Wednesday, 10 March 2010

Huu ni Ujuha au Ujuhaji?


Waznz hatutaki Njia zetu kuitwa majia ya makafiri hawa akina Mkapa na ndugu zake hawana historia zozote znz, kama mumeshindwa kuwa enzi wana vyuoni wetu basi bora muite jina la Bi Kitute Road wazanzibar tutarizika.

Wanao jizalilisha ni ccm-smz sio wazanzibar wote, kuna wana vyuoni wetu na watu wenye historia mzuri Zanzibar na wazanzibar wana zipenda kwa nini hamukuita mumekwenda kuita majina ya wauwaji na walioasha asari za viwete na vizuka. Wakadi kuna historia zetu wenyewe wazanzibar. Au ndio kutawaliwa smz huko? Mungeita barabara ya Sh Amer Tajo,Sh Abdalla Farth,Sitti Binti Sadi, Mwana wa Mwana na Mkama Tume. Hizi ndio historia zetu. Lakini ccm-smz mumeoza kwa watawala wa ki-Tanganyika kama. Kama tulivyo piga kelele iondoshwe historia mpovu isisomeswe maskulini watoto wetu isio wahusu wazanzibar na kuaswa historia yao wazanzibar nah ii ya bara bara iondoswe mara moja.

Zamani utaona watoto wetu wanasomeswa vita vya wahehe na wamanyema vita vya majimaji lakini hatujawahi hata siku moja kusomeswa watoto wetu kuhusu Mkama ndume na Mwana wa Mwana tunasomeswa watoto wetu makabila hata hapa Zanzibar hayapo. Wewe umeona wapi kabila la wahehe hapa? Au wamanema kama sio vishekesho bora kusema Wazaramu wapo Miembeni na kwahani na sasa tuna Wamasai Kiwengwa historia ya badae zenj. Kwa hio wazanzibar tustuke tusikubali kupashikizwa historia zisizo tuhusu.

Hiyo hapo juu ni nukuu toka Mzalendo.net

Baada ya kuisoma imebidi nijiulize kama imeandikwa kutokana na kutojua taratibu za utoaji wa Majina katika barabara, mitaa, na vitongoji au ni ujuhaji mwingi ambao upelekea kwa mhusika kuwa juha! Pichani juu kabisa ni baadhi ya barabara na mitaa ya Mkoa wa Mjini Magharibi.

Kama kawaida mtoa hoja kaficha jina lake, lakini kwa kuwa lengo lake isomwe na kujadiliwa hakuna tatizo katika hilo. Nitajaribu kumfahamisha taratibu za ubadilishaji wa majina ya mitaa, barabara na vitongoji katika Halmashauri ya Manispaa ya Zanzibar kwa mujibu wa sheria ya Manispaa ya Zanzibar ya mwaka 1995 namba 3.

Halmashauri ya Manispaa ya Zanzibar ndio yenye jukumu la kuhudumia na kusimamia barabara, mitaa na chochoro zote zilizopo ndani ya mipaka ya Manispaa hiyo, hii ikiwa ni pamoja na utoaji wa majina kwa barabara na mitaa. Mara ya mwisho ya kufanyika mabadiliko makubwa ya majina katika barabara na mitaa ya Zanzibar ilikuwa ni katika miaka ya tisini ambapo zaidi ya barabara kumi zilipatiwa majina mapya. Kazi hii ilifanya na kamati ya Mipango Mji kabla ya kuthibitisha na Baraza Kuu la Manispaa hiyo.

Vigezo vya ubadilishaji wa majina ya mitaa/barabara hufanywa na Madiwani, na kwa bahati nzuri tokea mwaka 1995 hadi leo Baraza la Manispaa hilo limekuwa na Madiwani toka CCM na CUF. Mtoa hoja katika nukuu hapo juu ametupa lawama kwa CCM - SMZ, napenda ajue kuwa Madiwani hata Madiwani wa CuF walikuwepo. Zaidi ni vema kujua kuwa Madiwani ni wawakilishi wa ngazi ya mwanzo ya wananchi na ndio wapo karibu kabisa na wananchi. Hivyo basi madiliko kama haya huwa kwa namna moja ama nyingine yanabeba maoni ya wananchi wao. Mtoa mada mada sijui anawakilisha maoni ya wadi gani au jimbo? Ni vema akaweka sawa kwenye mada yake ili iweze kufahamika anawawakilisha akina nani!

Ramani iliopo hapo juu pamoja na kutoonyesha barabara zote zilizopo ndani ya mipaka ya Manispaa, pia haionyeshi majina ya mitaa mingi ambayo tayali imeshapewa majina. Hili linaweza kuwa ni tatizo la muundaji/mchoraji wa ramani husika au tazizo la asasi zinazohusika na upasishaji wa ramani kwa matumizi ya jumuiya na watalii.

Hapa chini ni baadhi ya majina ya barabara zilizopo katika Manispaa ya Zanzibar:-

Kutoka Kinazin kwenda Bububu- Aboud Jumbe

Kiembe Samaki hadi Amani- Idrisa A. Wakili

Mnazi mmoja- Airport- Nyerere

Mkunazini hadi Kariakoo - Karume

Maisara - Michenzani kwenda Mlandege- Dr. Salmin Amour


Ule Uchochoro wa Darajani hadi Mlandege- Ali H.Mwinyi

Barabara toka Mazinini kwenda Chukwani - Barabara ya Bakari Jabu



Kwa mtoa hoja bado ana nafasi kubwa ya kuweka kwa majina ambayo anaona yana umuhimu kwa jamii na historia ya Zanzibar. Majina mengi bado yanahitajika na hasa katika Halmashauri ya Mji Magharibi. Ni vema kwake akawasilina na Halmashauri husika na kuona vipi anaweza kuchangia katika kutoa majina mapya.

Mwisho nimeona kuwa kuna utunzaji mbovu sana wa kumbukumbu au kuna njia za makusudi zinazofanyika katika kupotosha majina ya barabara na mitaa.

Mfano mkubwa ni kwa barabara ya Creek. Barabara hii ilishabadilishwa jina zaidi ya miaka ishirini sasa, lakini bado ramani zinazotoka kwa matumizi ya utalii zinatumia jina hilo. Hii ni pamoja na mtaa utakao Darajani hadi Mladenge. Ipo haja kwa vyombo husika kuliona hili.

Kwa upande wa Manispaa ni vema mkarudisha vibao vya majina ya mitaa na barabara, kumekuwepo na tabia ya kuweka vibao hivyo kwa barabara maarufu tu, ni vyema sasa mkaangalia na kuweka vibao katika sehemu ambazo sio maarufu lakini zenye uhumimu sawa na sehemu nyingine maarufu.

Tuesday, 9 March 2010

Leo Katika kumbukumbu: Zanzibar police ban veiled drivers


Zanzibar - A police ban on women drivers wearing veils came into effect on Tuesday across the Indian Ocean islands of Zanzibar, drawing some protests from the overwhelmingly Muslim population.

Zanzibar police commander Ramadhan Khatib said the measure was intended to curb a rise in traffic accidents which reached a record 680 - with 40 deaths and 100 injuries - in 2006.

"We have the responsibility of ensuring we decrease the accidents, and we think veil-wearers have to be included in this exercise as well," he told Reuters.

Police gave no indication of whether any of the accidents had been caused by women wearing veils.

Moves against veils and burqas are the subject of heated global debate, particularly in Europe where some governments see them impeding the integration of Muslims.

In Zanzibar, where 95 percent of the islands' one million inhabitants are Muslim, one Islamic group protested that the traffic order went against local culture.

"This is not acceptable. We do not see any legal basis for this order ... and we are going to challenge it," said Sheikh Khalid Azan, the Islamic Propagation Centre's leader.

"Wearing a veil is a virtue and an obligation to women ... we cannot understand if someone orders them not to wear it."

One woman driver wearing the veil - known as a niqab N said before the ban came into effect that it showed police in Zanzibar were barking up the wrong tree.

"If they do not have anything to do, they could chase underage drivers, they could search for fake licences and those who cheat on their insurance policies," said Asha Issa, covered in a veil as she leaned on her steering wheel.

"This is going too far into my religion...The only person who could take the niqab from me is my husband, and he would not do so because he knows his obligation in Islam."

Although semi-autonomous, the Zanzibar islands are part of Tanzania and lie just off its east coast.

Monday, 8 March 2010

Maalim Seif apata nafuu...


Maalim Seif akiwa hospitalini Hindu Mandal leo hii. Maalim amenukuliwa akisema kuwa ameshapoa na anategemea kupata ruhusa ya kutoka hospitalini hapo mara baada ya kuonana na daktari wake.


Picha kwa hisani ya Mzee wa Sumo

Sunday, 7 March 2010

Umeme umerudi Zenj...


Upo kwenye majaribio, uhakika wa kurudi ni kuanzia wiki kesho... Jioni njema

Stone Town- Zanzibar



Mabadiliko:
Kwenye no:2 ni barabara ya Benjamin Mkapa na sio Creek Road.

Saturday, 6 March 2010

Mambo ya Mwambao...


Weekend Njema..!

Thursday, 4 March 2010

Ubaguzi waanza kushika kasi Zanzibar....




Katika tembea tembea mtandaoni, nimekutana na mada hii hapa chini, yenye kila aina ya ubaguzi na chuki za waziwazi, kwa watanzania bara waishio visiwani humu. Hapa chini ni nukuu yake

mkuu wa vitambulisho vya uzanzibar Mohamed Juma Ame anasema waliokosa haki ya kujiandikisha wato hawana sifa za uzanzibar kwa hio sio wazanzibar bona watu wa tanga pangani,mafya na wamasai wa kiwengwa wote wamepata kuandikiswa hiwe nyie tu?

Maskini Mh Shabani Hamis Mloo mawazo yake na busara zake tutazienzi. Aliona mbali aliposema Zanzibar hatuna Serekali tuna kikundi cha wahuni tu. Leo ni Nchi gani ulimwenguni inayo wakataa wananchi wake na kuwanyima haki na kuwakumbatia wageni kwa kuwapa uhalali wa Nchi na usibiticho wa uzawa vyeti vya kuzaliwa na utambulicho wa Zanzibar. Au ndio Msh Karume tulifanya kosa Mh Amertajo alipokula kiapo cha Ushahidi kuwa Father K kazaliwa Mwera ndio kiapo kile kilituzuru wazanzibar wote? Kunahaja ya wazanzibar kujipanga safu na Kenosha mazila ya kila siku kama hatuja pigana coper basi mambo hayawi heat and running mealtime itumike Zanzibar si hivyo Nchi inakwenda na ccm ndio wabeba mashera.

Jina la mtoa mada hii halijabandikwa ila unaweza kutembelea tovuti ya mzalendo kwa maelezo zaidi.

Mada hiyo ni mfululizo wa mada kadhaa zilizoanza kuibuka baada ya mazungumzo ya maridhiano ya Rais Karume na Maalim Seif. Mara baada ya maridhiano hayo, maoni mengi yalielekezwa katika Zanzibar na Muungano wake chini ya kivuli cha utaifa,na kusahau kabisa lengo kuu la maridhiano/mapatano hayo ambayo yalikuwa na lengo la kuijenga Zanzibar moja iliyomeguka kutokana na siasa na kuathiri kwa kiwango kikubwa umoja na undugu wa wananchi wa visiwa hivyo tokea kuingia kwa mfumo wa vyama vingi.

Zanzibar ya leo uchumi wake kwa aslimia 80 unategemea watalii, tokea Zanzibar kufungua milango ya utalii, visiwa hivyo vimeshuhudia uingiaji wa wageni wengi, na wageni hawa wameingia kutokana na kukua kwa utalii na mahitaji ya utalii katika visiwa hivyo, ambayo kwa wakati huo na sasa wakaazi wake hawawezi kukidhi mahitaji ya utalii visiwani humo.

Kumekuwepo na hatua mbali mbali za kuondoa baadhi ya mahitaji ya utalii katika visiwa hivyo kwa nyakati tofauti. Miaka ya mwishoni ya tisini, kulifanyika zoezi kubwa la kuwaondoa wafanyabiashara za vinyago na batiki katika maeneo ya Kiwengwa pasipo mafanikio. Uundoaji wa wafanyabiashara hao ulishindikana kutokana na kuwa ulikuwa hauna maana yoyote zaidi ya chuki na ubinafsi wa baadhi ya viongozi ambao walijiweka nyuma ya pazia la udini.

Zoezi kama hilo lilirudiwa tena kwa wafanyabiashara wa vinyago na batiki katika mitaa ya gizenga na forodhani, na hata liliposhindikana wafanyabiashara hao walihamishiwa katika maeneo ya Maruhubi, na baadae Msikiti Mabluu. Hata hivyo maeneo hayo yalishindikana kufanyika kwa biashara hizo kwani zoezi hilo lilifanyika pasipo kuwepo kwa utafiti wa kina, na baadae ilikuja kujulikana kuwa limetokana na utashi wa baadhi ya watu dhidi ya wafanyabiashara hao.

Shughuli za Utalii hapo visiwani unaweza kuzigawa katika mafungu kadhaa. Kuna vijana ambao wanaitwa mapapasi hawa kazi yao kubwa ni kupokea na kuwazungusha watalii katika mitaa ya mji Mkongwe,kuwatafutia watalii hao sehemu za kumpuzika na kadhalika,Kundi hili linaaminika kujengwa na wazawa. Aidha kuna wakati kundi hili lilitakiwa kujiandikisha kama chombo rasmi ili kijulikane kisheria na kuweza kulipa kodi. Hata hivyo zoezi hili halikuweza kufanikiwa. Kuna kundi la wafanyabiashara ndogo ndogo za vinyago na batiki, kundi hili linaaminika kuundwa na wageni. Na ni kundi ambalo linapata misukosuko isiyo kwisha licha ya nafasi yake kubwa katika utalii visiwani hapo ikiwa ni pamoja na kuingiza mapato yake serikalini.

Mada toka Mzalendo inalalamikia kwa wageni hao kupata haki ya kupiga kura. Sifa mojawapo ya kuweza kupiga kura ni kukaa sehemu moja kwa zaidi ya miaka mitano. Hapana shaka wengi wa wafanyabiashara hawa wana zaidi ya miaka kumi visiwani huo. Hivyo kwa wao kuandikishwa kupiga kura sio suala la kushangaza na kuandikiwa kwa namna hiyo! Zaidi hawa ni watanzania na wana haki ya kwenda sehemu yoyote ya nchi.

Wednesday, 3 March 2010

Umeme sasa ni Machi 9 - ZECO


IMEDAIWA jana kuwa huduma ya umeme visiwani Zanzibar inatarajiwa kurudi Machi 9 baada ya kukamilika kazi za utengenezaji wa kituo cha kupokea umeme kilichopo Fumba, Mkoa wa Mjini Magharibi

Kaimu Meneja wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO), Hassan Ali Mbarouk, aliwaambia waandishi wa habari kuwa kutokana na kukamilika kwa matengenezo cha Fumba huduma hiyo itarejea punde na kuwaahidi wananchi wasiwe na wasiwasi huduma hiyo itarejea siku hiyo.

Alisema kazi iliyobakia ni kuunganisha waya za umeme kutoka nchi kavu na baharini na kazi hiyo ya kuunganishwa kwa waya kutoka katika vituo vya Fumba hadi Ras Kiromoni Tanzania Bara itachukua muda wa siku tatu.

Alisema hadi Jumapili ijayo kazi ya matengenezo itakuwa imemalizika na matarajio Machi 8 kutafanyika vipimo vya majaribio na Machi 9 ndiyo huduma hiyo inatarajiwa kuwashwa na kurudi rasmi kwa umeme visiwani humo.

Pia aliweza kuwaambia waandishi wa habari kuwa kuchelewa kwa huduma hiyo kumesababishwa na mafuta yaliyokuwemo ndani ya waya zinazoleta umeme kutokuwa safi na kulazimika kusafishwa kwa muda wa siku tatu.

Wakazi wa visiwani humo wamekosa huduma hiyo ya umeme tangu Desemba mwaka jana, baada ya kutokea hitilafu katika kituo cha kupokea umeme huo kutoka Ras Kiromoni hadi Fumba mjini Unguja.

Tuesday, 2 March 2010

Minister: Tourism Accounts for 80% of Zanzibar Revenue


Tourism in Zanzibar is a Sh163 billion industry and employs 10,500 people.

It is an indirect source of income for another 40,000 Zanzibaris, the minister of State in the President's Office (Finance and Economy), Dr Mwinyihaji Makame Mwadini, said.


He told The Citizen that the sector accounted for 80 per cent of government revenue. He attributed its increasing contribution to the national development to reforms adopted in the mid-1980s.

"The sector contributes about 22 per cent of GDP and about 80 per cent in government revenue. The overall growth of the sector, estimated at 9-10 per cent, has outpaced that of agriculture. But like most sectors of the economy, tourism has recently been affected by the global crisis," he said.

He believes that more jobs would have been created and household incomes boosted had it not been for the negative impact of the global recession in 2008. Zanzibar had a gross domestic product (GDP) of Sh738.7 billion in 2008.

The global recession cut the GDP growth rate to 5.4 per cent in the year from 6.3 per cent in 2007. The crisis also raised the cost of living to 20.6 per cent from 13.1 per cent during the same period as food became scarce and prices escalated.

The downturn also affected government revenues, capital inflows and export earnings but donors did not cut aid, which accounts for over 40 per cent of the government budget. However, he is optimistic that the industry will improve this year following signs of recovery in the second half of last year.

Members of the Zanzibar Association of Tourism Investors (Zati) are cautious that the rebound is not guaranteed. The Zanzibar Commission of Tourism (ZTC) reported that the number of tourists fell to 128,440 visitors in 2008 from 148, 283 the previous year.


However, a Zati report showed that the number of tourists increased to 97,711 in the first nine months of 2009 from 94,430 in the similar period the previous year.

"The global financial crisis made 2009 a bit difficult for Zanzibar's tourism and prospects for this year are clouded by the power problem," Zati chairman Simai Mohamed told The Citizen on the sidelines of the association's 2010 dinner party.

Monday, 1 March 2010

Bwawani Hoteli kuuzwa kwa deni la mchele?


The Zanzibar High Court has blocked the decision to auction Bwawani Hotel after the Isles government presented a petition to settle its debt worth 1.6 trillion outside the court.

Speaking to this paper on Friday, the High Court Registrar Yesaya Kayange said the hotel’s auction was scheduled to take place on January 26 this year, but the High Court halted the decision after the respondent, the Ministry of Finance and Economic Affairs pleaded to settle the matter out of court.

“We received a request from the respondents asking us to halt the auction because they were ready to settle the matter out of court,” said the registrar.

However, Kayange said should the parties fail to reach an understanding, the matter would revert to court.

He noted that for now the court would not interfere because it had awarded both the parties time to settle the matter.

The court had authorized the auction of the hotel following the Zanzibar Ministry of Finance and Economics’ failure to pay a debt of 1.6trn/- to Leamthore Rice Company Ltd which had been awarded tender to supply rice to the government.

The order was issued on November 12 last year by the same registrar to execute a judgment that was delivered by high Court Judge Wolfgang Dourado on May 16, 1997.

Earlier, the company had filed a civil case no. 47/1997 following the governments failure to pay a debt of USD 69.4m after receiving rice from the same company and selling it in the local markets.

The company was being represented by advocate Dr Masumbuko Lamwai who had asked the court to order confiscation of government properties including a farm in Kijichi area.

Judge Dourado reached the decision following failure by the ministry’s permanent secretary Omar Sheha to appear in court.

The court then ordered the ministry to pay the debt in full including an interest of 25 per cent and the costs of the case.

However the ministry failed to pay the debt on time which accumulated to 1.6trn/-.

Bwawani Hotel was built by the first phase President, the late Abeid Amani Karume, and reports show that high profile businessmen from the Isles and Tanzania Mainland had shown interest in buying the hotel.

Drug Free Zanzibar


Hivi karibu katika Hoteli ya Africa House kulifanyika onyesho la fund raising kwa ajili ya kuzuia utumiaji wa madawa ya kulevya kisiwani Zanzibar.

Hatua yoyote inayochukuliwa ili kuondoa matumizi ya madawa ya kulevya visiwani humo, inapaswa kuungwa mkono. Kwani athari za matumizi hayo sasa zimekuwa kubwa mno kiasi cha hata watoto wadogo kuanza kuathirika, kama ilivyoondika hapa.