mpya ya Zanzibar kwa mujibu wa Maalim Seif, ni historia isiyo na “doa” ya Zanzibar. Katika historia yake, Maalim Seif anaielezea Zanzibar katika mwanga wa uzuri wa paradiso. Anadai kuwa Zanzibar, licha ya udogo wake kama kisiwa, ilikuwa na umuhimu mkubwa katika eneo la Afrika ya Mashariki, Uarabuni, Bahari ya Hindi na Mashariki ya Mbali. Anadai kuwa umuhimu huo “ulitokana na maendeleo makubwa yaliyokuwa yamepigwa Zanzibar katika nyanja mbali mbali za maisha.”

Katika ‘maendeleo haya’ utumwa hautajwi wala kuhusishwa! (nitaliangalia hili mbele zaidi kwa wakati huu yatosha kuliweka mawazoni kama utumwa ni sehemu ya maendeleo ambayo Maalim Seif anaisifia Zanzibar!).

Mojawapo ya vitu vingine vya kihistoria ambavyo Maalim Seif amevionyesha katika kutangaza utukufu wa Zanzibar ni madai kuwa “Zanzibar inaelezwa kutajwa kwa majina tofauti tangu miaka 500 kabla ya kuzaliwa Nabii Issa (Yesu Kristo). Uvumbuzi wa karibuni wa mapango ya watu wa kale katika ukanda wa Mashariki Kusini mwa kisiwa cha Unguja unaonyesha kuwepo kwa makazi ya watu tokea zama za mawe ziitwazo ‘Stone Age’.

Katika kitabu maarufu chenye kumbukumbu za wasafiri wa kale wa Ugiriki waliotembelea mwambao wa Afrika Mashariki kiitwacho Periplus of the Erythrean Sea, kilichoandikwa mwaka 100 A.D. (kabla ya Nabii Issa), Zanzibar imetajwa kwa jina la ‘Menouthias’ ikiwa tayari ni nchi yenye watu mchanganyiko tena walio na ustaarabu wakiwa wanavaa nguo za hariri.”

Sasa alivyozungumza kwa uhakika ni kana kwamba wasomi wote duniani wanatambua kuwa “menouthias” ndiyo Zanzibar! Bila ya shaka Wazanzibari waliomsikia na kumsoma hivyo walifurahia mioyoni mwao kuwa kweli Zanzibar inatajwa katika maandishi ya kale.

Sitoshangaa kama watu wa Bara ambao hawajui historia yao waliinamisha vichwa vyao kwa sababu hawajui kama eneo lao linatajwa mahali popote au historia yao ndiyo imeanza mwaka 1884 au wanafikiria Bagamoyo ndiyo sehemu ya kale zaidi!

Kama Maalim Seif angependa kuwaambia ukweli wa Zanzibar juu ya miji ya kale na jamii za kale zilizowahi kutajwa kwenye maandishi ya kale, angewaambia watu wake juu ya mji wa kale wa Rhapta! Najua wengine mnajiuliza “ze what?”!

Katika kitabu hicho hicho cha maelezo ya safari za majini za kale katika bahari ya Hindi, kunatajwa vile vile mji wa Rhapta ambao tunaambiwa ulikuwa ni mji pwani ya Azania umbali wa usafiri wa kama siku mbili toka visiwa vya Menouthias.

Mmoja wa wataalamu wetu wa mambo ya kale Prof. Felix Chami anaweza kulielezea hili kwa kina kuwa siyo Zanzibar peke yake ambayo ina historia ya kale na kuwa watu wake walikuwa wakiishi katika jamii na kufanya biashara vizuri tu.

Ujio wa utawala wa Sultani

Katika historia yake hii mpya ya Zanzibar, Maalim Seif anadai kuwa “Mwaka 1503 Wareno waliivamia Zanzibar kupitia Unguja Ukuu na wakaitawala kwa muda mrefu wakifanya vitimbi vya kila aina. Waomani, kwa maombi ya wenyeji, walikuja katika Dola ya Zinj na kupambana na Wareno na hatimaye wakafanikiwa kuwatimua.” Katika hili tunaona mambo mawili yanayotajwa kwanza ni uvamizi wa Wareno (ambao kwa yeyote aneyejua historia haukukoma kwa visiwa hivyo tu) na pili “maombi ya wenyeji kwa Waoman”.

Kwamba Wareno walikuwa na vitimbi ni maneno machache; kwani historia yao inajulikana hadi Mombasa na Lamu. Tunapoambiwa kuwa wenyeji waliomba Oman ije kuwasaidia kuwaondoa Wareno, hatuambiwi ni wenyeji gani hao? Lakini wakati huo huo ni lazima tukumbuke kuwa utumwa ulikuwepo!

Yawezekana wenyeji waliotaka Oman kuja kuwaondoa Wareno walikuwa ni watumwa? Je watumwa walifaidika vipi na ujio wa Wa-Oman?

Balozi za kigeni huko Zanzibar

Maalim Seif anatuelezea katika hii historia mpya ya Zanzibar kuwa “Katika kipindi hiki Zanzibar iliweza kujitambulisha na kutambuliwa kama Dola huru katika ulimwengu. Zanzibar ikawa kituo muhimu cha kisiasa, kiuchumi na kibiashara katika Afrika Mashariki na Bahari ya Hindi.. Kutokana na umuhimu wake, madola makubwa yalifungua Ofisi za Kibalozi mjini Zanzibar : Marekani (1837), Uingereza (1841), Ufaransa (1844), na baada ya hapo Ureno, Utaliana, Ubelgiji na Ujarumani zikafuata.”

Mzanzibar ambaye hajui historia ya Zanzibar na mtu wa bara ambaye anayasoma maneno haya anaamini kabisa kuwa balozi hizo zilifunguliwa kwa sababu ya Zanzibar “kujitambulisha na kutambuliwa kama dola huru katika ulimwengu”.

Bahati mbaya ni kuwa kuna historia ambayo Maalim Seif hakutaka kuikiri hadharani inayohusiana na kufunguliwa kwa balozi hizo Zanzibar na siyo sehemu nyingine katika eneo letu hili. Naomba ruhusa nimkumbushe sehemu hii ya historia yetu.

Mwaka 1822 Sultan wa Oman, Sayyid Said Bin Sultan aliingia mkataba ujulikanao kama Mkataba wa Moresby. Mkataba huu, pamoja na mambo mengine, ulipiga marufuku uuzaji wa watumwa kwa nchi za Kikristu kutoka katika himaya yote ya Sultani huyo. Ni kutokana na mkataba huo na mingine iliyofuatia ndio nchi za Marekani, Uingereza , Ufaransa n.k zilipoamua kuanzisha ofisi zao za ubalozi huko ili kuhakikisha mojawapo ya mambo mengi kuwa Sultani wa Zanzibar anaheshimu makubaliano ya Moresby, Hamilton n.k

Ukiangalia tarehe ya kuanza kwa balozi hizo kama Maalim alivyoonyesha (1837) unaweza ukafikiria ni kwa bahati nzuri tu kuwa ndani ya miaka kama saba nchi mbalimbali za Kimagharibi zimefungua balozi zao huko?

Ikumbukwe kuwa mwaka 1832 (wanahistoria wengine wanaweka tarehe ya mbele kidogo) Sultani wa Oman alihamishia maskani yake kutoka Omani na kuwa Zanzibar makao makuu. Kutokana na ukaribu wake na nchi hizo za Magharibi Zanzibar hatimaye ilifanikiwa pole pole kukomesha utumwa na utumishi wa kulazimisha (servitude).

Omani, hata hivyo, ambayo tunaambiwa ndio walikuwa watu wema kwetu, waliendelea na hali hiyo kwa namna moja au nyingine hadi mwaka 1870 kufuatia mapinduzi yaliyomuingiza Sultan Qabus na Saudi Arabia yenyewe chini ya Mfalme Faysal ilifanya hivyo mwaka 1869!

Hii ni muhimu kuelewa kwa sababu ni sehemu ya Historia ya Zanzibar, na ni historia yetu vile vile. Hatuwezi kuikana, kujificha kwa haya au hata kuitaja kwa jina.

‘Uhuru’ wa Zanzibar ni uhuru?

Jambo jingine ambalo Maalim analielezea ni kuwa “Uingereza ilikabidhi uhuru kwa Zanzibar tarehe 10 Desemba 1963 chini ya Sultani na Serikali ya ZNP/ZPPP. ASP hawakuukubali uhuru huo na tarehe 12 Januari, 1964 ilifanya Mapinduzi na Zanzibar ikatangazwa kuwa Jamhuri.”

Wapo watu wanaoamini kabisa kuwa huu kweli ulikuwa ni “uhuru wa Zanzibar”. Ndio hawa ambao bado wanapata shida kuyatambua Mapinduzi ya Zanzibar na ulazima wa kwanini yalitokea. Unaweza kuliona hilo katika hotuba hiyo ya Maalim Seif.

Utaona mambo makubwa matatu ambayo ni sehemu ya historia ya Zanzibar hayatajwi kabisa na kama hilo hapo juu yanatajwa kama kwa kupita. Kwanza ni suala la utumwa na pili ni utawala wa Sultani wa Zanzibar na kama wananchi waliokuwa watumwa au watu weusi walinufaika na utawala huo.

Ndugu zangu, tunapotaka kujenga Zanzibar mpya na Tanzania mpya tuipendayo, hatuna budi kuwa wakweli kwa historia yetu. Tusiikane au kuona ni vibaya kuikiri. Wamarekani walikuwa na utumwa, Wamarekani walipigana wenyewe kwa wenyewe na zaidi ya nusu milioni walikufa.

Wamarekani walikuwa na ubaguzi wa rangi licha ya Katiba yao kutangaza usawa wa binadamu wote na haki zao. Leo hii Wamarekani wameweza kumchagua mtu mweusi kuwa Rais wao miaka chini ya hamsini tu tangu vurumai za mwamko wa haki za watu weusi nchini humo!

Bila ya kura za watu weupe Obama asingeweza kuwa Rais wa Marekani! Watu weusi wa Marekani ni kama asilimia 12 tu ya Wamarekani wote! Kwa maneno mengine, watu weupe ambao wamekuwa wakiangaliwa vibaya na kubebeshwa lawama za utumwa na ubaguzi na watu weusi walikubali historia yao na kuikumbatia na kujitokeza kumchagua mtu mweusi.

Hii ni historia yetu!

Hii ina maana kwetu leo hii. Waarabu, Wahindi, Washirazi na watu weusi wa Zanzibar na Tanzania Bara, ni lazima watambue kuwa hata tukimbie vipi, hata tujifiche vipi na hata tukwepe vipi, historia yetu imefungamana milele. Hata kina Maalim wasipotaja utumwa wasidhanie kuwa basi utafutika katika historia!

Na pia ni lazima tutambue kuwa kama taifa hatuwezi kuwabebesha Waarabu na Waoman wa leo mzigo wa dhambi ya utumwa na kuwaona kuwa ni waonevu juu yetu.

Kama vile Marekani, natambua wapo watu ambao bado hawamuoni mtu mweusi kuwa ana haki sawa na kumheshimu. Wapo watu weupe Marekani ambao hadi leo hii hawamtambui Obama kama Rais wao! Sitoshangaa wapo kati yetu uzao wa Wa-Oman na Waarabu wengine ambao wanaona watu weusi bado ni duni!

Na katika upotofu Fulani, wapo watu weusi ambao wanaamini kabisa kuwa bila ya wao kukubaliwa na Waarabu hao au na Washirazi, basi siyo binadamu hasa. Na wengine wamefikia hata kujiita “Waarabu” ili waonekane kukubalika. Huu ni upumbavu.

Waarabu wa Tanzania ni wananchi wenzetu na wana haki zote kama Watanzania wengine. Hawana haki au utu zaidi kwa sababu ya Uarabu wao.

Watu wenye asili ya Omani ambao vizazi vyao vimegawanyika Zanzibar na Oman wasijione kuwa wao ndiyo Waarabu hasa kulinganisha na Waarabu waliochangia damu na Wamanyema na Wanyamwezi wa Bara!

Wahindi ambao hawajachangia damu yoyote na watu weusi na wana vizazi Tanzania na India wasijifikirie kuwa wao ni watu bora zaidi na kuwa watu weusi bado ni maboi wao!

Nayasema haya ili ijulikane kwamba Tanzania tunayoitaka ni Tanzania yetu sote - historia ya Zanzibar ni historia ya Tanzania. Huu upuuzi wa kutaka kufanya watu wa Bara ni duni kwa sababu hawana historia ya taa za barabarani na televisheni za rangi, ni lazima ukome hata ukitolewa na wanasiasa tunaowapenda.

Huu mtindo wa “Zanzibar ilikuwa pepo na mapinduzi yakaharibu”, ni mtindo tunaopaswa kuukataa kwa nguvu zetu zote!

Ndiyo maana ni muhimu kujua kama kina Maalim Seif wanatambua ulazima wa mapinduzi yale na kuyakubali si kwa ajili ya kupata pointi za kisiasa bali kifalsafa na kimaadili. Ni lazima tujue kama kina Seif wanaweza kusema kuwa waliona matatizo yoyote ya utawala wa Sultani huko Zanzibar au wao bado wanaamini kuwa Sultani alionewa tu.

Na ndiyo maana katika haya pia mimi ninaamini kabisa kuwa mojawapo ya mambo ya kupatana Zanzibar ni lazima suala la Sultani lizungumzwe siku moja na kuhitimishwa, kwa sababu tunajua hadi leo hii Sultani wa Zanzibar hajakikana kiti chake cha Usultani wa Zanzibar na watoto wao bado wanaendelea kujitambua kuwa ni wana wa Sultan (Prince na Princesses).

Wote hawa ndugu zangu ni sehemu ya historia yetu na wakati umefika tuache kujitenga kwa mambo ya kijinga tukifirikia kuwa tunachofanya ni hekima na busara na ni uzalendo. Zanzibar haiwezi kukaa katika kivuli cha Sultani anayesubiri siku moja arudi na kukalia kiti chake!

Wananchi wa Zanzibar wasikubali hadaa ya maneno ya kisiasa, wasikubali kuimbiwa zumari za uongo na wao wakacheza.

Zanzibar ina historia yake na historia hiyo ina mazuri na mabaya yake kama vile ilivyo historia ya Uingereza, Japani, na China!

Historia hiyo ya Zanzibar ni historia ya Azania! Ni historia ya Tanzania yetu leo hii. Katika hili hatuna sababu ya kuomba radhi na Wazanzibari wasifikirie kuwa tutawaonea wivu. Wao ni sehemu yetu, sehemu ya damu yetu; kwani hatuwezi kamwe kuandika historia ya Tanganyika au Mwambao wa Afrika ya Mashariki bila kuandika historia ya Zanzibar.

Wana CCM Zanzibar wameliabisha taifa

Kitendo cha uongozi wa CCM Zanzibar kukubali na kukumbatia uongo kwa kisingizio cha “Zanzibar moja” ni cha hatari kwa muafaka wa taifa; kwani kinalenga kudhoofisha muungano na Rais Kikwete na Watanzania wasipoangalia ni ujumbe mkubwa wa kisiasa ambao matokeo yake hata kichaa anaweza kuyatabiri.

Wana CCM wa Zanzibar na Watanzania wa Zanzibar watambue kuwa wao ni sehemu ya jamhuri yetu, historia yetu ni historia yao na historia yao ni yetu. Tofauti za kisiasa na kimtizamo ni tofauti zinazozungumzika (hata leo hii majimbo ya Marekani na hata Uingereza wanazungumzia tofauti zao za kisiasa na kiutawala)

Katika kutafuta sifa za kisiasa, Rais wa Zanzibar asilipeleke taifa kwenye uchaguzi mbaya kwa kukumbatia uongo.

Vinginevyo, Dk. Karume atajikuta anafifisha na kudunisha na kudharau damu ya wale waliokufa katika mapinduzi na kufanya mapinduzi yale kuwa hayana maana yoyote! Historia itamhukumu vibaya sana akiendelea na maamuzi anayofanya sasa.

Kina Maalim wasitugawe sasa kwa historia wakifikiri wanatutendea hisani. Na nimeudhika kuona wana CCM wameingia katika mtego huu huko Zanzibar kiasi cha kupepea uongo kwa kanga zao za kijani na njano!

Ninaona fahari kuwa Zanzibar ni sehemu ya Tanzania. Ninaona fahari ya kujua historia yetu kama taifa.

Naomba niishie hapa. Nitajibu hoja zake za kisiasa alizozitoa wiki ijayo, inshallah.

Monday 18 January 2010

Bilal urges respect for isles constitution




AS calls for the extension of President Amani Abeid Karume presidency tenure mount among politicians here, former Chief Minister, Dr Mohammed Gharib Bilal, yesterday came out openly to say that the Zanzibar constitution that limits presidency to two terms should be respected.

He said that an argument by the opposition Civic United Front (CUF), for a change of the constitution to enable President Karume to seek a third term, ‘lacks legs to stand on.’

“This argument can not justify constitutional amendments and the postponement of the forthcoming general elections”, he said, adding: “We must respect and abide by the constitution.

Unfortunately, we still do not know much about an agreement between Karume and Hamad (CUF Secretary General).

Had we been aware, people would have discussed it in accordance with their agreement,” said Bilal, who vied for the presidency in the 2005 general elections, which saw Karume winning the slot. Dr Bilal said that CCM leaders would deliberate thoroughly on the issue, after receiving an official report.

“I recognise Karume/Hamad reconciliation and I also respect what the president said on constitutional presidency terms. However, I will respect the voice of the majority,” he added.

Dr Bilal shares sentiments with the CCM Deputy Secretary General for Zanzibar, Mr Salehe Ramadhan Feruz, who opposes the idea of constitutional change to allow Mr Karume to stand for a third term.

“I personally see no reason for changing the constitution, if the issue is to extend President Karume’s term, then it should be referred to party organs for deliberation,” Mr Feruzi said.

He maintains that the constitution should be respected and the amendment be accommodated in accordance with official party consensus.

Efforts to get comments from Zanzibar’s Speaker of the House of Representatives, Mr Pandu Ameir Kificho, Attorney General, Mr Idd Pandu Hassan, Minister of State in the Vice-

President’s Office (Union Matters), Mr Mohammed Seif Khatib and Deputy Chief Minister, Mr Ali Juma Shamuhuna, proved futile yesterday.

The push for extension of Mr Karume’s term agenda has been in limelight since he announced that the constitution does not allow him for another term.

Immediately, CUF came out strongly advocating for Karume to have another term in office, but with little public support from the CCM ranks.

CUF legislators are planning to meet this week to forge a common stand in lobbying and for delay of general elections, so as to allow President Karume's tenure in office.

CUF’s Secretary General and a senior official of the party, Mr Salum Bimani, have on different occasions been quoted supporting the adjournment of general elections in Zanzibar.

“We commend President Jakaya Kikwete for supporting the on-going reconciliation; there is no doubt that he will support every step.

We also thank Prof Issa Shivji for his open letter which fully supports the postponement of the elections,” the CUF leaders were quoted as saying on different occasions on Saturday, at a public rally held at Kibanda-maiti.

According to them, Zanzibar legislators (both from CCM and CUF), will unanimously support the adjournment of elections later this year and allow Mr Karume extra tenure in office.


Source: Daily News