Saturday 12 January 2008

Leo ni Miaka 44 ya Mapinduzi ya Zenj

Kila la heri kwa wanamapinduzi wote wa Visiwa vya Zenj, hali kadhalika kwa wasomaji wote wa blog hii...

Mapinduzi Daima...

Katika moja ya vituko vilivyotokea katika shehere za mwanzo za kusherherekea Mapinduzi ya Zenj ni pale Marehemu A. Karume alipokuwa akitoa hotuba yake ambayo ilikuwa ikielezea mafanikio na faida za Mapinduzi hayo. Kwa sauti yake nzito sawa na kilo kadhaa za Nyati, ambayo kwa upande fulani iliwafanya wasikilizaji wake kuwa na kauoga fulani, alitamba kuwa serikali ya mapinduzi (wakati ule) ina fedha nyingi za kigeni(us dollar)zaidi ya idadi ya waakazi wa visiwa hivyo. Aliendelea kwa kusema kuwa fedha hizo ni nyingi kiasi kwa anaweza kumpatia kila mwananchi dola mia za kimarekani na bado fedha ikabaki.

Kijana mmoja kiasi cha miaka kumi na mbili hivi, alinyosha mkono ili aweze kuuliza swali,Wazee waliokuwa karibu yake walijaribu kumzuia kijana huyo kutonyosha mkono. Purukushani hizo zilivuta idadi kubwa ya watu kutazama upande wao, badala ya kuendelea kusikiliza hotuba. Hali hii ilimfanya Marehemu Karume kumruhusu kijana huyo aulize swali lake. Huku akijiamini sana kijana huyo aliuliza hivi..

"Mhe. mimi naomba kupatiwa dola zangu mia sasa hivi..."

No comments: