Thursday, 13 August 2009

Wednesday, 12 August 2009

Usafirishaji wa Mizigo Zenj...








Usafirishaji wa mizigo kwa kutumia Wanyama ulipigwa marufuku kufanyika ndani ya mipaka ya Halmashauri ya Manispaa ya Zanzibar mara baada ya Mapinduzi. Hata hivyo kidogo kidogo magari ya mizigo ya Punda na Ng'ombe yamerudi tena kubeba mizigo ndani ya Manispaa.




Mkokoteni huko Pemba

Tuesday, 11 August 2009

Friday, 7 August 2009

Wapemba waendeleza ual-qaeda...!


Baada ya Uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1995,Visiwa vya Zenj vilishuhudia vituko kibao, ikiwa ni pamoja na mabomu ya baruti na ya petroli yakilipuriwa katika maeneo mbali mbali ya visiwa hivyo. Toka katika maakazi ya watu, ofisi za serikali na hata sehemu nyeti kama za usambazaji wa umeme visiwani humo zilipata makasheshe ya milipuko ya mabomu. Mabomu mengine yaliweza kulipuka huku mengine yakishindwa kulipuka.

Kipindi hicho kilikuwa ni kabla ya ulipuaji wa mpigo(sambamba)wa mabomu kuanza. Ni katika mwaka 1998 ambao ulipuaji wa sambamba uliponza na kukikuhisha kikundi maarufu cha Al-Qaeda, pale walipoweza kulipua kwa wakati mmoja ofisi ya balozi wa Marekani katika majiji ya Dar es Salaam na Nairobi.

Hapo Majuzi nyumba za Masheha huko Pemba ziliweza kulipuliwa kwa staili hiyo na kufanya wengi kufananisha milipuko hiyo kama ile ya kundi la Al-Qaeda. Huu ni muendeelezo wa ulipuaji wa mabomu huko Pemba kwa madai ya kuwa Masheha wanawanyima wakaazi wa huko kuandikishwa kwenye daftali la kudumu la kupiga kura.

Wapemba katika hili wapo mbele, kwa kumbukumbu za haraka haraka, tokea uchaguzi wa mwaka 1995, kumekuwepo na vituko vingi sana huko Pemba, kama vile vya kugeuza visima vya maji kuwa vyoo, kupaka vinyesi katika skuli,ili kuzuia wanafunzi kusoma, kunyang'nya polisi silaha na kuteka kituo cha polisi, kususia shughuli za maziko na arusi, kubagua watu wa kufanya biashara nao, talaka kwa wanandoa kutokana na tofauti za kisaisa na vituko vingine kaza wa kaza.

Pamoja na yote, ili la mabomu ambalo linaendela sasa, linatakiwa kuchukuliwa hatua za haraka la kulidhibiti, kwani litaweza kuleta madhara makubwa sana hapo mbele, na hasa siku ambayo Wapemba hao watakaweza kuwa na mabomu yenye nguvu(haya ya sasa hayana nguvu kubwa)au mabomu ya sumu! Hivyo basi ni vema kwa vyombo vinavyohusika kuwatafuta watu hawa wanaolipua mabomu na kuwafikisha kwenye vyombo husika. Na ni wakati wa kuanza kuitumia sheria ya magaidi iliyotungwa mara baada ya milipuko ya Dar na Nairobi.

7th August 2009

Nyumba za Masheha wawili zalipuliwakwa mpigo

Milipuko miwili tofauti imetokea sambamba nyumbani kwa masheha wawili kisiwani Pemba na kusababisha zaidi ya watu 30 kunusurika kifo.
Akizungumza na Nipashe juu ya matukio hayo yanayofanana na ile milipuko ya kupanga ya kikundi cha kigaidi cha Al- Qaeda kwa kulipuka kwa wakati mmoja, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, Yahya Bugi, alisema matukio hayo ni ya kupanga.
Alisema katika tukio la kwanza, watu wasiojulikana walitega bomu la kutengenezwa kienyeji kwa kutumia baruti (TNT) na kulilipua nyumbani kwa Sheha wa Mihogoni, Salim Said Salim (59).
Kamanda huyo aliliambia Nipashe kwamba nyumbani kwa Sheha Salim kulikuwa na mkusanyiko wa watu waliokuwa wakihudhuria harusi nyumbani kwake saa sita usiku wa kuamkia jana.
Alisema bomu hilo lililipuka wakati Sheha na wageni wake wakiwa wamelala na kusababisha athari kubwa kwenye ukuta wa nyumba yake na mabati sita yaliyoezekwa nyumba hiyo kung’oka.
Kamanda Bugi alisema kwa mujibu wa Sheha Salim, walisikia kishindo kikubwa kikitokea nyuma ya nyumba yao na baada ya kukimbilia katika eneo hilo waliwaona vijana wawili wakikimbilia eneo lenye migomba.



Zaidi: tembelea Nipashe

Thursday, 6 August 2009

Pinda amefulia...


Kwa kauli yake juu ya Muungano Waziri Mkuu Mizengo Pinda amefulia na ameonyesha ufahamu mdogo juu ya Muungano huu. Kauli yake ya kuondoa kero za muungano ni kuifuta SMZ haiwezi ikaachwa hivi hivi. Kauli ambayo aliitoa huku akijua kuwa hakuna dalili zozote za sasa za SMT kujaribu kuondoa kero za Muungano achilia mbali jitihada za kuona kuwa Muungano unakwenda vizuri zaidi ya kuburaza upande mmoja wa Muungano. Kauli yake inaweza kuwa sahihi iwapo Muungano huu utakuwa hauna kero yoyote na nchi zote mbili kuridhia kuwa hakuna kero.

Zaidi Pinda anahitaji kupatiwa tuition ya haraka kuhusu Muungano na mambo yote ambayo yahusianayo na Muungano huo. Hii itamuwezesha kujua na kupata ufahamu mkubwa wa Muungano huu kabla ya kujikuta akishitumiwa na kuandamwa na Katiba na kukimbilia kulia.

Wednesday, 5 August 2009

Tuesday, 4 August 2009

Mwakilishi adai wizi wa watoto umekithiri Zanzibar


WAJUMBE wa Baraza wameishauri Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kufuatilia kwa kina upoteaji wa watoto katika maeneo mbalimbali pamoja na kushughulikia suala la utumiaji wa dawa za kulevya nchini.

Walitoa ushauri huo jana walipokuwa wakichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Kazi Maendeleo ya Vijana, Wanawake na watoto kwa mwaka wa fedha 2009/10 katika kikao cha baraza la wawakilishi kinachoendelea Mjini Unguja.

Mwakilishi kupitia Wanawake (CCM), Raya Suleiman Hamad, alisema kuna haja kwa serikali kuanzisha uchunguzi huo kwani watoto wengi wanapotea ovyo katika mitaa yao, huku wazazi wao wakiwa wanahangaika kuwatafuta bila ya mafanikio.

Alisema kwamba inavyonekana wapo baadhi ya watu wanaoendesha biashara ya kuiba watoto jambo ambalo tayari limeanza kuwatia hofu baadhi ya wazazi nchini.

Mwakilishi huyo alisema kwamba watu wanaoendesha vitendo hivyo hutumia njia za kuwahadaa kwa kuwafuata watoto na kuwapa fedha kisha wanawasihi wawafuate ili wakawanunulie nguo.

Mwakilishi huyo alitoa mfano katika mtaa wa Nyerere kwamba kuna kesi za kupotea watoto wanne na kwamba hadi sasa hawajapatikana pia hawajulikani walipotea katika mazingira gani.

Aliitaka serikali ichukue hatua za kufanya utafiti juu ya suala hilo kwa vile tayari limeanza kuwatisha wananchi na linaweza kusababisha madhara makubwa baadaye

Alisema wakati serikali ikilitafakari hilo, ni vyema hivi sasa kuangaliwa uwezekano katika bandari na Viwanja vya Ndege watu wanaoonekana kubeba watoto wakahojiwa uhalali wao.

Mwakilishi huo pia alizungumzia suala ubakaji wa watoto kuendelea ikiwa pamoja na wagonjwa wa akili na kutaka vyombo vya sheria kutekeleza majukumu yao bila ya upendeleo kwani matendo kama hayo yakiachwa yanaweza kuhatarisha usalama kwa watoto .

Akitoa mifano Mwakilishi huyo alisema iliyowahi kujitokeza kisiwani Pemba baada ya mtoto mmoja kubakwa lakini kesi yake ilipopelekwa Polisi wamekuwa wakishindana na Polisi kwa kuwaeleza wahusika hawana la kufanya na waende wakamkamate mhusika wampeleke kituoni hapo.

Mwakilishi huyo pia alisema ni lazima serikali iandae mkakati maalum wa kukabiliana na tatizo hilo kwani suala la madawa ya kulevya linaonekana kama vile limeshindikana kutokana waletaji na wauzaji wa dawa hizo kuwa wanafahamika lakini hawachukuliwi hatua zozote za kisheria wakati vijana wengi wanazidi kuharibika na utumiaji wa madawa hayo.

Friday, 31 July 2009

SMZ:- Serikali Iliyokosa Dira




Ilikuwa ni katika awamu ya mwisho ya Komandoo, ambapo wazenj wengi walipata fursa ya kudhaminiwa na serikali yao ili kuongeza elimu yao na taaluma zao. Lengo lilikuwa ni kusomesha wazenji wengi kadiri uwezo wa serikali ya SMZ inavyoruhusu. Na ni kipindi hikohiko ambapo kulikuwa na wimbi la wakimbizi wa Kizenj kukimbilia hifadhi huko Uingereza. Ni kipindi hikohiko ambapo Komandoo alionekana kuwa ni msaliti baada ya jitihada zake za kubadili katiba kugonga ukuta. Zaidi ni kipindi hicho hicho ambacho wazenj waliona ongezeko kubwa la mapato yao na mabadiliko mengi katika miji yao. Kwa ufupi ni kipindi ambacho wizara ya fedha ilikuwa ni maarufu zaidi katika historia ya SMZ, ikifanya kazi nje ya uwezo wake huku ikivamia kazi za wizara zingine.

Ilikuwa ni mwaka 1996 ambapo SMZ kupitia Wizara ya fedha ilioanza kupeleka wafanyakazi wake na wasio wafanyakazi kwenda kusoma kwa wingi, hata hivyo kozi nyingi zilikuwa zile ambazo zinaweza kufanyika Tanzania Bara. Zenj ilishuhudia masekretari wakipelekwa kusoma UK na Malaysia, wakati kuna chuo cha Uhazili hapo Tabora, kozi za zilikuwa za chini ya mwaka mmoja na wengi hawakurudi tena kupiga chapa na kupokea wageni na sasa wanakula benefit zao huko UK wakijiita Wasomali ama Warundi. Na ni baada ya kuona wakimbizi wa kizenj wakifaidi benefit za UK. Kumbuka kuwa licha ya tofauti za kisiasa zinazo onekana nje ya wazenj, wengi wao wapo pamoja kimashauri na kimaisha kwani kwa namna moja ama nyingine wamehusiana.

Mwaka mmoja baade bila kupima mafanikio ya wanafunzi waliotangulia, SMZ ilikusanya masekreatari na wafanyakazi wengine na wake wasio na kazi na kuwapeleka Malaysia ili kuongeza ujuzi wao. Kwa wale ambao walikuwa hawana ajila katika SMZ walihaidiwa kupewa ajila mara watakapo maliza masomo yao.

Mtiririko mzima wa kwenda huko ulisimamiwa na wizara ya fedha, wala hapakuwa na haja ya kwenda Idara ya Utumishi ili kuweza kupata nafasi ya kwenda huko. Ilikuwa ni kwenda moja kwa moja wizara ya fedha na kueleza adhma yako ya kusoma, wao walitoa mkataba wao na biashara kuishia hapo hapo.

Kama katika mwaka uliotangulia wengi walikuwa ni masektretari, wakifuatiwa kwa karibu na wanafunzi waliopenda kusoma Computer Science, huku wengine wakitaka kusoma Business Management na baadhi kutoka katika idara za uhandisi. Tatizo kubwa lilikuwa hapa kwenye Uhandisi, kwani chuo ambacho SMZ iliingia nao mkataba hawakuwa na fani nyingi za uhandisi zaidi ya umeme! Hivyo kupelekea wafanyakazi toka idara ya Maji, TVZ, Manispaa kulazimika kusomea umeme! Kulikuwa na kundi lingine ambalo lilipenda kusomea Uhasibu na kundi la Sheria, hata hivyo wengi wao walipenda kozi hizo kutokana na ndota zao na walipoanza masomo walijikuta wakishindwa vibaja. Mbaya zaidi Idara ya Utumishi ilikataa kabisa kuwatambua kwa wale wachache waliorudi tena Zenj...

Muda wa kozi unatofutiana, hivyo masekretari walikuwa ndio wa mwanzo kurudi Zenj, katika kipindi chote ambacho walikuwepo hapa Kuala Lumpar na Petaling Jaya, Wanafunzi walishuhudia ziara zisizo na kikomo za viongozi wa ngazi za juu, malipo ya posho zao kwa wakati na kadhalika. Maisha yalikuwa ni mazuri sana na yenye neema nyingi.

Baada ya masekretari kuondoka, ndipo picha halisi ya SMZ kwa wanafunzi wake ilipoonekana. Huduma nyingi muhimu zilipunguwa ama kusimamishwa kabisa. Hii ilijenga chuki na hasira kwa wanafunzi juu ya serikali yao. Mbaya zaidi ni kujua kuwa hata wale ambao wamerudi Zenj wameshindwa kutambuliwa na Idara ya Kazi, hivyo ni sawa kama hawakusoma chochote kile.

Wanafunzi wengi walianza kufikilia kama kuna umuhimu wowote wa kurudi tena Zenj, hawa na pamoja na wale ambao tayali walikuwa wameajiliwa na SMZ. Huku ukumbizi ukizidi kuvuma visiwani humo, wengi waliona ni heri kutorudi tena visiwani huko. Tatizo lilikuwa ni fedha, kwani katika siku za mwisho mwisho SMZ ilikata kutuma fedha, na kutoa ahadi kuwa malipo yatafanyika mara wanafunzi watakaporudi visiwani. Kwao hili halikuwa tatizo kubwa. Na mara baada ya kurudi na kulipwa wengi walikimbilia UK na USA ambapo wapo hadi sasa.

Wanafunzi waliobaki Malaysia waliona joto ya jiwe,kwani walifikia kushindwa hata kulipia pango la nyumba zao na kujikuta wakifukuzwa. Hata hivyo wengi katika waliobaki walikuwa bado na mapenzi makubwa na SMZ hivyo baada ya miaka yao kadhaa walirudi nyumbani na kukutana na kadhia dhidi ya Idara ya Utumishi ambayo ilitaa kuwatambua, mbaya zaidi Komandoo alikuwa atayali amemaliza muda wake. hiki kilikuwa ni kipindi cha Karume ambaye aliamua kwa makusudi kutowatambua wanafunzi hao.

Cha msingi ni kujiuliza ni kwa nini SMZ chini ya Karume ilishindwa kuwatambua wanafunzi ambao waliona bora kurudi nyumbani ili kuendeleza maendeleo ya visiwa hivyo. Ukiangalia kwa kina utaona ni mabo mengi ambayo yalianzishwa na Komandoo yalibezwa na Karume, huku idara ya Utumishi ikilipa kisasi kwa kunyang'anywa kazi yake ya kusomesha wanafunzi wafanyakazi na wizara ya fedha. Mambo mengi yaliamuriwa kutokana na utashishi binafsi pasipo kufuata taratibu za kisheria, kiasi cha kuona kuwa SMZ haina dira yotote katika kumwendeleza mwanachi wake.

Leo hii ukiangalia ni wangapi katika mamia wale ambao walisomeshwa na SMZ, ambao bado wapo hapo visiwani ni kichekesho. Mpaka leo hii SMZ inadaiwa na wanafunzi hao, na Karume ambae mwakani anamaliza muda wake katia pamba masikioni mwake! Hataki kusikia chochote kuhusu madai wa wanafunzi hao! Na sio kama haoni mafanikio ya wale wachache waliobaki ili kuendeleza nchi hiyo bali ni kwa kuwa SMZ yote kwa ujumla haijui inafanya nini.... ipo ipo tu!

Wednesday, 29 July 2009

Kadhia hii kwisha yakianza kuchimbwa...?


Vespa inapokuwa inainamishwa upande mmoja ni dalili ya upungufu wa wese, hata hivyo kwa muda sasa kumekuwepo na malumbano marefu juu ya uchimbaji wa mafuta huko Zenj na umiliki wa mafuta hayo... Je iwapo mafuta hayo yatachimbwa chini ya umiliki wa Zenj, kadhia hii kwa maelfu wa wenye vyombo vya moto visiwani humo itakuwa imefikia kikomo?

Tuesday, 14 July 2009

Ngoma Africa Band Kupeleka Moto Mwingine Tampere! Finland




The Ngoma Africa Band aka FFU! wanatarajiwa kutumbuiza katika onyesho la
FEST AFRIKA, mjini Tampere, huko Finland siku ya Jumamosi 18-07-2009.

Katika maonyesho hayo pia kutakuwapo na bendi nyingine za mziki na vikundi vingine vingi vya sanaa za maonyesho kikiwemo kikundi maarufu cha The Mpondas Group chenye maskani yake mjini Tampere.bendi ya The Ngoma Africa ilikuwapo Ufini mwanzoni mwa mwezi wa February mwaka 2009 katika misimu wa barafu huko ufini,na kufanikiwa kuwasha moto wake wa mziki.

Wadau wa Scandinavia bendi yenu inakuja kufanya kazi mliyowatuma kufanya nanyo ni mziki moto moto!.

The Ngoma Africa bendi inayotingisha majukwaa kila kukicha bado inaendelea na kufuka majukwaa kama vile moto wa nyikani.

Wasilikize hapa www.myspace.com/thengomaafrica ukiwataka ngoma4u@googlemail.com

Sunday, 5 July 2009

Kujinafsi....