Friday 7 August 2009

Wapemba waendeleza ual-qaeda...!


Baada ya Uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1995,Visiwa vya Zenj vilishuhudia vituko kibao, ikiwa ni pamoja na mabomu ya baruti na ya petroli yakilipuriwa katika maeneo mbali mbali ya visiwa hivyo. Toka katika maakazi ya watu, ofisi za serikali na hata sehemu nyeti kama za usambazaji wa umeme visiwani humo zilipata makasheshe ya milipuko ya mabomu. Mabomu mengine yaliweza kulipuka huku mengine yakishindwa kulipuka.

Kipindi hicho kilikuwa ni kabla ya ulipuaji wa mpigo(sambamba)wa mabomu kuanza. Ni katika mwaka 1998 ambao ulipuaji wa sambamba uliponza na kukikuhisha kikundi maarufu cha Al-Qaeda, pale walipoweza kulipua kwa wakati mmoja ofisi ya balozi wa Marekani katika majiji ya Dar es Salaam na Nairobi.

Hapo Majuzi nyumba za Masheha huko Pemba ziliweza kulipuliwa kwa staili hiyo na kufanya wengi kufananisha milipuko hiyo kama ile ya kundi la Al-Qaeda. Huu ni muendeelezo wa ulipuaji wa mabomu huko Pemba kwa madai ya kuwa Masheha wanawanyima wakaazi wa huko kuandikishwa kwenye daftali la kudumu la kupiga kura.

Wapemba katika hili wapo mbele, kwa kumbukumbu za haraka haraka, tokea uchaguzi wa mwaka 1995, kumekuwepo na vituko vingi sana huko Pemba, kama vile vya kugeuza visima vya maji kuwa vyoo, kupaka vinyesi katika skuli,ili kuzuia wanafunzi kusoma, kunyang'nya polisi silaha na kuteka kituo cha polisi, kususia shughuli za maziko na arusi, kubagua watu wa kufanya biashara nao, talaka kwa wanandoa kutokana na tofauti za kisaisa na vituko vingine kaza wa kaza.

Pamoja na yote, ili la mabomu ambalo linaendela sasa, linatakiwa kuchukuliwa hatua za haraka la kulidhibiti, kwani litaweza kuleta madhara makubwa sana hapo mbele, na hasa siku ambayo Wapemba hao watakaweza kuwa na mabomu yenye nguvu(haya ya sasa hayana nguvu kubwa)au mabomu ya sumu! Hivyo basi ni vema kwa vyombo vinavyohusika kuwatafuta watu hawa wanaolipua mabomu na kuwafikisha kwenye vyombo husika. Na ni wakati wa kuanza kuitumia sheria ya magaidi iliyotungwa mara baada ya milipuko ya Dar na Nairobi.

7th August 2009

Nyumba za Masheha wawili zalipuliwakwa mpigo

Milipuko miwili tofauti imetokea sambamba nyumbani kwa masheha wawili kisiwani Pemba na kusababisha zaidi ya watu 30 kunusurika kifo.
Akizungumza na Nipashe juu ya matukio hayo yanayofanana na ile milipuko ya kupanga ya kikundi cha kigaidi cha Al- Qaeda kwa kulipuka kwa wakati mmoja, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, Yahya Bugi, alisema matukio hayo ni ya kupanga.
Alisema katika tukio la kwanza, watu wasiojulikana walitega bomu la kutengenezwa kienyeji kwa kutumia baruti (TNT) na kulilipua nyumbani kwa Sheha wa Mihogoni, Salim Said Salim (59).
Kamanda huyo aliliambia Nipashe kwamba nyumbani kwa Sheha Salim kulikuwa na mkusanyiko wa watu waliokuwa wakihudhuria harusi nyumbani kwake saa sita usiku wa kuamkia jana.
Alisema bomu hilo lililipuka wakati Sheha na wageni wake wakiwa wamelala na kusababisha athari kubwa kwenye ukuta wa nyumba yake na mabati sita yaliyoezekwa nyumba hiyo kung’oka.
Kamanda Bugi alisema kwa mujibu wa Sheha Salim, walisikia kishindo kikubwa kikitokea nyuma ya nyumba yao na baada ya kukimbilia katika eneo hilo waliwaona vijana wawili wakikimbilia eneo lenye migomba.



Zaidi: tembelea Nipashe

Thursday 6 August 2009

Pinda amefulia...


Kwa kauli yake juu ya Muungano Waziri Mkuu Mizengo Pinda amefulia na ameonyesha ufahamu mdogo juu ya Muungano huu. Kauli yake ya kuondoa kero za muungano ni kuifuta SMZ haiwezi ikaachwa hivi hivi. Kauli ambayo aliitoa huku akijua kuwa hakuna dalili zozote za sasa za SMT kujaribu kuondoa kero za Muungano achilia mbali jitihada za kuona kuwa Muungano unakwenda vizuri zaidi ya kuburaza upande mmoja wa Muungano. Kauli yake inaweza kuwa sahihi iwapo Muungano huu utakuwa hauna kero yoyote na nchi zote mbili kuridhia kuwa hakuna kero.

Zaidi Pinda anahitaji kupatiwa tuition ya haraka kuhusu Muungano na mambo yote ambayo yahusianayo na Muungano huo. Hii itamuwezesha kujua na kupata ufahamu mkubwa wa Muungano huu kabla ya kujikuta akishitumiwa na kuandamwa na Katiba na kukimbilia kulia.

Wednesday 5 August 2009

Tuesday 4 August 2009

Mwakilishi adai wizi wa watoto umekithiri Zanzibar


WAJUMBE wa Baraza wameishauri Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kufuatilia kwa kina upoteaji wa watoto katika maeneo mbalimbali pamoja na kushughulikia suala la utumiaji wa dawa za kulevya nchini.

Walitoa ushauri huo jana walipokuwa wakichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Kazi Maendeleo ya Vijana, Wanawake na watoto kwa mwaka wa fedha 2009/10 katika kikao cha baraza la wawakilishi kinachoendelea Mjini Unguja.

Mwakilishi kupitia Wanawake (CCM), Raya Suleiman Hamad, alisema kuna haja kwa serikali kuanzisha uchunguzi huo kwani watoto wengi wanapotea ovyo katika mitaa yao, huku wazazi wao wakiwa wanahangaika kuwatafuta bila ya mafanikio.

Alisema kwamba inavyonekana wapo baadhi ya watu wanaoendesha biashara ya kuiba watoto jambo ambalo tayari limeanza kuwatia hofu baadhi ya wazazi nchini.

Mwakilishi huyo alisema kwamba watu wanaoendesha vitendo hivyo hutumia njia za kuwahadaa kwa kuwafuata watoto na kuwapa fedha kisha wanawasihi wawafuate ili wakawanunulie nguo.

Mwakilishi huyo alitoa mfano katika mtaa wa Nyerere kwamba kuna kesi za kupotea watoto wanne na kwamba hadi sasa hawajapatikana pia hawajulikani walipotea katika mazingira gani.

Aliitaka serikali ichukue hatua za kufanya utafiti juu ya suala hilo kwa vile tayari limeanza kuwatisha wananchi na linaweza kusababisha madhara makubwa baadaye

Alisema wakati serikali ikilitafakari hilo, ni vyema hivi sasa kuangaliwa uwezekano katika bandari na Viwanja vya Ndege watu wanaoonekana kubeba watoto wakahojiwa uhalali wao.

Mwakilishi huo pia alizungumzia suala ubakaji wa watoto kuendelea ikiwa pamoja na wagonjwa wa akili na kutaka vyombo vya sheria kutekeleza majukumu yao bila ya upendeleo kwani matendo kama hayo yakiachwa yanaweza kuhatarisha usalama kwa watoto .

Akitoa mifano Mwakilishi huyo alisema iliyowahi kujitokeza kisiwani Pemba baada ya mtoto mmoja kubakwa lakini kesi yake ilipopelekwa Polisi wamekuwa wakishindana na Polisi kwa kuwaeleza wahusika hawana la kufanya na waende wakamkamate mhusika wampeleke kituoni hapo.

Mwakilishi huyo pia alisema ni lazima serikali iandae mkakati maalum wa kukabiliana na tatizo hilo kwani suala la madawa ya kulevya linaonekana kama vile limeshindikana kutokana waletaji na wauzaji wa dawa hizo kuwa wanafahamika lakini hawachukuliwi hatua zozote za kisheria wakati vijana wengi wanazidi kuharibika na utumiaji wa madawa hayo.