Wednesday 25 February 2009

Wikipedia ya Kiswahili

Watanzania wote wanakaribishwa kuchangia habari za mahali wanapoishi au wanapotoka katika wikipedia ya Kiswahili! (sw.wikipedia.com) Ijulikane ya kwamba wikipedia ni mradi mkubwa wa elimu unaojengwa na wachangiaji wanaojitolea bila malipo yoyote. Kila mtu anakaribishwa kuchangia!

Kwa sasa tumeanzisha makala fupi za kila kata kwenye mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Iringa, Kilimanjaro, Kigoma, Lindi, Mara, Mwanza, Mbeya, Manyara, Morogoro, Mtwara, Pwani na Tanga.

Angalia mfano huu: sw.wikipedia.org/wiki/Mkoa_wa_Mjini_Magharibi_Unguja

Chini kuna sanduku inayoonyesha mikoa yote. Ukiingia katika mkoa fulani unapata majina ya wilaya. Kila safari ukibonyeza kwenye neno lenye rangi ya buluu unapelekwa kwenye makala mpya. Ukifika kwenye wilaya utaona sanduku lenye majina ya kata za eneo hili. Makala mengi yana habari fupi tu kama "ABC ni kata ya wilaya DEF katika Mkoa wa XYZ. Idadi ya wakazi wake ilihesabiwa kuwa xxxxx katika sensa ya 2002". Kila mtu yuko huru kubonyeza kwenye sehemu ya "hariri" juu ya makala na kuongeza habari.

Baada ya kuongeza habari unabonyeza sehemu ya "Hifadhi ukurasa" iliyoko chini.


Taarifa hii imeletwa kwenu kwa hisani kubwa ya Bw. Kipala anayesimamia kamusi hiyo

3 comments: