Thursday 28 January 2010

BLW: Hoja ya Serikali ya Kitaifa Yawasilishwa Leo...




Dondoo 5 za hoja ya msingi ni -

1. BLW liyaridhie na kuyapa nguvu Maridhiaano.

2. Uanzishwe mfumo serikali ya Umoja wa Kitaifa itayohusisha vyama vya siasa vyenye wajumbe ndani ya BLW.

3. Serikali hiyo ya Umoja wa Kitaifa izingatie uwiano kwa mujibu wa kura za urais.

4. Baraza lifanye marekebisho ya vifungu vya 39, 42 na 62 ili kuweka utaratibu wa serikali ya Umoja wa kitaifa.

5. Baraza liweke utaratibu wa kura za maoni, referendum.


Source: JF

Tuesday 26 January 2010

Maridhiano: Alichosahau Maalim Seif...


Maalim Seif katika taarifa yake ya Maridhiano na Mustakbali wa Zanzibar, amezungumzia mengi juu ya Zanzibar ilipotoka hadi ilipo sasa. Cha ajabu hakuzungumzia kabisa juu ya kuwepo kwa utumwa visiwani humo, kama inavyoonekana kwenye picha hapo juu.

Sunday 24 January 2010

Maridhiano: Sasa yaandaliwa sherehe...



CUF kusherehekea ushindi

Wakati hali ya kisiasa Visiwani ikiingia katika historia mpya, taarifa zilizopatikana mjini hapa zimedai kuwa Chama cha CUF kinafanya maandalizi ya kusherehekea ushindi baada ya kufanikiwa kuwashawishi baadhi ya vigogo wa CCM Zanzibar kukubali kuundwa kwa Serikali ya mseto kabla ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu uliopangwa kufanyika mwezi Oktoba.

Katika maandalizi hayo ambayo inasemekana yanafanyika kwa usiri mkubwa, viongozi wa CUF wanaelezwa kukubaliana na mapendekezo ya Baraza la Mawaziri ambalo litajumuisha na wenzao wa CCM katika Serikali ya muda itakayoongozwa na Rais wa sasa wa Zanzibar, Amani Abeid Karume.

Chanzo cha habari hizi kimedai kuwa chini ya mapendekezo hayo, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad atakuwa Waziri Kiongozi nafasi ambayo kwa sasa inashikiliwa na Shamsi Vuai Nahodha ambaye anakusudiwa kutupwa nje ya Baraza jipya la Mawaziri.

Wengine waliopendekezwa na Wizara zao zikiwa kwenye mabano ni Mansoor Yussuf Himid–CCM (Mafuta na Nishati), Samia Suluhu Hassan-CCM (Afya), Juma Dui Haji – CUF (Biashara Utalii na Uwekezaji), Nassor Mazrui-CUF (Fedha), Dk. Mwinyihaji Makame Mwadini-CCM( Kilimo, Ardhi na Maji).

Wengine ni Fatma Abdulhabib Ferej-CUF (Wanawake, Watoto Maendeleo ya Vijana), Burhan Saadat Haji-CCM (Mawasiliano), Machano Othman Said-CCM (Waziri wa Tawala za Mikoa na Vikosi Maalum), Asha Abdulla Juma-CCM (Elimu), Abbas Juma Muhunzi-CUF( Ofisi ya Waziri Kiongozi), Ali Juma Shamuhuna – CCM (Ofisi ya Rais).

Kiongozi wa Upinzani katika Baraza la Wawakilishi, Abubakar Khamis Bakar amependekezwa kuwa Waziri wa Katiba na Utawala Bora.

Chanzo hicho kimedai kuwa mapendekezo hayo ya Baraza la Serikali ya muda yamekuwa yakisambazwa kwa vigogo wa CUF tu ikiwa ni ishara kwao ya ushindi wa suala walilokuwa wakilitaka la kuwepo ndani ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Pamoja na hali hiyo, kundi la wajumbe ambao wanapinga harakati hizo ni kubwa na ambalo linaundwa na wanasiasa wenye ushawishi mkubwa wa siasa za Tanzania na kwa namna hali inavyokwenda kikao hicho cha Kamati Maalum kitatawaliwa na vijembe vingi na upinzani mkali kwa watu waliopachikwa jina la ‘Uhafidhina’.

Tayari Kiongozi wa Upinzani katika Baraza la Wawakilishi Abubakar Khamis Bakar ameshawasilisha hoja binafsi kwa Katibu wa Baraza akitaka kufanyike marekebisho ya katiba yatakayoruhusu kubadilisha mfumo wa utawala wa SMZ kwa kuwa na Serikali ya mseto.

Idadi kubwa ya wafuasi wa CCM na viongozi wamekuwa wakipinga suala la kuongezwa muda kwa Rais Karume pamoja na kuwepo kwa Serikali ya mseto Zanzibar wakidai kuwa mazingira hayaruhusu kwa uundwaji wa serikali hiyo na kusisitiza msimamo wa utekelezaji wa azimio la CCM Butiama.

Saturday 23 January 2010

Umeme wa uhakika kurudi 2012 huko Zenj...


New power supply cable for Isles to be built in 2012

The Zanzibar government yesterday disclosed that the project to lay-down a new sub-marine cable for power supply to the Isles from Tanzania Mainland will be completed in 2012, after the US government reduced the project implementation timeframe.

This was said by Isles Minister for Water, Construction, Energy and Lands Mansour Yussuf Himid, when responding to questions by Members of the House of Representatives here yesterday.

He said previously, the project was set for completion by 2013, but the Isles government requested the US Government to reduce the timeframe due to power problems facing Zanzibar.

The minister told the House that the tendering process had been floated and would be opened on February 19, this year.

Himid said already various companies had applied for the implementation of the long-awaited project adding that the financier of the project, Millennium Challenge Corporation (MCC), would go through all processes of picking the winner from the bidding firms.

The new power supply route would have the capacity of 100MW from the Tanzania Electric Supply Company Limited (Tanesco), he said, adding that the cable would pass under the Indian Ocean from Kiromono Cape on the Mainland to Fumba in Zanzibar.

Zanzibar spends 1.2bn/- every month in power expenses from the Mainland, however Isles customers have been living without hydro-electric power supply since December last year, after a key electric device exploded at Fumba main power station.