Wednesday 18 February 2009

E-governance for African Municipalities...Ni Wizi Mtupu....!


Zenj mara nyingi imekuwa ikiingia kwenye rekodi mbalimbali barani Afrika na Duniani kutokana na matukio ya maisha maendeleo na teknologia. Rekodi kadhaa zimeandikwa ndani ya visiwa hivyo, hivyo kuongeza umaarufu wake na wakati huo huo kuboresha huduma mbalimbali kwa wananchi wake.

Zanzibar inaendelea kujivunia rekodi zake mbalimbali hadi wakati huu ingawa zingine zilishindwa kuendelezwa na hivyo kubakia kwenye kumbukumbu tu na kuwa hadithi kwa vijana kutambiana na hasa wanapokuwa katika ubishi na wenzao wa bara. Mapema mwaka huu Zenj iliibuka tena na kujiwekea rekodi nyingine mpya katika Afrika ya Mashariki, na iwapo rekodi hii itakuwa na mafanikio hapana shaka itaanza kusambaa taratibu kwa nchi zote za jirani. Safari hii rekodi hiyo haikupokelewa vizuri na nchi jirani, hata hivyo nina hakika baada ya muda wataifuata tu. Hii ni rekodi ya kuwa nchi ya kwanza katika Afrika ya Mashariki kutoa leseni ya udereva yenye kumbukumbu zote muhimu za mwenye leseni pamoja na namba yake ya ulipaji kodi. Hii ni hatua nzuri na kubwa kwa nchi zenye matatizo ya ukusanyaji wa kodi.

Mafanikio haya yote siku zote yanakuwa na lengo moja kubwa la urahisishaji wa utendaji na uongezaji wa ufanisi katika utoajo wa huduma, ambapo ni hatua muhimu ya kuondokana na ukiritimba ambao umekuwa ukichangia kwa asilimia kubwa kuwepo na rushwa na hatimae ufisadi.

Hata hivyo sio mambo yote ambayo yamekusudiwa kufanikisha na kurahisisha utoaji huduma katika Zanzibar yamefanikiwa. Ni watu wachache ambao watakumbuka kuwepo na mradi wa E-governance for African Municipalities kwa Manispaa tano tu barani Afrika ikiwemo Zanzibar, Manispaa zingine zilikuwa ni Bamako (Mali), Maputo (Mozambique), Niamey (Niger) na Lusaka (Zambia). Lengo la mradi huu ambao ulianza mwaka 2001 ilikuwa ni kuziunganisha Manispaa hizo tano katika mtandao mmoja aidha kuwezesha Manispaa hizo kuwa karibu na wananchi wake kwa utoaji wa huduma ya habari kwa njia ya mtandao. Kwa Manispaa ya Zanzibar kupitia mtandao uliofungwa katika Idara zake zote ilikusudiwa kurahisisha ubadirishanaji wa habari za kiutendaji katika idara hizo kwa njia ya umeme(electronically). Zaidi ilikusudiwa kutoa habari juu upatakanaji wa leseni mbalimbali kwa wananchi wake kupitia kwenye tovuti yake, pamoja na wananchi hao kupata nafasi ya kutumia mtandao huo bure katika sehemu maalumu kwa ajili ya kupata habari juu ya sheria ndogo ndogo mpya, muhtasari wa vikao vya kamati za Manispaa na Baraza Kuu, ukusanyaji wa mapato na matumizi yake na kuweza kujionea bajeti ya Manispaa hiyo ndani ya mtandao.

Mradi huu ambao ulikuwa unadhaminiwa na DANIDA/UNESCO, ulikamilika mwaka 2003, ambapo pamoja na Manispaa kupatiwa vitendea kazi vyote na taaluma kwa watendaji wake, wadhamini hao waligharamia na uanzishaji wa tovuti ya manispaa hiyo, ambayo tokea mwaka 2003 hadi leo hii imedumaa. Huu ni wizi mtupu.

Mradi huu ulikuwa wa thamani ya dola za kimarekani elfu arobaini haukuweza kuendelea kama ilivyokusudiwa kwa sababu zisizo na msingi zaidi ya kuendeleza tabia za ukiritimba ndani ya vyombo vya utoaji wa huduma ambapo ni wizi mtupu.

Madiwani ambao kwa namna moja ama nyingine ndio wanao wawakilisha wananchi wao katika Manispaa, ilitegemewa wawe mstali wa mbele kuona huduma hii muhimu iliyokuwa inaweza kuwapunguzia bughuza za waombaji wa fomu kugonga milango ya nyumba zao alfajili, kuwabana wahusika kuikamilisha tovuti hiyo ili kuwezesha wananchi kujaza fomu online walikaa kimya na kufumbia macho kudumaa kwa mradi huu ili waweze kuendelea kuwazungusha wananchi wao juu ya upatikanaji wa fomu mablimbali... Huu ni wizi mtupu!

Mkurugenzi wa Manispaa ama kwa kutojua ama kushindwa kwenda na mabadiliko katika utoaji wa huduma nae alishindwa kuendeleza mradi huu. Kwa nafasi yake angeweza kuhakikisha kuwa kila Idara inapeleka taarifa zake za mapato katika tovuti hiyo na kila idara inaweka fomu za maombi katika tovuti hiyo na hivyo kupunguza ama kuondoa foleni zisizo na ulazima wowote katika Ofisi ya manipaa hiyo. Hata hivyo kwa miaka saba sasa amekaa kimya tokea alipoweka ada za kupaki magari mwaka 2003... Wizi mtupu!

Mstaki Meya ambae huwa anaalikwa kwenye matukio muhimu yote yanayofanyika katika Manispaa yake nae ameshindwa kumbana afisa uhusiano kuona kuwa Matukio muhimu yote yanawekwa katika tovuti hiyo, hii ingekuwa ni njia mojawapo ya kuelekea kuweka hata matangazo ya matukio kwa njia ya kulipia hivyo kuifanya tovuti hiyo kuingiza mapato. Nae kama wengine ameamua kukaa kimya... Ni wizi mtupu!

Tovuti ya Baraza la Manispaa ilifanyiwa marekebisho kwa mara ya mwisho mwaka 2003, na hata yale ambayo yamo katika tovuti hiyo yanatia kichefuchefu. Yaliyoandikwa humo yana uhusiano mdogo kabisa na shughuli za Manispaa hiyo huu ni wizi mtupu. Hata design na layout ya tovuti hiyo ni vichekesho vitupu... Yaaaani ni Wizi mtupu!

Thursday 12 February 2009

Ni wiki ya Sauti za Busara (Sounds of Wisdom) huko Zanzibar



Tamasha la sita la Sauti za Busara limeshaanza rasmi siku ya Jana kwa maanandamo ya ufunguzi wa tamasha hilo ambalo sasa ni mojawapo ya tamasha kubwa kabisa barani Afrika. Tamasha hili litadumu kwa muda wa siku sita(12-18/02/2009)na tokea kuanza kwake limekuwa likifanyika katika wiki ya pili ya mwezi wa pili.

Tamasha la mwaka huu litatumbuizwa na wasanii maarufu toka karibu pande zote nne za Afrika, kwa mjibu wa tovuti ya sauti za busara wasanii ambao wana washabiki wengi kwa mwaka huu ni Bi Kidude, Culture Musical Club, DJ Yusuf, Samba Mapangala & Orchestre Virunga, Jagwa Music, Best of WaPi, Iddi Achien'g, Natacha Atlas, Segere Original na Joh Makini

Kwa habari zaidi tembelea hapa chini

Tuesday 10 February 2009

Kichekesho kingine toka kwa Shamsi Vuai Nahodha



Mwishoni mwa mwezi Januari mwaka huu, Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi alinifanya nicheke kwa kauli yake ya kuamua kushika fagio na kuanza kufagia barabara za Zenj kutokana na barabara hizo kujaa michanga na vumbi kiasi cha kutojulikana kama ni za kiwango cha lami au la. Hii si mara ya kwanza kwa Mh. Nahodha kujitolea kusafisha Halmashauri ya Manispaa ya Zanzibar. Hata hivyo pamoja na juhudi zake hizo kwa Halmashauri hiyo ambayo kipindi fulani kupitia kwa Mkurugenzi wake Mr Mabrouk Makame Jabu ilikuwa ikidai kupewa hadhi ya Jiji(Sina hakika kama tayali ombi hili limeshakubaliwa)bado mji huo umeendelea kuwa mchafu.

Juhudi zote za Waziri Kiongozi zimekuwa na mafanikio ya muda mfupi, kwani huwa zinafanyika katika mtindo wa Operation ambao siku zote huwa hauna uendelevu wa aina yoyote, kwani operation inapokwisha shughuli nzima uwekwa kando na watu wakaendelea na shughuli zao zingine, huku wakisubiri kutokea kwa operation mpya. Watendaji wengi na hasa wa kimacha chini upenda aina hii ya utendaji kwani ndio wakati wao wa kuwa na kipato zaidi kutokana na overtime. Kwa Waziri Kiongozi ambae mara kwa mara amekuwa akisisitiza kuwepo na utendaji wa uendelevu katika shughuli za serikali, kilimo na biashara huku akiongoza kufanya operation za usafi ni kichekesho kitupu. Inakuaje unahutubia kila siku mambo ya uendelevu huku kazi unafanya za kizima moto kama sio vituko vitupu!

Moja ya barabara ambao siku zote huwa inajaa michanga na kusababisha vumbi la kuweza kusababisha chafya kila baada ya sekunde kadhaa, na hatari ya kupata kikohozi kikali ni barabara ya Benjamin Mkapa(zamani creek road). Barabara hii ndio inatenganisha Mji Mkongwe na Ng'ambo, ni moja ya barabara yenye pilika kubwa kabisa katika Zenj ikipitiwa na magari mengi zaidi, itumiwayo na wapanda baiskeli wengi zaidi na wapanda vespa,huku wakipigana vikumbo na mamia ya watembeao kwa miguu. Ndio barabara pekee visiwani humo yenye taa za kuongozea magari, kwa ufupi ndio barabara maarufu kabisa visiwani humo.

Kwa miaka nenda rudi barabara hiyo imekuwa ikifagiliwa pasipo kutakata na sasa naona imeshakuwa sugu, na kama hakuna mipango ya kuweza kujua ni kwa nini barabara hiyo haikosi vumbi licha ya kuwa ndio picha ya mji wa Zenj, kamwe haitokuja kuwa safi na ni wazi kuwa vumbi litaendelea kuwepo tu, licha ya ombi la watendaji wa Halmshauri hiyo kununuliwa gari la kufagia barabara hivi karibuni.


Barabara hiyo pamoja na kupita katika bustani za Mnazi Mmoja, Jamhuri, Donge na viwanja vya Malindi, haikupaswa kabisa kuwa na vumbi. Lakini kutokana na sababu za kutokuwa na mipangilio mizuri vumbi limeendelea kuwepo licha ya ufagiaji wa kila siku. Kitu cha kwanza ambacho kina kasoro kubwa katika barabara hiyo ni kukosekana kwa njia ya watembeao kwa miguu. Kama kungekuwa na njia hiyo ingetumika vile vile kama buffer ya kutenganisha barabara na sehemu zinazoingiza michanga barabarani na kusababisha vumbi. Aidha aina za kuegesha magari na hasa teski katika barabara hiyo unachangia kuingia kwa michanga barabarani, kuna maegesho ya magari ya mizigo na haya uegeshwa karibu kabisa na barabara hiyo, hivyo uchangia kuingia kwa michanga barabarani.Kwa upande mwingine Feeder road zinazo ingia katika barabara hiyo vile vile uchangia kuingiza michanga.

Ili kumfanya Waziri Kiongozi aendelee kufanya kazi zake za kawaida, badala ya kutafuta fagio, upo umuhimu wa lazima kuona kuwa barabara ya Benjamin Mkapa inafanyiwa mabadiliko makubwa ili kukidhi mahitaji ya watumiao barabara hiyo ambao ni maelfu. Kuna umuhimu wa kuweka njia kwa watembeao kwa miguu ambayo iwe inafanya kazi ya kuzuia kuingia kwa michanga katika barabara hiyo. Kuboresha maegesho ya teski na magari ya mizigo kama kituo cha daladala kilivyoboreshwa, kufanyia matengenezo feeder roads ambazo huingiza michanga kwa wingi na hasa wakati wa masika. Kuangalia tena eneo la Darajani kwani nalo linachangia sana katika uchafuzi wa barabara hiyo. Maeneo mengine kama Mkunazi,Donge, Ben Bella na Ofisi za Zec zinatakiwa kuangaliwa kwa vizuri zaidi.

Kwa utengenezaji wa njia ya wapita kwa miguu, Halmashauri ya Manispaa ya Zenj, inaweza kufanya kazi hiyo kwa kutumia mitambo yake mikubwa ya kutengeneza vigae, kwa kuweka vigae pembeni ya barabara hiyo. Hizo milioni 135,000,000 ambazo Manispaa wanahitaji kwa ununuzi wa mashine ya kusafisha barabara mnaweza kuwapa japo nusu yake ili waweze kutumia kwa utengenezaji wa vigae.

Friday 6 February 2009

Athari za Utalii kwa Mazingira ya Zanzibar




Moja ya masharti wanayopewa watalii mara waingiapo Zenj, ni juu ya uvaaji wa nguo ambazo hazistiri mwili mzima, yaani uvaaji wa suruali kipande, vichupi, ama kutembea vifua wazi ni sawa na kwenda uchi ndani ya Zenj. Hivyo watalii uambiwa wavae nguo zinazofunika mwili wote wakati wao wote watakapo kuwepo visiwani humo. Kwa watalii sharti hili ulipokea kwa shingo upande kwani wanapotoka ni sehemu za baridi na kwa muda mrefu wanakuwa wakivaa nuo nyingi kujikinga na baridi, na hivyo wanapotalii katika nchi za joto hupenda kuipa nafasi miili yao kufaidi joto hilo ambalo kwao ni adimu.

Hata hivyo linapokuja suala la ujenzi wa hoteli za kitalii Masharti na Taratibu zake hazijulikana kabisa, kwani vyombo vinavyosimamia ujenzi huo havina ushirikiano wa moja kwa moja na Idara ya Mazingira ambayo ipo kisheria kusimamia mazingira ya Visiwa hivyo chini ya sheria ya mwaka 1996.

Utalii katika visiwa vya Zanzibar sasa umeshapanuka sana na visiwa hivyo vimeshashuhudia mambo mengi yaliyokuja na utalii, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa hoteli nyingi za kitalii karibu kwa fukwe zote visiwani humo pamoja na visiwa vidogo dogo, ongezeko la wageni wahamiaji kwa ajili ya kazi za kitalii, ongezeko la uvuvi kwa ajili ya vyakula vya watalii, ongezeko la safari za anga na ardhini, ongezeko la maduka rasmi kwa ajili ya watalii na mambo mengine mengi yanayoendana na utalii kwa ujumla.

Mengi katika haya yalikuja pasipo kwa wenyeji wengi kujiandaa na sasa inakaribia miaka ishirini tokea mfumuko wa utalii visiwani kuanza, na kumekuwepo na malalamiko mengi toka ndani ya visiwa hivyo na nje ya visiwa hivyo kwa jinsi suala zima la utalii lilivyobadili mambo mengi visiwani humo. Wenyeji wengi wanalalamikia sehemu kubwa ya ajila kushikwa na wageni, ongezeko la bei kwa vyakula vya baharini, kupigwa marufuku kutembea ama kuvua katika baadhi ya hoteli hizo. Huku asasi za kimataifa zikipigia kelele uharibifu wa mazingira kutokana na aina za ujenzi wa baadhi za hoteli visiwani humo, uharibifu wa coral reef kutokana na uvuvi uliokithiri, kutokuwepo na miundo mbinu ya kutosha kwa ajili ya kuhifadhi maji taka na utupaji holela wa taka toka mahotelini humo.

Hadi kufikia mwaka 2003 takwimu za ZIPA zinaonyesha kuwa, jumla ya miradi 242 ilidhinishwa yenye thamani ya jumla ya dola za kimarekani milioni 403. Mwaka 2001 Zanzibar iliingiza dola za kimarekani milioni 46 kutokana na utalii pekee ikiwa ni asilimia 15 ya GDP. Makisio yanaonyesha kuwa kutakuwa na ongezeko la asilimia 21 la GDP kufikia mwaka 2012 na kufanya mgawanyo wa mapato kufikia million 116(makadirio haya yalifanyika kabla ya Global recessionya mwaka huu).

Ripoti ya maendeleo ya utalii ya Zanzibar iliyoandaliwa na na UNDP inaonyesha kuwa katika mwaka 1983 kulikuwa na sehemu kumi tu za malazi visiwani humo zenye vyumba 215 na jumla ya vitanda 467 ambazo hazikuwa kwenye daraja la aina yoyote(utalii au malazi ya wageni wa kawaida). Leo hii sekta ya utalii visiwani humo ina sehemu zaidi ya 180 za malazi, zenye zaidi ya vyumba 3160 na zaidi ya vitanda 6490.

Kufikia mwishoni mwa mwaka 2006, ripoti ya Umoja wa Mataifa(UN) ilionya kuwa Zanzibar imekuwa mojawapo ya nchi duniani inayoongoza kwa uchafuzi wa mazingira ya baharini kutokana na umwagaji wa maji taka katika bahari ya Hindi pamoja na uharibifu wa vyanzo vya maji. Mtafiti Stefan Gossling toka Sweden, yeye alionya kuwepo na uharibifu mkubwa wa coral reef kwa lengo la uuzaji wa viumbe vyake kwa watalii. Maeneo yenye uharibifu mkubwa wa mazingira kutokana na utalii visiwani humo ni ya Kaskazini na yale ya Mashariki.

Ukuaji wa utalii, licha ya kuendelea kuharibu mazingira umesababisha kuwepo na ushirikiano mdogo kati ya serikali na wananchi wake. Kwa upande wa mazingira wananchi wengi wanalalamikia hatua kadhaa za wenye hotel kuwanyima sehemu zao za uvuvi, ulimaji(seaweeds), minazi na hata kutembea karibu na hotel hizo. Mwaka 2002 wananchi wenye hasira katika kijiji cha Kendwa walichoma moto hoteli ya kitalii kwa madai ya hoteli hiyo kuharibu coral reef, tabia hii ilisambaa kwa baaadhi ya vijiji vya Nungwi.

Baadhi ya hotel( Fundu lagoon, Matemwe Bungalow, Blue Bay, Mnemba Island na Chumbe) zimeonyesha kujali athari ambazo zinatokana na ujenzi wa hoteli zao kwa mazingira. Wamejitahidi kufuata aina za ujenzi usio tumia resources kwa wingi, aidha wamejitahidi kufuata aina ya ujenzi wa nyumba za vijiji zinavyowazunguka. Hivyo kupunguza uharibifu wa maji safi na bahari.

Serikali kwa upande wake imeendelea kutoa vibali vya ujenzi pasi kuzingatia uharibifu wa mazingira au namna ya kujenga pasipo kuwepo na uharibifu wa mazingira. Hoteli zinaendelea kujengwa pasipo kuwepo na mfumo unaotambulika wa ukusanyaji na usafishaji wa maji taka, ukusanyaji na utupaji wa taka ngumu na utunzaji wa vyanzo vya maji. Aidha hakuna taratibu zozote ambazo zinatolewa kwa kutumia materials ambazo zinaendana na mazingira ya fukwe zinazojengwa.

Na kama kawaida yao, mambo yanapokwenda kombo, viongozi huja na amri kede kede. Nakumbuka miaka miwili iliyopita Mh. Mansour Yussuf Himid alinukuliwa akisema;
“Serikali imegundua ukiukwaji wa taratibu za utunzaji wa mazingira katika ukanda wa fukwe”
Aidha alikubali kuwa sekta ya utalii ndio inaongoza katika uchafuzi wa mazingira visiwani humo na kuzitaka Idara zinazohusika kujipanga kukabiliana na tatizo hilo hilo, huku Ofisi ya Mwanasheria Mkuu ikisema kuwa yeyote ambae atakiuka taratibu za Mazingira ataburuzwa mahakamani na kupigwa faini ya Sh million 2 ama kwenda Chuo cha Mafunzo kwa kipindi cha miezi sita.

Wednesday 4 February 2009

Child Custody after Divorce



In Tanzania, custody is governed by civil law, regardless of the type of marriage. The 1963 Law of Persons Act declared that children born inside marriage belonged to the father. However, the 1971 Marriage Act requires custody to be decided in the best interest of the child, but routinely defers to custom in individual cases. Prior to 1971, custody of Muslim children was administered under Islamic Law; however, the uniform codification of the Marriage Act included child custody regulations. Practically, if a woman files for custody, the father will not contest the motions. Here means that when woman open a case for custody father will not be able block the case. However, in absence of contestation, the father generally gets custody. Further, the Marriage Act provides that a father is responsible for maintenance of children until 18 years of age, regardless of custody
Custody patterns also vary depending on local lineage patterns. Among the matrilineal Muslims, the child belongs to his or her mother and her lineage, and remains with the mother in case of divorce, until age of 7; courts also directed to consider: customs of community to which parents belong; economic circumstances of both parents; housing that both parents can provide; and behaviour of mother and whether she contributed to marital breakdown If the mother dies, the child still remains with the members of the matriline and is usually maintained by a maternal uncle.

Looking to law governing marriage and divorce in Tanzania Act of 1971 (LMA) Section 125 of LMA provide for custody of children after divorce that may be granted either to the father or mother or any third party who is in position to provide for welfare of the children.
Section 126 provides for condition to custody order and section 127 provides for principle of welfare of child and in determining custody of children the welfare of the child is paramount and the court will grant custody to the one who is in better position to grant custody, however court always prefer before deciding on granting custody divorce parties to agree themselves to whom the child will leave with.

Welfare of the child including food, clothes, shelter, education, culture as well as good moral or attitude of the parent. So this is not only a matter of financial position of the parent.
Looking to the cases concerned the child custody after divorce in Tanzania based on the group focus, “why always mother have more right to be granted custody of child”. Here are examples which shows that even father can be granted custody of child

In case of Vestina Kibutu vs. Mbaya (1985) Tanzania Law Report (TLR) 42 custody was granted to the father because he was in the position to provide education and psychological development.
Another case of Re Steven Christopher Newborn (1975) TLR 24, courts in discussing welfare of the child takes into consideration social aspect and culture of divorcee. In this case spouses were English and divorced in Mwanza Tanzania. Mother decided to stay in Tanzania with her son Steven, Husband wanted to go England with his son. Court in its decision said it is better for father to go with his son England to be raised with English culture.

Monday 2 February 2009

Mapenzi ya Tanzania Bara na Zanzibar mashakani...


Wengi wetu siku hizi tunapenda kufananisha muungano wa Tanganyika na Zanzibar na ndoa ya watu wawili wapendano. Ndoa huja baada ya wawili walioshibana kuamua kuishi pamoja kwa muda wote wa maisha yao. Zipo aina kadha wa kadha za ndoa zote hizo huwa na lengo moja la kuunganisha wale wapendanao.

Mapenzi siku zote uzaliwa na kukua na hatimae kupevuka, siku zote mapenzi hukuzwa na wapendanao kwa kujaribu kuheshimu yale apendayo mwenza wake. Hii ni kwa kila upande na sio jukumu la mmoja tu ndani ya hayo mapenzi. Yapo mambo mengi ambayo ufanyika kwa lengo la kudumisha na kuendeleza mapenzi. Na haya yote hufanyika kwa moyo wa dhati ili mradi tu kuona penzi linakuwa kila siku.

Tofauti ndogo ndogo siku zote uwepo katika mapenzi, na wale ambao hupenda kuona mafanikio na kudumisha mapenzi yao hupenda kuzijadili tofauti hizo kungali mapema ili kuzuia tofauti hizo kuwa tatizo baina yao. Hii ni mojawapo ya vitu vya msingi sana katika ndoa zinazojali mapenzi.

Ndoa ya Tanzania Bara na Zanzibar sasa ipo kwa muda mrefu kiasi cha kusema kuwa imekomaa ila mapenzi katika ndoa hii muhimu yamekuwa yakipungua kila siku na katika spidi kubwa kiasi cha kuhatarisha ndoa yenyewe.Vitu vyote muhimu katika kukuza penzi zimewekwa kando badala yake chuki na kusingamana vimechukua nafasi.

Katika nyakati tofauti tumeshuhudia mambo kadha wa kadha yakifanyiwa marekebisho ili mradi kulienzi penzi na kudumisha ndoa, tokea wakati ule wa kusafiri kwa passport hadi kuongezwa kwa mambo kadhaa ndani ya ndoa hiyo. Hata hivyo kwa upande mmoja wa wanandoa hawa amekuwa akiburuzwa mno, mambo mengi amekuwa akinyang'anya tokea kuwa na sauti ya pili kwa ukuu ndani ya ndoa hiyo hadi sasa ambapo hana sauti yoyote, hata uhalali wake umeanza kuhojiwa, mbaya zaidi pamoja na kukubali kufutwa kwa kutumia karatasi baina ya nchi mbili hizi, inashangaza sana kuona kuwa makaratasi yameondolewa kwa binadamu tu.Iwapo una gari ukitokea upande wa Visiwani, gari hilo linabidi kuwa na karatasi ili liweze kutembea upande wa pili wa ndoa.

Kuna kero zingine zinachosha sana, na wala hazisaidii kurutubisha ndoa zaidi ya kuitia ubovu ambao mwisho wake ni kuvunjika tu.

Friday 30 January 2009

Wazenj na Mashairi




PONGEZI kwake Shamhuna, pamoja na Ali Mzee
SMZedi kujikuna, na kuridhisha wazee
Shabashi na kujivuna, Zanzibar isiteketee!

Zanzibar isiteketee, vigogo kuyabaini
Mwakanjuki atutetee, nahodha wa mapinduzi
Na Salmini tuletee, salamu za uzinduzi!

Salamu za uzinduzi, kutia ghera na moyo
Kumbukeni mapinduzi, ni kombozi si uchoyo
Zanzibar si Bata Shuzi, si Lindi si Bagamoyo!

Si Lindi si Bagamoyo, Dola ya Mwinyi Mkuu
Isikatwe yake roho, Dunga ... Unguja Ukuu
Nayo Pemba si Mohoro, imefungasha na Bweju!

Kufungasha na Bweju, Mafia na huko Kilwa
Lakini hayo ni makuu, Mrima kukaripiwa
Na tudai Siku Kuu, Zanzibar kuheshimiwa!.

Wednesday 28 January 2009

Walevi Tende kumbe wapo wengi...


Ziara ya Prez Kikwete kule PBA na Zenj ambayo imemalizika hivi karibuni, imeacha maneno mengi na hasa kutokana na hotuba zake ambazo alizitoa wakati wa ziara hiyo. Huku wengi akilidhika na yale yote ambayo alihutubia katika mikutano ya hadhara na wakati wa funguzi mbalimbali wa miradi, wachache wakiongozwa na chama cha maalim wameendelea kubeza kama kawaida yao.

Kwa upande wangu ziara hiyo ilikuja katika wakati muafaka kabisa na ni baada ya sherehe za Mapinduzi ambazo zinakumbuka Mapinduzi yaliyo zaa serikali ya walio wengi visiwani humo. Mapinduzi haya yalikuja mwezi mmoja baada ya Uhuru wa mashaka uliotolewa na Waingereza kwa Waarabu wachache na jamaa zao huko visiwani zikiwaacha wananchi walio wengi katika giza la kitwana. Historia ya mapinduzi hayo kwa sasa itakuwa inafahamika vizuri kwa kila mtanzania kwani imeshapita miaka 45 tokea yatokee na kila mwaka yamekuwa yakikumbukwa. Na hivi leo anapotokea mtu ama kikundi cha watu kuhoji ama kubeza mapinduzi hayo, inafaa umtizame mara mbili mbili kama tayali ameshapata vinibu kadhaa ama la!

Mwaka jana kuna kundi ambalo linadai kuwa linahusu Uhuru wa Zenj, ambalo liliamua kuadhimisha sherehe haramu za uhuru! Mpaka sasa sijajua walikusudia nini katika maadhimisho hayo, ingawa wao walikuwa na haya ya kusema

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kiongozi maandalizi ya sherehe hizo, Daud Jabil Seif, alisema wameamua kuadhimisha sikukuu hiyo ili kuwaenza waasisi wa uhuru wa Zanzibar wa mwaka 1963 ambao hawakumbuliwi na serikali.


Sasa hii maana yake ni nini kama sio kuanzisha chokochoko dhidi ya Mapinduzi ya mwaka 1964. Hapana shaka kabisa huu ni ulevi wa tende toka katika mtaimbo wa kwanza. Kwa zaidi ya miaka 40 imekuwa ikielezwa maana ya mapinduzi ya Zenj na kwa nini yalifanyika na kwa nini yataendelea kudumishwa.

Walevi wengine wa tende wanajaribu kuingiza mfumo wa vyama vingi na hatima ya Mapinduzi ya Zenj. Wao huku macho yao yakiwa mekundu kutokana na ulevi wa tende na asusa za mapera mchana wa jua la utosini huku wakivuja mijasho wanasema kuwa
Lakini kauli ambayo nataka zaidi kwa leo kumhusisha nayo Rais Kikwete ni ile ya kulileta tena suala la Mapinduzi ya Zanzibar ya 1964 na kama kawaida linapotajwa suala hilo malaika huwasisimka watu. Alisema haiwezekani kabisa kuchezea Mapinduzi hayo ambayo sasa yana umri wa miaka 45.

"Kama hajipendi ajaribu…kama hajitaki ajaribu…Yote chezeeni Mapinduzi hapana…ukiyachezea Mapinduzi unawarudisha watu kwenye utumwa, unawarudisha watu kwenye utwana. Hili liliondoka Januari 12, 1964 na halitarudi tena….haiwezekani."



Hiyo ndio kauli aliyoitoa Rais Kikwete ambayo inanifanya nijiulize masuala chungu nzima na hasa kuhusisha kauli hiyo na suala zima la demokrasia na ushiriki wa kisiasa hapa Zanzibar.


Mlevi huyu amesahau kuwa vyama vingi vimekuja baada ya Mapinduzi na vimeidhinishwa na Baraza la Wawakilishi ambalo ndio utunga sheria kwa serikali ya mapinduzi. Hapana shaka mlevi huyu ambae ni mwandishi wa makala kadhaa, bado ana faida za tende na kusahau kuwa Chama chochote cha siasa ambacho kitashindwa kuyatambua mapinduzi ya Zenj hakina nafasi ya kutawala huko Zenj. Maalim na madevu yake alijaribu mara kadhaa na joto lake ameliona na sasa amefyata mkia. Hata hivyo sio rahisi kuaminika kwani jamaa wale walipelekewa tu taarifa za Mapinduzi hivyo hawajui uchungu wake... Na Wengi wanajua kuwa Uchungu wa mwana aujuae mzazi

Pamoja na mambo mengine Prez JK aliwaambia waziwazi wale wote ambao wanabeza maendeleo ya SMZ na JMT katika visiwa hivyo ni sawa na walevi wa tende, kauli ambayo naona inawafaa sana maruuni hao.

Wednesday 14 January 2009

Tukiwa bado kwenye wiki ya Sherehe za Mapinduzi



Wakati tuneendelea kujadili hotuba ya Mhe Prez wa Zenj wakati wa shehere za miaka 45 ya Mapinduzi na yale yote yaliyojili katika sherehe hizo,ambapo kama kawaida yamezua mazungumzo marefu sana sehemu mbalimbali hapa duniani...

Leo hebu tuangalie jina la mtaa maarufu wa Darajani, Jina hili limetokana na kuwepo na daraja katika eneo hilo. Zaidi daraja hilo lilikuwa limepambwa na taa za umeme na kulifanya kuvutia sana na kupitika hata wakati wa usiku. Kumbukumbu za kuwepo na taa hizo inakwenda nyuma mwanzoni mwa miaka ya 1900.

Hali ya sasa hapo darajani inasikitisha sana, umaridadi wake umepotea na imekuwa ni kadhia tu kupita katika mtaa huo sio mchana wala usiku. Eneo la darajani ambalo limepakana na barabara ya Benjamin Mkapa(greek road), kwa sasa halina taa na linategemea taa zenye mwanga hafifu toka kwenye maduka na makontena,huku yakiongezewa nguvu na kandiri za wauza vitambaa.

Kama kawaida sababu tele za kujaza pakacha la mkaa zinaweza kutolewa kutokana na uchakavu wa eneo hilo, pasipo kutoa hatua madhubuti ambazo zinaweza kuchukuliwa japo kuboresha eneo hilo maarufu kwa biashara.

Labda tuwasubiri Agha Khan wakimaliza kukarabati soko la chakula la jioni, labda watawakumbuka wauza vitambaa wa hapo darajani. Maanake sio Manispaa ya Mji wala hao wenye Mamlaka ya Hifadhi na Uendelezaji wa Mji Mkongwe wenye nia na uwezo wa kuboresha eneo hilo.

Thursday 6 November 2008

"Migogoro ya Kisiasa katika SMZ"- Hayo ni Mavuno...

Hivi karibuni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Kiongozi, alinukuliwa akisema kuwa migogoro ya kisiasa katika SMZ imekuwa chanzo cha ucheleweshaji wa mipango ya maendeleo ya wananchi wake. Kauli hii sio ngeni miongoni mwa wananchi wa visiwa vya Zenj hali kadhalika kwa maelfu ya watendaji wa vyombo mbalimbali ya SMZ. Migogoro inayozungumziwa na Mhe. huyo ni matokeo ya sera za umimi na uwale zilizozaliwa wakati Visiwa hivyo vilipoanza kuingia katika mfumo wa vyama vingi mapema katika miaka ya tisini.

Siasa katika vyombo vya SMZ ilikuwa ni kwa manufaa ya chama tawala, hii ni kwa watendaji wote kuanzia wa ngazi za chini hadi za juu. Kila mfanyakazi aliaminika kuwa ni mwanachama wa chama tawala na ameajiliwa ili kutekeleza sera za chama. Hii ilikuwa inadhibitisha na ushirika wa asasi za SMZ katika shughuli za kichama ambapo ilifikia hatua za kufunga ofisi kabla ya muda wake ili kutoa nafasi kwa wafanyakazi kushiriki katika mikutano ya hadhara ya chama tawala. Nahisi katika kipindi hicho hadi sasa ni shurti uwe mwanachama wa chama tawala kabla ya makablasha yako ya uombaji kazi kujadiliwa.

Hata hivyo kuingia kwa mfumo wa vyama vingi kulibadilisha mtazamao wa wafanyakazi kuhusu umuhimu wa kuwa katika chama tawala ili kuendelea kuwatumikia wananchi. Mabadiliko haya yaliguza wafanyakazi katika ngazi zote. Wafanyakazi wa ngazi za juu ambao wengi walikuwa katika nyadhifa zingine chamani, huku wakipata misukumo toka chamani, bila kujijua walianza kupandikiza mbegu mbaya mno ndani ya vyombo vya SMZ.

Katika moja ya mikutano ya kampeni ya 1995 Kiongozi wa ngazi ya juu chamani na katika SMZ alitamka maneno ya kejeli mno kwa watendaji wa SMZ ambao wamehusu kisiwa cha pili. Hotuba yake hiyo ilijukuwa imejaa ubaguzi na shutuma nyingi kwa wafanyakazi na wananchi toka katika kisiwa cha pili haikuweza kujenga bali ilikuwa ndio mwanzo wa migogoro katika Idara zote za SMZ, ambapo Mhe. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri kiongozi anazungumzia.

Nakumbuka siku mbili baada ya hotuba ile, mmoja wa mfanyakazi katika idara ya kutoa huduma ambae alikuwa ni rafiki yangu aliniambia kuwa pamoja na kuwa na mapenzi ya muda mrefu na chama tawala lakini maneno yaliyozungumzwa na kiongozi huyo ni matusi makubwa kwao watokao kisiwa cha pili, hivyo anajitoa rasmi katika chama tawala, na yupo tayali kwa lolote ambalo litamtokea kwa hatua hiyo yake.

Mbaya zaidi, baada ya hotuba hiyo wafanyakazi wengi waliohusu kisiwa cha pili ambao walionyesha mapenzi tofauti walijikuta wakipoteza kazi zao, wengine wakinyanyaswa na kutegwa kwa sababu za kisiasa tu na tena kwa sababu ya SMZ kuunganisha siasa na serikali.

Haya aliyozungumza Mhe. Waziri hayana kificho, kwani katika moja ya miafaka ilikubalika kuwarudisha makazi wale wote ambao walifukuzwa kazi kwa tofauti za kisiasa. Ni wajibu wake iwapo anataka kuona migogoro hiyo inakwisha kuchukua hatua za vitendo katika kuona kuwa siasa katika Idara za SMZ zinawekwa kando, ikiwa ni pamoja na kuwarudisha wale wote ambao walitimiliwa kwa ajili ya mitazamo yao ya kisiasa. Kwa upande wa ajila mpya zisiangalie siasa bali uwezo wa mfanyakazi.

Zaidi Mhe anatakiwa kuona kuwa utengano katika idara za SMZ unakwisha ili kuweza kuongeza kasi ya kutoa huduma na kuleta maendeleo kwa wananchi wa visiwa hivyo.

Wednesday 8 October 2008

Mbolea ya Mboji katika mjadala


Waalimu wawili wakuu wa shule ya Msingi za Kahama na Kirumba pamoja na Mwalimu toka shule ya msingi Isenga, wakifuatana na Mratibu wa Mradi wa Tampere - Mwanza wametembelea chuo cha TAMK Tampere kujadili maendeleo ya mradi wa utengenezaji wa mbolea katika shule zao jioni ya leo. Pichani Waalimu hao wakitoa maelezo juu ya mradi huo ambao kwa ufupi umekuwa ni wa mafanikio makubwa.

Aidha wanafunzi wa TAMK walipata kutoa shukrani zao juu ya ushirikiano mkubwa wakati wa uanzishaji wa mradi huo wa aina yake wenye lengo la kuwashirikisha wanafunzi katika utengenezaji wa mboji.



Hadi sasa shule zote tano ambazo zipo kwemye mradi huu zimefanikiwa kuzalisha mbolea hiyo, huku shule ya msingi ya Isenga ikiwa tayali imeanza kutumia mbolea hiyo kwa upandaji wa miti katika shule yao. Mwalimu toka Isenga alisema kuwa mafanikio hayo yameanza kuvuka mipaka ya shule hiyo kwa baadhi ya wakaazi wa karibu na shule hiyo kuanza kutengeneza mbolea ya mboji.

Mipango ya baadae ni kuendelea kutoa elimu ya utengenezaji wa mboji kwa shule nyingi zaidi katika Jiji la Mwanza. Aidha kutoa nafasi kwa wanafunzi na wananchi wa jiji hilo kupitia vikundi kazi kutembelea jiji la Tampere ili kutoa ujuzi wao wa kutengeneza mbolea kwa wakaazi wa jiji la Tampere. Hii itakuwa ni nafasi nzuri zaidi kwao, kwani matumizi ya artificial fertilizer yanategemewa kupungua kwa kasi katika nchi ya Finland kutokana na kuongezeka kwa bei yake kwa kiwango cha asilimia 300.

Kwa upande wa TAMK wanafunzi wameonyesha kulidhika sana na mradi huo kiasi kwamba idadi ya wanafunzi wanaotegemewa kwenda kwenye awamu ya pili ya mradi huo imeongezeka. Hii ni changamoto kwa Jiji la Mwanza kuandaa shughuli nyingi kadili ya idadi ya wanafunzi hao ili kuweza kunufaika vema na utaalamu wao.

Tuesday 30 September 2008

Idd Mubaraka


Napenda kuwapa mkono wa idd wadau wote wa blog hii. Sikukuu njema

Monday 29 September 2008

Wanafunzi na Mazingira...Case: Mwanza





Mazingira ya shule ya Msingi Igoma. Shule hii ina klabu ya mazingira ya wanafunzi na moja ya kazi zake ni kutunza mazingira ya shule hiyo.




Wanafunzi wa shule ya Msingi Kirumba wakiandaa shimo kwa ajili ya utengenezaji wa mbolea kwa taka za jikoni. Klabu ya Mazingira katika shule hiyo hujishughulisha na usafishaji wa mazingira katika kata yao ya Kirumba.


Uandaji wa mashimo kwa ajili ya kutengeneza mboji kutokana na taka za jikoni, katika shule ya Msingi Isenga

Wednesday 24 September 2008

Chumbe...Na sifa zake





Chumbe ni kisiwa chenye ukubwa wa hekta 20 na kipo umbali wa kilomita 6 toka Mji Mkongwe - Zanzibar. Ni rahisi sana kukiona kisiwa hiki ukiwa unaingia ama kutoka Zanzibar kwa njia ya bahari... aidha iwapo unaingia kwa njia ya anga unaweza kukiona kisiwa hiki kilichojaliwa utajili wa mazingira ya baharini.

Umaarufu wa Chumbe kwa wakaazi wengi wa Zenj hautokani na umaarufu unaojulikana duniani kote katika mazingira ya kisiwa hicho, bali ni kutokana na kauli za viongozi wa kisiasa wa visiwa hivyo wakitumia kisiwa hicho kama mpaka wa mambo mengi ya kisiasa baina ya Zanzibar na Tanzania Bara. Viongozi wengi kuanzia Marehemu A.Karume, rais wa kwanza wa visiwa hivyo amehawi kunukuliwa akisema baadhi ya mambo ya Tanzania Bara mwisho wake ni Chumbe.... na wengi kwa wakati tofauti wamekuwa wakiendelea kutumia kisiwa hicho kutenganisha mambo ya SMZ na JMT.... Pengine hata sasa kwenye sakata la mgao wa mafuta wengi watadai kuwa JMT mwisho wao ni Chumbe...

Zaidi ya mambo ya kisiasa kisiwa hicho kinajulikana duniani kama ni kisiwa cha kwanza duniani kuwa na "Coral Park" inayomilikiwa kibinafsi, kisiwa cha kwanza katika Tanzania kuwa na "Marine Park" aidha ina hoteli ambayo ipo kwenye hoteli 20 bora duniani kimazingira "Eco Hotel". Zaidi, kisiwani humo unaweza kuwaona kobe kadhaa, na kuna kobe mwenye miaka zaidi ya 125 ndani ya kisiwa hicho.. Zaidi kisiwa hicho kimewahi kushinda tuzo ya British Airways- Tourism for Tomorrow, mwaka 2000

Saturday 20 September 2008

Jumba la Maajabu- Beit al Ajaib - House of Wonders....Ni kwanini likaitwa hivyo?



Ni rahisi kuliona unapoingia Zanzibar kwa njia ya bahari. Ni jumba lenye historia ndefu sana katika kisiwa cha Zenj. Leo hii Jumba hilo lenye zaidi ya nguzo 40 linatimiza miaka 125 tokea kujengwa kwake. Mengi yamelikuta jumba hilo kiasi cha kuwa mojawapo ya vivutio vya utalii katika Zanzibar.

Katika kusherehekea miaka 125 ya Jumba hilo ni vema kujikumbusha historia yake na umuhimu wake katika historia ya Zanzibar. Ubunifu wa jumba hili ulifanywa na askari wa meli toka Scottland na lilijengwa na surtan Barghash bin Said katika mwaka wa 1883, kwa ajili ya ofisi yake. Zaidi matumizi ya jumba hilo yamekuwa yakibadilika kadiri miaka ilivyokuwa ikienda na jinsi tawala zilivyokuwa zikibadilika visiwani humo.

Matumizi ya jumba hilo kati ya mwaka 1870-1888(miaka 120 nyuma)ilikuwa ni kwa ajili ya sherehe za kitaifa, kumbuka wakati huo Zenj ilikuwa chini ya utawala wa kisultan... Hadi kufikia mwaka 1913 Waingereza walilifanya jumba hilo kuwa ofisi ya serikali za mitaa. ofisi hizo zilidumu hadi wakati wa uhuru na baadae mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964. Kati ya mwaka 1964 na 1977 Jumba hilo maarufu lilitumika kama jumba la kumbukumbu za ASP na SMZ kwa ujumla... Kwa mfano ndio ilikuwa sehemu pekee ya kuweza kuona magari ya Rais wa kwanza wa Zanzibar Marehemu Abeid Karume.

Ilipoundwa CCM mwaka 1977, Jumba hili liliendelea kutumika kama makumbusho ya ASP na taifa na kama ofisi ya CCM, hali ya jumba haikuwa ya kuridhisha sana pamoja na kuwa na historia ndefu.


Kuja kwa mamlaka ya hifadhi na uendelezaji mji mkongwe kulifungua ukurasa mpya wa hifadhi ya mji mkongwe hii ilikuwa katika miaka ya mwisho ya 1988 hadi mwaka 1994 ambapo sheria ya mamlaka ya hifadhi na uendelezaji mji mkongwe ilipopata baraka za Baraza la wawakilishi na siginecha ya prezidenti.. Mwaka 1992 nilipata kufanya kazi na UNDP kaatika kukarabati Jumba hili na ni hapo nilipopata nafasi ya kuweza kuvinjari jumba hilo kwa mapana na marefu... ni wakati ambapo nilipenda kujua ni kwa nini jumba hilo likaitwa la maajabu, ni wakati ambapo nilipenda zaidi fani yangu ya ujenzi na nilikuwa na kila raha nafuraha ya kushiriki katika matengenezo/ukarabati wa jengo hilo...

Moja ya sifa kubwa ya ya jumba hili ni vita vilivyodumu kwa muda mfupi kabisa katika historia ya vita duniani! Vita hivi vilitokea mwaka 1896, na baada ya vita hivi ndio picha halisi ya jumba hilo kwa leo inavyoonekana. Hii ni baada ya kuunganisha mnara wa saa uliokuwa mbele ya jengo hilo na jengo lenyewe.

Lakini ni kwa nini likaitwa jumba la maajabu?... Wataalamu wa histori ya Zenj wanasema umarufu wa jengo hilo umejengwa kwa sifa zifuatazo;-
1. Ni jumba la kwanza Afrika ya Mashariki kuwa na Umeme.
2. Ni jumba la kwanza Afrika ya Mashariki kuwa na lifti( elevator)
3. Ni jumba la kwanza Afrika ya Mashariki kuwa na mfereji ndani ya nyumba( Bomba la maji)

Lakini kwa nini Jumba hilo sio maarufu sana miongoni mwa wakaazi wa visiwa hivyo? Hii inatokana na imani kuwa katika nguzo zaidi ya arobaini za jumba hilo ni makaburi ya watumwa waliozikwa wakiwa hai...

Thursday 18 September 2008

Ndoto inapoyeyuka....


Kwa muda mrefu kumekuwepo na uvumi wa kuwepo kwa mafuta katika visiwa vya Zanzibar, hii ni kutokana na chunguzi mbalimbali zilizowahi kufanyika katika visiwa hivyo katika nyakati tofauti. Uvumi huo kwa kiasi uliweza kuwafanya Wazenj waanza kutembea vifua mbele wakiwa na imani siku moja itafika na mafuta yatachimbwa katika visiwa hivyo katika kiwango cha biashara. Hii ilipelekea hata serikali ya muungano kuingiza kinyamela suala la gesi asilia na mafuta katika mambo ya muungano, na kufanya neema hiyo kama itakuwepo basi itakuwa ni ya muungano.

Taarifa za hivi karibuni kuwa kuna uwezekano mdogo wa kuwepo kwa mafuta hayo kumesababisha Wawakilishi kutoamini masikio yao toka kwa mtaalamu wa uchunguzi wa mafuta.... Kwa maelezo zaidi soma hapa

Monday 15 September 2008

Ngoma Afrika Band na Ziara yao Ulaya...









Bendi ya mziki wa dansi ya The Ngoma Africa inayoongozwa na mwanamziki nguli Ebrahim Makunja alimaarufu Ras Makunja hilifanikiwa kuufunga mtaa mrefu katikati ya jiji la mji mashuhuri wa Hamburg,katikati ya eneo maarufu hamburg-Haltona,
kulikuwa pata shika ya Nguo Kuchanika wakati bendi hiyo mashuhuri kwa kuwadatisha washabiki hakili na mziki wao wa dansi "Bongo dansi" kutoka Tanzania ukiwa unarindima
Live katikati ya mji katika tamasha kubwa la aina yake Afrika-Festival.

Hilikuwa majira ya saa 2.30 usiku wakali wa mziki wa dansi barani ulaya "The Ngoma Africa band walipanda jukwaani na kuanza kuporomosha nyimbo zao za kiswahili zilizo sindikizwa na mdundo mkali wa dansi ! mziki ambao uliweza kuwazoa mashabiki kwa kasi
ya aina yake na kuwatia kiwewe maelfu ya washabiki katika tamasha hilo.

*Ni Ras Makunja na Bendi ya The Ngoma Africa !
siku hiliyofuatia 30-08-2008 wakali wetu hawa walipanda jukwaa kubwa katikati ya
mji wa Krefeld,katika onyesho kubwa la wiki ya mwafrika (Africa Week) huko nako kuwa
patashika washabiki wamataifa mbali mbali wakiwa wamechanganyikiwa na mdundo wa
dansi wa Tanzania,jukwaa lilikuwa limezungukwa na walinzi wenye suti na miwani meusi,
Ras Makunja na kikosi chake wakiwa jukwaani na kuhakikisha mdundo huo unawamtingisha kila mtu.

Bendi hiyo ambayo imefanikiwa kuwanasa washabiki wa ulaya na mziki wao wa dansi
kutoka bongo Tanzania,inasemekana ndio bendi pekee ya mziki wa dansi iliyoweza kugusa hisia za kila mshabiki,si watoto wala wakubwa,vijana kwa wazee,wake kwa waume,wazungu na weusi hili mradi dansi lao linatingisha.

Taarifa hii imeletwa kwa hisani kubwa na Msema Kweli

Sunday 14 September 2008

Madawa ya kulevya na Zenj...Watoto matatani!




Matumizi ya madawa ya kulevya huko Zanzibar sasa yamechukua sura mpya ambayo ni mbaya sana na ya kutisha katika historia ya matumizi ya madawa hayo Visiwani humo. Athari za mwanzo kwa jamii ya visiwa hivyo ilikuwa ni pamoja na kuvunjika kwa ndoa, umalaya na wizi. Hatua ya sasa ni kuambukiza watoto wadogo virusi vya ukimwi kwa kuwachoma sindano zenye damu isiyo salama. Huu ni unyama wa aina yake kutokea huko visiwani.

Hadi kufikia mwaka 2001, Zanzibar ilikuwa tayali imepata umaarufu mkubwa wa kuwa bandari ya kupitishia madawa ya kulevya. Umaarufu huu ulisadikiwa kufunika hata umaarufu wa soko la watumwa uliotokea miaka mia mbili iliyopita. Ukuuaji wa biashara ya ya madawa ya kulevya katika Zanzibar ulikwenda sambamba na uporomokaji wa bei ya karufuu katika soko la dunia na kupanda chati kwa biashara ya utalii.

Awali, Zanzibar ilikuwa ni pepo ya wasafiri watumiao Bangi. Hii ilitokana na urahisi mkubwa wa kupatikana kwa bangi visiwani humo. Taratibu madawa mengine ya kulevya yalianza kuingia visiwani na kufikia kilele katika miaka ya tisini.

Zanzibar kuwa pitisho kubwa la madawa ya kulevya katika ukanda wa Afrika ya Mashariki, kunahusishwa sana na mabadiliko ya ya kiutawala huko Afrika ya Kusini, ambapo utawala wa kibaguzi ulifikia kikomo. Ulinzi mkali katika bandari ya Mombasa baada ya ulipuaji wa balozi za USA huko Nairobi na Dar es Salaam ni sababu nyingine inayotajwa ya Zanzibar kuwa kimbilio la kupitishwa kwa madawa hayo. Aidha ubinafishwaji wa Uwanja wa ndege wa Zanzibar katika miaka ya mwishoni ya tisini umetajwa kuchangia kwa kiasi kikubwa kukua kwa upitishaji wa madawa hayo katika Zanzibar.

Matumizi ya madawa ya kulevya yamekuwa yakienda pamoja na uongezekaji wa maambukizi ya virusi vya ukimwi. Hii hasa kwa wale wanaojidunga sindano. Uchunguzi unaonyesha kuwa asilimia 46 ya watumiaji wa madawa hayo hushare sindano, huku zaidi ya asilimia 50 wakifanya ngono (group sex na anal sex) ili kupata madawa hayo. Baadhi ya vijana huweza kutumia hadi US$ 240 kwa mwezi kupta madawa hayo.

Matumizi ya sindano yaliweza kuingia katika sura mpya katika miaka ya hivi karibuni, baada ya kuongezeka kwa watumiaji wasio kuwa na uweo wa kununua madawa hayo. Njia maarufu ya "flash blood" iligunduliwa ambapo mtumiaji wenye nazo mfukoni, hujidunga sindano yenye heroin, na akimaliza kijidunga ufyonza damu yake kutumia sindano hiyohiyo na kumpatia asie na uwezo damu yake ilichanganyika na heroin(diluted). Mchanganyiko huu uweza kumpatia nishai asiye kuwa na uwezo wa kununua herion.

Hali ya sasa ni mbaya mno kama si ya kutisha. Kwani watumiaji wa madawa hayo sasa hupita mitaani na kuwachoma sindano watoto wadogo, sindano hizo ni zile ambazo wanatoka kuzitumia kwa madawa yao ya kulevya, hivyo kuwepo na uwezekano mkubwa wa kuwapatia watoto hao maambukizi ya virusi vya ukimwi. Huu ni unyama mkubwa kabisa katika historia ya matumizi ya madawa hayo pamoja na ugonjwa wa ukimwi visiwani hapo. Kwa ufupi wazazi wengi wapo katika hali ya hofu na hasa wale wanoishi katika mitaa yanye vijana wengi wa kubembea, aidha kwa watoto ni adha kubwa mno kwao kwani inabidi kukaa ndani tu kwa usalama wao...

Saturday 13 September 2008

Weekend Njema...




Forodhani bado inaendelea kufanyiwa mabadiliko makubwa ambayo yatawezesha kupatikana kwa huduma bora kwa wadau wote watumiao eneo hilo maarufu sana hapo Zenj... Zaidi hata umiliki wa eneo hilo la historia utabadilika na kuwa chini ya Agha Khan Foundation. Kiutawala kuna mengi ndani ya eneo hilo, kuna migongano kati ya Mamlaka ya Mji Mkongwe, Baraza la Manispaa, Idara ya Mipango Miji, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi na Ofisi ya Waziri Kiongozi.. Hata NGO nazo kwa wakati mmoja au mwingine zimeweza kulitaka eneo hilo, mojawapo ni ZAYADESA...Upande mwingine wafanyabiashara hasa wale wauza vyakula usiku nao udai kuwa hilo ni eneo lao.

Lakini cha msingi eneo hilo linafanyiwa ukarabati katika muda muafaka, na ni ukarabati mkubwa kabisa kufanyika katika eneo hilo. Cha msingi ili eneo hilo liendelee kuwa katika mvuto na kupunguza uharibifu baada ya kufunguliwa tena, ni vema kwa sasa wadau wa eneo hilo wakapatiwa mafunzo juu ya kutunza mazingira ya eneo hilo. Hii isisubiri mpaka uchakavu mwingine utakapotokea. Wote tunajua kuwa "Samaki mkunje angali mbichi" Hivyo hatua za makusudi zinapaswa kuchukuliwa sasa kwa kutoa elimu ya utunzaji na matumizi ya eneo hilo kwa wadau wote watumiao eneo hilo kwa njia moja ama nyingine.

Wednesday 10 September 2008

SMZ Imejichokea....

Mwishoni mwa wiki iliyopita, Waziri wa kazi na maendeleo ya watoto katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar(SMZ) alinukuliwa akisema kuwa nusu ya wanzibari milioni wenye uwezo wa kufanya kazi hawana kazi. Hii ni kusema asilimia 50 ya watu wenye uwezo wa kufanya kazi hawana kazi. Ni idadi kubwa sana na yenye kutakiwa kufanyiwa kazi. Hesabu hii inajumuisha sekta rasmi na sekta zisizo rasmi visiwani humo.

Kama kawaida wimbo ukawa ni ule ule wa kushaauri kuwa wote wasio na kazi waande makondeni(mashambani) kwa ajili ya kulima, au kwa ufupi wawe wakulima, ila safari hii wimbo huo uliongezewa vionyo vingine kuwa wawe wakulima wa mazao ya biashara. Lakini kila nikijaribu kuangalia idadi ya watu hao na konde zilizopo sasa huko visiwani napata mashaka kama bado hili ni wazo madhubuti la kuondokana na ukosefu wa ajila visiwani humo.

Ikumbukwe kuwa wananchi wengi wa visiwa hivyo walishawahi kugaiwa ardhi kwa ajili ya kilimo, maarufu kama eka tatu. Wakati SMZ ikitoa eka hizo kwa wananchi wake ilikuwa na lengo la kuwafanya wengi wawe wakulima. Hata hivyo ugawaji wake haukuweza au kulenga wale wasio na ajila. Eka tatu hizo kwa sasa ni wachache mno ambao wamendelea kuzitumia kwa shughuli za kilimo, wengi wao walishaziuza kupisha ujenzi wa nyumba za kuishi na biashara.

Zanzibar ni nchi ambayo imekulia katika sekta kubwa ya kibiashara zaidi ya kilimo. Ingawa iliwahi kuvuma sana kwa kilimo cha karafuu, nchi hiyo haijawahi hata mara moja kujitoshereza kwa kilimo cha mazao mengine, pamoja na kuwa mbele sana kwa vifaa na taaluma katika sekta hiyo ya kilimo. Ukiondoa mazao ya Nazi na karafuu na matunda kuna mazao mengi yanalimwa huko kama mpunga ambapo bado kufikia nafasi ya kutosheleza mahitaji ya nchi nzima. Karafuu sasa imeanguka katika soko la dunia, Zao la nazi nalo lipo katika mashaka kutokana na kuongezeka kwa ujenzi wa nyumba. Viwanda ambavyo hapo awali vikitoa ajila kwa wakaazi wengi vingi vimekwisha vungwa na kufutika kabisa katika ramani ya utengenezaji wa ajila visiwani humo.

Kuanguka kwa zao la karufuu kulifungua milango kwa utalii, na serikali hiyo ikaona njia nyingine ya kuongeza pato lake ni kupitia utalii. Kuja kwa utalii kulileta sekta isiyo rasmi ya kutembeza watalii maarufu ka upapasi. Awali ilikuwa ni vita kati ya serikali na mapapasi, hii ilitokana na serikali kukataa kuwatambua hao au kukataa ukweli wa kuwepo na sekta isiyo rasmi visiwani humo. Ilichukuwa muda mrefu kwa mapapasi kuweza kutambuliwa na wizara ya utalii kama ni sehemu mojawapo ya utalii aidha inatoa ajila kwa vijana wa hapo zenj.

Kupanuka kwa utalii Zanzibar kulienda sambamba na ujenzi wa hoteli nyingi za kitalii, hii ilitoa picha kuwepo kwa ajila nyingi visiwani humo. Hata hivyo sio serikali au wananchi wa visiwa hivyo ambao walikuwa wamejiandaa na mabadiliko hayo. Kwani kuanzia kazi za ujenzi ziliwezwa kushika na wageni toka Kenya na baadhi ya watanzania Bara...hii iliianza kutoa malalamiko ya chini chini kuhusu ajila kuchukuliwa na wageni.
SMZ ina hotel zake za kitalii chini ya wizara ya utalii, na ina chuo chake cha utalii hapo Maruhubi,wafanyakazi wachache waliosoma hapo Maruhubi uajiliwa moja kwa moja katika hizo hoteli chache za SMZ Sijui ni kwanini SMZ kupitia wizara na chuo hicho walishindwa kuwavuta wananchi wengi kujiunga na chuo hicho ili kuweza kujipatia ajila katika hoteli lukuki zilizokuwa zikijengwa. mkakati wa kitaifa wa kuona kuwa wananchi wananufaika na hoteli hizo. Hata katikati ya miaka ya tisini wakati SMZ ilipokuwa ikipeleka wanafunzi kusoma nje ya nchi kwa mafungu, idadi ya waliokuwa wakienda huko kwa ajili ya masomo ya utalii ilikuwa ni ndogo mmno kulinganisha na wanafunzi wengine ambao kozi zao zinapatikana kwa wingi katika vyuo kibao Tanzania bara.

Mwishoni mwa miaka ya tisini Zenj iliweza kunufaika na mradi wa miji endelevu, ambao pamoja na mambo mengine ulikuwa na lengo la kutatua kero za wananchi, kwa kuwashirikisha wananchi hao katika kuzitatua. Moja ya mradi ambao uliweza kutengeneza ajila ni ule wa ukusanyaji na utupaji wa taka katika wadi ya Mkele. Ingawa idadi ya walioajiliwa mwanzo wa mradi huu walikuwa kidogo, mradi huu ulilenga kutengeneza ajila kwa wananchi, aidha ukiwa kama mradi kiongozi ulitakiwa kupata kila aina ya msaada ili kuendelea na kupanuka ili wadi na asasi zingine ziweze kuiga mfano na kuweza kutoa ajila kwa wengi. Pamajo na kushirikisha asasi zote tokea Wizara ya Kazi na Maendeleo ya watoto, Tawala za mikoa, Ofisi ya Waziri Kiongozi, ILO na Manispaa ya Mji, mradi huu ulikufa kutokana na baadhi ya Wadau katika asasi hizo kutuupa nafasi ya kuendelea.

Miaka ya elfu mbili, ILO walikuja na wazo jingine la kutoa ajila kwa vijana katika Mji Mkongwe na kama kawaida utashi binafsi wa watendaji wa SMZ mradi huo ulishindwa kufanyika.

SMZ imekuwa kama inawaweka wananchi wake kama rasilimali ya kushinda chaguzi tu, kwani kila ukaribiapo uchaguzi asasi za ulinzi visiwani humo hutangaza ajila lukuki kwa vijana. Ni vema sasa kuangalia sehemu nyingine ambazo zinaweza kutoa ajila kwa utaratibu mzuri na wa kuvutia kama vile uvuvi

Sekta ya uvuvi kwa miaka mingi sijapata kusikia kuwavuta wavuvi wapya kujiunga nao, kama ilivyo kwa sekta ya kilimo. Nina imani kama sekta hii nayo itaweza kupew msukumo kama kilimo ambacho vijana wengi hawapo tayali kujiunga nayo licha ya uchache wa konde zilizopo inaweza kutatua kwa kiasi kibubwa tatizo la ajila visiwani humo. Cha msingi ni namna gani ya kuwashirikisha vijana katika shughuli za uvuvi, kwani soko lake ni kubwa na bado uvuvi unahitaji watu wengi zaidi.

Kwa upande wa utalii ni vema kwa SMZ kutilia mkazo kwa wananchi wake na hasa vijana kusomea fani hiyo, ipo haya ya kupanua chuo kilichopo cha utalii sambamba na mahitaji ya hoteli zilizopo. Nina hakika wenye hoteli hizo watapenda kuajili wazaliwa wa hapo kwani wigo wao wa ufahamu wa visiwa hivyo ni mkubwa kuliko wageni na hili ni moja ya chachundu katika biashara ya utalii. Hili linawezekana kwani bado wazenj wengi hasa wazazi wanamtazamo tofauti sana na utalii.

Saturday 6 September 2008

Bandarini Zenj






Pilika pilika bandarini Zenj... Wikiendi njema na Ramadhani njema..

Friday 5 September 2008

Zenj Majaribuni tena....




Mwezi ujao tarehe 24, kisiwa cha Zanzibar kitawakaribisha visura wa Afrika kuweka kambi yao kabla ya kuanza safari ya kumtafuta kisura wa Afika(M-Net, Face Of Africa) visiwani humo. Jumla ya visura 24 watakuwepo kwenye kambi hiyo ambayo itaisha kwa kumchagua kisura wa Afrika katika kisiwa hicho. Aidha kwa Visura wa Tanzania watachujwa mapema wiki ijayo kabla ya kujiunga na wenzao 12 kutoka kona nchi kadhaa barani Afrika.

Zanzibar mara nyingi imekuwa ikipinga aina hii ya mashindano, ingawa kwa nyakati tofauti wazenj wamewahi kushiriki katika mashindano ya kutafuta mrembo wa zenj wa kushiriki Miss World. Nakumbuka niliwahi kuona Miss Aspen katika miaka ya tisini huko Zenj ambapo alikuwa akisakwa Miss Zenj, aidha ilikuwa ni vituko tupu, tofauti na jinsi warembo wanavyotafutwa huko Bara.

Wananchi wengi wa visiwani humo hupinga vikali aina yoyote ya ushindanishaji wa wasichana na hasa namna ya ushiriki katika mashindano kama hayo kwa kuwa yanaenda tofauti na maadili ya visiwa hivyo. Kuna wakati Miss Zenj aliwahi kutafutiwa katika mkoa wa Dar baada yakuwepo na upinzani wa hali ya juu kwa mashindano ya aina hii.

Wengi bado wanakumbuka jinsi washichana/wanawake toka Bara na Kenya walivyokuwa wakichezea fimbo huko Zenj na hasa katika mtaa wa Darajani na kundi moja la watoto wa simba. Pamoja na kundi hilo kujulikana hakuna hatua zozote zilizowahi kuchukuliwa dhidi yao na vyombo vinavyohusika kwa mashumbulio yao kwa wanawake ambao walivaa suruali ama sketi au kutovaa hijabu.

Nina mategemeo kuwa kambi hii ya kutafuta kisura wa Afrika haitopata kadhia za kupigwa bakora, kwani nina imani kuwa kambi yao itawekwa nje ya eneo la mji. Aidha ninategemea kuwa waandaji wa mashindano hayo watawapa kanuni za uvaaji kwa wasichana hao iwapo watatembelea huko mjini. Kwa upande mwingine hii ni mojawapo ya nafasi nzuri ya kisiwa hicho kuendelea kujitangaza ndani ya Afrika. Mshindi atakaepatikana hapo nategemea ataondoka na sifa nzuri za Tanzania na hasa Zanzibar kama hatochezea bakora....

Thursday 4 September 2008

Huu ni mwezi mgumu kwenda Zanzibar


Seagull ikishusha abiria hapo Zenj wakitokea Dar mwishoni mwa wiki iliyopita.


Sea Express ikushusha abiria tokea kisiwa cha pili


Msongamano wa abiria wa kwenda Zenj kabla ya mfungo wa Ramadhani katika bandari ya Dar.


Kwa wale ambao husafiri mara kwa mara kati ya Zenj na Dar au Zenj na Kisiwa Cha Pili watakubaliana nami kuwa sasa kwenye boti kuna viti vya kulala na ni tofauti kabisa na siku kadhaa zilizopita au kwa maneno mafupi kabla ya kuanza kwa mwezi wa Ramadhani. Kwa kawaida mwezi wa Ramadhani abiria wa boti na hata ndege hupungua sana kati ya Zenj-Dar na Pemba.

Sababu kubwa ya kupungua kwa wasafiri ipo wazi, kwani huu ni mwezi ambao wengi hufunga na hasa wakaazi wa visiwa hivi viwili, Hivyo wengi wao hawapendi kusafiri ili kuepuka adha ya kupata futari na misukosuko mingine ambayo inaweza kuwasababisha kufuturu kabla ya wakati. Zaidi waumini wengi utumia muda huu kuhudhuria sala zote za siku ili kukamilisha funga yenye uhakika na iliyokamilika.

Wageni ambao hupenda kufakamia kila wakati, nao ujiepusha kwenda Zenj ama Kisiwa cha Pili, kwani kuanzia mama lishe, migahawa na hoteli hufungwa hivyo kuwafanya kuwa katika hali ngumu sana ya kushawishi matumbo yao kuwa hakuna chakula asubuhi wala mchana... Hii uwakuta hata watalii ambao zaidi ya kukimbia kutofunga hata mavazi yao huwa hayana nafasi visiwani humo.

Hata hivyo, baada ya futari hakuna sehemu nyingine hapo Bongo ambayo unaweza kufaidi misosi ya nguvu kama Zenj... Kwani sehemu nyingi hufunguliwa na kuuza misosi ya nguvu hadi saa sita ya usiku. Maduka huwa wazi usiku na hata zile baa zinazojificha mchana na kuuza ulabu kwa mlango wa nyuma huwa wazi. Kwa ufupi Usiku huwa kunachangamka sana kuliko usiku wa miezi ya kawaida. Wengi ambao hawapendi kuamka alfajili kwa kuwahi daku hupenda kushindilia misosi hiyo hadi mishale ya saa sita na akilala inakuwa imetoka.

Wednesday 3 September 2008

Military Sonar and Life of Marine Mammals





In 2006 April, 28 Zanzibar villagers were in shock after their coastline was covered with 400 dead dolphins. Zanzibar government went on imposing warning to the villagers and fishermen not to consume the dead dolphins as the reason of their death is not know.

From that peace of story from my country which happened about two year ago, rises my eyebrow when I was thinking what should I write concerned the effects of military vessels on the whales. Soon after that incident in Zanzibar, different comments on what might be the cause of their death were discussed. For example, some scientists believe that, the death may be a result of loud burst of sonar, from miles away and can be heard in water therefore scare marine mammals causing them to surface too quickly. This type of movement is known as bends whereby is occur to the people who dive for feeling severe pains and difficulty in breathing as result come to the surface too quickly. Shortly is when sudden decompression forms nitrogen bubbles in tissue. Other speculates the death to be caused by U.S. Navy task force which patrols the coast of East Africa as part of counterterrorism operations. The villagers themselves were thinking that the cause of death was disoriented of those animals which lead them to shallow water and died. Later on the U.S Navy acknowledged that sonar is likely to contribute to the death of those dolphins.

According to Oxford Advanced Learner’s Dictionary, Sonar is described “as a device or system for finding objects under water by means of reflected sound waves.” The history of sonar goes back after the World War I where Britain and U.S develop the technology of navigating by sound in the sea. In the World War II sonar were used to counter attack the German ship. It was until the cold war era where the sonar technology was improved and was much used. In Word War II sonar was passive: essentially big microphones that listened for the distinctive sounds emitted by large submarines. Nowadays there are mid frequencies active sonar designed to find a new generation of smaller, stealthy submarine. Active sonar is working by sending out sound waves and listening for the reflections of the objects, as this provide the location of object detected.


This improvement and advanced system of sonar have been designed and used despite the knowledge of its effects to sea mammals. Even after the end of cold war, sonar has been used in military testing causing whales and dolphins to stranded and dead. The exercise of Navy using mid-frequency sonar which operates from 2,000 to 10,000 hertz has resulting in increasing to the numbers of mammal stranding. As this technology seem not enough to the military, they have now develop the new technology of sonar known as low – frequency sonar which is believed to cause wide range of sound travel. Environmentalists explain fear to this new technology as it will increase the number of whales and dolphins to stranding. Up to date there are numbers of cases which have been reported due to the effect of sonar, as will be mentioned in the following paragraphs.

In September 2002, fourteen beaked whales were stranded in the Canary Island close to the site of international naval exercise. This happened four hours after the mid frequency sonar was deployed. The effect of this tragedy is lost of ability to navigate for the whiles which force them to strand.

In 2003 US Navy Sonar in Pacific Northwest was direct linked to the number of death of whales. This blast draws attentions to many institutes. One of them was Natural Resources Defense Council (NRDC) which went on to stop US Navy of using the powerful active sonar system known as SURTASS LFA. NRDC was also involving other countries on restriction of using the sonar as to prevent the life of marine mammals.

The battle of protecting marine mammals with sonar have take a new look this January 2008, when President G.W Bush allow US Navy ships to use sonar during exercises off the California coast. The exercises is planned to take place in San Diego, where aircraft carries have been permitted to use sonar on detecting submarines. This decision of President Bush is opposing the court order of stopping the uses of sonar in the vicinity of whales.

Going back to my country four hundred dolphins were dead after beached, there is a need of positive thinking this effects which are caused by sonar. Further studies show that there even more effects to these sea mammals such as the reproduction of this endangered species; to disrupt the feeding of orcas; and to cause porpoises and other species to leap from the water, or panic and flee.

Nevertheless there is other dangerous noise which may also contribute on disturbing marine life. These dangerous sources of noise in the sea are manmade. There is ship traffic; the world is now witness increase of ships due to the increased of global business. These ships generate noise from their propeller, engine, generator and bearing. The propeller is one part of ship which provide a noise pollution to undersurface of sea. Propeller can provide noise from frequency range from 20Hz - 300Hz throughout the sea. Sea mammal such as whales whom they use frequency for navigating and communicating can be direct effected with this kind of noises which are traveling hundred of kilometer in the sea.

Bia zenye Vilemba.....


Huko Zenj bia ikifunguliwa shurti ivishwe kilemba...

Saturday 30 August 2008

Zenj yakaribia kuanza kusahau Metakelfin, Chloroquine.....

Akiwa katika ziara yake huko USA, Prez wa TZ Jakaya Mrisho Kikwete, akimshukuru Prez G. W Bush, alisema kuwa huko Zenj wapo karibu kabisa kutokomeza ugonjwa wa malaria. Aliendelea kwa kusema pale sipitali ya Mnazi Mmoja kesi za malaria zimepungua kwa kasi toka asilimia 30 hadi asilimia 1.

Mpaka leo hii Malaria ndio ugonjwa unaouwa watu wengi duniani. Kila mwaka zaidi ya watu milioni moja hufariki kutokana na ugonjwa huu. Hivyo juhudi zozote za kuondfoa ugonjwa huu hazipaswi kupitwa bila kuungwa mkono na kama sio kuzipongeza.

Zenj kwa miaka mingi kupitia misaada mbalimbali imekuwa ikijitahidi kuangamiza mazalio ya mbu ambao husababisha malaria. Hali ya hewa ya visiwa hivyo ni nzuri sana kwa mbu wengi kuzaliana na hivyo kusababisha kuwepo kwa malaria. Njia iliyokuwa ikitumika ni kunyunyuzia dawa za kuangamiza mazalio ya mbu katika kila kona ya mji wa zanzibar, toka mji mkongwe hadi ng´ambo, vita hivyo vya kuangamiza mazalio ya mbu ilibaki kidogo kufanikiwa na ilikuwa ni katika ile miaka ya sabini, hadi hivyo haikuweza kufanikiwa. Kurudi kwa mradi huu katika miaka ya hivi karibuni kulitoa tena faraja kwa wengi katika vita hivi.

Malaria na hasa vijidudu visababishao ugomjwa huu hatari kabisa wamekuwa wajanja na kuendelea kubadilika badilika na kushindana na kinda pamoja na dawa za kutibu ugonjwa huu. Kwangu mimi kesi ya kwanza kabisa ya malaria ilinipata kisiwani Zenj karibu miaka ishirini na tano iliyopita. Dozi ya kwanza kupewa ilikuwa ni Chloroquine, haikuweza kupambana na malaria yangu, baada ya wiki mbili bila mafanikio nilipatiwa dozi nyingine ya Quinine ambayo niliitumia kwa kipindi kingine cha wiki mbili na ilifanikiwa kunitibu. Miaka kumi baadae nikapata tena malaria nikiwa huko huko visiwani,dozi ya kwanza kupewa ilikuwa ni Metakelfin, baada ya wiki vidudu vya malaria vilikuwa bado vikitamba, dr. akanipa Phansider nayo ikashindwa kufanya kazi tena baada ya kuirudia katika wiki mbili mfulurizo. Mwishoe nikaambia nijaribu Halfan.. hapo nikapona

Tatizo la malaria katika nchi za Afrika kwa upande mwingine limefungua mlango wa watengenezaji wa madawa yasio pimwa madhara yake kwa binadamu, na kuuuzwa kwetu Afrika... kwa kisingizio kuwa dawa hizo ni za bei nafuu. Kila kukicha kunatangazwa dawa mpya za kutibu malaria na nyingi kati ya hizo huwa zina side effect kubwa mno kwa mtumiaji.

Vyandarua kwa upande mmoja zimesaidia sana katika vita hivi, ingawa sio wananchi wengi wenye uwezo wa kumudu kununua vyandarua, lakini mchango wake ni muhimu sana . Hili la kuangamiza mazalio ya mbu ndio la msingi. Na iwapo takwimu za ugonjwa huu zinaanza kushuka katika zahanati na sipitalini ni dalili nzuri kuwa kuna mafanikio. Cha msingi ni kwa wananchi wote kuunga mkono juhudi hizi ili kutokomeza kabisa ugomjwa huu wa malaria.

Habari ndio hiyo...

Friday 29 August 2008

Mwezi wa gharama wakaribia huko Zenj...

Unapokaribia mwezi mtukufu wa Ramadhani, Jiji la zenj hujaa pilikapilika nyingi mno, ni rahisi sana kutofautisha jinsi watu wanavyoishi kabla ya mwezi huo kwani kila mtu huwa kwenye pilika za hali ya juu, tofauti kabisa na miezi mengine yoyote katika mwaka.

Kijana mmoja aliwahi kunilalamikia kuwa ingependeza kama kufunga mwezi Mtukufu wa Ramadhani ikawa kama fainali za kombe la dunia kutokea mara moja kwa miaka minne tena katika nchi tofauti. Akiwa na maana iwapo itakuwa zamu ya Tanzania kufunga mwaka huu nchi zingine hazitofunga mpaka zamu yao ikifika....! Sikupata picha kamili ingekuaje kwa nchi zaidi ya mia mbili duniani humu.. Mawazo kama haya uzaliwa kichwani mwa mtu kutokana na majukumu mengi katika mwezi huo.

Kabla ya mwezi kufika wengi hupata mialiko ya kuhudhuria shughuli za arusi, hii yote ni katika kujiandaa na mfungo, kwani wengi hupenda kufuturu majumbani mwao, hivyo vijana wengi hupenda kufunga ndoa katika kipindi kama hichi ili mradi tu awe na uhakika wa kupata futari murua akiwa kwake.

Hali halisi ya Zenj na hasa katika kuandaa futari husababisha ugumu mkubwa katika mwezi huu. Bei za bidhaa hupanda maradufu hivyo kuwa usumbufu mkubwa kwa waakazi wengi wa kipato cha kati visiwani hapo. Ikiwa bado siku kadhaa kabla mwezi huo kuanza bei ya nyama kwa kilo sasa ni zaidi ya sh. 5,000 huu ni mzigo mkubwa. Ikumbukwe bidhaa za vyakula kisiwani humo nyingi hutoka Bara na Pemba, hata hivyo uonekana kama havitoshi pamoja na ukubwa wa gharama.

Sina hakika kama kisiwa cha pili bado wataendeleza mgomo wao wa kutopeleka vyakula huko Zenj, baada ya muafaka kurudishwa tena mezani, na sina hakika hali itakuaje baada ya kasheshe za karibu miezi mitatu kuhusu Zenj kama nchi zitaathiri vipi mfungo wa mwaka huu. Kawaida pamoja na rais wa Zenj kutembelea kwenye markiti akiwaomba wauzaji kupunguza bei, bei hubaki palepale. Safari hii rais atavuka hatua ya kwenda markiti, kwani itabidi kuwashawishi waletaji bidhaa kufanya hivyo na kuweka siasa kando katika mwezi huu.

Ikumbukwe kuwa wananchi hao hujiandaa kwa muda wa miezi kumi kuja kufunga kwa mwezi mmoja, kwani bila ya kujiandaa na kujiwekea akiba unaweza kuja kuumbuka katika kutafuta futari hivyo kuufanya mfungo kuwa mgumu zaidi. Zaidi ya wao wenyewe kujiandaa, ndugu wengi waishio nje ya Zenj na hasa nje ya Afrika wamekuwa mstari wa mbele kusaidia kupunguza makali ya mwezi huu, kwa kujaza wazenj wengi katika ofisi za west union. Kwani pamoja na kujiandaa na futari pia ni mwanzo wa maandalizi ya sikukuu ya Idd ambayo usheherekewa kwa muda wa siku nne mfululizo. Sherehe hizo ni kubwa sana hasa kwa watoto ambao uwakera wazazi wao kwa kudai nguo mpya na maridadi, toys na kadhia zingine ziendanazo na sherehe hizo.

Mie binafsi napenda kuwatakia Wafungaji wote Mfungo mwema....

Sunday 27 July 2008

Zenj imejaa tele Bara


Hivi karibuni nilitembelea katika Jiji la Mwanza na kubahatika kukutana na bango hili, nilijaribu bila mafanikio kuitafita ofisi hiyo ya Bima ambayo ni mojawapo wa Ofisi zinazojiendesha zenyewe visiwani Zenj. Hapana shaka pamoja na kero zinazozungumziwa Shirika hili linafaidi Muungano kwa kuweza kujitanua hadi Jijini Mwanza.

Pengine Mashirika makubwa huko Zenj, ukiondoa Shirika la magari ambalo limepigwa stop kwa namba zake za magari kutumika huko Bara zikafuata mfano wa Shirika la Bima. Asasi zingine ambazo zinaweza kujitatumua huko Bara ni kama asasi ya jeshi la kujenga uchumi, wao wanaweza kuingia katika masuala ya ulinzi, kwani ni soko ambalo linakuwa kwa kasi... Jamaa wa Zenj state engineering ambao pamoja na uwezo wa kujenga nyumba ndani ya siku saba wameendelea kudorora kama sio kufa kibudu kwa kukosa kazi huko zenji, wanayo nafasi nzuri ya kufufuka iwapo wataweza kufuata nyayo za Zantel na Shirika la Bima Zenj

Friday 8 February 2008

Lowassa Ajiwekea Rekodi Zake...



Siku ya jana imeingia katika kumbukumbu za serikali na maelfu ya wananchi wa Tz na wengine wenye uhusiano na Tz kwa namna moja ama nyingine.

Katika kuangalia angalia habari ya Lowassa nimekuja kufahamu kuwa ndie Waziri Mkuu wa kwanza kujiuzuru kutokana na tuhumu ambazo nimemgusa moja kwa moja tokea mwaka 1961. Hii ni rekodi kwake na rekodi ya kumbukumbu kwa viongozi wa ngazi za juu ambao kwa namna moja ama nyingine walijiuzuru, pasipo kuwa na tuhumu zinazowakuga wao Binafsi...

Kama vile haitoshi, Bw. Lowassa ameweka rekodi nyingine mpya ya kuwa kiongozi wa juu kabisa kujiuzuru huku akitizamwa na kusikilizwa na maelfu ya Watanzania kupitia Television ya Taifa (TVT). Rekodi nyingine ambayo ameiweka hapo jana ni kujiuzuru mbele ya Bi. Lowassa. Kwa ufupi Bw. Lowassa amejiwekea rekodi kama tatu hivi katika kipindi kifupi kabisa katika historia ya kujiuzuru kwa viongozi hapo Tz.

Mbaya zaidi, ni kuweka rekodi ya kiongozi wa kwanza kujiuzuru muda mfupi kabla ya ziara ya Prezedent Bush, ambaye anatoka huko kulikosababisha Bw. huyo kujiuzuru. Pichani hapo juu ni picha ambayo inaonyesha mapenzi yake na nchi ya Prez. Bush, ambapo sasa anaweza kumwona kwa kupanga foleni kama wananchi wa kawaida.

Sunday 20 January 2008

Friday 18 January 2008

Mambo ya Mapinduzi....


Tukiwa bado tunasheherekea Mapinduzi ya Zenj, nimeona bora leo tujikumbushe baadhi ya misukosuko ya wakati ule wa mapinduzi........

Monday 14 January 2008

Wazenj na Mechi za Bure...

Tangu kuchukua nafasi ya Ukurugenzi wa wa timu ya Miembeni, Amani Makungu amekuwa akitoa ofa kadhaa kwa washabiki ya soka visiwani humo kwenda kuona mechi bure. Miembeni ni mojawapo ya timu kongwe visiwani, ambayo imewahi kuwa na mafanikio makubwa kisoka miaka ya nyuma, kabla ya kudorora na kupotea katika ramani ya soka hasa kipindi cha ufadhili cha miaka ya tisini.

Timu hiyo ambayo ipo kwenye kitongoji cha Miembeni ambacho kinajulikana sana visiwani humo kwa makasheshe, ilitwaa ubingwa wa visiwa hivyo mara ya mwisho yapata miaka ishirini(1987). Mwaka jana imefanikiwa tena kuchukua ubingwa wa ligi visiwani humo chini ya ukurugenzi wa A. Makungu na kocha Suleiman Mahmoud Jabri.

Ufadhili wa Mkurugenzi huyu umewawezesha wapenda soka na washabiki wengi wa timu hiyo kuweza kuona mechi kubwa ya klabu hiyo bila ya viingilio. Mechi yakaribuni ya bure ni ile ya kombe la mapinduzi ambapo Miembeni iliweza kutwaa kombe hilo baada ya kuifunga timu ya Polisi kwa mabao 2-1. Mechi hiyo ya dezo ilihidhuriwa pia na Mh. Aman Karume Rais Zanzibar.

Wengi wamenufaika na hili, lakini ni vema vilevile kuangalia nini athari zake kwa soka la visiwa hivyo. Baada ya wadhafili wakubwa kujitoa kugharamia timu kubwa huko visiwani, soka la visiwani lilianguka sana, kuanzia katika mechi za ndani hadi za kimataifa. Ukiangalia nyuma kidogo kama miaka kumi iliyopita hasa katika kipindi cha miaka ya 1996-1998, kulikuwa na upinzani mkubwa wa vilabu kutokana na utajili wa wafadhili wao. Timu ambazo zilikuwa zikivuma kipindi hicho ni Mlandege, Malindi na Shangani, ambazo zote zilikuwa chini ya ufadhili wa wafanyabiashara. Timu kama ya Malindi iliweza hata kusajili wachezaji toka Ulaya ya Mashariki na Afrika vilevile. Klabu kama Miembeni, Kikwajuni na Small Simba ambazo hazikuwa na wafadhili ziliporomoka vibaya katika kiwango cha soka visiwani humo.

Lakini nini kilitokea baada ya wafadhili kujitoa kwenye klabu hizo? Ni kufanya vibay kwa timu hizo, kuwepo na migogoro na kadhia zingine. Sasa klabu zinazomilikiwa na asasi za serikali zikanza kuibuka upya. Timu kama KMKM ambayo ilikuwa tishio katika miaka ya 80 ikarudi tena, huku timu ya Polisi ikiibuka na kuchukua ubingwa wa Zenj na kujiwekea historia yake. Mafanikio ya kablu hizi ni kutokana na wachezaji wake kuwa ni waajiliwa wa asasi hizo.

Miembeni inawapasa kutofumba macho katika suala la kuona timu hiyo inabaki kung'ara kama zamani. Ni wajibu wa kila mwanachama, mpenzi na shabiki wa klabu hiyo kukuna kichwa ni kwa namna gani anaweza kuchangia kuona timu hiyo inakuwa na maendeleo endelevu, badala ya kuendelea kumtazama mtu mmoja akifanya kila kitu kwa klabu hiyo kongwe visiwani. Matokea ya ufadhili wa mtu mmoja/mfanyabiashara yapo wazi kwa kablu kadhaa za visiwani humo. Hivyo ni vema kujifunza kutokana na makosa yaliyofanyika katika kablu hizo. Huu usiwe muda wa kuchekelea kuingia uwanjani bure, bali uwe muda wa kuangalia ni kwa vipi timu hiyo itaweza kukaa katika chati ya juu na kufanikiwa kisoka bila ya kutegemea ofa.

Saturday 12 January 2008

Leo ni Miaka 44 ya Mapinduzi ya Zenj

Kila la heri kwa wanamapinduzi wote wa Visiwa vya Zenj, hali kadhalika kwa wasomaji wote wa blog hii...

Mapinduzi Daima...

Katika moja ya vituko vilivyotokea katika shehere za mwanzo za kusherherekea Mapinduzi ya Zenj ni pale Marehemu A. Karume alipokuwa akitoa hotuba yake ambayo ilikuwa ikielezea mafanikio na faida za Mapinduzi hayo. Kwa sauti yake nzito sawa na kilo kadhaa za Nyati, ambayo kwa upande fulani iliwafanya wasikilizaji wake kuwa na kauoga fulani, alitamba kuwa serikali ya mapinduzi (wakati ule) ina fedha nyingi za kigeni(us dollar)zaidi ya idadi ya waakazi wa visiwa hivyo. Aliendelea kwa kusema kuwa fedha hizo ni nyingi kiasi kwa anaweza kumpatia kila mwananchi dola mia za kimarekani na bado fedha ikabaki.

Kijana mmoja kiasi cha miaka kumi na mbili hivi, alinyosha mkono ili aweze kuuliza swali,Wazee waliokuwa karibu yake walijaribu kumzuia kijana huyo kutonyosha mkono. Purukushani hizo zilivuta idadi kubwa ya watu kutazama upande wao, badala ya kuendelea kusikiliza hotuba. Hali hii ilimfanya Marehemu Karume kumruhusu kijana huyo aulize swali lake. Huku akijiamini sana kijana huyo aliuliza hivi..

"Mhe. mimi naomba kupatiwa dola zangu mia sasa hivi..."

Friday 11 January 2008

Wazenj na Kuzamia Ulaya

Kwa miaka mingi kumekuwepo na njia mbalimbali zilizotumiwa na vijana kwenda kutafuta kile wanachodai ni maisha bora. Njia ambazo zilipata umaarufu mkubwa ni ile ya kuzamia kwenye meli.Hii ilikuwa ni katika ile miaka ya themanini ambapo soko la ubaharia lilikuwa kubwa kwa vijana wa kiafrika. Vijana wa Zenj nao hawakuwa nyuma katika hili, wengi waliacha shule na kukimbilia kuzamia meli kwa lengo la kufika ulaya.

Mwishoni wa miaka ya themanini na mwanzoni miaka ya tisini, njia ya kwenda ulaya ilibadilika toka kuzamia meli na kupanda pipa (ndege). Hamu ya kwenda ulaya ilizidi kuwa kubwa mno miongoni wa vijana, na wengine walidiriki hata kuteka ndege(ATC)ili tu waweze kufika huko ulaya. Zaidi wengi waliweza kutumia njia nyingi za kulaghai familia zao au kuiba ili tu waweze kufika huko Ulaya.

Miaka ya tisini, wasomi wa kizenj nao wakaingia katika anga ya kuzamia huko Ulaya na Marekani. Ushawishi mkubwa ulitokana na wingi wa vijana kukimbilia ulaya na hasa Uingereza kwa madai ya ukimbizi kutokana na mfumo wa vyama vingi. Wasomi wengi ambao walibahatika kusomeshwa na SMZ asilimia kubwa wameamua kutorudi tena Zenj na sasa wanaendelea na kutafuta maisha yao huko Ulaya na Marekani. Katika kundi hili wapo pia wale walioacha kazi zao muhimu katika SMZ na mashirika ya SMZ.

Katika karne hii mpya imeibuka njia nyingine ya kuzamia huko ulaya, hii ipo katika uwanja wa michezo na utamaduni. Baada ya mwanamasumbi wa Tanzania Bara kuzamia huko Australia katika michuano ya jumuiya ya madola mwaka 2006, wachezaji wawili wa Zenj Heroes nao waliingia mitini, hii ilikuwa ni mwaka 2007. Mwaka huu nao imeripotiwa kuwa wasanii wawili nao wameingia mitini baada ya kumaliza masomo yao huko nchini Norway.

Kwa ufupi hizo ni njia mbalimbali ambazo wazenj wameona ndio nzuri kabisa ili kuweza kufika huko ulaya. Zaidi kumekuwepo na mafanikio katika ngazi ya kifamilia kwa baadhi ya wazenj waliokimbilia huko ulaya. Wengine wamekutana na maadhibu makubwa ikiwa ni pamoja na kuukana uraia wa nchi yao, kiasi kwamba kwa sasa wanaweza kuja nchini mwao kwa kuomba viza. Wapo ambao wametekwa na mambo ya huko ulaya ambayo hayana faida yoyote kwao zaidi ya mashaka makubwa ya afya zao. Hawa ni wale waliojiingiza katika kutumia madawa ya kulevya na ukahaba.Wapo vile vile wauzaji wa madawa ya kulevya ambao wanaendelea kuwaangamiza wenzao watumiayo madawa hayo.