Tuesday 24 July 2012

Tetesi: Karume atakiwa kurudisha kadi ya CCM

Makamo Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar Abeid Karume, Mshika Fedha wa CCM, na baadhi ya wajumbe wa baraza la wawakilishi watakiwa kurejesha kadi za CCM haraka baada ya kukiuka maadili ya chama chao.

Monday 23 July 2012

Hamad Masoud Amejiuzulu...


Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Hamad Masoud amejiuzulu rasmi leo jioni.

Sunday 22 July 2012

Nahodha Katapika


"Watu wameiba mamilioni ya fedha, wamepora maekari ya ardhi ya waznz lakini Leo hii akisimama na kusema hautaki muungano anaoenekana ndio mtetezi wa waznz" mh. Shamsi Nahodha

Wednesday 18 July 2012

Meli Kwa Jina la Skagit Imezama Karibu na Chumbe

Ilikuwa ikitokea Dar es Salaam kwenda Unguja, ikiwa na abiria 200. Kazi za uokoji zimeshaanza.

Boat za Sea Star na Kilimanjaro zimekwenda kwenye eneo la tukio kwa ajili ya uokoaji.. Habari zinasema kuwa miili ya abiria imeanza kuonekana ikielea. Hali ya bahari ina upepo mwingi kwa sasa.

Aidha kutokana na hali mbaya ya hewa meli moja imeshindwa kufika katika eneo la tukio na imerudi bandarini.

Mamia ya watu wapo bandarini Malindi wakiendelea kusubiri watakao okolewa.


Baadhi ya abiria waliookolewa